< Eyüp 10 >

1 “Yaşamımdan usandım, Özgürce yakınacak, İçimdeki acıyla konuşacağım.
Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
2 Tanrı'ya: Beni suçlama diyeceğim, Ama söyle, niçin benimle çekişiyorsun.
Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
3 Hoşuna mı gidiyor gaddarlık etmek, Kendi ellerinin emeğini reddedip Kötülerin tasarılarını onaylamak?
ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
4 Sende insan gözü mü var? İnsanın gördüğü gibi mi görüyorsun?
Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
5 Günlerin ölümlü birinin günleri gibi, Yılların insanın yılları gibi mi ki,
Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
6 Suçumu arıyor, Günahımı araştırıyorsun?
hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
7 Kötü olmadığımı, Senin elinden beni kimsenin kurtaramayacağını biliyorsun.
ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
8 “Senin ellerin bana biçim verdi, beni yarattı, Şimdi dönüp beni yok mu edeceksin?
Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
9 Lütfen anımsa, balçık gibi bana sen biçim verdin, Beni yine toprağa mı döndüreceksin?
Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
10 Beni süt gibi dökmedin mi, Peynir gibi katılaştırmadın mı?
Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
11 Bana et ve deri giydirdin, Beni kemiklerle, sinirlerle ördün.
Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
12 Bana yaşam verdin, sevgi gösterdin, İlgin ruhumu korudu.
Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
13 “Ama bunları yüreğinde gizledin, Biliyorum aklındakini:
Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
14 Günah işleseydim, beni gözlerdin, Suçumu cezasız bırakmazdın.
kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
15 Suçluysam, vay başıma! Suçsuzken bile başımı kaldıramıyorum, Çünkü utanç doluyum, çaresizim.
Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
16 Başımı kaldırsam, aslan gibi beni avlar, Şaşılası gücünü yine gösterirsin üstümde.
Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
17 Bana karşı yeni tanıklar çıkarır, Öfkeni artırırsın. Orduların dalga dalga üzerime geliyor.
Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
18 “Niçin doğmama izin verdin? Keşke ölseydim, hiçbir göz beni görmeden!
Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
19 Hiç var olmamış olurdum, Rahimden mezara taşınırdım.
Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
20 Birkaç günlük ömrüm kalmadı mı? Beni rahat bırak da biraz yüzüm gülsün;
Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
21 Dönüşü olmayan yere gitmeden önce, Karanlık ve ölüm gölgesi diyarına,
kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
22 Zifiri karanlık diyarına, Ölüm gölgesi, kargaşa diyarına, Aydınlığın karanlığı andırdığı yere.”
ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”

< Eyüp 10 >