< Числа 28 >

1 І Господь промовляв до Мойсея, говорячи:
Bwana akamwambia Mose,
2 „Накажи Ізраїлевим синам, і скажи їм: Ви будете пильнувати жертву Мою, хліб Мій для огняни́х Моїх же́ртов, пахощі любі Мої, щоб прино́сити Мені означеного ча́су.
“Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’
3 І скажи їм: Оце огняна́ жертва, що принесете Господе́ві: безвадні однорічні ягнята, — двоє на день, цілопа́лення за́вжди.
Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku.
4 Одне ягня принесеш уранці, а ягня друге принесеш на́двечір.
Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni,
5 І десяту частину ефи пшеничної муки на хлібну жертву, мішану в то́вченій оливі чверть гіна.
kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini ya mafuta ya zeituni.
6 Це стале цілопа́лення, принесене на Сінайській горі на пахощі любі, огняна́ жертва для Господа.
Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
7 А лита жертва його — чверть гіна для одного ягняти. У святині принесеш литу жертву вина для Господа.
Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu.
8 А друге ягня принесеш на́двечір, принесеш як хлі́бну жертву ра́нку й як жертву литу його, — це огняна́ жертва, любі пахощі для Господа.
Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
9 А суботнього дня — двоє однорічних безвадних ягнят, і дві десяті пшеничної муки, жертва хлібна, мішана в оливі, і жертва лита його.
“‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta.
10 Це суботнє цілопа́лення щосуботи його, — окрім цілопа́лення ста́лого та його литої жертви.
Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.
11 А першого дня ваших місяців принесе́те цілопа́лення для Господа: бички, молоде з великої худоби — два, і одного барана, однорічні ягнята — сім безвадних,
“‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari.
12 і три десяті ефи пшеничної муки, жертву хлібну, мішану в оливі, для одно́го бичка, і дві десяті пшеничної муки, жертву хлібну, мішану в оливі, для одно́го барана,
Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa, uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta;
13 і по десятій частині ефи пшеничної муки, жертву хлібну, мішану в оливі, для одно́го ягняти. Це цілопа́лення, пахощі любі, огняна́ жертва для Господа.
pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana.
14 А їхні литі жертви: пів гіна вина буде для бика, а третина гіна для барана, а четвертина гіна для ягняти. Це новомісячне цілопа́лення кожного молодика, для всіх молодиків року.
Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini, na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka.
15 І буде принесений один козел на жертву за гріх для Господа, крім сталого цілопа́лення, і лита жертва його.
Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.
16 А першого місяця, чотирна́дцятого дня місяця — Па́сха для Господа.
“‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana.
17 А п'ятна́дцятого дня того місяця — свято, сім день опрі́сноки їсти.
Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
18 Першого дня — святі збори, жодного робочого зайня́ття не будете робити.
Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida.
19 І принесе́те огняну́ жертву, цілопа́лення для Господа: бички, молоде з великої худоби — два, і одного барана, і сім однорічних ягнят, — безвадні вони будуть у вас.
Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
20 А їхня хлібна жертва — пшенична мука, мішана в оливі, принесете три десяті ефи для бичка й дві десяті для барана.
Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa;
21 По десятій частині ефи́ принесеш для одно́го ягняти, так для семи ягнят.
pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa.
22 І одного козла жертви за гріх на очи́щення вас,
Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu.
23 окрім цілопа́лення ранку, що належить до сталого цілопа́лення, принесе́те оце.
Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi.
24 Як оце, бу́дете прино́сити щоденно сім день хліб огняно́ї жертви, любі пахощі для Господа; окрім сталого цілопа́лення буде це принесене, і лита жертва його́.
Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji.
25 А сьо́мого дня будуть для вас святі збори, — жодного робочого зайняття не будете робити.
Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
26 А дня первопло́дів, коли приносите нову́ хлібну жертву для Господа в ваших тижнях, будуть для вас святі збори, — жодного робочого зайня́ття не будете робити.
“‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
27 І принесе́те цілопа́лення на любі пахощі для Господа: бички, молоде з великої худоби — два, барана одного, сім ягнят однорічних.
Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
28 А їхня хлі́бна жертва: пшенична мука, мішана в оливі, три десяті ефи для одного бичка, дві десяті для одного барана,
Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini;
29 по десятій частині ефи для одного ягняти, так для семи ягнят.
na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba.
30 Козел один, — на очи́щення вас,
Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
31 окрім сталого цілопалення та хлібної його жертви це принесете, — вони будуть безвадні у вас, — і їхні литі жертви.
Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.

< Числа 28 >