< Çölde Sayim 19 >

1 RAB Musa'yla Harun'a şöyle dedi:
Bwana akamwambia Mose na Aroni:
2 “RAB'bin buyurduğu yasanın kuralı şudur: İsrailliler'e size kusursuz, özürsüz, boyunduruk takmamış kızıl bir inek getirmelerini söyleyin.
“Hivi ndivyo sheria ambayo Bwana ameagiza itakavyo: Waambie Waisraeli wakuletee mtamba mwekundu asiye na dosari wala waa, na ambaye hajapata kufungwa nira.
3 İnek Kâhin Elazar'a verilsin; ordugahın dışına çıkarılıp onun önünde kesilecek.
Mpeni kuhani Eleazari huyo mtamba; naye atatolewa nje ya kambi na kuchinjwa mbele yake huyo kuhani.
4 Kâhin Elazar parmağıyla kanından alıp yedi kez Buluşma Çadırı'nın önüne doğru serpecek.
Kisha kuhani Eleazari atachukua baadhi ya damu yake kwenye kidole chake na kuinyunyiza mara saba kuelekea upande wa mbele ya Hema la Kukutania.
5 Sonra Elazar'ın gözü önünde inek, derisi, eti, kanı ve gübresiyle birlikte yakılacak.
Wakati angali akitazama, mtamba huyo atateketezwa: ngozi yake, nyama yake, damu na sehemu zake za ndani.
6 Kâhin biraz sedir ağacı, mercanköşkotu ve kırmızı iplik alıp yanmakta olan ineğin üzerine atacak.
Kuhani atachukua kuni za mti wa mwerezi, hisopo na sufu nyekundu, na kuvitupa kwenye huyo mtamba anayeungua.
7 Sonra giysilerini yıkayacak, yıkanacak. Ancak o zaman ordugaha girebilir. Ama akşama dek kirli sayılacaktır.
Baada ya hayo, kuhani lazima afue nguo zake, na aoge mwili wake kwa maji. Kisha anaweza kurudi kambini, lakini atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada mpaka jioni.
8 İneği yakan kişi de giysilerini yıkayacak, yıkanacak. O da akşama dek kirli sayılacak.
Mtu amchomaye huyo mtamba lazima naye pia afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye pia atakuwa najisi mpaka jioni.
9 “Temiz sayılan bir kişi ineğin külünü toplayıp ordugahın dışında temiz sayılan bir yere koyacak. İsrail topluluğu temizlenme suyu için bu külü saklayacak; bu, günahtan arınmak içindir.
“Mtu ambaye ni safi atakusanya majivu ya mtamba huyo na kuyaweka mahali ambapo ni safi nje ya kambi kwa taratibu za kiibada. Yatahifadhiwa na jumuiya ya Kiisraeli kwa matumizi katika maji ya utakaso; ni kwa ajili ya kutakasa kutoka dhambini.
10 İneğin külünü toplayan adam giysilerini yıkayacak, akşama dek kirli sayılacak. Bu kural hem İsrailliler, hem de aralarında yaşayan yabancılar için kalıcı olacaktır.
Mtu akusanyaye majivu ya huyo mtamba ni lazima pia afue nguo zake, kadhalika naye pia atakuwa najisi hadi jioni. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa Waisraeli na kwa wageni wanaoishi miongoni mwao.
11 “Herhangi bir insan ölüsüne dokunan kişi yedi gün kirli sayılacaktır.
“Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote atakuwa najisi kwa siku saba.
12 Üçüncü ve yedinci gün temizlenme suyuyla kendini arındıracak, böylece paklanmış olacak. Üçüncü ve yedinci gün kendini arındırmazsa, paklanmış sayılmayacak.
Ni lazima ajitakase mwenyewe kwa maji katika siku ya tatu na siku ya saba, ndipo atakuwa safi. Lakini kama hatajitakasa mwenyewe katika siku ya tatu na ya saba, hatakuwa safi.
13 Herhangi bir insan ölüsüne dokunup da kendini arındırmayan kişi RAB'bin Konutu'nu kirletmiş olur. O kişi İsrail'den atılmalı. Temizlenme suyu üzerine dökülmediği için kirli sayılır, kirliliği üzerinde kalır.
Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote na kushindwa kujitakasa mwenyewe hunajisi Maskani ya Bwana. Mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na Israeli. Kwa sababu hajanyunyiziwa maji ya utakaso, yeye ni najisi; unajisi wake unabaki juu yake.
14 “Çadırda biri öldüğü zaman uygulanacak kural şudur: Çadıra giren ve çadırda bulunan herkes yedi gün kirli sayılacaktır.
“Hii ndiyo sheria itumikayo wakati mtu amekufa ndani ya hema: Yeyote aingiaye ndani ya hema hilo na yeyote aliye ndani yake watakuwa najisi kwa muda wa siku saba,
15 Kapağı iple bağlanmamış, ağzı açık her kap kirli sayılacaktır.
nacho kila chombo kisicho na kifuniko juu yake kitakuwa najisi.
16 “Kırda kılıçla öldürülmüş ya da doğal ölümle ölmüş birine, insan kemiğine ya da mezara her dokunan yedi gün kirli sayılacaktır.
“Mtu yeyote aliyeko nje mahali pa wazi agusaye mtu aliyeuawa kwa upanga au mtu aliyekufa kwa kifo cha kawaida, au mtu yeyote agusaye mfupa wa mtu aliyekufa au kaburi, atakuwa najisi kwa siku saba.
17 “Kirli sayılan kişi için bir kabın içine yakılan günah sunusunun külünden koyun, üstüne duru su dökeceksiniz.
“Kwa mtu aliye najisi, weka majivu ya sadaka ya utakaso wa dhambi ndani ya chombo, umimine maji safi juu yao.
18 Temiz sayılan bir adam mercanköşkotunu alıp suya batıracak. Sonra çadırın, bütün eşyaların ve orada bulunanların üzerine serpecek. Kemiğe, öldürülmüş ya da doğal ölümle ölmüş kişiye ya da mezara dokunanın üzerine de suyu serpecek.
Kisha mtu aliye safi kwa kawaida za kiibada atachukua hisopo, achovye ndani ya maji, na kunyunyizia hema na vifaa vyote pamoja na watu ambao walikuwamo. Pia ni lazima amnyunyizie mtu yeyote ambaye amegusa mfupa wa mtu aliyekufa, au kaburi, au mtu ambaye ameuawa, au mtu ambaye amekufa kifo cha kawaida.
19 Temiz sayılan adam, üçüncü ve yedinci gün kirli sayılanın üzerine suyu serpecek. Yedinci gün onu arındıracak. Arınan kişi giysilerini yıkayacak, yıkanacak ve akşam temiz sayılacak.
Mtu ambaye ni safi ndiye atakayemnyunyizia yeyote ambaye ni najisi siku ya tatu na siku ya saba, na katika siku ya saba atamtakasa mtu huyo. Mtu ambaye ametakaswa lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, na jioni ile atakuwa safi.
20 Ancak, kirli sayılan biri kendini arındırmazsa topluluğun arasından atılmalı. Çünkü RAB'bin Tapınağı'nı kirletmiştir. Temizlenme suyu üzerine dökülmediği için kirli sayılır.
Lakini ikiwa mtu ambaye ni najisi hakujitakasa mwenyewe, ni lazima akatiliwe mbali na jumuiya, kwa sababu ameinajisi Maskani ya Bwana. Maji ya utakaso hayajanyunyizwa juu yake, naye ni najisi.
21 Onlar için bu kural kalıcı olacaktır. Temizlenme suyunu serpen kişi de giysisini yıkamalı. Temizlenme suyuna dokunan kişi akşama dek kirli sayılacak.
Hii ni sheria ya kudumu kwao. “Mtu yeyote ambaye ananyunyiza yale maji ya utakaso lazima pia afue nguo zake, na yeyote ambaye hugusa maji ya utakaso atakuwa najisi mpaka jioni.
22 Kirli sayılan birinin dokunduğu nesne kirli sayılır; o nesneye dokunan da akşama dek kirli sayılır.”
Kitu chochote anachogusa mtu aliye najisi kitakuwa najisi, na yeyote akigusaye huwa najisi mpaka jioni.”

< Çölde Sayim 19 >