< Hâkimler 20 >

1 Gilat başta olmak üzere Dan'dan Beer-Şeva'ya kadar, bütün İsrail halkı yola çıkıp Mispa'da, RAB'bin önünde tek beden gibi toplandı.
Ndipo Waisraeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na wa kutoka nchi ya Gileadi wakatoka kama mtu mmoja wakakusanyika mbele za Bwana huko Mispa.
2 Tanrı halkı İsrail'in bütün oymak önderleri bu toplantıda hazır bulundular. Eli kılıç tutan dört yüz bin yayaydılar.
Viongozi wote wa kabila za Israeli wakakaa kwenye nafasi zao katika kusanyiko la watu wa Mungu, askari 400,000 waendao kwa miguu wenye panga.
3 –Bu arada Benyaminoğulları İsrailliler'in Mispa'da toplandığını duydular.– İsrailliler, “Anlatın bize, bu korkunç olay nasıl oldu?” diye sordular.
(Wabenyamini wakasikia kuwa Waisraeli wamepanda kwenda Mispa.) Ndipo Waisraeli wakasema, “Tuelezeni jinsi jambo hili ovu lilivyotendeka.”
4 Öldürülen kadının Levili kocası şöyle yanıtladı: “Cariyemle birlikte geceyi geçirmek üzere Benyamin bölgesinin Giva Kenti'ne girdik.
Hivyo yule Mlawi, mume wa yule mwanamke aliyeuawa, akasema, “Mimi na suria wangu tulifika Gibea ya Benyamini ili tulale huko.
5 Giva'dan bazı adamlar gece beni öldürmeyi tasarlayarak gelip evi kuşattılar. Cariyemin ırzına geçtiler, ölümüne neden oldular.
Wakati wa usiku watu wa Gibea wakanijia na kuizingira nyumba, wakitaka kuniua. Wakambaka suria wangu mpaka akafa.
6 Onun ölüsünü alıp parçaladım, her bir parçasını İsrail'in mülk aldığı bir bölgeye gönderdim. Çünkü bu alçakça rezalet İsrail'de işlendi.
Ndipo nikamchukua suria wangu, nikamkatakata vipande vipande na kuvipeleka katika nchi yote ya urithi wa Israeli, kwa kuwa wametenda uasherati mkubwa na jambo la aibu katika Israeli.
7 Ey İsrailliler! İşte hepiniz buradasınız. Düşünceniz, kararınız nedir, söyleyin.”
Sasa, ninyi Waisraeli wote, semeni na mtoe uamuzi wenu.”
8 Oradakilerin hepsi ağız birliği etmişçesine, “Bizden hiç kimse çadırına gitmeyecek, evine dönmeyecek” dediler,
Watu wote wakainuka wakasema, kama mtu mmoja, “Hakuna hata mmoja wetu atakayekwenda nyumbani. Wala hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake.
9 “Yapacağımız şu: Giva'ya kura ile saldıracağız.
Sasa hili ndilo tutakaloitendea Gibea: Tutaikabili jinsi kura itakavyotuongoza.
10 Halka yiyecek sağlamak için bütün İsrail oymaklarından nüfuslarına göre, her yüz kişiden on, bin kişiden yüz, on bin kişiden bin kişi seçeceğiz. Bunlar Benyamin'in Giva Kenti'ne geldiklerinde kentlilerden İsrail'de yaptıkları bu alçaklığın öcünü alsınlar.”
Tutatoa watu kumi katika kila 100 kutoka kwenye kabila zote za Israeli, watu 100 katika watu 1,000 na watu 1,000 katika 10,000, ili waende wakalete mahitaji kwa ajili ya jeshi. Basi wakati jeshi litakapofika Gibea ya Benyamini, watawatendea yale wanayostahili, kwa ajili ya uovu huu wa aibu waliotenda katika Israeli.”
11 Giva'ya karşı toplanmış olan İsrailliler tam bir birlik içindeydi.
Hivyo wanaume wote wa Israeli wakakutanika pamoja na kujiunga kama mtu mmoja dhidi ya huo mji.
12 İsrail oymakları, Benyamin oymağına adamlar göndererek, “Aranızda yapılan bu alçaklık nedir?” diye sordular,
Makabila ya Israeli yakatuma watu kwenda katika kabila la Benyamini lote na kuwaambia, “Ni uovu gani huu wa kutisha uliotendeka katikati yenu?
13 “Giva'daki o serserileri bize hemen teslim edin. Onları öldürüp İsrail'deki kötülüğün kökünü kazıyalım.” Ama Benyaminoğulları İsrailli kardeşlerini dinlemediler.
Basi watoeni hao watu waovu kabisa walioko Gibea, ili tupate kuwaua na kuondoa uovu katika Israeli.” Lakini Wabenyamini hawakuwasikia ndugu zao, Waisraeli.
14 İsrailliler'le savaşmak üzere öbür kentlerden akın akın Giva'ya geldiler.
Wakatoka katika miji yao, wakakutanika Gibea ili kupigana na Waisraeli.
15 Giva halkından olan yedi yüz seçme adam dışında, öbür kentlerden gelen ve eli kılıç tutan Benyaminoğulları'nın sayısı o gün yirmi altı bini buldu.
Siku ile Wabenyamini wakakusanya watu 26,000 kutoka miji yao, waliojifunga panga, mbali na hao 700 waliochaguliwa miongoni mwa hao waliokaa Gibea.
16 Solak olan yedi yüz seçme adam da bunların arasındaydı. Hepsi de bir kılı sapanla vuracak kadar iyi nişancıydı.
Miongoni mwa hao askari wote kulikuwa na watu 700 bora waliochaguliwa watumiao mkono wa kushoto, kila mmoja wao aliweza kutupa jiwe kwa kombeo na kulenga unywele mmoja bila kukosa.
17 Benyaminoğulları'nın yanısıra İsrailliler de sayıldı. Eli kılıç tutan dört yüz bin askerleri vardı. Hepsi de yaman savaşçılardı.
Nao watu wa Israeli, mbali na hao wa Benyamini, wakakusanya watu waume 400,000, wenye kutumia panga, wote hao walikuwa mashujaa.
18 Beytel'e çıkan İsrailliler Tanrı'ya, “Benyaminoğulları'na karşı önce hangimiz savaşacak?” diye sordular. RAB, “Önce Yahudaoğulları savaşacak” dedi.
Waisraeli wakapanda Betheli na kumuuliza Mungu, “Ni nani miongoni mwetu atakayetangulia mbele yetu ili kupigana na Wabenyamini?” Bwana akawajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia.”
19 İsrailliler sabah kalkıp Giva'nın karşısında ordugah kurdular.
Asubuhi yake Waisraeli wakaamka na kupiga kambi karibu na Gibea.
20 Benyaminoğulları'yla savaşmak üzere ilerleyip Giva'da savaş düzenine girdiler.
Waisraeli wakatoka kupigana na Wabenyamini, nao Waisraeli wakajiweka kwenye nafasi zao katika vita dhidi yao huko Gibea.
21 Giva'dan çıkan Benyaminoğulları, o gün İsrailliler'den yirmi iki bin kişiyi yere serdiler.
Wabenyamini wakatoka Gibea na kuwaua watu 22,000 wa Israeli siku ile.
22 Ama İsrailliler birbirlerini yüreklendirerek önceki gün savaş düzenine girdikleri yerde mevzilendiler.
Lakini Waisraeli wakatiana moyo kila mmoja na mwenzake, nao wakajiweka kwenye nafasi zao katika vile vita mara ya pili mahali pale walipokuwa wamejiweka mara ya kwanza.
23 Sonra Beytel'de RAB'bin önünde akşama dek ağladılar. RAB'be, “Kardeşlerimiz olan Benyaminoğulları'yla yine savaşmaya çıkalım mı?” diye sordular. RAB, “Evet, onlarla savaşın” dedi.
Waisraeli wakapanda mbele za Bwana na kulia mbele zake mpaka jioni, nao wakamuuliza Bwana wakisema, “Je, tupande tena kupigana vita na Wabenyamini, ndugu zetu?” Bwana akajibu, “Pandeni mkapigane nao.”
24 Bunun üzerine İsrailliler ikinci gün yine Benyaminoğulları'na yaklaştılar.
Ndipo Waisraeli wakawakaribia Wabenyamini siku ya pili.
25 Benyaminoğulları da aynı gün Giva'dan onların üzerine yürüyerek on sekiz bin kişiyi daha yere serdiler. Ölenlerin hepsi eli kılıç tutan savaşçılardı.
Wakati huu, Wabenyamini walipotoka Gibea ili kupigana nao, wakawaua watu Waisraeli 18,000, wote wakiwa wamejifunga panga.
26 Bütün İsrailliler, bütün halk çekilip Beytel'e döndü. Orada, RAB'bin önünde durup ağladılar, o gün akşama dek oruç tuttular. RAB'be yakmalık sunular ve esenlik sunuları sundular.
Ndipo Waisraeli, watu wote, wakapanda Betheli, huko wakakaa mbele za Bwana wakilia. Wakafunga siku ile mpaka jioni na kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya amani kwa Bwana.
27 Tanrı'nın Antlaşma Sandığı o sırada Beytel'deydi. Harun oğlu Elazar oğlu Pinehas o sırada sandığın önünde görev yapıyordu. İsrailliler RAB'be, “Kardeşimiz Benyaminoğulları'yla savaşmaya devam edelim mi, yoksa vaz mı geçelim?” diye sordular. RAB, “Savaşın” dedi, “Çünkü onları yarın elinize teslim edeceğim.”
Nao Waisraeli wakauliza kwa Bwana. (Katika siku hizo Sanduku la Agano la Mungu lilikuwa huko
na Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Aroni, alikuwa anahudumu mbele za hilo Sanduku.) Wakauliza, “Je, tupande kwenda vitani kupigana tena na Wabenyamini ndugu zetu, au la?” Bwana akajibu, “Nendeni, kwa kuwa kesho nitawatia mikononi mwenu.”
29 İsrailliler dört bir yandan Giva'nın çevresinde pusuya yattılar.
Basi Waisraeli wakaweka waviziao kuizunguka Gibea.
30 Üçüncü gün Benyaminoğulları'na karşı harekete geçerek önceki gibi kentin karşısında savaş düzenine girdiler.
Kisha Waisraeli wakapanda kupigana na Wabenyamini katika siku ya tatu na kujiweka kwenye nafasi zao dhidi ya Gibea kama walivyokuwa wamefanya hapo kwanza.
31 Saldırıya geçen Benyaminoğulları kentten epey uzaklaştılar. Beytel'e ve Giva'ya giden ana yollarda, kırlarda önceki çarpışmalarda olduğu gibi İsrailliler'e kayıplar verdirmeye başladılar; otuz kadarını öldürdüler.
Wabenyamini wakatoka ili kukabiliana nao, Waisraeli wakawavuta Wabenyamini watoke katika mji. Wakaanza kupigana na kuua watu wapatao thelathini wa Israeli, kama walivyofanya nyakati nyingine, katika njia kuu, moja iendayo Betheli na nyingine Gibea.
32 “Geçen seferki gibi onları yine bozguna uğratıyoruz” dediler. İsrailliler ise birbirlerine, “Kaçalım da onları kentten uzağa, ana yollara çekelim” diyerek bulundukları yerden çıkıp Baal-Tamar'da savaş düzenine girdiler. Giva'nın batısında pusuya yatanlar da birden yerlerinden fırladı.
Wabenyamini wakafikiri, “Wanapigwa mbele yetu kama hapo kwanza.” Waisraeli wakasema, “Sisi na turudi nyuma ili tuwavute wauache mji waende kuelekea barabarani.”
Watu wote wa Israeli wakaondoka kwenye sehemu zao na kujipanga huko Baal-Tamari, nao wale waviziaji wa Waisraeli, wakatoka hapo walipokuwa kwenye uwanda wa magharibi ya Gibea.
34 Böylece bütün İsrail'den seçme on bin kişi Giva'ya cepheden saldırdı. Savaş iyice kızışmıştı. Benyaminoğulları başlarına gelecek felaketten habersizdi.
Ndipo watu 10,000 bora waliochaguliwa katika Israeli wote, wakaja kuishambulia Gibea. Vita vilikuwa vikali sana, hata Wabenyamini hawakutambua kuwa maangamizi yalikuwa karibu nao kwa kiasi hicho.
35 RAB onları İsrail'in önünde bozguna uğrattı. İsrailliler o gün Benyaminoğulları'ndan eli kılıç tutan yirmi beş bin yüz kişiyi öldürdüler.
Bwana akawashinda Wabenyamini mbele ya Waisraeli na siku ile Waisraeli wakawaua Wabenyamini watu waume 25,100, wote wakiwa wenye kujifunga silaha za vita.
36 Benyaminoğulları yenildiklerini anladılar. İsrailliler onların geçmesine izin verdiler; çünkü Giva çevresinde pusuda yatanlara güveniyorlardı.
Hivyo Wabenyamini wakaona kuwa wamepigwa. Basi Waisraeli walikuwa wameondoka mbele ya Wabenyamini, kwa sababu Waisraeli waliwategemea hao waviziaji waliokuwa wamewaweka dhidi ya Gibea.
37 Pusudakiler ansızın Giva'ya saldırdılar. Bütün kente dağılarak halkı kılıçtan geçirdiler.
Wale waviziaji wakafanya haraka kuingia Gibea, wakasambaa na kuwaua watu wote wa mji kwa upanga.
38 Pusuya yatanlarla öbür İsrailliler arasında bir işaret kararlaştırılmıştı: Kenti ateşe verip büyük bir duman bulutu oluşturacaklardı.
Waisraeli walikuwa wamepatana na hao waviziaji kuwa wangefanya lipande wingu kubwa la moshi kutoka huo mji,
39 O zaman savaş alanındaki İsrailliler birden geri dönecekti. Bu arada Benyaminoğulları İsrailliler'e kayıplar verdirmeye başlamış, otuz kadarını vurmuşlardı. Daha önceki savaşta olduğu gibi, İsrailliler'i kesin bir bozguna uğrattıklarını sandılar.
ndipo watu wa Waisraeli wangegeuka kupigana. Watu wa Benyamini walikuwa wameanza kuwapiga na kuua watu wa Israeli (wapatao thelathini), hivyo wakafikiri, “Hakika tutawapiga, kama tulivyowashinda katika vita hapo kwanza.”
40 Ama dönüp kente baktıklarında orada hortum gibi göğe yükselen duman bulutunu gördüler. Yanan kentin dumanı göğü kaplamıştı.
Lakini wakati lile wingu la moshi lilipoanza kupanda kutoka ule mji, Wabenyamini wakageuka na kuona moshi wa mji mzima unapaa juu angani.
41 İsrailliler'in döndüğünü gören Benyaminoğulları paniğe kapıldı. Çünkü başlarına gelecek felaketi sezmişlerdi.
Ndipo watu wa Israeli wakawageukia, nao Wabenyamini wakatiwa hofu, kwa kuwa walitambua kwamba maafa yamewajia.
42 İsrailliler'in önüsıra kırlara doğru yöneldilerse de savaştan kaçamadılar. Çeşitli kentlerden çıkagelen İsrailliler onları kuşatıp yok etti.
Basi wakakimbia mbele ya Waisraeli kuelekea nyikani, lakini hawakuweza kukwepa vile vita. Nao watu wa Israeli waliotoka katika ile miji wakawaua huko.
43 Geri kalan Benyaminoğulları'nı kovaladılar. Giva'nın doğusunda konakladıkları yere dek onları yol boyunca vurup yere serdiler.
Wakawazingira Wabenyamini pande zote, wakawafuatia na kuwapata hapo walipopumzika katika viunga vya Gibea upande wa mashariki.
44 Benyaminoğulları'ndan on sekiz bin kişi vuruldu. Hepsi de yiğit savaşçılardı.
Wakaanguka Wabenyamini 18,000 ambao wote ni mashujaa.
45 Sağ kalanlar dönüp kırlara, Rimmon Kayalığı'na doğru kaçmaya başladı. İsrailliler yol boyunca bunlardan beş bin kişi daha öldürdü. Gidom'a kadar onları adım adım izleyerek iki binini daha vurup yere serdiler.
Walipogeuka na kukimbia kuelekea nyikani hata kufikia mwamba wa Rimoni, Waisraeli wakawaua watu 5,000 wakiwa njiani. Wakawafuata kwa kasi mpaka Gidomu huko wakawaua watu wengine 2,000.
46 O gün Benyaminoğulları'ndan öldürülenlerin toplam sayısı yirmi beş bin kişiyi buldu. Hepsi de eli kılıç tutan yiğit savaşçılardı.
Siku ile wakawaua Wabenyamini 25,000 waliokuwa mashujaa wa vita.
47 Kırlara kaçıp Rimmon Kayalığı'na sığınanların sayısı altı yüzdü. Kayalıkta dört ay kaldılar.
Lakini watu 600 wakakimbia kuelekea nyikani katika mwamba wa Rimoni, na kukaa huko muda wa miezi minne.
48 İsrailliler Benyamin kentlerine döndüler; insanları, hayvanları ve oradaki bütün canlıları kılıçtan geçirdiler, rastladıkları bütün kentleri ateşe verdiler.
Waisraeli wakarudi na kuua watu wote wa Benyamini, pamoja na wanyama na kila walichokikuta. Pia kila mji waliouona waliuchoma moto.

< Hâkimler 20 >