< Hâkimler 1 >

1 İsrailliler, Yeşu'nun ölümünden sonra RAB'be, “Bizim için Kenanlılar'la savaşmaya ilk kim gidecek?” diye sordular.
Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamuuliza Bwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?”
2 RAB, “Yahuda oymağı gidecek” dedi, “Kenan ülkesini onun eline teslim ediyorum.”
Bwana akajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.”
3 Yahudaoğulları, kardeşleri Şimonoğulları'na, “Kenanlılar'la savaşmak için payımıza düşen bölgeye bizimle birlikte gelin” dediler, “Sonra biz de payınıza düşen bölgeye sizinle geliriz.” Böylece Şimonoğulları Yahudaoğulları'yla birlikte gitti.
Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. Sisi pia tutakwenda pamoja nanyi katika sehemu yenu mliyopewa.” Basi Wasimeoni wakaenda pamoja nao.
4 Yahudaoğulları saldırıya geçti. RAB Kenanlılar'la Perizliler'i ellerine teslim etti. Bezek'te onlardan on bin kişiyi öldürdüler.
Yuda aliposhambulia, Bwana akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao, nao wakawaua watu 10,000 huko Bezeki.
5 Adoni-Bezek'le orada karşılaşıp savaşa tutuştular, Kenanlılar'la Perizliler'i yenilgiye uğrattılar.
Huko ndiko walipomkuta huyo Adoni-Bezeki, nao wakapigana naye na kuwafanya Wakanaani na Waperizi wakimbie.
6 Adoni-Bezek kaçtı, ama peşine düşüp onu yakaladılar; elleriyle ayaklarının başparmaklarını kestiler.
Adoni-Bezeki pia alikimbia, nao wakamfuata na kumkamata, wakamkata vidole vyake gumba vya mikono na vya miguu.
7 O zaman Adoni-Bezek şöyle dedi: “Elleriyle ayaklarının başparmakları kesilmiş yetmiş kral, soframdan düşen kırıntıları toplayıp yerdi. Tanrı bana onlara yaptıklarımın karşılığını veriyor.” Adoni-Bezek'i Yeruşalim'e götürdüler; orada öldü.
Ndipo Adoni-Bezeki akasema, “Nimewatendea wafalme sabini kama nilivyotendewa na kuwalisha makombo ya chakula chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa haya, kama yale niliyowatendea.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
8 Yahudaoğulları Yeruşalim'e saldırıp kenti aldılar; halkı kılıçtan geçirerek kenti ateşe verdiler.
Watu wa Yuda wakashambulia pia Yerusalemu na kuiteka. Wakaupiga mji kwa upanga na kuuchoma kwa moto.
9 Sonra dağlık bölgede, Negev'de ve Şefela'da yaşayan Kenanlılar'la savaşmak üzere güneye yöneldiler.
Baada ya hayo, watu wa Yuda wakateremka kupigana na Wakanaani walioishi katika nchi ya vilima, yaani, Negebu na nchi chini ya vilima vya magharibi.
10 Eski adı Kiryat-Arba olan Hevron'da yaşayan Kenanlılar'ın üzerine yürüyerek Şeşay, Ahiman ve Talmay'ı yenilgiye uğrattılar.
Yuda wakakabiliana na Wakanaani walioishi Hebroni (ambayo hapo kwanza iliitwa Kiriath-Arba) na kuwashinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
11 Oradan eski adı Kiryat-Sefer olan Devir Kenti halkının üzerine yürüdüler.
Kutoka huko wakasonga mbele kukabiliana na watu walioishi Debiri (ambao hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi.)
12 Kalev, “Kiryat-Sefer halkını yenip orayı ele geçirene kızım Aksa'yı eş olarak vereceğim” dedi.
Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.”
13 Kenti Kalev'in küçük kardeşi Kenaz'ın oğlu Otniel ele geçirdi. Bunun üzerine Kalev kızı Aksa'yı ona eş olarak verdi.
Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, akawashinda, kwa hiyo Kalebu akamtoa binti yake Aksa akaolewa naye.
14 Kız Otniel'in yanına varınca, onu babasından bir tarla istemeye zorladı. Kalev, eşeğinden inen kızına, “Bir isteğin mi var?” diye sordu.
Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”
15 Kız, “Bana bir armağan ver” dedi, “Madem Negev'deki toprakları bana verdin, su kaynaklarını da ver.” Böylece Kalev yukarı ve aşağı su kaynaklarını ona verdi.
Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Ndipo Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.
16 Musa'nın kayınbabasının torunları olan Kenliler, Yahudaoğulları'yla birlikte Hurma Kenti'nden ayrılıp Arat'ın güneyindeki Yahuda Çölü'nde yaşamaya gittiler.
Wazao wa yule Mkeni, baba mkwe wa Mose, wakapanda pamoja na watu wa Yuda kutoka Mji wa Mitende, wakaenda kuishi miongoni mwa watu wa jangwa ya Yuda huko Negebu karibu na mji wa Aradi.
17 Bundan sonra Yahudaoğulları, kardeşleri Şimonoğulları'yla birlikte gidip Sefat Kenti'nde oturan Kenanlılar'ı yenilgiye uğrattılar. Kenti tümüyle yıktılar ve oraya Horma adını verdiler.
Basi watu wa Yuda wakaenda na Wasimeoni ndugu zao kushambulia Wakanaani waishio Sefathi, nao wakauangamiza huo mji kabisa. Kwa hiyo huo mji ukaitwa Horma
18 Yahudaoğulları Gazze'yi, Aşkelon'u, Ekron'u ve bunlara bağlı toprakları da ele geçirdiler.
Watu wa Yuda wakatwaa pia Gaza, Ashkeloni na Ekroni, kila mji na vijiji vyake vinavyouzunguka.
19 RAB Yahudaoğulları'yla birlikteydi. Yahudaoğulları dağlık bölgeyi ele geçirdilerse de ovada yaşayan halkı kovamadılar. Çünkü bunların demirden savaş arabaları vardı.
Bwana alikuwa pamoja na watu wa Yuda. Wakaimiliki nchi ya vilima, lakini hawakuweza kuwafukuza watu waliokaa katika hiyo tambarare, kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
20 Musa'nın sözü uyarınca Hevron'u Kalev'e verdiler. Kalev de Anak'ın üç torununu oradan sürdü.
Kama vile Mose alivyoahidi, Kalebu alipewa Hebroni, naye akawafukuza wana watatu wa Anaki.
21 Bununla birlikte Benyaminoğulları Yeruşalim'de yaşayan Yevuslular'ı kovmadılar. Yevuslular bugün de Yeruşalim'de Benyaminoğulları'yla birlikte yaşıyorlar.
Hata hivyo, Wabenyamini walishindwa kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wanaishi Yerusalemu; hivyo hadi leo Wayebusi huishi humo pamoja na Wabenyamini.
22 Yusuf'un soyundan gelenler Beytel'in üzerine yürüdüler. RAB onlarla birlikteydi.
Basi nyumba ya Yosefu wakashambulia Betheli, naye Bwana alikuwa pamoja nao.
23 Eski adı Luz olan Beytel Kenti hakkında bilgi toplamak için gönderdikleri casuslar kentten çıkan bir adam gördüler. Ona, “Kentin girişini bize gösterirsen, sana iyi davranırız” dediler.
Walipotuma watu kwenda kupeleleza Betheli (ambao hapo kwanza uliitwa Luzu),
wale wapelelezi wakaona mtu anatoka mjini, nao wakamwambia, “Tuonyeshe jinsi ya kuingia mjini nasi tutakutendea wema.”
25 Kentin girişini gösteren adamla ailesini serbest bıraktılar, kent halkını ise kılıçtan geçirdiler.
Hivyo akawaonyesha, nao wakaupiga mji kwa upanga lakini wakamhifadhi hai yule mtu na jamaa yake yote.
26 Adam Hitit topraklarına göç ederek Luz adında bir kent kurdu; kent bugün de bu adla anılıyor.
Yule mtu akaenda hadi nchi ya Wahiti, ambapo aliujenga mji na kuuita Luzu, ambao ndio jina lake hadi leo.
27 Manaşşeoğulları Beytşean, Taanak, Dor, Yivleam, Megiddo ve bunların çevre köylerindeki halkı kovmadı. Çünkü Kenanlılar bu topraklarda kalmakta kararlıydı.
Lakini Manase hawakuwafukuza watu wa Beth-Shani na vijiji vyake, au watu wa Taanaki na vijiji vyake, au watu wa Dori na vijiji vyake, au watu wa Ibleamu na vijiji vyake, au watu wa Megido na vijiji vyake, lakini Wakanaani waliazimu kuishi katika nchi ile.
28 İsrailliler Kenan halkını tümüyle kovmadılar; ama zamanla güçlenince onları angaryasına çalıştırdılar.
Israeli walipopata nguvu, wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa, lakini kamwe hawakuwafukuza watoke kabisa.
29 Efrayimoğulları Gezer'de yaşayan Kenanlılar'ı buradan sürmediler. Kenanlılar Gezer'de İsrailliler'in arasında yaşadılar.
Wala Efraimu hawakuwafukuza kabisa Wakanaani walioishi Gezeri, bali Wakanaani waliendelea kuishi humo miongoni mwao.
30 Zevulun da Kitron ve Nahalol halklarını kovmadı. İsrailliler arasında yaşayan bu Kenanlılar angarya işler yaptılar.
Vivyo hivyo Zabuloni hawakuwafukuza Wakanaani walioishi huko Kitroni, wala walioishi Nahaloli, ambao walibaki miongoni mwao; bali waliwatia katika kazi ya kulazimishwa.
31 Aşeroğulları'na gelince, onlar da Akko, Sayda, Ahlav, Akziv, Helba, Afek ve Rehov halklarını kovmadılar.
Wala Asheri hawakuwafukuza wale walioishi huko Ako, Sidoni, Alabu, Akzibu, Helba, Afeki wala Rehobu
32 Bu topraklardaki Kenanlılar'ı kovmayıp onlarla birlikte yaşadılar.
na kwa sababu ya jambo hili Waasheri wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi.
33 Naftali Beytşemeş ve Beytanat halkını kovmadı. Buraların halkı olan Kenanlılar'la birlikte yaşayıp onları angaryasına çalıştırdı.
Wala Naftali hawakuwafukuza wale walioishi Beth-Shemeshi wala wale walioishi Beth-Anathi; lakini Naftali nao pia wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi, nao wale walioishi Beth-Shemeshi na Beth-Anathi wakawa watumishi wao katika kazi ya kulazimishwa.
34 Amorlular Danoğulları'nı ovaya inmekten alıkoyarak dağlık bölgelerde tuttular.
Waamori wakawazuilia Wadani kwenye nchi ya vilima, kwa maana hawakuwaacha washuke kuingia kwenye sehemu tambarare.
35 Amorlular Heres Dağı'nda, Ayalon'da ve Şaalvim'de kalmakta kararlıydılar. Yusuf'un torunları güçlenince onları angaryasına çalıştırmaya başladılar.
Waamori pia wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi, katika Aiyaloni na Shaalbimu, lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawalemea, nao wakashindwa hata wakalazimika kuingia katika kazi ya kulazimishwa.
36 Amorlular'ın sınırı Akrep Geçidi'nden Sela'ya ve ötesine uzanıyordu.
Mpaka wa Waamori ulikuwa kuanzia Genge la Akrabimu, kuendelea hadi Sela na kuelekea juu.

< Hâkimler 1 >