< Єзекіїль 1 >
1 І сталося тридцятого року, четвертого місяця, п'ятого дня місяця, коли я був серед полоне́них над річкою Кева́р, відкри́лося небо, і побачив я Божі виді́ння.
Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.
2 П'ятого дня місяця, — це п'ятий рік поло́ну царя Єгояки́ма, —
Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini,
3 сталося Господнє слово до Єзекіїля, сина Бузі́, священика, у халдейському кра́ї над річкою Кева́р, і була там над ним Господня рука.
neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.
4 І побачив я, аж ось бурхли́вий вітер насува́в із пі́вночі, велика хмара та палю́чий огонь; а навколо неї — ся́йво, а з сере́дини його — ніби блискуча мідь, з-посеред огню.
Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto.
5 А з сере́дини його — подоба чотирьох живих істо́т, а оце їхній вид: вони мали подобу люди́ни.
Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu,
6 І кожна мала чотири обли́ччі, і кожна з них мала чотири крилі́.
lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne.
7 А їхня нога — нога про́ста, а стопа́ їхньої ноги — як стопа телячої ноги, і вони ся́яли, як ніби блискуча мідь.
Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa.
8 А під їхніми кри́лами були лю́дські руки на чотирьох сторона́х їхніх, і вони четверо мали свої обличчя та свої кри́ла.
Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa,
9 Їхні кри́ла приляга́ли одне до о́дного, не оберта́лися в ході своїй, — кожне ходило просто наперед себе.
nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.
10 А подо́ба їхнього обличчя — обличчя люди́ни та обличчя лева мали вони четверо з прави́ці, а обличчя вола мали вони четверо з ліви́ці, і обличчя орла мали вони четверо.
Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai.
11 А їхні обличчя та їхні кри́ла були розді́лені вгорі́; у кожного двоє крил злучувалнся одне з о́дним, і двоє закривали їхнє тіло.
Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake.
12 І кожна ходила просто перед себе. Туди, куди бажа́в дух ходити, вони йшли, не оберта́лися в ході своїй.
Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka.
13 А подоба тих істо́т була на вид вугі́лля з огню, вони палали на вигляд смолоски́пів; той огонь прохо́джувався поміж істо́тами. І огонь мав сяйво, і з огню вихо́дила бли́скавка.
Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi.
14 І ті живі істо́ти бігали й верталися, немов бли́скавка.
Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.
15 І придивився я до тих істот, аж ось по одно́му колесі на землі при тих живих істотах, при чотирьох їхніх обличчях.
Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne.
16 Вид тих коле́с та їхній ви́ріб — як вигляд хризолі́ту, й одна подоба їм чотирьом, а їхній вид та їхній виріб — ніби ко́лесо в колесі.
Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake.
17 Вони ходили в ході своїй на чотири бо́ки, не оберта́лися в ході́ своїй.
Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda.
18 А їхні обі́ддя були високі та страшні́; і їхнє обі́ддя довко́ла в чотирьох їх було повне оче́й.
Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.
19 І коли ходили ті живі істоти, ходили й ті коле́са при них; а коли ті істоти підіймалися з-над землі, підіймалися й ті коле́са.
Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka.
20 Куди бажав дух ходити, ішли, куди мав той дух іти; і ті коле́са підіймалися з ними, бо в коле́сах був дух істот.
Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
21 Коли ті йшли, ходили й вони; а коли ті стояли — стояли й вони; а коли ті підійма́лися з-над землі, підіймалися з ними й ті коле́са, бо був дух істот у тих коле́сах.
Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
22 А на головах тих живих істот була подоба небозво́ду, ніби грізний кришта́ль, розтя́гнений над їхніми голова́ми згори.
Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha.
23 А під цим небозво́дом були їхні про́сті кри́ла, зве́рнені одне до о́дного. У кожної було по двоє крил, що закривали їм їхні тіла́.
Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake.
24 А коли вони йшли, чув я шум їхніх крил, як шум великої води, як голос Всемогу́тнього, звук га́мору, як табо́ру. А коли вони ставали, опадали їхні крила.
Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi, kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.
25 І розлягався голос з-над небозво́ду, що над їхньою головою. І коли вони ставали, опадали їхні кри́ла.
Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa.
26 А згори небозво́ду, що над їхньою головою, була подоба трону на вигляд каменя сапфі́ру; а на подобі трону була подоба на вигляд люди́ни, на ньому згори.
Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu.
27 І бачив я ніби блискучу мідь, на вид огню в сере́дині його навколо, від виду сте́гон його й вище, а від виду сте́гон його й до долу бачив я ніби огонь та ся́йво навко́ло нього.
Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka.
28 Як ви́гляд весе́лки, що буває в хмарі в дощови́й день, такий був ви́гляд сяйва навко́ло. Це був ви́гляд подоби Господньої слави! І коли я це побачив, я впав на обличчя своє, і почув голос, що говорив.
Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka. Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.