< Vahiy 11 >

1 Bana değneğe benzer bir ölçü kamışı verilip şöyle dendi: “Git, Tanrı'nın Tapınağı'nı ve sunağı ölç, orada tapınanları say!
Ndipo nikapewa mwanzi uliokuwa kama ufito wa kupimia, nikaambiwa, “Nenda ukapime hekalu la Mungu pamoja na madhabahu, nawe uwahesabu wale waabuduo humo.
2 Tapınağın dış avlusunu bırak, orayı ölçme. Çünkü orası, kutsal kenti kırk iki ay ayaklarıyla çiğneyecek olan uluslara verildi.
Lakini usiupime ua wa nje wa Hekalu, uache, kwa sababu ua huo wamepewa watu wa Mataifa. Hao wataukanyagakanyaga mji mtakatifu kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
3 İki tanığıma güç vereceğim; çul giysiler içinde bin iki yüz altmış gün peygamberlik edecekler.”
Nami nitawapa mashahidi wangu wawili uwezo, nao watoe unabii kwa muda wa siku 1,260, wakiwa wamevaa nguo za gunia.”
4 Bunlar yeryüzünün Rabbi önünde duran iki zeytin ağacıyla iki kandilliktir.
Hawa ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili vya taa visimamavyo mbele za Bwana Mungu wa dunia yote.
5 Biri onlara zarar vermeye kalkışırsa, ağızlarından ateş fışkıracak ve düşmanlarını yiyip bitirecek. Onlara zarar vermek isteyen herkesin böyle öldürülmesi gerekir.
Kama mtu yeyote akitaka kuwadhuru, moto hutoka vinywani mwao na kuwateketeza adui zao. Hivi ndivyo impasavyo kufa mtu yeyote atakayetaka kuwadhuru.
6 Peygamberlik ettikleri sürece yağmur yağmasın diye göğü kapamaya yetkileri vardır. Suları kana dönüştürme ve yeryüzünü, kaç kez isterlerse, her türlü belayla vurma yetkisine sahiptirler.
Watu hawa wanao uwezo wa kufunga anga ili mvua isinyeshe wakati wote watakapokuwa wanatoa unabii wao. Nao watakuwa na uwezo wa kuyabadili maji kuwa damu na kuipiga dunia kwa kila aina ya mapigo mara kwa mara kama watakavyo.
7 Tanıklık görevleri sona erince dipsiz derinliklerden çıkan canavar onlarla savaşacak, onları yenip öldürecek. (Abyssos g12)
Basi watakapokuwa wamemaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika lile Shimo atapigana nao vita, atawashinda na kuwaua. (Abyssos g12)
8 Cesetleri, simgesel olarak Sodom ve Mısır diye adlandırılan büyük kentin anayoluna serilecek. Onların Rabbi de orada çarmıha gerilmişti.
Maiti zao zitabaki katika barabara ya mji mkubwa, ambao kwa fumbo unaitwa Sodoma na Misri, ambapo pia Bwana wao alisulubiwa.
9 Her halktan, oymaktan, dilden, ulustan insan üç buçuk gün cesetlerini seyredecek, cesetlerinin mezara konulmasına izin vermeyecekler.
Kwa muda wa siku tatu na nusu, watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa wataziangalia hizo maiti zao na hawataruhusu wazikwe.
10 Yeryüzünde yaşayanlar onların bu durumuna sevinip bayram edecek, birbirlerine armağanlar gönderecekler. Çünkü bu iki peygamber yeryüzünde yaşayanlara çok eziyet etmişti.
Watu waishio duniani watazitazama kwa furaha maiti za hao manabii wawili na kushangilia kwa kupeana zawadi kwa sababu hao manabii waliwatesa watu waishio duniani.
11 Üç buçuk gün sonra iki peygamber, Tanrı'dan gelen yaşam soluğunu alınca ayağa kalktılar. Onları görenler dehşete kapıldı.
Lakini baada ya zile siku tatu na nusu, pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu ikawaingia, nao wakasimama kwa miguu yao na wote waliowaona wakaingiwa na hofu kuu.
12 İki peygamber gökten gelen yüksek bir sesin, “Buraya çıkın!” dediğini işittiler. Sonra düşmanlarının gözü önünde bir bulut içinde göğe yükseldiler.
Kisha wale manabii wawili wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, “Njooni huku juu!” Nao wakapaa mbinguni katika wingu, wakati adui zao wakiwa wanawatazama.
13 Tam o saatte şiddetli bir deprem oldu, kentin onda biri yıkıldı. Depremde yedi bin kişi can verdi. Geriye kalanlar dehşete kapılıp gökteki Tanrı'yı yücelttiler.
Saa iyo hiyo, kukatokea tetemeko kubwa la nchi na sehemu ya kumi ya mji ikaanguka. Watu elfu saba wakauawa katika tetemeko hilo, nao walionusurika wakaogopa sana, wakamtukuza Mungu wa mbinguni.
14 İkinci “vay” geçti. İşte, üçüncü “vay” tez geliyor.
Ole ya pili imekwisha kupita, tazama ole ya tatu inakuja upesi.
15 Yedinci melek borazanını çaldı. Gökte yüksek sesler duyuldu: “Dünyanın egemenliği Rabbimiz'in ve Mesihi'nin oldu. O sonsuzlara dek egemenlik sürecek.” (aiōn g165)
Yule malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake, pakawa na sauti kubwa mbinguni iliyosema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atatawala milele na milele.” (aiōn g165)
16 Tanrı'nın önünde tahtlarında oturan yirmi dört ihtiyar yüzüstü yere kapandı. Tanrı'ya tapınarak şöyle dediler: “Her Şeye Gücü Yeten, Var olan, var olmuş olan Rab Tanrı! Sana şükrediyoruz. Çünkü büyük gücünü kuşanıp Egemenlik sürmeye başladın.
Nao wale wazee ishirini na wanne, waliokuwa wameketi mbele za Mungu, kwenye viti vyao vya enzi, wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu,
wakisema: “Tunakushukuru, Bwana Mungu Mwenyezi, uliyeko na uliyekuwako, kwa kuwa umetwaa uweza wako mkuu na ukaanza kutawala.
18 Uluslar gazaba gelmişlerdi. Şimdiyse senin gazabın üzerlerine geldi. Ölüleri yargılamak, Kulların olan peygamberleri, kutsalları, Küçük olsun büyük olsun, Senin adından korkanları ödüllendirmek Ve yeryüzünü mahvedenleri mahvetmek zamanı da geldi.”
Mataifa walikasirika nao wakati wa ghadhabu yako umewadia. Wakati umewadia wa kuwahukumu waliokufa na kuwapa thawabu watumishi wako manabii na watakatifu wako pamoja na wale wote wanaoliheshimu Jina lako, wakubwa kwa wadogo: na kuwaangamiza wale wanaoiangamiza dunia.”
19 Ardından Tanrı'nın gökteki tapınağı açıldı, tapınakta O'nun Antlaşma Sandığı göründü. O anda şimşekler çaktı, uğultular, gök gürlemeleri işitildi. Yer sarsıldı, şiddetli bir dolu fırtınası koptu.
Ndipo hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana humo ndani. Kukatokea mianga ya umeme wa radi, ngurumo, sauti za radi, tetemeko la nchi na mvua kubwa ya mawe.

< Vahiy 11 >