< Süleyman'In Özdeyişleri 14 >
1 Bilge kadın evini yapar, Ahmak kadın evini kendi eliyle yıkar.
Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 Doğru yolda yürüyen, RAB'den korkar, Yoldan sapan, RAB'bi hor görür.
Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
3 Ahmağın sözleri sırtına kötektir, Ama bilgenin dudakları kendisini korur.
Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
4 Öküz yoksa yemlik boş kalır, Çünkü bol ürünü sağlayan öküzün gücüdür.
Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
5 Güvenilir tanık yalan söylemez, Yalancı tanıksa yalan solur.
Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
6 Alaycı bilgeliği arasa da bulamaz, Akıllı içinse bilgi edinmek kolaydır.
Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
7 Akılsız kişiden uzak dur, Çünkü sana öğretecek bir şeyi yok.
Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
8 İhtiyatlı kişinin bilgeliği, ne yapacağını bilmektir, Akılsızların ahmaklığıysa aldanmaktır.
Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
9 Ahmaklar suç sunusuyla alay eder, Dürüstler ise iyi niyetlidir.
Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
10 Yürek kendi acısını bilir, Sevinciniyse kimse paylaşmaz.
Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
11 Kötü kişinin evi yerle bir edilecek, Doğru kişinin konutuysa bayındır olacak.
Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
12 Öyle yol var ki, insana düz gibi görünür, Ama sonu ölümdür.
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
13 Gülerken bile yürek sızlayabilir, Sevinç bitince acı yine görünebilir.
Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
14 Yüreği dönek olan tuttuğu yolun, İyi kişi de yaptıklarının ödülünü alacaktır.
Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
15 Saf kişi her söze inanır, İhtiyatlı olansa attığı her adımı hesaplar.
Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
16 Bilge kişi korktuğu için kötülükten uzaklaşır, Akılsızsa büyüklük taslayıp kendine güvenir.
Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
17 Çabuk öfkelenen ahmakça davranır, Düzenbazdan herkes nefret eder.
Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
18 Saf kişilerin mirası akılsızlıktır, İhtiyatlı kişilerin tacı ise bilgidir.
Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
19 Alçaklar iyilerin önünde, Kötüler doğruların kapısında eğilirler.
Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
20 Komşusu bile yoksulu sevmez, Oysa zenginin dostu çoktur.
Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
21 Komşuyu hor görmek günahtır, Ne mutlu mazluma lütfedene!
Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
22 Kötülük tasarlayan yolunu şaşırmaz mı? Oysa iyilik tasarlayan sevgi ve sadakat kazanır.
Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
23 Her emek kazanç getirir, Ama boş lakırdı yoksulluğa götürür.
Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
24 Bilgelerin tacı servetleridir, Akılsızlarsa ahmaklıklarıyla tanınır.
Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
25 Dürüst tanık can kurtarır, Yalancı tanık aldatıcıdır.
Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
26 RAB'den korkan tam güvenliktedir, RAB onun çocuklarına da sığınak olacaktır.
Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
27 RAB korkusu yaşam kaynağıdır, İnsanı ölüm tuzaklarından uzaklaştırır.
Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
28 Kralın yüceliği halkının çokluğuna bağlıdır, Halk yok olursa hükümdar da mahvolur.
Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
29 Geç öfkelenen akıllıdır, Çabuk sinirlenen ahmaklığını gösterir.
Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
30 Huzurlu yürek bedenin yaşam kaynağıdır, Hırs ise insanı için için yer bitirir.
Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
31 Muhtacı ezen, Yaradanı'nı hor görüyor demektir. Yoksula acıyansa Yaradan'ı yüceltir.
Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
32 Kötü kişi uğradığı felaketle yıkılır, Doğru insanın ölümde bile sığınacak yeri var.
Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
33 Bilgelik akıllı kişinin yüreğinde barınır, Akılsızlar arasında bile kendini belli eder.
Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
34 Doğruluk bir ulusu yüceltir, Oysa günah herhangi bir halk için utançtır.
Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
35 Kral sağduyulu kulunu beğenir, Utanç getirene öfkelenir.
Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.