< Çölde Sayim 10 >

1 RAB Musa'ya şöyle dedi:
Bwana akamwambia Mose:
2 “Dövme gümüşten iki borazan yapacaksın; bunları topluluğu çağırmak ve halkın yola çıkması için kullanacaksın.
“Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
3 İki borazan birden çalınınca, bütün topluluk senin yanında, Buluşma Çadırı'nın girişi önünde toplanacak.
Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
4 Yalnız biri çalınırsa, önderler, İsrail'in oymak başları senin yanında toplanacak.
Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
5 Borazan kısa çalınınca, doğuda konaklayanlar yola çıkacak.
Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
6 İkinci kez kısa çalınınca da güneyde konaklayanlar yola çıkacak. Borazanın kısa çalınması oymakların yola çıkması için bir işarettir.
Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
7 Topluluğu toplamak için de borazan çaldırt, ama kısa olmasın.
Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
8 “Borazanları kâhin olan Harunoğulları çalacak. Borazan çalınması sizler ve gelecek kuşaklar için kalıcı bir kural olacak.
“Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
9 Sizi sıkıştıran düşmana karşı ülkenizde savaşa çıktığınızda, borazan çalın. O zaman Tanrınız RAB sizi anımsayacak, sizi düşmanlarınızdan kurtaracak.
Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
10 Sevinçli olduğunuz günler –kutladığınız bayramlar ve Yeni Ay Törenleri'nde– yakmalık sunular ve esenlik kurbanları üzerine borazan çalacaksınız. Böylelikle Tanrınız'ın önünde anımsanmış olacaksınız. Ben Tanrınız RAB'bim.”
Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
11 İkinci yılın ikinci ayının yirminci günü bulut Levha Sandığı'nın bulunduğu konutun üzerinden kalktı.
Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
12 İsrailliler de Sina Çölü'nden göç etmeye başladılar. Bulut Paran Çölü'nde durdu.
Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
13 Bu, RAB'bin Musa aracılığıyla verdiği buyruk uyarınca ilk göç edişleriydi.
Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
14 Önce Yahuda sancağı bölükleriyle yola çıktı. Yahuda bölüğüne Amminadav oğlu Nahşon komuta ediyordu.
Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
15 İssakar oymağının bölüğüne Suar oğlu Netanel,
Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
16 Zevulun oymağının bölüğüne de Helon oğlu Eliav komuta ediyordu.
naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
17 Konut yere indirilince, onu taşıyan Gerşonoğulları'yla Merarioğulları yola koyuldular.
Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
18 Sonra Ruben sancağı bölükleriyle yola çıktı. Ruben bölüğüne Şedeur oğlu Elisur komuta ediyordu.
Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
19 Şimon oymağının bölüğüne Surişadday oğlu Şelumiel,
Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
20 Gad oymağının bölüğüne de Deuel oğlu Elyasaf komuta ediyordu.
naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
21 Kehatlılar kutsal eşyaları taşıyarak yola koyuldular. Bunlar varmadan konut kurulmuş olurdu.
Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
22 Efrayim sancağı bölükleriyle yola çıktı. Efrayim bölüğüne Ammihut oğlu Elişama komuta ediyordu.
Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
23 Manaşşe oymağının bölüğüne Pedahsur oğlu Gamliel,
Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
24 Benyamin oymağının bölüğüne de Gidoni oğlu Avidan komuta ediyordu.
naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
25 En sonunda Dan sancağı ordunun artçı kolu olan bölükleriyle yola çıktı. Dan bölüğüne Ammişadday oğlu Ahiezer komuta ediyordu.
Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
26 Aşer oymağının bölüğüne Okran oğlu Pagiel,
Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
27 Naftali oymağının bölüğüne de Enan oğlu Ahira komuta ediyordu.
naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
28 Yola koyulduklarında İsrailli bölüklerin yürüyüş düzeni böyleydi.
Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
29 Musa, kayınbabası Midyanlı Reuel oğlu Hovav'a, “RAB'bin, ‘Size vereceğim’ dediği yere gidiyoruz” dedi, “Bizimle gel, sana iyi davranırız. Çünkü RAB İsrail'e iyilik edeceğine söz verdi.”
Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
30 Hovav, “Gelmem” diye yanıtladı, “Ülkeme, akrabalarımın yanına döneceğim.”
Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
31 Musa, “Lütfen bizi bırakma” diye üsteledi, “Çünkü çölde konaklayacağımız yerleri sen biliyorsun. Sen bize göz olabilirsin.
Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
32 Bizimle gelirsen, RAB'bin yapacağı bütün iyilikleri seninle paylaşırız.”
Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
33 RAB'bin Dağı'ndan ayrılıp üç günlük yol aldılar. Konaklayacakları yeri bulmaları için RAB'bin Antlaşma Sandığı üç gün boyunca önleri sıra gitti.
Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
34 Konakladıkları yerden ayrıldıklarında da RAB'bin bulutu gündüzün onların üzerinde duruyordu.
Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
35 Sandık yola çıkınca Musa, “Ya RAB, kalk! Düşmanların dağılsın, Senden nefret edenler önünden kaçsın!” diyordu.
Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
36 Sandık konaklayınca da, “Ya RAB, binlerce, on binlerce İsrailli'ye dön!” diyordu.
Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”

< Çölde Sayim 10 >