< Romalilar 14 >
1 İmanı zayıf olanı aranıza kabul edin, ama tartışmalı konulara girmeyin.
Mkaribisheni yeye ambaye imani yake ni dhaifu, lakini si kwa kugombana na kubishana juu ya mawazo yake.
2 Biri her şeyi yiyebileceğine inanır; imanı zayıf olansa yalnız sebze yer.
Mtu mmoja imani yake inamruhusu kula kila kitu, lakini mwingine ambaye imani yake ni dhaifu, hula mboga tu.
3 Her şeyi yiyen, yemeyeni hor görmesin. Her şeyi yemeyen, yiyeni yargılamasın. Çünkü Tanrı onu kabul etmiştir.
Yeye alaye kila kitu asimdharau yeye asiyekula. Wala yeye asiyekula kila kitu asimhukumu yule alaye kila kitu, kwa maana Mungu amemkubali.
4 Sen kimsin ki, başkasının kulunu yargılıyorsun? Kulu haklı çıkaran da haksız çıkaran da efendisidir. Kul haklı çıkacaktır. Çünkü Rab'bin onu haklı çıkarmaya gücü vardır.
Wewe ni nani hata umhukumu mtumishi wa mtu mwingine? Kwa bwana wake tu anasimama au kuanguka. Naye atasimama kwa sababu Bwana anaweza kumsimamisha.
5 Kimi bir günü başka bir günden üstün sayar, kimi her günü bir sayar. Herkesin kendi görüşüne tam güveni olsun.
Mtu mmoja anaitukuza siku fulani kuwa ni bora kuliko nyingine, na mwingine anaona kuwa siku zote ni sawa. Basi kila mmoja awe na hakika na yale anayoamini.
6 Belli bir günü kutlayan, Rab için kutlar. Her şeyi yiyen, Tanrı'ya şükrederek Rab için yer. Bazı şeyleri yemeyen de Rab için yemez ve Tanrı'ya şükreder.
Yeye anayehesabu siku moja kuwa takatifu kuliko nyingine, hufanya hivyo kwa kumheshimu Bwana. Naye alaye nyama hula kwa Bwana, kwa maana humshukuru Mungu, naye akataaye kula nyama hufanya hivyo kwa Bwana na humshukuru Mungu.
7 Hiçbirimiz kendimiz için yaşamayız, hiçbirimiz de kendimiz için ölmeyiz.
Kwa kuwa hakuna hata mmoja wetu anayeishi kwa ajili yake mwenyewe, wala hakuna hata mmoja wetu afaye kwa ajili yake mwenyewe.
8 Yaşarsak Rab için yaşarız; ölürsek Rab için ölürüz. Öyleyse, yaşasak da ölsek de Rab'be aitiz.
Kama tunaishi, tunaishi kwa Bwana, nasi pia tukifa tunakufa kwa Bwana. Kwa hiyo basi, kama tukiishi au kama tukifa, sisi ni mali ya Bwana.
9 Mesih hem ölülerin hem yaşayanların Rabbi olmak üzere ölüp dirildi.
Kwani kwa sababu hii hasa, Kristo alikufa na akawa hai tena kusudi apate kuwa Bwana wa wote, yaani, waliokufa na walio hai.
10 Sen neden kardeşini yargılıyorsun? Ya sen, kardeşini neden küçümsüyorsun? Tanrı'nın yargı kürsüsü önüne hepimiz çıkacağız.
Basi kwa nini wewe wamhukumu ndugu yako? Au kwa nini wewe unamdharau ndugu yako? Kwa kuwa sote tutasimama mbele ya kiti cha Mungu cha hukumu.
11 Yazılmış olduğu gibi: “Rab şöyle diyor: ‘Varlığım hakkı için her diz önümde çökecek, Her dil Tanrı olduğumu açıkça söyleyecek.’”
Kwa kuwa imeandikwa: “‘Kama vile niishivyo,’ asema Bwana, ‘kila goti litapigwa mbele zangu, na kila ulimi utakiri kwa Mungu.’”
12 Böylece her birimiz kendi adına Tanrı'ya hesap verecektir.
Hivyo basi kila mmoja wetu atatoa habari zake mwenyewe kwa Mungu.
13 Onun için, artık birbirimizi yargılamayalım. Bunun yerine, hiçbir kardeşin yoluna sürçme ya da tökezleme taşı koymamaya kararlı olun.
Kwa hiyo tusiendelee kuhukumiana: Badala yake mtu asiweke kamwe kikwazo au kizuizi katika njia ya ndugu mwingine.
14 Rab İsa'ya ait biri olarak kesinlikle biliyorum ki, hiçbir şey kendiliğinden murdar değildir. Ama bir şeyi murdar sayan için o şey murdardır.
Ninajua tena nimehakikishiwa sana katika Bwana Yesu kwamba hakuna kitu chochote ambacho ni najisi kwa asili yake. Lakini kama mtu anakiona kitu kuwa ni najisi, basi kwake huyo kitu hicho ni najisi.
15 Yediğin bir şey yüzünden kardeşin incinmişse, artık sevgi yolunda yürümüyorsun demektir. Mesih'in, uğruna öldüğü kardeşini yediklerinle mahvetme!
Kama ndugu yako anahuzunishwa kwa sababu ya kile unachokula, basi huenendi tena katika upendo. Usiruhusu kile unachokula kiwe sababu ya kumwangamiza ndugu yako ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.
16 Size göre iyi olanın kötülenmesine fırsat vermeyin.
Usiruhusu kile ambacho unakiona kuwa chema kisemwe kuwa ni kiovu.
17 Çünkü Tanrı'nın Egemenliği, yiyecek içecek sorunu değil, doğruluk, esenlik ve Kutsal Ruh'ta sevinçtir.
Kwa maana Ufalme wa Mungu si kula na kunywa, bali ni haki, amani na furaha katika Roho Mtakatifu.
18 Mesih'e bu yolda hizmet eden, Tanrı'yı hoşnut eder, insanların da beğenisini kazanır.
Kwa sababu mtu yeyote anayemtumikia Kristo kwa jinsi hii, anampendeza Mungu na kukubaliwa na wanadamu.
19 Öyleyse kendimizi esenlik getiren ve karşılıklı gelişmemizi sağlayan işlere verelim.
Kwa hiyo na tufanye bidii kutafuta yale yaletayo amani na kujengana sisi kwa sisi.
20 Yiyecek uğruna Tanrı'nın işini bozma! Her yiyecek temizdir, ama yedikleriyle başkasının sürçmesine yol açan kişi kötülük etmiş olur.
Usiiharibu kazi ya Mungu kwa ajili ya chakula. Hakika vyakula vyote ni safi, lakini ni kosa kula kitu chochote kinachomsababisha ndugu yako ajikwae.
21 Et yememen, şarap içmemen, kardeşinin sürçmesine yol açacak bir şey yapmaman iyidir.
Ni afadhali kutokula nyama wala kunywa divai au kufanya jambo lingine lolote litakalomsababisha ndugu yako ajikwae.
22 Bu konulardaki inancını Tanrı'nın önünde kendine sakla. Onayladığı şeyden ötürü kendini yargılamayan kişi ne mutludur!
Je, wewe unayo imani? Ile imani uliyo nayo, uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiye na sababu ya kujihukumu nafsi yake kwa ajili ya kile anachokifanya.
23 Ama bir yiyecekten kuşkulanan kişi onu yerse yargılanır; çünkü imanla yemiyor. İmana dayanmayan her şey günahtır.
Lakini kama mtu ana shaka kuhusu kile anachokula, amehukumiwa, kwa sababu hakula kwa imani. Kwa kuwa chochote kinachofanywa pasipo imani ni dhambi.