< Rut 3 >

1 Kaynanası Naomi bir gün Rut'a, “Kızım, iyiliğin için sana rahat edeceğin bir yer aramam gerekmez mi?” dedi.
Kisha Naomi akamwambia mkwewe, “Binti yangu, je, nisingelikutafutia pumziko ambako utatunzika vyema?
2 “Hizmetçileriyle birlikte bulunduğun Boaz akrabamız değil mi? Bak şimdi, bu akşam Boaz harman yerinde arpa savuracak.
Je, Boazi, ambaye umekuwa pamoja na watumishi wake wasichana, si jamaa yetu wa karibu? Usiku wa leo atakuwa anapepeta ngano kwenye sakafu ya kupuria.
3 Yıkan, kokular sürün, giyinip harman yerine git. Ama adam yemeyi içmeyi bitirene dek orada olduğunu belli etme.
Basi oga na ukajipake marashi, ujivalie nguo zako nzuri. Kisha uende kwenye sakafu ya kupuria, lakini angalia asijue kwamba upo pale mpaka atakapomaliza kula na kunywa.
4 Adam yatıp uyuduğunda, nerede yattığını belle; sonra gidip onun ayaklarının üzerindeki örtüyü kaldır ve oracıkta yat. Ne yapman gerektiğini o sana söyler.”
Atakapokwenda kulala, angalia mahali atakapolala. Kisha uende ufunue miguu yake, ulale. Naye atakuambia utakalofanya.”
5 Rut ona, “Söylediğin her şeyi yapacağım” diye karşılık verdi.
Ruthu akajibu, “Lolote usemalo nitatenda.”
6 Harman yerine giderek kaynanasının her dediğini yaptı.
Basi akashuka mpaka kwenye sakafu ya kupuria, akafanya kila kitu mama mkwe wake alichomwambia kufanya.
7 Boaz yiyip içti, keyfi yerine geldi. Sonra harman yığınının dibinde uyumaya gitti. Rut da gizlice yaklaştı, onun ayaklarının üzerindeki örtüyü kaldırıp yattı.
Wakati Boazi alipomaliza kula na kunywa, naye akawa amejawa na furaha, alikwenda kulala mwisho wa lundo la nafaka. Ruthu akanyemelea polepole, akafunua miguu yake, na akalala.
8 Gece yarısı adam ürktü; yattığı yerde dönünce ayaklarının dibinde yatan kadını ayrımsadı.
Usiku wa manane, kitu kilimshtua Boazi, akajigeuza, akagundua yupo mwanamke amelala miguuni pake.
9 Ona, “Kimsin sen?” diye sordu. Kadın, “Ben kölen Rut'um” diye yanıtladı. “Kölenle evlen. Çünkü sen yakın akrabamızsın” dedi.
Akauliza, “Wewe ni nani?” Akajibu, “Ni mimi Ruthu, mjakazi wako. Uitande nguo yako juu yangu, kwa sababu wewe ndiwe jamaa wa karibu wa kutukomboa.”
10 Boaz, “RAB seni kutsasın, kızım” dedi. “Bu son iyiliğin, ilkinden de büyük. Çünkü yoksul olsun, zengin olsun, gençlerin peşinden gitmedin.
Akamwambia, “Binti yangu, ubarikiwe na Bwana. Wema huu wa sasa ni mkuu kushinda hata ule ulioonyesha mwanzoni. Hukuwakimbilia vijana, wakiwa matajiri au maskini.
11 Ve şimdi, korkma kızım; her istediğini yapacağım. Bütün kent halkı senin erdemli bir kadın olduğunu biliyor.
Sasa, binti yangu, usiogope. Nitakufanyia yote uliyoomba. Kwa maana mji wote wa watu wangu wanakujua ya kwamba wewe ni mwanamke mwenye tabia nzuri.
12 Yakın akrabanız olduğum doğrudur. Ama benden daha yakın biri var.
Ingawa ni kweli kwamba mimi ndiye jamaa aliye karibu, bado kuna mtu mwingine wa jamaa aliye karibu zaidi wa kukomboa kuliko mimi.
13 Geceyi burada geçir. Sabah olduğunda eğer adam senin için akrabalık görevini yaparsa ne âlâ, varsın yapsın. Ama o, akrabalık görevini yapmak istemezse, yaşayan RAB'be ant içerim ki, bu görevi ben üstlenirim. Sen sabaha kadar yat.”
Wewe kaa hapa usiku huu, kisha asubuhi kama akikubali kukomboa, vyema na akomboe. La sivyo kama hayuko tayari, hakika kama Bwana aishivyo nitafanya hivyo. Lala hapa mpaka asubuhi.”
14 Böylece Rut sabaha kadar Boaz'ın ayakları dibinde yattı. Ama ortalık insanların birbirini seçebileceği kadar aydınlanmadan önce kalktı. Çünkü Boaz, ‘Harman yerine kadın geldiği bilinmemeli’ demişti.
Hivyo huyo mwanamke akalala miguuni pake mpaka asubuhi, akaondoka mapema pasipo mtu kuweza kumtambua mwenzake, maana Boazi alisema, “Isijulikane kabisa ya kuwa mwanamke alifika kwenye sakafu ya kupuria.”
15 Boaz Rut'a, “Sırtındaki şalı çıkar, aç” dedi. Rut şalı açınca Boaz içine altı ölçek arpa boşaltıp onun sırtına yükledi. Sonra Rut kente döndü.
Pia akamwambia, “Leta shela yako uliyoivaa, uitandaze.” Naye alipoitandaza, akamimina vipimo sita vya shayiri, akamtwika. Kisha Ruthu akarudi zake mjini.
16 Rut geri dönünce kaynanası, “Nasıl geçti kızım?” diye sordu. Rut, Boaz'ın kendisi için yaptığı her şeyi anlattı.
Basi Ruthu alipofika kwa mama mkwe wake Naomi, akamuuliza, “Je, binti yangu, ilikuwaje huko?” Ndipo akamwelezea kila kitu Boazi alichomfanyia.
17 Sonra ekledi: “‘Kaynanana eli boş dönme’ diyerek bana bu altı ölçek arpayı da verdi.”
Akaendelea kusema, “Amenipa shayiri vipimo sita akisema, ‘Usiende kwa mama mkwe wako mikono mitupu.’”
18 Naomi, “Kızım, bu işin ne olacağını öğreninceye kadar evde kal” dedi. “Çünkü Boaz bugün bu işi bitirmeden rahat edemeyecek.”
Kisha Naomi akasema, “Subiri binti yangu, mpaka utakapojua kwamba hili jambo limekwendaje. Kwa sababu mtu huyu hatatulia mpaka akamilishe jambo hili leo.”

< Rut 3 >