< Mezmurlar 2 >
1 Nedir uluslar arasındaki bu kargaşa, Neden boş düzenler kurar bu halklar?
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2 Dünyanın kralları saf bağlıyor, Hükümdarlar birleşiyor RAB'be ve meshettiği krala karşı.
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 “Koparalım onların kayışlarını” diyorlar, “Atalım üzerimizden bağlarını.”
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4 Göklerde oturan Rab gülüyor, Onlarla eğleniyor.
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5 Sonra öfkeyle uyarıyor onları, Gazabıyla dehşete düşürüyor
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6 Ve, “Ben kralımı Kutsal dağım Siyon'a oturttum” diyor.
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 RAB'bin bildirisini ilan edeceğim: Bana, “Sen benim oğlumsun” dedi, “Bugün ben sana baba oldum.
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
8 Dile benden, miras olarak sana ulusları, Mülk olarak yeryüzünün dört bucağını vereyim.
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
9 Demir çomakla kıracaksın onları, Çömlek gibi parçalayacaksın.”
Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
10 Ey krallar, akıllı olun! Ey dünya önderleri, ders alın!
Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
11 RAB'be korkuyla hizmet edin, Titreyerek sevinin.
Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
12 Oğulu öpün ki öfkelenmesin, Yoksa izlediğiniz yolda mahvolursunuz. Çünkü öfkesi bir anda alevleniverir. Ne mutlu O'na sığınanlara!
Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.