< 1 Beresosɛm 2 >
1 Israel mmabarima yɛ Ruben, Simeon, Lewi, Yuda, Isakar, Sebulon,
Hawa ndio waliokuwa wana wa Israeli: Reubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zabuloni,
2 Dan, Yosef, Benyamin, Naftali, Gad ne Aser.
Dani, Yosefu, Benyamini, Naftali, Gadi na Asheri.
3 Yuda ne Kanaannibea Bat-Sua woo mmabarima baasa. Na wɔn din de Er, Onan ne Sela. Nanso na abakan Er no yɛ omumɔyɛfo nti, Awurade kum no.
Wana wa Yuda walikuwa: Eri, Onani na Shela. Hawa watatu walizaliwa kwake na mkewe Mkanaani, binti wa Shua. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa Bwana, kwa hiyo Bwana alimuua.
4 Akyiri no, Yuda ne nʼase kunafo Tamar woo nta. Na wɔn din de Peres ne Serah. Enti Yuda woo mmabarima baanum.
Tamari, mkwewe Yuda, alimzalia wana wawili: Peresi na Zera. Yuda alikuwa na jumla ya wana watano.
5 Na Peres mmabarima din de Hesron ne Hamul.
Wana wa Peresi walikuwa: Hesroni na Hamuli.
6 Serah mmabarima din de Simri, Etan, Heman, Kalkol ne Dara; wɔyɛ baanum.
Wana wa Zera walikuwa: Zimri, Ethani, Hemani, Kalkoli na Dara. Jumla ya wana wa Zera walikuwa watano.
7 Akar a ɔyɛ Karmi babarima ne Serah asefo no mu baako nam fa a ɔfaa asade a wogyaw maa Awurade no so, de amanehunu baa Israelfo so.
Mwana wa Karmi alikuwa: Akari, ambaye alileta taabu kwa Waisraeli kwa kukiuka onyo la kutokuchukua vitu vilivyokuwa vimewekwa wakfu.
8 Na Etan babarima ne Asaria.
Mwana wa Ethani alikuwa: Azariya.
9 Hesron mmabarima din de Yerahmeel, Ram ne Kaleb.
Wana wa Hesroni walikuwa: Yerameeli, Ramu na Kalebu.
10 Ram yɛ Aminadab agya. Aminadab yɛ Nahson a na ɔyɛ Yuda ntuanoni no agya.
Ramu alimzaa Aminadabu, na Aminadabu akamzaa Nashoni, kiongozi wa kabila la Yuda.
11 Nahson yɛ Salma agya. Na Salma nso yɛ Boas agya.
Nashoni akamzaa Salmoni, Salmoni akamzaa Boazi,
12 Boas yɛ Obed agya. Obed yɛ Yisai agya.
Boazi akamzaa Obedi, Obedi akamzaa Yese.
13 Yisai abakan yɛ Eliab nea ɔto so abien yɛ Abinadab na nea ɔto so abiɛsa yɛ Simea.
Yese akawazaa Eliabu mwanawe wa kwanza; wa pili Abinadabu, wa tatu Shimea,
14 Na nea ɔto so anan yɛ Netanel na Radai to so anum.
wa nne Nethaneli, wa tano Radai,
15 Ne babarima a ɔto so asia no din de Osem na Dawid na na ɔto so ason.
wa sita Osemu, na wa saba Daudi.
16 Na wɔn nuabeanom din de Seruia ne Abigail. Na Seruia woo mmabarima baasa a wɔn din yɛ Abisai, Yoab ne Asahel.
Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa watatu: Abishai, Yoabu na Asaheli.
17 Abigail waree ɔbarima bi a ne din de Yeter a ɔyɛ Ismaelni na wɔwoo ɔbabarima a wɔtoo no din Amasa.
Abigaili alikuwa mama yake Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri, Mwishmaeli.
18 Na Hesron babarima Kaleb wɔ yerenom baanu a wɔne Asuba ne Yeriot. Na Asuba mmabarima din de Yeser, Sobab ne Ardon.
Kalebu mwana wa Hesroni akazaa wana na mkewe Azuba (na pia na Yeriothi). Hawa ndio wana Azuba aliomzalia Kalebu: Yesheri, Shobabu na Ardoni.
19 Asuba wu akyi no, Kaleb waree Efrata. Wɔwoo ɔbabarima too no din Hur.
Azuba alipofariki, Kalebu akamwoa Efrathi, ambaye alimzalia Huri.
20 Hur woo Uri. Uri nso woo Besaleel.
Huri akamzaa Uri, Uri akamzaa Bezaleli.
21 Bere a Hesron dii mfe aduosia no, ɔwaree Gilead nuabea a na ɔyɛ Makir babea. Wɔwoo ɔbabarima too no din Segub.
Hatimaye, Hesroni akakutana kimwili na binti wa Makiri babaye Gileadi (ambaye alimwoa alipokuwa na umri wa miaka sitini), naye akamzaa Segubu.
22 Segub woo Yair a odii nkurow aduonu abiɛsa so wɔ Gilead asase so no.
Segubu akamzaa Yairi, ambaye alitawala miji ishirini na mitatu katika Gileadi.
23 (Akyiri no, Gesur ne Aram gyee Yair nkurow, san gyee Kenat ne ne nkuraa aduosia a atwa ho ahyia no nyinaa.) Na eyinom nyinaa yɛ Makir a ɔyɛ Gilead agya no asefo.
(Lakini Geshuri na Aramu wakateka miji ya Hawoth-Yairi, pamoja na Kenathi na viunga vyake; jumla ilikuwa miji sitini.) Wote hawa walikuwa wazao wa Makiri babaye Gileadi.
24 Hesron wuu wɔ kurow Kaleb-Efrata mu akyi no, ne yere Abia woo ɔbabarima a wɔtoo no din Asur (Tekoa agya).
Baada ya Hesroni kufa huko Efrathi, Abiya mjane wa Hesroni akamzalia Ashuru, aliye baba wa Tekoa.
25 Hesron abakan Yerahmeel mmabarima a ɔwoo wɔn no din yɛ Ram (abakan), Buna, Oren, Osem ne Ahiya.
Wana wa Yerameeli mzaliwa wa kwanza wa Hesroni walikuwa: Ramu mzaliwa wake wa kwanza, Buna, Oreni, Osemu na Ahiya.
26 Na Yerahmeel wɔ ɔyere a ɔto so abien a wɔfrɛ no Atara, na ɔno na ɔwoo Onam.
Yerameeli alikuwa na mke mwingine, aliyeitwa Atara, aliyekuwa mama yake Onamu.
27 Ram a ɔyɛ Yerahmeel abakan no mmabarima yɛ Maas, Yamin ne Eker.
Wana wa Ramu mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli walikuwa: Maasi, Yamini na Ekeri.
28 Onam mmabarima yɛ Samai ne Yada. Na Samai mmabarima yɛ Nadab ne Abisur.
Wana wa Onamu walikuwa: Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa: Nadabu na Abishuri.
29 Na Abisur ne ne yere Abihail mmabarima yɛ Ahban ne Molid.
Mke wa Abishuri aliitwa Abihaili, ambaye alimzalia Abani na Molidi.
30 Na Nadab mmabarima yɛ Seled ne Apaim. Seled wui a wanwo mma;
Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa bila kuzaa watoto.
31 na Apaim de, ɔwoo ɔbabarima a wɔfrɛ no Yisi. Na Yisi woo Sesan. Na Sesan nyaa nʼaseni bi a wɔfrɛ no Ahlai.
Apaimu akamzaa: Ishi ambaye alikuwa baba wa Sheshani. Sheshani akamzaa Alai.
32 Na Samai nuabarima Yada woo Yeter ne Yonatan. Na Yeter wui a wanwo ba biara,
Wana wa Yada, nduguye Shamai walikuwa: Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa bila kuzaa watoto.
33 nanso Yonatan woo mmabarima baanu a na wɔfrɛ wɔn Pelet ne Sasa. Na eyinom nyinaa yɛ Yerahmeel asefo.
Wana wa Yonathani walikuwa: Pelethi na Zaza. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yerameeli.
34 Na Sesan annya mmabarima, onyaa mmabea. Na ɔwɔ Misraimni somfo bi a ne din de Yarha.
Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, ila wasichana tu. Alikuwa na mtumishi Mmisri aliyeitwa Yarha.
35 Sesan de ne mmabea no mu baako maa Yarha aware na wɔwoo ɔbabarima too no din Atai.
Sheshani akamwoza huyu mtumishi wake Yarha binti yake, akamzalia mwana jina lake Atai.
36 Atai woo Natan na Natan woo Sabad.
Atai akamzaa Nathani, Nathani akamzaa Zabadi,
37 Sabad woo Efial. Efial woo Obed.
Zabadi akamzaa Eflali, Eflali akamzaa Obedi,
38 Obed woo Yehu na Yehu woo Asaria.
Obedi akamzaa Yehu, Yehu akamzaa Azaria,
39 Asaria woo Heles. Heles woo Eleasa.
Azaria akamzaa Helesi, Helesi akamzaa Eleasa,
40 Eleasa woo Sisemai na Sisemai woo Salum.
Eleasa akamzaa Sismai, Sismai akamzaa Shalumu,
41 Salum woo Yekamia, na Yekamia woo Elisama.
Shalumu akamzaa Yekamia, naye Yekamia akamzaa Elishama.
42 Yerahmeel nua Kaleb babarima piesie ne Mesa a ɔyɛ Sif agya. Na Kaleb babarima a ɔto so abien din de Maresa a ɔyɛ Hebron agya.
Wana wa Kalebu nduguye Yerameeli walikuwa: Mesha mzaliwa wake wa kwanza alimzaa Zifu, naye mwanawe Maresha akamzaa Hebroni.
43 Na Hebron mmabarima yɛ Kora, Tapua, Rekem ne Sema.
Hebroni alikuwa na wana wanne: Kora, Tapua, Rekemu na Shema.
44 Na Sema woo Raham. Raham woo Yorkeam. Na Rekem woo Samai.
Shema alikuwa baba yake Rahamu na Rahamu alikuwa baba wa Yorkeamu na Rekemu alikuwa baba wa Shamai.
45 Na Samai woo Maon. Maon woo Bet-Sur.
Shamai akamzaa Maoni na Maoni akamzaa Beth-Suri.
46 Na Kaleb mpena Efa woo Haran, Mosa ne Gases. Na Haran woo Gases.
Efa, suria wa Kalebu alikuwa mamaye Harani, Mosa na Gazezi. Harani alikuwa baba wa Gazezi.
47 Na Yahdai mmabarima yɛ Regem, Yotam, Gesan, Pelet, Efa ne Saaf.
Wana wa Yadai walikuwa: Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa na Shaafu.
48 Kaleb mpena foforo bi a wɔfrɛ no Maaka woo Seber ne Tirhana.
Maaka suria wa Kalebu alikuwa mamaye Sheberi na Tirhana.
49 Ɔsan woo Saaf a na ɔyɛ Madmana agya ne Sewa a na ɔyɛ Makbena ne Gibea agya. Na Kaleb woo ɔbabea a ne din de Aksa.
Pia Maaka akamzaa Shaafu babaye Madmana, na Sheva babaye Makbena na Gibea. Kalebu alikuwa na binti jina lake Aksa.
50 Eyinom nyinaa yɛ Kaleb asefo. Kaleb yere Efrata abakan Hur mmabarima yɛ Sobal a ɔyɛ Kiriat-Yearim agya
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Kalebu. Wana wa Huri, mzaliwa mkuu wao wa Efrathi, walikuwa: Shobali akamzaa Kiriath-Yearimu,
51 Salma a ɔyɛ Betlehem agya ne Haref a ɔyɛ Bet-Gader agya.
Salma akamzaa Bethlehemu, naye Harefu akamzaa Beth-Gaderi.
52 Sobal a ɔyɛ Kiriat-Yearim agya no mmabarima yɛ Haroe a ne fa yɛ Manahatini
Wazao wa Shobali, baba yake Kiriath-Yearimu, walikuwa: Haroe, nusu ya wakazi wa mji wa Menuhothi,
53 na ne fa a aka no fi Kiriat-Yearim mmusua mu. Sobal asefo a wɔka ho ne Yitrifo, Putifo, Sumatifo ne Misraimfo, wɔn mu na Sorafo ne Estaolfo fi.
pamoja na koo za Kiriath-Yearimu ambazo ni: Waithiri, Waputhi, Washumathi na Wamishrai. Kutokana na watu hawa walizaliwa Wasorathi na Waeshtaoli.
54 Salma asefo yɛ Betlehem, Netofafo, Atrot-Bet-Yoabfo, Manahatafo fa bi, Sorifo,
Wazao wa Salma walikuwa: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, nusu ya Wamanahathi, Wasori,
55 ne akyerɛwfo mmusua a wɔte Yabes no, Tirafo, Simeafo ne Sukatfo. Eyinom nyinaa yɛ Kenifo, Hamat a ɔyɛ Rekab agya no asefo.
pamoja na koo za waandishi zilizoishi katika mji wa Yabesi: yaani Watirathi, Washimeathi na Wasukathi. Hawa ndio Wakeni waliotokana na Hamathi, baba wa nyumba ya Rekabu.