< Çölde Sayim 21 >
1 Negev'de yaşayan Kenanlı Arat Kralı, İsrailliler'in Atarim yolundan geldiğini duyunca, onlara saldırarak bazılarını tutsak aldı.
Mfalme wa Kikanaani wa Aradi aliyeishi huko Negebu aliposikia kwamba Waisraeli walikuwa wanakuja kwa njia ya Atharimu, aliwashambulia Waisraeli na kuwateka baadhi yao.
2 Bunun üzerine İsrailliler, “Eğer bu halkı tümüyle elimize teslim edersen, kentlerini büsbütün yok edeceğiz” diyerek RAB'be adak adadılar.
Ndipo Israeli akaweka nadhiri hii kwa Bwana: “Ikiwa utawatia watu hawa mikononi mwetu, tutaiangamiza kabisa miji yao.”
3 RAB İsrailliler'in yalvarışını işitti ve Kenanlılar'ı ellerine teslim etti. İsrailliler onları da kentlerini de büsbütün yok ettiler. Oraya Horma adı verildi.
Bwana akasikiliza ombi la Waisraeli, naye akawapa ushindi juu ya Wakanaani. Wakawaangamiza kabisa na miji yao; hivyo mahali pale pakaitwa Horma.
4 Edom ülkesinin çevresinden geçmek için Kamış Denizi yoluyla Hor Dağı'ndan ayrıldılar. Ama yolda halk sabırsızlandı.
Waisraeli wakasafiri kutoka mlima Hori kupitia njia inayoelekea Bahari ya Shamu, kuizunguka Edomu. Lakini watu wakakosa uvumilivu njiani,
5 Tanrı'dan ve Musa'dan yakınarak, “Çölde ölelim diye mi bizi Mısır'dan çıkardınız?” dediler, “Burada ne ekmek var, ne de su. Ayrıca bu iğrenç yiyecekten de tiksiniyoruz!”
wakamnungʼunikia Mungu na Mose, wakisema, “Kwa nini umetupandisha kutoka Misri ili tufe jangwani? Hakuna mkate! Hakuna maji! Nasi tunachukia sana chakula hiki duni!”
6 Bunun üzerine RAB halkın arasına zehirli yılanlar gönderdi. Yılanlar ısırınca İsrailliler'den birçok kişi öldü.
Ndipo Bwana akapeleka nyoka wenye sumu katikati yao; wakawauma watu, nao Waisraeli wengi wakafa.
7 Halk Musa'ya gelip, “RAB'den ve senden yakınmakla günah işledik. Yalvar da, RAB aramızdan yılanları kaldırsın” dedi. Bunun üzerine Musa halk için yalvardı.
Watu wakamjia Mose na kusema, “Tumetenda dhambi wakati tuliponena dhidi ya Bwana na dhidi yako. Mwombe Bwana ili atuondolee hawa nyoka.” Hivyo Mose akawaombea hao watu.
8 RAB Musa'ya, “Bir yılan yap ve onu bir direğin üzerine koy. Isırılan herkes ona bakınca yaşayacaktır” dedi.
Bwana akamwambia Mose, “Tengeneza nyoka wa shaba na umweke juu ya mti; yeyote aliyeumwa na nyoka anaweza kumtazama na akaishi tena.”
9 Böylece Musa tunç bir yılan yaparak direğin üzerine koydu. Yılan tarafından ısırılan kişiler tunç yılana bakınca yaşadı.
Kwa hiyo Mose akatengeneza nyoka wa shaba na kumweka juu ya mti. Kisha wakati mtu yeyote aliumwa na nyoka, naye akamtazama yule nyoka wa shaba, aliishi.
10 İsrail halkı yola koyulup Ovot'ta konakladı.
Waisraeli waliendelea na safari yao na wakapiga kambi huko Obothi.
11 Sonra Ovot'tan ayrılıp doğuda Moav'a bakan çölde, İye– Haavarim'de konakladı.
Kisha wakaondoka Obothi na kupiga kambi huko Iye-Abarimu, katika jangwa linalotazamana na Moabu kuelekea mawio ya jua.
12 Oradan da ayrılıp Zeret Vadisi'nde konakladı.
Kutoka hapo waliendelea mbele wakapiga kambi kwenye Bonde la Zeredi.
13 Oradan da ayrılıp Amorlular'ın sınırına dek uzanan çölde, Arnon Vadisi'nin karşı yakasında konakladılar. Arnon Moav'la Amorlular'ın ülkesi arasındaki Moav sınırıdır.
Wakasafiri kutoka hapo na kupiga kambi kando ya Mto Arnoni, ambao uko katika jangwa lililoenea hadi nchi ya Waamori. Arnoni ni mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori.
14 RAB'bin Savaşları Kitabı'nda şöyle yazılıdır: “... Sufa topraklarında Vahev Kenti, vadiler, Arnon Vadisi,
Ndiyo sababu Kitabu cha Vita vya Bwana kinasema: “…Mji wa Wahebu nchini Seifa na mabonde ya Arnoni,
15 Ar Kenti'ne dayanan ve Moav sınırı boyunca uzanan vadilerin yamaçları ...”
na miteremko ya mabonde inayofika hadi mji wa Ari na huelekea mpakani mwa Moabu.”
16 Oradan RAB'bin Musa'ya, “Halkı bir araya topla, onlara su vereceğim” dediği kuyuya, Beer'e doğru yol aldılar.
Kutoka hapo waliendelea mbele hadi kisima cha Beeri; kwenye kisima ambacho Bwana alimwambia Mose, “Wakusanye watu pamoja, nami nitawapa maji.”
17 O zaman İsrailliler şu ezgiyi söylediler: “Suların fışkırsın, ey kuyu! Ezgi okuyun ona.
Kisha Israeli akaimba wimbo huu: “Bubujika, ee kisima! Imba kuhusu maji,
18 O kuyu ki, onu önderlerle Halkın soyluları Asayla, değnekle kazdılar.” Bundan sonra çölden Mattana'ya,
kuhusu kisima ambacho kilichimbwa na wakuu, ambacho watu mashuhuri walikifukua, watu mashuhuri wakiwa na fimbo za utawala na bakora.” Kisha wakatoka jangwani kwenda Matana,
19 Mattana'dan Nahaliel'e, Nahaliel'den Bamot'a,
kutoka Matana wakafika Nahalieli, kutoka Nahalieli wakafika Bamothi,
20 Bamot'tan Moav topraklarındaki vadiye, çöle bakan Pisga Dağı'nın eteklerine gittiler.
na kutoka Bamothi wakafika kwenye bonde lililoko Moabu, mahali ambapo kilele cha Pisga kinatazamana na nyika.
21 İsrailliler Amorlular'ın Kralı Sihon'a ulaklarla şu haberi gönderdi:
Israeli akawatuma wajumbe kumwambia Sihoni mfalme wa Waamori:
22 “İzin ver, ülkenden geçelim. Tarlalardan, bağlardan geçmeyeceğiz, hiçbir kuyudan su içmeyeceğiz. Sınırından geçinceye dek, Kral yolundan yolumuza devam edeceğiz.”
“Uturuhusu tupite katika nchi yako. Hatutageuka kando kwenda katika mashamba au mashamba ya mizabibu, ama kunywa maji kutoka kisima chochote. Tutasafiri kwenye njia kuu ya mfalme hata tutakapokuwa tumekwisha kupita katika nchi yako.”
23 Ne var ki Sihon, ülkesinden İsrailliler'in geçmesine izin vermedi. İsrailliler'le savaşmak üzere bütün halkını toplayıp çöle çıktı. Yahesa'ya varınca, İsrailliler'e saldırdı.
Lakini Sihoni hakumruhusu Israeli apite katika nchi yake. Alilikutanisha jeshi lake lote, wakaondoka kwenda jangwani ili kupigana na Israeli. Alipofika huko Yahazi, akapigana na Israeli.
24 İsrailliler onu kılıçtan geçirip Arnon'dan Yabbuk'a, Ammonlular'ın sınırına dek uzanan topraklarını aldılar. Az Kenti Ammon sınırını oluşturuyordu.
Hata hivyo, Israeli alimshinda kwa upanga na kuiteka ardhi yake kutoka Arnoni mpaka Yaboki, lakini ni hadi kufikia nchi ya Waamoni tu, kwa sababu mipaka yake ilikuwa imezungushwa ukuta.
25 İsrailliler Heşbon ve çevresindeki köylerle birlikte Amorlular'ın bütün kentlerini ele geçirerek orada yaşamaya başladılar.
Israeli akaiteka miji yote ya Waamori na kuikalia, pamoja na Heshboni na makazi yote yanayoizunguka.
26 Heşbon Amorlular'ın Kralı Sihon'un kentiydi. Sihon eski Moav Kralı'na karşı savaşmış, Arnon'a dek uzanan topraklarını elinden almıştı.
Heshboni ulikuwa mji wa Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alikuwa amepigana dhidi ya mfalme wa Moabu aliyetangulia na akawa amechukua ardhi yake yote mpaka Arnoni.
27 Bunun için ozanlar şöyle diyor: “Heşbon'a gelin, Sihon'un kenti yeniden kurulsun Ve sağlamlaştırılsın.
Ndiyo sababu watunga mashairi husema: “Njoo Heshboni na ujengwe tena; mji wa Sihoni na ufanywe upya.
28 Heşbon'dan ateş, Sihon'un kentinden alev çıktı; Moav'ın Ar Kenti'ni, Arnon tepelerinin efendilerini yakıp yok etti.
“Moto uliwaka kutoka Heshboni, mwali wa moto kutoka mji wa Sihoni. Uliteketeza Ari ya Moabu, raiya wa mahali pa Arnoni palipoinuka.
29 Vay sana, ey Moav! İlah Kemoş'un halkı, yok oldun! Kemoş senin oğullarının Amorlular'ın Kralı Sihon'a kaçmasını, Kızlarının ona tutsak olmasını önleyemedi.
Ole wako, ee Moabu! Umeharibiwa, enyi watu wa Kemoshi! Amewatoa wanawe kuwa wakimbizi, na binti zake kama mateka kwa Mfalme Sihoni wa Waamori.
30 Onları bozguna uğrattık; Heşbon Divon'a dek yıkıma uğradı. Medeva'ya uzanan Nofah'a dek onları yıkıma uğrattık.”
“Lakini tumewashinda; Heshboni umeharibiwa hadi Diboni. Tumebomoa hadi kufikia Nofa, ulioenea hadi Medeba.”
31 Böylece İsrail halkı Amorlular'ın ülkesinde yaşamaya başladı.
Kwa hiyo Israeli akaishi katika nchi ya Waamori.
32 Musa Yazer'i araştırmak için adamlar gönderdi. Sonra İsrailliler Yazer çevresindeki köyleri ele geçirerek orada yaşayan Ammonlular'ı kovdular.
Baada ya Mose kutuma wapelelezi kwenda mji wa Yazeri, Waisraeli waliteka viunga vya mji huo na kuwafukuza Waamori waliokuwa wanaishi huko.
33 Bundan sonra dönüp Başan'a doğru ilerlediler. Başan Kralı Og'la ordusu onlarla savaşmak için Edrei'de karşılarına çıktı.
Kisha wakageuka na kwenda katika njia inayoelekea Bashani, naye Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote wakatoka kupigana nao huko Edrei.
34 RAB Musa'ya, “Ondan korkma!” dedi, “Çünkü onu da ordusuyla ülkesini de senin eline teslim ettim. Amorlular'ın Heşbon'da yaşayan Kralı Sihon'a yaptığının aynısını ona da yapacaksın.”
Bwana akamwambia Mose, “Usimwogope Ogu, kwa sababu nimeshamkabidhi mikononi mwako, pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Mtendee kama ulivyomtendea Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
35 Böylece İsrail halkı kimseyi sağ bırakmadan Og'la oğullarını ve ordusunu yok etti, ülkeyi ele geçirdi.
Kwa hiyo wakamuua, pamoja na wanawe na jeshi lake lote, bila ya kumwacha hata mtu mmoja hai. Nao wakaimiliki nchi yake.