< Vahiy 22 +

1 Melek bana Tanrı'nın ve Kuzu'nun tahtından çıkan billur gibi berrak yaşam suyu ırmağını gösterdi.
Kisha malaika akanionyesha mto wa maji ya uzima maangavu kama kioo yakitoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu na Mwanakondoo.
2 Kentin anayolunun ortasında akan ırmağın iki yanında on iki çeşit meyve üreten ve her ay meyvesini veren yaşam ağacı bulunuyordu. Ağacın yaprakları uluslara şifa vermek içindir.
Mto huo ulitiririka kupitia katikati ya barabara kuu ya mji. Kandokando ya mto huo kulikuwa na mti wa uzima unaozaa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, yaani kila mwezi; na majani yake ni dawa ya kuwaponya watu wa mataifa.
3 Artık hiçbir lanet kalmayacak. Tanrı'nın ve Kuzu'nun tahtı kentin içinde olacak, kulları O'na tapınacak.
Hapana kitu chochote kilicholaaniwa kitakachokuwa katika mji huo. Kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwanakondoo kitakuwa katika mji huo, na watumishi wake watamwabudu.
4 O'nun yüzünü görecek, alınlarında O'nun adını taşıyacaklar.
Watauona uso wake, na jina lake litaandikwa juu ya paji za nyuso zao.
5 Artık gece olmayacak. Çıra ışığına da güneş ışığına da gereksinmeleri olmayacak. Çünkü Rab Tanrı onlara ışık verecek ve sonsuzlara dek egemenlik sürecekler. (aiōn g165)
Usiku hautakuwako tena, wala hawatahitaji mwanga wa taa au wa jua, maana Bwana Mungu atawaangazia, nao watatawala milele na milele. (aiōn g165)
6 Melek bana, “Bu sözler güvenilir ve gerçektir” dedi. “Peygamberlerin ruhlarının Tanrısı olan Rab, yakın zamanda olması gereken olayları kullarına göstermek için meleğini gönderdi.”
Kisha malaika akaniambia, “Maneno haya ni ya kweli na ya kuaminika. Bwana Mungu ambaye huwapa manabii Roho wake, alimtuma malaika wake awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo lazima yatukie punde.
7 “İşte tez geliyorum! Bu kitaptaki peygamberlik sözlerine uyana ne mutlu!”
“Sikiliza! Naja upesi. Heri yake anayeyazingatia maneno ya unabii yaliyo katika kitabu hiki.”
8 Bunları işiten ve gören ben Yuhanna'yım. İşitip gördüğümde bunları bana gösteren meleğe tapmak için ayaklarına kapandım.
Mimi Yohane, niliyaona na kusikia mambo haya. Nilipokwisha sikia na kuona nikajitupa chini mbele ya miguu ya huyo malaika aliyenionyesha mambo hayo, nikataka kumwabudu.
9 Ama o bana, “Sakın yapma!” dedi, “Ben senin, peygamber kardeşlerin ve bu kitabın sözlerine uyanlar gibi bir Tanrı kuluyum. Tanrı'ya tap!”
Lakini yeye akaniambia, “Acha! Mimi ni mtumishi tu kama wewe na ndugu zako manabii na wote wanaoyatii maagizo yaliyomo katika kitabu hiki. Mwabudu Mungu!”
10 Sonra bana, “Bu kitabın peygamberlik sözlerini mühürleme” dedi, “Çünkü beklenen zaman yakındır.
Tena akaniambia, “Usiyafiche kama siri maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, maana wakati wa kutimizwa kwake umekaribia.
11 Kötülük yapan, yine kötülük yapsın. Kirli olan, kirli işlerini sürdürsün. Doğru olan, yine doğruyu yapsın. Kutsal olan kutsal kalsın.”
Kwa sasa anayetenda mabaya na aendelee kutenda mabaya, na aliye mchafu aendelee kuwa mchafu. Mwenye kutenda mema na azidi kutenda mema, na aliye mtakatifu na azidi kuwa mtakatifu.”
12 “İşte tez geliyorum! Vereceğim ödüller yanımdadır. Herkese yaptığının karşılığını vereceğim.
“Sikiliza!” Asema Yesu, “Naja upesi, pamoja na tuzo nitakalompa kila mmoja kufuatana na matendo yake.
13 Alfa ve Omega, birinci ve sonuncu, başlangıç ve son Ben'im.
Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho, wa kwanza na wa mwisho.”
14 “Kaftanlarını yıkayan, böylelikle yaşam ağacından yemeye hak kazanarak kapılardan geçip kente girenlere ne mutlu!
Heri yao wale wanaoosha mavazi yao, kwani watakuwa na haki ya kula tunda la mti wa uzima, na haki ya kuingia mjini kwa kupitia milango yake.
15 Köpekler, büyücüler, fuhuş yapanlar, adam öldürenler, putperestler, yalanı sevip hile yapanların hepsi dışarıda kalacaklar.
Lakini mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu na wote wanaopenda kusema uongo, watakaa nje ya mji.
16 “Ben İsa, kiliselerle ilgili bu tanıklığı sizlere iletsin diye meleğimi gönderdim. Davut'un kökü ve soyu Ben'im, parlak sabah yıldızı Ben'im.”
“Mimi, Yesu, nimemtuma malaika wangu awathibitishieni mambo haya katika makanisa. Mimi ni mzawa wa ukoo wa Daudi. Mimi ni nyota angavu ya asubuhi!”
17 Ruh ve Gelin, “Gel!” diyorlar. İşiten, “Gel!” desin. Susayan gelsin. Dileyen, yaşam suyundan karşılıksız alsın.
Roho na Bibiarusi waseme, “Njoo!” Kila mtu asikiaye hili, na aseme, “Njoo!” Kisha, yeyote aliye na kiu na aje; anayetaka maji ya uzima na apokee bila malipo yoyote.
18 Bu kitaptaki peygamberlik sözlerini duyan herkesi uyarıyorum! Her kim bu sözlere bir şey katarsa, Tanrı da bu kitapta yazılı belaları ona katacaktır.
Mimi Yohane nawapa onyo wote wanaosikia maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki: mtu yeyote akiongeza chochote katika mambo haya, Mungu atamwongezea mabaa yaliyoandikwa katika kitabu hiki.
19 Her kim bu peygamberlik kitabının sözlerinden bir şey çıkarırsa, Tanrı da bu kitapta yazılı yaşam ağacından ve kutsal kentten ona düşen payı çıkaracaktır.
Na mtu yeyote akipunguza chochote katika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, Mungu atamnyang'anya sehemu yake katika ule mti wa uzima, na sehemu yake katika mji mtakatifu, ambavyo vimeelezwa katika kitabu hiki.
20 Bunlara tanıklık eden, “Evet, tez geliyorum!” diyor. Amin! Gel, ya Rab İsa!
Naye anayetoa ushahidi wake juu ya mambo haya asema: “Naam! Naja upesi.” Amina. Na iwe hivyo! Njoo Bwana Yesu!
21 Rab İsa'nın lütfu kutsallarla birlikte olsun! Amin.
Nawatakieni nyote neema ya Bwana Yesu. Amen.

< Vahiy 22 +