< Mezmurlar 18 >
1 Müzik şefi için - RAB'bin kulu Davut'un mezmuru - RAB kendisini bütün düşmanlarının pençesinden ve Saul'un elinden kurtardığı gün Davut RAB'be şu ezgiyi okudu: Seni seviyorum, gücüm sensin, ya RAB!
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi: Nakupenda wewe, Ee Bwana, nguvu yangu.
2 RAB benim kayam, sığınağım, kurtarıcımdır, Tanrım, kayam, sığınacak yerimdir, Kalkanım, güçlü kurtarıcım, korunağımdır!
Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.
3 Övgüye değer RAB'be seslenir, Kurtulurum düşmanlarımdan.
Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
4 Ölüm iplerine dolanmıştım, Yıkım selleri basmıştı beni,
Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
5 Ölüler diyarının bağları sarmıştı, Ölüm tuzakları çıkmıştı karşıma. (Sheol )
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
6 Sıkıntı içinde RAB'be yakardım, Yardıma çağırdım Tanrım'ı. Tapınağından sesimi duydu, Haykırışım kulaklarına ulaştı.
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.
7 O zaman yeryüzü sarsılıp sallandı, Titreyip sarsıldı dağların temelleri, Çünkü RAB öfkelenmişti.
Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
8 Burnundan duman yükseldi, Ağzından kavurucu ateş Ve korlar fışkırdı.
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
9 Kara buluta basarak Gökleri yarıp indi.
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
10 Bir Keruv'a binip uçtu, Rüzgar kanatlar takarak hızla geldi.
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
11 Karanlığı örtündü, Kara bulutları kendine çardak yaptı.
Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
12 Varlığının parıltısından, Bulutlardan dolu ve korlar savruluyordu.
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
13 RAB göklerden gürledi, Duyurdu sesini Yüceler Yücesi, Dolu ve alevli korlarla.
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
14 Savurup oklarını düşmanlarını dağıttı, Şimşek çaktırarak onları şaşkına çevirdi.
Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.
15 Denizin dibi göründü, Yeryüzünün temelleri açığa çıktı, ya RAB, Senin azarlamandan, Burnundan çıkan güçlü soluktan.
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.
16 RAB yukarıdan elini uzatıp tuttu, Çıkardı beni derin sulardan.
Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
17 Beni zorlu düşmanımdan, Benden nefret edenlerden kurtardı, Çünkü onlar benden güçlüydü.
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
18 Felaket günümde karşıma dikildiler, Ama RAB bana destek oldu.
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
19 Beni huzura kavuşturdu, Kurtardı, çünkü benden hoşnut kaldı.
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
20 RAB doğruluğumun karşılığını verdi, Beni temiz ellerime göre ödüllendirdi.
Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
21 Çünkü RAB'bin yolunda yürüdüm, Tanrım'dan uzaklaşarak kötülük yapmadım.
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
22 O'nun bütün ilkelerini göz önünde tuttum, Kurallarından ayrılmadım.
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
23 O'nun gözünde kusursuzdum, Suç işlemekten sakındım.
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
24 Bu yüzden RAB beni doğruluğuma Ve gözünde pak olan ellerime göre ödüllendirdi.
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.
25 Sadık kuluna sadakat gösterir, Kusursuz olana kusursuz davranırsın.
Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.
26 Pak olanla pak olur, Eğriye eğri davranırsın.
Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.
27 Alçakgönüllüleri kurtarır, Gururluların başını eğersin.
Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.
28 Işığımın kaynağı sensin, ya RAB, Tanrım! Karanlığımı aydınlatırsın.
Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka; Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.
29 Desteğinle akıncılara saldırır, Seninle surları aşarım, Tanrım.
Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
30 Tanrı'nın yolu kusursuzdur, RAB'bin sözü arıdır. O kendisine sığınan herkesin kalkanıdır.
Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu, neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
31 Var mı RAB'den başka tanrı? Tanrımız'dan başka kaya var mı?
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
32 Tanrı beni güçle donatır, Yolumu kusursuz kılar.
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
33 Ayaklar verdi bana, geyiklerinki gibi, Doruklarda tutar beni.
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
34 Bana savaşmayı öğretti, Kollarımla tunç bir yayı gereyim diye.
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
35 Bana zafer kalkanını bağışlarsın, Sağ elin destekler, Alçakgönüllülüğün yüceltir beni.
Hunipa ngao yako ya ushindi, nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, unajishusha chini ili kuniinua.
36 Bastığım yerleri genişletirsin, Burkulmaz bileklerim.
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
37 Kovalayıp yetiştim düşmanlarıma, Hepsi yok olmadan geri dönmedim.
Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
38 Ezdim onları, kalkamaz oldular, Ayaklarımın altına serildiler.
Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
39 Savaş için beni güçle donattın, Bana başkaldıranları önümde yere serdin.
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
40 Düşmanlarımı kaçmak zorunda bıraktın, Benden nefret edenleri yok ettim.
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
41 Feryat ettiler, ama kurtaran çıkmadı; RAB'bi çağırdılar, ama O yanıt vermedi.
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
42 Ezdim onları, rüzgarın savurduğu toza döndüler, Sokak çamuru gibi savurup attım.
Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
43 Halkımın çekişmelerinden beni kurtardın, Ulusların önderi yaptın, Tanımadığım halklar bana kulluk ediyor.
Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
44 Duyar duymaz sözümü dinlediler, Yabancılar bana yaltaklandılar.
Mara wanisikiapo hunitii, wageni hunyenyekea mbele yangu.
45 Yabancıların betleri benizleri attı, Titreyerek çıktılar kalelerinden.
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
46 RAB yaşıyor! Kayam'a övgüler olsun! Yücelsin kurtarıcım Tanrı!
Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!
47 O'dur öcümü alan, Halkları bana bağımlı kılan.
Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, awatiishaye mataifa chini yangu,
48 Düşmanlarımdan kurtarır, Başkaldıranlardan üstün kılar beni, Zorbaların elinden alır.
aniokoaye na adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
49 Bunun için uluslar arasında sana şükredeceğim, ya RAB, Adını ilahilerle öveceğim.
Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana; nitaliimbia sifa jina lako.
50 RAB kralını büyük zaferlere ulaştırır, Meshettiği krala, Davut'a ve soyuna Sonsuza dek sevgi gösterir.
Humpa mfalme wake ushindi mkuu, huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.