< Hâkimler 3 >

1 Kenan'daki savaşların hiçbirine katılmamış olan İsrailliler'i sınamak ve hiç savaş deneyimi olmayan yeni kuşaklara savaş eğitimi vermek için RAB'bin dokunmadığı uluslar şunlardır:
Haya ndiyo mataifa Bwana aliyoyaacha ili kuwajaribu Waisraeli wote ambao hawakujua vita vyovyote vya Kanaani
2
(alifanya hivi ili tu kuwafundisha wazao wa Waisraeli ambao hawakuwa wamejua vita hapo awali):
3 Beş Filist Beyliği, bütün Kenanlılar, Saydalılar, Baal-Hermon Dağı'ndan Levo-Hamat'a kadar uzanan Lübnan dağlarında yaşayan Hivliler.
wafalme watano wa Wafilisti, Wakanaani wote, Wasidoni, Wahivi waishio katika milima ya Lebanoni kuanzia Mlima wa Baal-Hermoni hadi Lebo-Hamathi.
4 RAB İsrailliler'i sınamak, Musa aracılığıyla atalarına verdiği buyrukları yerine getirip getirmeyeceklerini görmek için bu ulusları ülkelerinde bıraktı.
Waliachwa ili kuwajaribu Waisraeli kuona kama wangetii amri za Bwana, alizokuwa amewapa baba zao kwa mkono wa Mose.
5 Böylece İsrailliler Kenan, Hitit, Amor, Periz, Hiv ve Yevus halkları arasında yaşadılar.
Waisraeli wakaishi miongoni mwa Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
6 Onlardan kız aldılar, kızlarını onların oğullarına verdiler ve onların ilahlarına taptılar.
Wakawaoa binti zao, nao wakawatoa binti zao waolewe na wana wa hayo mataifa, na kuitumikia miungu yao.
7 RAB'bin gözünde kötü olanı yapan İsrailliler Tanrıları RAB'bi unutup Baallar'a ve Aşera putlarına taptılar.
Waisraeli wakafanya maovu machoni pa Bwana, wakamsahau Bwana Mungu wao na kutumikia Mabaali na Maashera.
8 Bunun üzerine RAB İsrail'e öfkelendi ve onları Aram-Naharayim Kralı Kuşan-Rişatayim'in eline teslim etti. İsrailliler sekiz yıl Kuşan-Rişatayim'in boyunduruğunda kaldılar.
Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli, hivyo akawauza na kuwatia mikononi mwa Kushan-Rishathaimu mfalme wa Aramu-Naharaimu ambaye Israeli walikuwa chini yake wakimtumikia kwa muda wa miaka minane.
9 Ama RAB'be yakarmaları üzerine RAB onlara Otniel adında bir kurtarıcı çıkardı. Kalev'in küçük kardeşi Kenaz'ın oğlu Otniel onları kurtardı.
Waisraeli walipomlilia Bwana, yeye akawainulia mwokozi, Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa Kalebu, ambaye aliwaokoa.
10 RAB'bin Ruhu Otniel'in üzerine indi. Otniel İsrailliler'i yönetti, onlar için savaştı. RAB Aram-Naharayim Kralı Kuşan-Rişatayim'i onun eline teslim etti. Artık Otniel ondan daha güçlüydü.
Roho wa Bwana akaja juu yake, hivyo akawa mwamuzi wa Israeli, akaenda vitani. Bwana akamtia Kushan-Rishathaimu mfalme wa Aramu mikononi mwa Othnieli, naye akamshinda.
11 Ülke Kenaz oğlu Otniel'in ölümüne dek kırk yıl barış içinde yaşadı.
Hivyo nchi ikawa na amani kwa muda wa miaka arobaini, mpaka Othnieli mwana wa Kenazi alipofariki.
12 Sonra İsrailliler yine RAB'bin gözünde kötü olanı yaptılar. RAB gözünde kötü olanı yaptıkları için Moav Kralı Eglon'u onlara karşı güçlendirdi.
Waisraeli wakafanya maovu mbele za Bwana tena, kwa kuwa walifanya maovu hayo Bwana akamtia nguvu Egloni mfalme wa Moabu dhidi ya Israeli.
13 Kral Eglon Ammonlular'la Amalekliler'i kendi tarafına çekerek İsrail'e saldırdı. Onları bozguna uğratarak Hurma Kenti'ni ele geçirdi.
Egloni akawataka Waamoni na Waamaleki waungane naye, akaja kuishambulia Israeli, nao wakatwaa Mji wa Mitende
14 İsrailliler on sekiz yıl Moav Kralı Eglon'un boyunduruğu altında kaldılar.
Waisraeli wakawa chini ya Egloni mfalme wa Moabu kwa muda wa miaka kumi na minane.
15 Ama RAB'be yakarmaları üzerine RAB onlar için Ehut adında bir kurtarıcı çıkardı. Benyaminli Gera'nın oğlu Ehut solaktı. İsrailliler Ehut'un eliyle Moav Kralı Eglon'a haraç gönderdiler.
Waisraeli wakamlilia tena Bwana, naye akawapa mwokozi: Ehudi, mtu wa shoto, mwana wa Gera, Mbenyamini. Waisraeli wakatuma kwa Egloni mfalme wa Moabu ushuru kwa mkono wa Ehudi.
16 Ehut kendine bir arşın uzunluğunda iki ağızlı bir kama yaptı ve bunu sağ kalçası üzerine, giysisinin altına sakladı.
Basi Ehudi alikuwa ametengeneza upanga wenye ukatao kuwili, urefu wake ni kama dhiraa moja, akaufunga upanga huo ndani ya nguo yake kwenye paja lake la mkono wa kuume.
17 Varıp haracı Moav Kralı Eglon'a sundu. Eglon çok şişman bir adamdı.
Akamkabidhi ushuru Egloni mfalme wa Moabu, ambaye alikuwa mtu mnene sana.
18 Ehut haracı sunduktan sonra, haracı taşımış olan adamlarını salıverdi.
Baada ya Ehudi kumkabidhi ule ushuru, wale watu waliokuwa wameubeba huo ushuru aliwaruhusu waende zao.
19 Ama kendisi Gilgal yakınındaki taş putlardan geri döndü. “Ey kral, sana gizli bir haberim var” dedi. Kral ona, “Sus” diyerek yanındaki adamların hepsini dışarı çıkardı.
Yeye mwenyewe akafuatana nao hadi kwenye sanamu ya kuchora kwenye mawe karibu na Gilgali, ndipo yeye akarudi, akafika kwa Egloni na kusema, “Ee Mfalme, ninao ujumbe wa siri kwa ajili yako.” Mfalme akasema, “Nyamazeni kimya!” Nao wale waliomhudumia wote wakamwacha, wakatoka nje.
20 Ehut, üst kattaki serin odasında yalnız kalan krala yaklaşarak, “Tanrı'dan sana bir haber getirdim” deyince kral tahtından kalktı.
Ndipo Ehudi akamsogelea alipokuwa ameketi peke yake kwenye chumba cha juu cha jumba lake la kifalme la majira ya kiangazi, na kusema, “Ninao ujumbe kutoka kwa Mungu kwa ajili yako.” Mfalme alipokuwa anainuka kutoka kwenye kiti chake,
21 Ehut sol eliyle sağ kalçası üzerindeki kamayı çekti ve kralın karnına sapladı.
Ehudi akaunyoosha mkono wake wa kushoto na kuufuta ule upanga aliokuwa ameufunga kwenye paja lake la kulia, akamdunga Mfalme Egloni tumboni mwake.
22 Kamanın ucu kralın sırtından çıktı. Bıçağın ardından kabza da ete saplanmıştı. Ehut kamayı çekmeyince kama kralın yağlı karnına gömüldü.
Hata mpini nao ukazama tumboni pamoja na upanga wenyewe, nao upanga ukatokea mgongoni mwake. Ehudi hakuuchomoa huo upanga, nayo mafuta yakashikamana juu ya upanga.
23 Ehut sofaya çıktı, üst kattaki odanın kapısını ardından çekip kilitledi.
Ehudi akatoka nje barazani; akamfungia milango ya chumba cha juu na kuifunga kwa funguo.
24 O çıktıktan sonra, geri gelen kralın hizmetkârları üst kattaki odanın kapılarını kilitli buldular. Birbirlerine, “Su döküyor olmalı” dediler.
Baada ya kuondoka, watumishi wakaja na kukuta milango ya chumba cha juu imefungwa kwa funguo. Wakasema, “Bila shaka amejipumzisha kwenye chumba cha ndani cha nyumba yake ya majira ya kiangazi.”
25 Uzun süre bekledilerse de kral odanın kapılarını açmadı. Bunun üzerine bir anahtar bulup kapıyı açtılar. Efendilerinin ölüsü yerde yatıyordu.
Wakangoja hata wakawa na fadhaa, basi wakati hakufungua milango ya chumba, wakachukua funguo na kuifungua. Tazama wakaona bwana wao amelala sakafuni, amekufa.
26 Onlar beklerken Ehut kaçmış, taş putları geçerek Seira'ya yönelmişti.
Walipokuwa wangali wanangoja, Ehudi akatoroka, akapita hapo kwenye sanamu ya kuchora kwenye mawe na kukimbilia Seira.
27 Oraya varınca Efrayim'in dağlık bölgesine çıkıp boru çaldı. İsrailliler onunla birlikte dağlardan indiler. Ehut önden gidiyordu.
Alipofika huko, akapiga tarumbeta katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao Waisraeli wakateremka pamoja naye kutoka vilimani, yeye akiwa anawaongoza.
28 Onlara, “Beni izleyin” dedi, “RAB düşmanlarınızı, Moavlılar'ı elinize teslim etti.” Ehut'u izleyen İsrailliler, Moav'a giden Şeria geçitlerini tuttular, kimseyi geçirmediler.
Akawaagiza, “Nifuateni, kwa kuwa Bwana amewatia Moabu, adui zenu, mikononi mwenu.” Kwa hiyo wakateremka wakamfuata, wakavishika vivuko vya Yordani kuelekea Moabu, wala hawakuacha mtu yeyote kuvuka.
29 Moav'ın güçlü yiğitlerinden on bin kadarını vurup öldürdüler; hiç kurtulan olmadı.
Wakati huo wakawaua Wamoabu watu waume wapatao 10,000 ambao wote walikuwa wenye nguvu na mashujaa; hakuna mtu yeyote aliyetoroka.
30 Moav o gün İsrailliler'in boyunduruğuna girdi. Ülke seksen yıl barış içinde yaşadı.
Siku ile Moabu wakashindwa na Israeli, nayo nchi ikawa na amani kwa miaka themanini.
31 Ehut'tan sonra Anat oğlu Şamgar başa geçti. Şamgar Filistliler'den altı yüz kişiyi üvendireyle öldürerek İsrailliler'i kurtardı.
Baada ya Ehudi akaja Shamgari mwana wa Anathi, aliyewapiga Wafilisti 600 kwa fimbo iliyochongoka ya kuongozea ngʼombe. Naye pia akawaokoa Waisraeli.

< Hâkimler 3 >