< Çölde Sayim 1 >

1 İsrailliler'in Mısır'dan çıkışının ikinci yılı, ikinci ayın birinci günü RAB Sina Çölü'nde, Buluşma Çadırı'nda Musa'ya şöyle seslendi:
Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
2 “Sen ve Harun İsrail topluluğunun bütün boylarıyla ailelerinin sayımını yapın. Bütün erkekleri bir bir sayıp adlarını yazın. İsrailliler'den savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştaki bütün erkekleri sayıp bölüklere ayırın.
“Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
3
Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
4 Size yardım etmek için yanınızda her oymaktan birer adam bulunsun; bu kişiler aile başı olmalı.
Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
5 Size yardımcı olacak adamların adları şunlardır: “Ruben oymağından: Şedeur oğlu Elisur,
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
6 Şimon oymağından: Surişadday oğlu Şelumiel,
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
7 Yahuda oymağından: Amminadav oğlu Nahşon,
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 İssakar oymağından: Suar oğlu Netanel,
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
9 Zevulun oymağından: Helon oğlu Eliav,
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
10 Yusufoğulları'ndan Efrayim oymağından: Ammihut oğlu Elişama, Manaşşe oymağından: Pedahsur oğlu Gamliel,
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
11 Benyamin oymağından: Gidoni oğlu Avidan,
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
12 Dan oymağından: Ammişadday oğlu Ahiezer,
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13 Aşer oymağından: Okran oğlu Pagiel,
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
14 Gad oymağından: Deuel oğlu Elyasaf,
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
15 Naftali oymağından: Enan oğlu Ahira.”
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
16 Bunlar İsrail topluluğundan atanmış adamlardı; atalarının soyundan gelen oymak önderleri, İsrail'in boy başlarıydı.
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
17 Musa'yla Harun adları bildirilen bu adamları getirttiler.
Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
18 RAB'bin buyruğu uyarınca ikinci ayın birinci günü bütün halkı topladılar. Yirmi ve daha yukarı yaştakileri boylarına, ailelerine göre birer birer sayıp adlarını yazdılar. Böylece Musa Sina Çölü'nde halkın sayımını yaptı.
wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
20 İsrail'in ilk oğlu Ruben'in soyundan olanlar: Savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştaki bütün erkekler bağlı oldukları boy ve aileye göre adlarıyla birer birer kayda geçirildi.
Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
21 Ruben oymağından sayılanlar 46 500 kişiydi.
Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
22 Şimon'un soyundan olanlar: Savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştaki bütün erkekler bağlı oldukları boy ve aileye göre adlarıyla birer birer belirlenip kayda geçirildi.
Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
23 Şimon oymağından sayılanlar 59 300 kişiydi.
Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
24 Gad'ın soyundan olanlar: Savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştakiler bağlı oldukları boy ve aileye göre adlarıyla kayda geçirildi.
Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
25 Gad oymağından sayılanlar 45 650 kişiydi.
Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
26 Yahuda'nın soyundan olanlar: Savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştakiler bağlı oldukları boy ve aileye göre adlarıyla kayda geçirildi.
Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
27 Yahuda oymağından sayılanlar 74 600 kişiydi.
Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
28 İssakar'ın soyundan olanlar: Savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştakiler bağlı oldukları boy ve aileye göre adlarıyla kayda geçirildi.
Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
29 İssakar oymağından sayılanlar 54 400 kişiydi.
Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
30 Zevulun'un soyundan olanlar: Savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştakiler bağlı oldukları boy ve aileye göre adlarıyla kayda geçirildi.
Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
31 Zevulun oymağından sayılanlar 57 400 kişiydi.
Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
32 Yusufoğulları'ndan, Efrayim soyundan olanlar: Savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştakiler bağlı oldukları boy ve aileye göre adlarıyla kayda geçirildi.
Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
33 Efrayim oymağından sayılanlar 40 500 kişiydi.
Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
34 Manaşşe'nin soyundan olanlar: Savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştakiler bağlı oldukları boy ve aileye göre adlarıyla kayda geçirildi.
Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
35 Manaşşe oymağından sayılanlar 32 200 kişiydi.
Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
36 Benyamin'in soyundan olanlar: Savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştakiler bağlı oldukları boy ve aileye göre adlarıyla kayda geçirildi.
Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
37 Benyamin oymağından sayılanlar 35 400 kişiydi.
Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
38 Dan'ın soyundan olanlar: Savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştakiler bağlı oldukları boy ve aileye göre adlarıyla kayda geçirildi.
Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
39 Dan oymağından sayılanlar 62 700 kişiydi.
Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
40 Aşer'in soyundan olanlar: Savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştakiler bağlı oldukları boy ve aileye göre adlarıyla kayda geçirildi.
Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
41 Aşer oymağından sayılanlar 41 500 kişiydi.
Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
42 Naftali'nin soyundan olanlar: Savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştakiler bağlı oldukları boy ve aileye göre adlarıyla kayda geçirildi.
Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
43 Naftali oymağından sayılanlar 53 400 kişiydi.
Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
44 Musa, Harun ve İsrail'in on iki önderi tarafından sayılanlar bunlardı. Her önder bağlı olduğu aileyi temsil ediyordu.
Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
45 İsrail'de savaşabilecek durumda yirmi ve daha yukarı yaştakilerin tümü bağlı oldukları aileye göre sayıldılar.
Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
46 Sayılanların toplamı 603 550 kişiydi.
Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
47 Ne var ki, Levi oymağından olanlar öbürleriyle birlikte sayılmadı.
Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
48 Çünkü RAB Musa'ya şöyle demişti:
Bwana alikuwa amemwambia Mose:
49 “Ancak Levi oymağını sayma, öbür İsrailliler arasında yaptığın sayıma onları katma.
“Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
50 Levililer'i Levha Sandığı'nın bulunduğu konuttan, eşyalardan ve konuta ait her şeyden sorumlu kıl. Konutu ve bütün eşyalarını onlar taşısın; konutun bakımını onlar yapsın, çevresinde ordugah kursun.
Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
51 Konut taşınırken onu Levililer toplayacak; konaklanacağı zaman da onlar kuracak. Levililer dışında konuta yaklaşan ölüm cezasına çarptırılacak.
Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
52 İsrailliler çadırlarını bölükler halinde kuracaklar. Herkes kendi ordugahında, kendi sancağının altında bulunacak.
Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
53 Ancak İsrail topluluğunun gazabıma uğramaması için Levililer Levha Sandığı'nın bulunduğu konutun çevresinde konaklayacak ve konuta bekçilik edecekler.”
Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
54 İsrailliler bütün bunları tam tamına RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibi yaptılar.
Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

< Çölde Sayim 1 >