< До римлян 11 >
1 Глаголю ж оце: Чи вже ж відопхнув Бог людей своїх? Нехай не буде! Бо й я Ізраїльтянин, із насіння Авраамового, із роду Беняминового.
Basi, nauliza: je, Mungu amewakataa watu wake? Hata kidogo! Mini binafsi ni Mwisraeli mzawa wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.
2 Не відопхнув Бог людей своїх, котрих перше знав. Хиба не відаєте, що про Ілию глаголе писаннє? як він обертаєть ся до Бога проти Їзраїля глаголючи:
Mungu hakuwakataa watu wake aliowateua tangu mwanzo. Mnakumbuka yasemavyo Maandiko Matakatifu juu ya Eliya wakati alipomnung'unikia Mungu kuhusu Israeli:
3 Господи, пророки Твої повбивали, і жертівнї Твої порозкидали; я зоставсь один, і шукають души моєї.
“Bwana, wamewaua manabii wako na kubomoa madhabahu yako. Ni mimi tu peke yangu niliyebaki, nao wanataka kuniua?”
4 Що ж глаголе йому Божа відповідь? Зоставив я собі сїм тисяч мужів, що не приклонили колїна перед Ваалом.
Je, Mungu alimjibu nini? Alimwambia: “Nimejiwekea elfu saba ambao hawakumwabudu Baali.”
5 Оттак же і в теперішнім часї єсть останок по вибору благодаті.
Basi, ndivyo ilivyo pia wakati huu wa sasa: ipo idadi ya waliobaki ambao Mungu aliwateua kwa sababu ya neema yake.
6 Коли ж по благодаті, то не по дїлам; ато благодать не була б уже більш благодаттю. Коли ж по ділам, то більш нема благодаті; ато дїло не було б уже більш дїлом.
Uteuzi wake unatokana na neema yake, na si kwa sababu ya matendo yao. Maana, kama uteuzi wake ungetegemea matendo ya watu, neema yake haingekuwa neema tena.
7 Що ж? чого шукав Ізраїль, того не осяг, а вибір осяг, инші ж ослїпли,
Sasa, je? Watu wa Israeli hawakukipata kile walichokuwa wanakitafuta; lakini wote walioteuliwa walikipata. Wengine walipumbazwa,
8 (яко ж писано: Дав їм Бог духа дрімоти; очі, щоб не бачили, й уші, щоб не чули) до днешнього дня.
kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mungu ameifanya mioyo yao kuwa mizito, na mpaka leo hii hawawezi kuona kwa macho yao wala kusikia kwa masikio yao.”
9 І Давид глаголе: Нехай буде трапеза їх на сїть і на ловитву, і на поблазнь, і на відплату їм.
Naye Daudi anasema: “Karamu zao na ziwe mtego wa kuwanasa, waanguke na kuadhibiwa.
10 Нехай оморочать ся очі їх, щоб не бачили, і хребет їх завсїди зігнутий.
Macho yao yatiwe giza wasiweze kuona. Migongo yao ipindike kwa taabu daima!”
11 Глаголю й питаю теперь: Чи вони спіткнулись, щоб (на завсїди) упали? Нехай не буде! їх-то упадком і спасеннє поганам, щоб завдати їм зависти.
Basi, nauliza: je, Wayahudi wamejikwaa hata wakaangamia kabisa? Hata kidogo! Kutokana na kosa lao ukombozi umewajia watu wa mataifa mengine, ili Wayahudi wapate kuwaonea wivu.
12 Коли ж упадок їх багацтво сьвіту, і відпаденнє їх багацтво поган, скільки ж більше повнота їх?
Kosa la Wayahudi limesababisha baraka nyingi kwa ulimwengu, na utovu wao kwa kiroho umeleta baraka nyingi kwa watu wa mataifa mengine. Basi, ni dhahiri zaidi kwamba utimilifu wao utasababisha baraka nyingi zaidi.
13 Вам бо, поганам, глаголю, на скільки я апостол поганам: Службу мою прославляю,
Basi, sasa nawaambieni ninyi watu wa mataifa mengine: Maadamu mimi nimekuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine, ninajivunia huduma yangu,
14 чи не завдам як зависти тїлу моєму, і не спасу которих із них.
nipate kuwafanya wananchi wenzangu wawaonee ninyi wivu, na hivyo nipate kuwaokoa baadhi yao.
15 Коли бо відкинуттє їх примиреннє сьвітові, що ж (буде) прийняттє, коли не життє з мертвих?
Maana ikiwa kukataliwa kwao kulisababisha ulimwengu upatanishwe na Mungu, itakuwaje wakati watakapokubaliwa na Mungu? Wafu watafufuka!
16 Коли ж росчина сьвята, то й заміс; і коли корінь сьвят, то й віттє.
Ikiwa kipande cha kwanza cha mkate kimewekwa wakfu, mkate wote umewekwa wakfu; mizizi ya mti ikiwa mizuri, na matawi yake huwa mazuri pia.
17 Коли ж деякі з віття відломились, а ти, бувши дикою оливиною, прищепивсь єси замість них, і спільником коріння і туку оливного зробивсь єси,
Naam, baadhi ya matawi ya mzeituni bustanini yalikatwa, na mahali pake tawi la mzeituni mwitu likapandikizwa. Ninyi watu wa mataifa mengine ndio hilo tawi la mzeituni mwitu; na sasa mnashiriki nguvu na utomvu wa mzeituni bustanini.
18 то не величай ся перед віттєм. Коли ж величаєш ся, то (знай) не ти кореня носиш, а корінь тебе.
Basi, msiwadharau wale waliokatwa kama matawi! Na, hata kama kuna la kujivunia, kumbukeni kwamba si ninyi mnaoitegemeza mizizi, bali mizizi ndiyo inayowategemeza ninyi.
19 Ти ж кажеш: Відломилось віттє, щоб я прищепив ся.
Lakini utasema: “Matawi yalikatwa kusudi mimi nipandikizwe mahali pake.”
20 Добре: невірою відломились вони, ти ж вірою стоїш. Не носись високо, а бій ся.
Sawa! Yalikatwa kwa sababu ya kukosa imani, bali wewe unasimama kwa imani yako. Lakini usijivune; ila uwe na tahadhari.
21 Коли бо Бог природнього віття не пощадив, (гледи) що й тебе не пощадить.
Kwa maana, ikiwa Mungu hakuwahurumia Wayahudi ambao ni kama matawi ya asili, je, unadhani atakuhurumia wewe?
22 Вбачай же благость і непощадіннє Боже: на тих, що відпали, непощадіннє; на тебе ж благость, коли пробувати меш у благости; коли ж нї, то й ти будеш відтятий.
Kumbuka, basi, jinsi Mungu alivyo mwema na mkali. Yeye ni mkali kwa wale walioanguka, na ni mwema kwako wewe ikiwa utaendelea katika wema wake; la sivyo, nawe pia utakatwa.
23 І вони ж, як не зостануть ся в невірстві, прищепляться; здолїе бо Бог знов прищепити їх.
Nao Wayahudi, hali kadhalika; wakiacha utovu wao wa imani, watapandikizwa tena. Maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena.
24 Коли бо ти відтятий від оливини, дикої по природі, і проти природи прищеплений до доброї оливини, то як більш сї, що по природі прищеплять ся до своєї сливини.
Ninyi watu wa mataifa mengine, kwa asili ni kama tawi la mzeituni mwitu, lakini mmeondolewa huko, mkapandikizwa katika mzeituni bustanini mahali ambapo kwa asili si penu. Lakini, Wayahudi kwa asili ni kama mzeituni bustanini, na itakuwa jambo rahisi zaidi kwao kupandikizwa tena katika mti huohuo wao.
25 Не хочу бо, щоб ви не відали тайни сієї, брати (щоб не були самі в собі мудрими), що ослїпленнє від части Ізраїлеві стало ся, доки сповненнє поган увійде.
Ndugu zangu, napenda mjue ukweli huu uliofichika msije mkajiona wenye akili sana. Ukaidi wa Wayahudi ulikuwa ni wa muda tu, mpaka watu wa mataifa mengine watakapokuwa wamemfikia Mungu.
26 І так увесь Ізраїль спасеть ся, яко ж писано: Прийде з Сіону Збавитель, і одверне безбожже від Якова;
Hapo ndipo taifa lote la Israeli litakapookolewa, kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: “Mkombozi atakuja kutoka Sioni, atauondoa uovu wa Yakobo.
27 і се їм од мене завіт, коли зниму гріхи їх.
Hili ndilo agano nitakalofanya nao wakati nitakapoziondoa dhambi zao.”
28 По благовістю (вони) вороги задля вас; по вибранню ж полюблені задля отцїв.
Kwa sababu wanaikataa Habari Njema, Wayahudi wamekuwa adui wa Mungu, lakini kwa faida yenu nyinyi watu wa mataifa. Lakini, kwa kuwa waliteuliwa, bado ni rafiki wa Mungu kwa sababu ya baba zao.
29 Бо в даруваннях і покликанню Бог не каєть ся.
Maana Mungu akisha wapa watu zawadi zake na kuwateua, hajuti kwamba amefanya hivyo.
30 Бо, як і ви колись противились Богові, тепер же помилувані через непокору сих,
Hapo awali ninyi mlikuwa mmemwasi Mungu, lakini sasa mmepata huruma yake kutokana na kuasi kwao.
31 так і сї тепер противились, щоб через ваше помилуваннє і їх помилувано.
Hali kadhalika, kutokana na huruma mliyojaliwa ninyi, Wayahudi wanamwasi Mungu sasa ili nao pia wapokee sasa huruma ya Mungu.
32 Зачинив бо Бог усїх у непокору, щоб усїх помилувати. (eleēsē )
Maana Mungu amewafunga watu wote katika uasi wao ili wapate kuwahurumia wote. (eleēsē )
33 О, глибино багацтва і премудрости і розуму Божого! як не довідомі присуди Його і не досліджені дороги Його!
Utajiri, hekima na elimu ya Mungu ni kuu mno! Huruma zake hazichunguziki, na njia zake hazieleweki! Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:
34 Хто бо зрозумів ум Господень? або хто порадником Йому був?
“Nani aliyepata kuyajua mawazo ya Bwana? Nani awezaye kuwa mshauri wake?
35 або хто наперед дав Йому, щоб Він віддав йому?
Au, nani aliyempa yeye kitu kwanza hata aweze kulipwa tena kitu hicho?”
36 Бо з Него, і Ним, і в Него все. Єму слава на віки. Амінь. (aiōn )
Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, vyote vipo kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Utukufu na uwe kwake hata milele! Amina. (aiōn )