< Süleyman'In Özdeyişleri 28 >
1 Kötü kişi kendisini kovalayan olmasa bile kaçar, Doğrularsa genç aslan gibi yüreklidir.
Mtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza, bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
2 Ayaklanan ülke çok başlı olur, Ama akıllı, bilgili kişi düzeni sağlar.
Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi, bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.
3 Yoksulu ezen yoksul, Ürünü harap eden sağanak yağmur gibidir.
Mtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.
4 Yasayı terk eden kötüyü över, Yerine getirense kötüye karşı çıkar.
Wale waiachao sheria huwasifu waovu, bali wale waishikao sheria huwapinga.
5 Kötüler adaletten anlamaz, RAB'be yönelenlerse her yönüyle anlar.
Watu wabaya hawaelewi haki, bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.
6 Dürüst bir yoksul olmak, Yolsuzlukla zengin olmaktan yeğdir.
Afadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.
7 Kutsal Yasa'yı yerine getiren çocuk akıllıdır, Oburlarla arkadaşlık edense babasını utandırır.
Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali rafiki wa walafi humwaibisha baba yake.
8 Faiz ve tefecilikle malına mal katan kişi, Bunu yoksullara acıyan için biriktirir.
Yeye aongezaye utajiri wake kwa riba kubwa mno hukusanya kwa ajili ya mwingine, ambaye atawahurumia maskini.
9 Yasaya kulağını tıkayanın Duası da iğrençtir.
Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
10 Dürüst kişileri kötü yola saptıran Kendi kazdığı çukura düşer. İyiliği, özü sözü bir olanlar miras alacak.
Yeye ambaye humwongoza mwenye haki kwenye mapito mabaya, ataanguka kwenye mtego wake mwenyewe, bali wasio na lawama watapokea urithi mwema.
11 Zengin kendini bilge sanır, Ama akıllı yoksul onun içini okur.
Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua.
12 Doğruların zaferi coşkuyla kutlanır, Ama kötüler egemen olunca insan kaçacak yer arar.
Mwenye haki ashindapo, kuna furaha kubwa, bali waovu watawalapo, watu hujificha.
13 Günahlarını gizleyen başarılı olmaz, İtiraf edip bırakansa merhamet bulur.
Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema.
14 Günahtan çekinen ne mutludur! İnatçılık edense belaya düşer.
Amebarikiwa mtu ambaye siku zote humcha Bwana, bali yeye afanyaye moyo wake kuwa mgumu huangukia kwenye taabu.
15 Yoksul halkı yöneten kötü kişi Kükreyen aslan, saldırgan ayı gibidir.
Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge.
16 Gaddar önderin aklı kıttır; Haksız kazançtan nefret edense uzun ömürlü olur.
Mtawala dhalimu hana akili, bali yeye achukiaye mapato ya udhalimu atafurahia maisha marefu.
17 Adam öldürmekten vicdan azabı çeken, mezara dek kaçacaktır; Kimse ona yardım etmesin.
Mtu mwenye kusumbuliwa na hatia ya kuua atakuwa mtoro mpaka kufa; mtu yeyote na asimsaidie.
18 Alnı ak yaşayan kurtulur, Yolsuzluk yapan ansızın yıkıma uğrar.
Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama hulindwa salama, bali yeye ambaye njia zake ni potovu ataanguka ghafula.
19 Toprağını işleyenin ekmeği bol olur, Hayal peşinde koşansa yoksulluğa doyar.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.
20 Güvenilir kişi bolluğa erer, Zengin olmaya can atansa beladan kurtulamaz.
Mtu mwaminifu atabarikiwa sana, bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka hataacha kuadhibiwa.
21 Hatır gözetmek iyi değildir, Çünkü insan bir lokma ekmek için bile suç işler.
Kuonyesha upendeleo si vizuri, hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate.
22 Cimri servet peşinde koşar, Yoksulluğa uğrayacağını düşünmez.
Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri, naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.
23 Başkasını azarlayan sonunda Pohpohlayandan daha çok beğeni kazanır.
Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi, kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili.
24 Annesini ya da babasını soymayı günah saymayan, Haydutla birdir.
Yeye amwibiaye babaye au mamaye na kusema, “Si kosa,” yeye ni mwenzi wa yule aharibuye.
25 Açgözlü kavga çıkarır, RAB'be güvenense bolluk içinde yaşar.
Mtu mwenye tamaa huchochea fitina, bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa.
26 Kendine güvenen akılsızdır, Bilgece davranan güvenlikte olur.
Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu, bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama.
27 Yoksula verenin eksiği olmaz, Yoksulu görmezden gelense bir sürü lanete uğrar.
Yeye ampaye maskini hatapungukiwa na kitu chochote, bali yeye awafumbiaye maskini macho hupata laana nyingi.
28 Kötüler egemen olunca insan kaçacak yer arar, Ama kötüler yok olunca doğrular çoğalır.
Wakati waovu watawalapo, watu huenda mafichoni, bali waovu wanapoangamia, wenye haki hufanikiwa.