< Matta 9 >
1 İsa tekneye binip karşı kıyıya geçti ve kendi kentine gitti.
Yesu akaingia kwenye boti, akavuka na akafika kwenye mji alipokuwa anaishi.
2 Kendisine, yatak üzerinde felçli bir adam getirdiler. İsa onların imanını görünce felçliye, “Cesur ol, oğlum, günahların bağışlandı” dedi.
Tazama, wakamletea mtu aliyepooza amelazwa kwenye godoro. alipooiona imani yao, Yesu akamwambia mtu aliyepooza, “Mwanangu, uwe na furaha, Dhambi zako zimesamehewa”
3 Bunun üzerine bazı din bilginleri içlerinden, “Bu adam Tanrı'ya küfrediyor!” dediler.
Tazama, Baadhi ya walimu wa sheria wakasemezana wao kwa wao, “Huyu mtu anakufuru”
4 Onların ne düşündüklerini bilen İsa dedi ki, “Yüreğinizde neden kötü düşüncelere yer veriyorsunuz?
Yesu akatambua mawazo yao na kusema, “Kwa nini mnawaza maovu moyoni mwenu?
5 Hangisi daha kolay? ‘Günahların bağışlandı’ demek mi, yoksa ‘Kalk, yürü’ demek mi?
Kipi kilicho rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema, 'Simama na utembee?'
6 Ne var ki, İnsanoğlu'nun yeryüzünde günahları bağışlama yetkisine sahip olduğunu bilesiniz diye...” Sonra felçliye, “Kalk, yatağını topla, evine git!” dedi.
Lakini mtambue ya kwamba Mwana wa Adamu anao uwezo wa kusamehe dhambi...” aliyasema haya kwa yule aliyepooza, “Simama, chukua godoro lako, na uende nyumbani kwako”
7 Adam da kalkıp evine gitti.
Ndipo yule mtu akasimama na kuondoka kwenda nyumbani kwake.
8 Halk bunu görünce korkuya kapıldı. İnsana böyle bir yetki veren Tanrı'yı yücelttiler.
Makutano walipoona hayo, walishangaa na kumsifu Mungu, ambaye amewapa uwezo huo watu.
9 İsa oradan geçerken, vergi toplama yerinde oturan birini gördü. Matta adındaki bu adama, “Ardımdan gel” dedi. Adam da kalkıp İsa'nın ardından gitti.
Na Yesu alipokuwa akipita kutoka hapo, alimwona mtu ambaye aliitwa kwa jina la Mathayo, ambaye alikuwa amekaa sehemu ya watoza ushuru. Naye akamwambia, “Nifuate mimi” Naye akasimama na kumfuata.
10 Sonra İsa, Matta'nın evinde sofrada otururken, birçok vergi görevlisiyle günahkâr gelip O'nunla ve öğrencileriyle birlikte sofraya oturdu.
Na Yesu alipoketi ili ale chakula ndani ya nyumba, wakaja watoza ushuru wengi na watu waovu wakashiriki chakula pamoja na Yesu na wanafunzi wake.
11 Bunu gören Ferisiler, İsa'nın öğrencilerine, “Sizin öğretmeniniz neden vergi görevlileri ve günahkârlarla birlikte yemek yiyor?” diye sordular.
Ndipo Mafarisayo walipoona hayo, wakawaambia wanafunzi “Kwa nini mwalimu wenu anakula chakula pamoja na watoza ushuru na watu waovu?”
12 İsa bunu duyunca şöyle dedi: “Sağlamların değil, hastaların hekime ihtiyacı var.
Yesu aliposikia hayo, naye alisema “Watu walio na afya nzuri hawahitaji mganga, isipokuwa wale walio wagonjwa.
13 Gidin de, ‘Ben kurban değil, merhamet isterim’ sözünün anlamını öğrenin. Çünkü ben doğru kişileri değil, günahkârları çağırmaya geldim.”
Inawapasa muende mkajifunze maana yake, “Ninapenda rehema na siyo dhabihu” Kwa kuwa nilikuja, si kwa wenye haki kutubu, lakini kwa wenye dhambi.
14 Bu arada Yahya'nın öğrencileri gelip İsa'ya, “Neden biz ve Ferisiler oruç tutuyoruz da senin öğrencilerin tutmuyor?” diye sordular.
Ndipo wanafunzi wa Yohana wakaja kwake na kusema, “Kwa nini sisi na mafarisayo tunafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?”
15 İsa şöyle karşılık verdi: “Güvey aralarındayken, davetliler yas tutar mı? Ama güveyin aralarından alınacağı günler gelecek, o zaman oruç tutacaklar.
Yesu akawaambia, Je wasindikizaji wa arusi wanaweza kuwa na huzuni pindi Bwana arusi anapokuwa pamoja nao? Lakini siku zinakuja ambapo Bwana arusi atachukuliwa kutoka kwao, na ndipo watakapofunga.
16 Hiç kimse eski giysiyi yeni kumaş parçasıyla yamamaz. Çünkü yeni kumaş çeker, giysiden kopar, yırtık daha beter olur.
Hakuna mtu anayeweka kipande cha nguo mpya kwenye nguo ya zamani, kiraka kitatatuliwa kutoka kwenye nguo na mpasuko mkubwa utatokea.
17 Hiç kimse yeni şarabı eski tulumlara doldurmaz. Yoksa tulumlar patlar; hem şarap dökülür, hem de tulumlar mahvolur. Yeni şarap yeni tulumlara konur, böylece her ikisi de korunmuş olur.”
Hakuna watu wanaoweka mvinyo mpya katika chombo cha mvinyo wa zamani, ikiwa watafanya, ngozi itachanika, mvinyo utatoweka na ngozi itaharibika. Badala yake, huweka mvinyo mpya katika ngozi mpya na vyote vitakuwa salama.
18 İsa onlara bu sözleri söylerken bir havra yöneticisi gelip O'nun önünde yere kapanarak, “Kızım az önce öldü. Ama sen gelip elini onun üzerine koyarsan, dirilecek” dedi.
Wakati Yesu alipokuwa akiwaambia mambo hayo, tazama, afisa akaja akasujudu mbele yake, Naye akasema, “Binti yangu amefariki punde, lakini njoo na uweke mkono wako juu yake na yeye ataishi tena.
19 İsa kalkıp öğrencileriyle birlikte adamın ardından gitti.
Ndipo Yesu akasimama na kumfuata na wanafunzi wake pia.
20 Tam o sırada, on iki yıldır kanaması olan bir kadın İsa'nın arkasından yetişip giysisinin eteğine dokundu.
Tazama, mwanamke ambaye alikuwa anatokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, akaja karibu na Yesu na akagusa sehemu ya pindo la vazi lake.
21 İçinden, “Giysisine bir dokunsam kurtulurum” diyordu.
Kwa kuwa alisema, “Endapo nitagusa vazi lake, nami nitapata uponyaji.”
22 İsa arkasına dönüp onu görünce, “Cesur ol, kızım! İmanın seni kurtardı” dedi. Ve kadın o anda iyileşti.
Yesu akageuka na kumtazama na kumwambia. “Binti, jipe moyo, imani yako imekufanya upone,” Na muda huo huo mwanamke akapata uponyaji muda huo.
23 İsa, yöneticinin evine varıp kaval çalanlarla gürültülü kalabalığı görünce, “Çekilin!” dedi. “Kız ölmedi, uyuyor.” Onlar ise kendisiyle alay ettiler.
Na Yesu alipofika kwenye nyumba ya afisa, naye aliwaona wapiga tarumbeta na umati wa watu ulikuwa ukipiga kelele.
Naye akasema, “Tokeni hapa, kwa kuwa binti hajafa, bali amelala. Lakini wao walicheka na kumkebehi.
25 Kalabalık dışarı çıkarılınca İsa içeri girip kızın elini tuttu, kız ayağa kalktı.
Na wale watu walipotolewa nje, naye akaingia chumbani na kumshika mkono na msichana akaamka.
26 Bu haber bütün bölgeye yayıldı.
Na habari hizi zikaenea katika mji mzima.
27 İsa oradan ayrılırken iki kör, “Ey Davut Oğlu, halimize acı!” diye feryat ederek O'nun ardından gittiler.
Ndipo Yesu alipokuwa akipita kutoka pale, wanaume wawili vipofu wakamfuata. Waliendelea kupaza sauti wakisema, “Tunaomba uturehemu, Mwana wa Daudi.”
28 İsa eve girince körler yanına geldi. Onlara, “İstediğinizi yapabileceğime inanıyor musunuz?” diye sordu. Körler, “İnanıyoruz, ya Rab!” dediler.
Pindi Yesu apokuwa amefika kwenye nyumba, wale vipofu wakaja kwake. Yesu akawaambia, “Mnaamini kwamba ninaweza kutenda?” Nao wakamwambia “Ndiyo, Bwana”
29 Bunun üzerine İsa körlerin gözlerine dokunarak, “İmanınıza göre olsun” dedi.
Ndipo Yesu akagusa macho yao na kusema “Na ifanyike hivyo kwenu kama imani yenu ilivyo”
30 Ve adamların gözleri açıldı. İsa, “Sakın kimse bunu bilmesin” diyerek onları sıkı sıkı uyardı.
Na macho yao yakafumbuka. Ndipo Yesu akasisitiza akawaamuru na kusema “Angalieni mtu yeyote asifahamu kuhusu jambo hili.”
31 Onlar ise çıkıp İsa'yla ilgili haberi bütün bölgeye yaydılar.
Lakini watu hawa wawili wakaondoka na kutangaza habari hizi sehemu zote za mji.
32 Adamlar çıkarken İsa'ya dilsiz bir cinli getirdiler.
Ndipo wale wanaume wawili walipokuwa wakienda zao, Tazama, mtu mmoja bubu aliyepagawa na pepo akaletwa kwa Yesu.
33 Cin kovulunca adamın dili çözüldü. Halk hayret içinde, “İsrail'de böylesi hiç görülmemiştir” diyordu.
Na pepo walipomtoka, yule mtu bubu akaanza kuongea. Umati ukashangazwa na kusema “Hii haijawahi kutokea katika Israel.
34 Ferisiler ise, “Cinleri, cinlerin önderinin gücüyle kovuyor” diyorlardı.
Lakini mafarisayo walikuwa wakisema “Kwa wakuu wa pepo, anawafukuza mapepo”
35 İsa bütün kent ve köyleri dolaşarak havralarda öğretiyor, göksel egemenliğin Müjdesi'ni duyuruyor, her hastalığı, her illeti iyileştiriyordu.
Yesu akaenda kwenye miji yote na vijiji. Naye akaendelea kufundisha katika masinagogi, akihubiri injili ya ufalme, na kuponya magonjwa ya kila aina na udhaifu wa aina zote.
36 Kalabalıkları görünce onlara acıdı. Çünkü çobansız koyunlar gibi şaşkın ve perişandılar.
Wakati alipotazama umati, naye aliwaonea huruma, kwa sababu walisumbuka na kuvunjika moyo. Walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji.
37 O zaman İsa öğrencilerine, “Ürün bol, ama işçi az” dedi,
Naye akawaambia wanafunzi wake. “Mavuno ni mengi, lakini wafanya kazi ni wachache.
38 “Bu nedenle ürünün sahibi Rab'be yalvarın, ürününü kaldıracak işçiler göndersin.”
Hivyo basi upesi mwombeni Bwana wa mavuno, ili kwamba atume wafanya kazi katika mavuno yake.”