< 1 Berɛsosɛm 6 >

1 Na Lewi mmammarima yɛ: Gerson, Kohat ne Merari.
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
2 Na Kohat asefoɔ nso yɛ: Amram, Ishar, Hebron ne Usiel.
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
3 Na Amram mma yɛ: Aaron, Mose ne Miriam. Na Aaron mmammarima yɛ: Nadab, Abihu, Eleasa ne Itamar.
Amramu alikuwa na wana: Aroni, Mose, na Miriamu. Aroni alikuwa na wana: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
4 Eleasa woo Pinehas. Pinehas woo Abisua.
Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
5 Abisua woo Buki, na Buki woo Usi,
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi,
6 Usi woo Serahia, Serahia woo Meraiot,
Uzi akamzaa Zerahia, Zerahia akamzaa Merayothi,
7 Meraiot woo Amaria, na Amaria woo Ahitub,
Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
8 Ahitub woo Sadok, na Sadok woo Ahimaas,
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi,
9 Ahimaas woo Asaria, Asaria woo Yohanan,
Ahimaasi akamzaa Azaria, Azaria akamzaa Yohanani,
10 Yohanan woo Asaria, a ɔno na na ɔyɛ ɔsɔfopanin wɔ asɔredan a Salomo sii wɔ Yerusalem no mu.
Yohanani akamzaa Azaria (ndiye alifanya kazi ya ukuhani katika Hekalu alilojenga Mfalme Solomoni huko Yerusalemu),
11 Asaria woo Amaria, Amaria woo Ahitub,
Azaria akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
12 Ahitub woo Sadok, Sadok woo Salum,
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Shalumu,
13 Salum woo Hilkia, Hilkia woo Asaria.
Shalumu akamzaa Hilkia, Hilkia akamzaa Azaria,
14 Asaria woo Seraia, Seraia woo Yehosadak.
Azaria akamzaa Seraya, Seraya akamzaa Yehosadaki.
15 Wɔtwaa Yehosadak asuo ɛberɛ a Awurade de Yudafoɔ ne Yerusalemfoɔ kɔɔ nnommum mu a na wɔhyɛ Nebukadnessar ase no.
Yehosadaki alihamishwa wakati Bwana aliwapeleka uhamishoni watu wa Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Mfalme Nebukadneza.
16 Na Lewi mmammarima din de: Gersom, Kohat ne Merari.
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
17 Na Libni ne Simei ka Gerson asefoɔ ho.
Haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni: Libni na Shimei.
18 Na Amram, Ishar, Hebron ne Usiel ka Kohat asefoɔ no ho.
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
19 Na Mahli ne Musi ka Merari asefoɔ no ho. Yeinom ne Lewifoɔ mmusua sɛdeɛ wɔn mpanimfoɔ nnidisoɔ teɛ.
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Zifuatazo ni koo za Walawi zilizoorodheshwa kufuatana na baba zao:
20 Na Gerson asefoɔ yɛ: Libni, Yahat, Sima,
Wazao wa Gershoni: Gershoni akamzaa Libni, Libni akamzaa Yahathi, Yahathi akamzaa Zima,
21 Yoa, Ido, Serah ne Yeaterai.
Zima akamzaa Yoa, Yoa akamzaa Ido, Ido akamzaa Zera, Zera akamzaa Yeatherai.
22 Na Kohat asefoɔ ne Aminadab, Kora, Asir,
Wazao wa Kohathi: Kohathi akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Kora, Kora akamzaa Asiri,
23 Elkana, Ebiasaf, Asir,
Asiri akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Ebiasafu, Ebiasafu akamzaa Asiri,
24 Tahat, Uriel, Usia ne Saulo.
Asiri akamzaa Tahathi, Tahathi akamzaa Urieli, Urieli akamzaa Uzia, Uzia akamzaa Shauli.
25 Na Elkana asefoɔ ne: Amasai, Ahimot,
Wazao wa Elikana walikuwa: Amasai na Ahimothi,
26 Sofai, Nahat,
Ahimothi akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Sofai, Sofai akamzaa Nahathi,
27 Eliab, Yeroham, Elkana ne Samuel.
Nahathi akamzaa Eliabu, Eliabu akamzaa Yerohamu, Yerohamu akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Samweli.
28 Na Samuel mmammarima din ne: Yoɛl a ɔyɛ ɔpanin ne Abiya a ɔtɔ so mmienu no.
Wana wa Samweli walikuwa: Yoeli mzaliwa wake wa kwanza, na Abiya mwanawe wa pili.
29 Na Merari mma ne: Mahli, Libni, Simei, Usa,
Wafuatao ndio wazao wa Merari: Merari akamzaa Mahli, Mahli akamzaa Libni, Libni akamzaa Shimei, Shimei akamzaa Uza,
30 Simea, Hagia ne Asaia.
Uza akamzaa Shimea, Shimea akamzaa Hagia, Hagia akamzaa Asaya.
31 Dawid maa saa nnipa a wɔn din didi soɔ yi dii Awurade fie nnwom anim, ɛberɛ a wɔde Apam Adaka no sii hɔ no.
Hawa ndio watu ambao Daudi aliwaweka kuwa viongozi wa uimbaji katika nyumba ya Bwana, baada ya Sanduku la Agano kuletwa ili kukaa huko.
32 Wɔde nnwom kaa wɔn som ho wɔ Ahyiaeɛ Ntomadan no mu hɔ, kɔsii sɛ Salomo sii Awurade asɔredan no wɔ Yerusalem. Afei, wɔnam mmara a wɔde maa wɔn so dii wɔn dwuma wɔ hɔ.
Walihudumu kwa kuimba mbele ya Maskani, Hema la Kukutania, mpaka hapo Mfalme Solomoni alipojenga Hekalu la Bwana huko Yerusalemu. Walitimiza wajibu wao kulingana na taratibu walizokuwa wamewekewa.
33 Saa mmarima yi na wɔne wɔn mma somm wɔ hɔ no. Heman, dwom ho nimdefoɔ no, na ɔfiri Kohat abusua mu. Wɔto nʼabusuadua ana firi Yoɛl, Samuel,
Wafuatao ni watu waliohudumu pamoja na wana wao: Kutoka ukoo wa Kohathi walikuwa: Hemani, mpiga kinanda, alikuwa mwana wa Yoeli, mwana wa Samweli,
34 Elkana, Yeroham, Eliel, Yoa,
mwana wa Elikana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elieli, mwana wa Toa,
35 Suf, Elkana, Mahat, Amasai,
mwana wa Sufu, mwana wa Elikana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai,
36 Elkana, Yoɛl, Asaria, Sefania,
mwana wa Elikana, mwana wa Yoeli, mwana wa Azaria, mwana wa Sefania,
37 Tahat, Asir, Ebiasaf, Kora,
mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora,
38 Ishar, Kohat, Lewi ne Israel ase;
mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli;
39 Herman abadiakyire a ɔdi ɛkan no din de Asaf, a na ɔfiri Gerson abusua mu. Wɔto Asaf abusuadua ana firi Berekia, Simea,
na msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliyesimama mkono wa kuume: Asafu mwana wa Berekia, mwana wa Shimea,
40 Mikael, Baaseia, Malkia,
mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya,
41 Etni, Serah, Adaia,
mwana wa Ethni, mwana wa Zera, mwana wa Adaya,
42 Etan, Sima, Simei,
mwana wa Ethani, mwana wa Zima, mwana wa Shimei,
43 Yahat, Gersom ne Lewi ase.
mwana wa Yahathi, mwana wa Gershoni, mwana wa Lawi.
44 Herman abadiakyire a ɔtɔ so mmienu no din de Etan, a na ɔfiri Merari abusua mu. Wɔto Etan abusuadua ana firi Kisi, Abdi, Maluk,
Na kutoka kwa walioshirikiana nao, Wamerari, mkono wake wa kushoto: Ethani mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki,
45 Hasabia, Amasia, Hilkia,
mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia,
46 Amsi, Bani, Semer,
mwana wa Amsi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri,
47 Mahli, Musi, Merari ne Lewi ase.
mwana wa Mahli, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.
48 Na wɔn abusuafoɔ a wɔyɛ Lewifoɔ no nso, wɔmaa wɔn dwuma ahodoɔ bi dii wɔ Ahyiaeɛ Ntomadan a ɛyɛ Onyankopɔn fie no mu.
Ndugu zao wengine Walawi walipewa huduma nyingine za kuhudumia hema takatifu, nyumba ya Mungu.
49 Aaron ne nʼasefoɔ nko na wɔsom sɛ asɔfoɔ. Na wɔde afɔrebɔdeɛ gu ɔhyeɛ afɔrebukyia ne ohwam afɔrebukyia so, na wɔdi dwuma biara a ɛfa kronkron mu kronkron hɔ ho. Wɔnam mmara a Onyankopɔn ɔsomfoɔ Mose de maa wɔn no so yɛɛ mpatadeɛ maa Israel.
Lakini Aroni na uzao wake ndio waliokuwa na wajibu wa kutoa sadaka katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba pamoja na yote yaliyofanyika pa Patakatifu, wakifanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, sawasawa na yale yote aliyoagiza Mose mtumishi wa Mungu.
50 Na Aaron asefoɔ yɛ: Eleasa, Pinehas, Abisua,
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Aroni: Aroni akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
51 Buki, Usi, Serahia,
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi, Uzi akamzaa Zerahia,
52 Meraiot, Amaria, Ahitub,
Zerahia akamzaa Merayothi, Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
53 Sadok ne Ahimaas.
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi.
54 Yei ne abakɔsɛm a ɛfa nkuro ne asase a wɔnam ntontobɔ kronkron so de maa Aaron ne nʼasefoɔ a wɔfiri Kohat abusua mu no.
Zifuatazo ni sehemu walizopewa ziwe nchi yao kwa ajili ya makazi yao (walipewa wazao wa Aroni waliotoka katika ukoo wa Wakohathi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
55 Na Hebron ne mmoa adidibea nsase a atwa ho ahyia wɔ Yuda no ka ho.
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda pamoja na sehemu ya malisho inayouzunguka.
56 Nanso, kuro no ho mfuo ne ɛho nkuraa no deɛ, wɔde maa Yefune babarima Kaleb.
Lakini mashamba pamoja na vijiji vilivyouzunguka mji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 Enti, saa nkuro yi a mmoa adidibea atwa ebiara ho ahyia na wɔde maa Aaron asefoɔ: Hebron a ɛyɛ dwanekɔbea kuro, Libna, Yatir, Estemoa,
Kwa hiyo wazao wa Aroni walipewa miji ifuatayo pamoja na eneo la malisho: Hebroni (mji wa makimbilio), Libna, Yatiri, Eshtemoa,
58 Hilen, Debir,
Hileni, Debiri,
59 Asan, Yuta ne Bet-Semes.
Ashani, Yuta na Beth-Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho.
60 Na wɔmaa wɔn Gibeon, Geba, Alemet ne Anatot firii Benyamin asase mu a mmoa adidibea ka emu biara ho. Enti, nkurotoɔ dumiɛnsa na wɔde maa Aaron asefoɔ.
Kutoka kabila la Benyamini walipewa Gibeoni, Geba, Alemethi na Anathothi, pamoja na maeneo yake ya malisho. Miji hii kumi na mitatu iligawanywa miongoni mwa koo za Wakohathi.
61 Na Kohat asefoɔ a wɔkaeɛ no nso, wɔnyaa nkurotoɔ edu a wɔnam ntontobɔ kronkron so firii Manase abusua fa no asase so.
Wazao waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za nusu ya kabila la Manase.
62 Gerson asefoɔ nam ntontobɔ kronkron so nyaa nkurotoɔ dumiɛnsa firii Isakar, Aser ne Naftali nsase so. Wɔnyaa bi nso firii Basan pɔ mu a ɛyɛ Manase dea, a ɛwɔ Yordan apueeɛ fam no.
Wazao wa Gershoni, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na mitatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri na Naftali kutoka sehemu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 Merari asefoɔ nam ntontobɔ kronkron so, nyaa nkurotoɔ dumienu firii Ruben, Gad ne Sebulon nsase so.
Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
64 Enti, Israelfoɔ de saa nkuro yi ne mmoa adidibea yi nyinaa maa Lewifoɔ.
Kwa hiyo Waisraeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yake ya malisho.
65 Wɔnam ntontobɔ kronkron so na wɔde nkuro a ɛwowɔ Yuda, Simeon ne Benyamin nsase so maeɛ sɛdeɛ wɔaka dada no.
Kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini walipewa miji iliyotajwa hapo juu.
66 Saa nkurotoɔ yi ne ɛho mmoa adidibea na Kohat asefoɔ nya firii Efraim asase so:
Baadhi ya koo za Wakohathi walipewa kama nchi yao miji kutoka kabila la Efraimu.
67 Sekem a ɛyɛ dwanekɔbea kuro a ɛwɔ Efraim bepɔ asase no so, Geser,
Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji wa makimbilio) na Gezeri,
68 Yokmeam, Bet-Horon,
Yokmeamu, Beth-Horoni,
69 Ayalon ne Gat-Rimon.
Aiyaloni na Gath-Rimoni, pamoja na maeneo yake ya malisho.
70 Kohat asefoɔ nkaeɛ no, wɔde saa nkurotoɔ a ɛfiri Manase abusua fa no mu na ɛmaa wɔn: Aner ne Bileam a emu biara mmoa adidibea ka ho.
Kutoka nusu ya kabila la Manase, Waisraeli waliwapa koo za Wakohathi waliobaki miji ya Aneri na Bileamu pamoja na maeneo yake ya malisho.
71 Gerson asefoɔ nyaa kuro a wɔfrɛ no Golan a ɛwɔ Basan no firii Manase abusua fa asase so a Astarot ka ho, a ne nyinaa mmoa adidibea da ho.
Wagershoni walipokea miji ifuatayo pamoja na maeneo yake ya malisho: Katika nusu ya kabila la Manase: walipewa Golani katika Bashani na pia Ashtarothi.
72 Isakar asase so nso, wɔmaa wɔn Kedes, Daberat,
Kutoka kabila la Isakari walipokea Kedeshi, Daberathi,
73 Ramot ne Anem a wɔn mmoa adidibea ka ho.
Ramothi na Anemu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
74 Aser asase so, wɔnyaa Masal, Abdon,
Kutoka kabila la Asheri walipokea Mashali, Abdoni,
75 Hukok ne Rehob a na emu biara mmoa adidibea ka ho.
Hukoki na Rehobu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
76 Naftali asase so, wɔde Kedes a ɛwɔ Galilea, Hamon ne Kiriataim maa wɔn, a na mmoa adidibea ka emu biara ho.
Kutoka kabila la Naftali walipokea Kedeshi katika Galilaya, Hamoni na Kiriathaimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
77 Merari asefoɔ nkaeɛ no nyaa Yokneam, Karta, Rimon ne Tabor nkuro firi Sebulon asase so, a na mmoa adidibea ka ebiara ho.
Wamerari (Walawi waliobakia) walipokea miji ifuatayo: kutoka kabila la Zabuloni walipokea Yokneamu, Karta, Rimoni na Tabori pamoja na maeneo yake ya malisho.
78 Ruben asase a ɛda Asubɔnten Yordan apueeɛ fam a ɛne Yeriko di nhwɛanim no nso, wɔnyaa Beser a ɛyɛ anweatam kuro, Yahas,
Kutoka kabila la Reubeni, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko walipokea Bezeri ulioko jangwani, Yahasa,
79 Kedemot ne Mefaat a mmoa adidibea ka emu biara ho.
Kedemothi na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
80 Na Gad asase so nso, wɔnyaa Ramot a ɛwɔ Gilead, Mahanaim,
Na kutoka kabila la Gadi walipokea Ramothi huko Gileadi, Mahanaimu,
81 Hesbon ne Yaser a mmoa adidibea ka ebiara ho.
Heshboni na Yazeri, pamoja na maeneo yake ya malisho.

< 1 Berɛsosɛm 6 >