< Yeremya 6 >

1 “Güvenliğiniz için kaçın, ey Benyamin halkı! Yeruşalim'den kaçın! Tekoa'da boru çalın! Beythakkerem'e bir işaret koyun. Çünkü kuzeyden bir felaket, Büyük bir yıkım gelecek gibi görünüyor.
“Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini! Kimbieni kutoka Yerusalemu! Pigeni tarumbeta katika Tekoa! Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu! Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini, na uharibifu wa kutisha.
2 Siyon kızını, o güzel, narin kızı yok edeceğim.
Nitamwangamiza Binti Sayuni, aliye mzuri sana na mwororo.
3 Çobanlar sürüleriyle ona geliyor, Çevresinde çadırlarını kuracaklar. Herkes kendi sürüsünü otlatacak.”
Wachungaji pamoja na makundi yao watakuja dhidi yake; watapiga mahema yao kumzunguka, kila mmoja akichunga kundi lake mwenyewe.”
4 “Yeruşalim'e karşı savaş hazırlığı yapın! Kalkın, öğleyin saldırıya geçelim! Vay halimize, gün kararıyor! Akşamın gölgeleri gitgide uzuyor.
“Jiandaeni kwa vita dhidi yake! Inukeni tumshambulie mchana! Lakini, ole wetu, mchana unaisha, na vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu.
5 Haydi, gece saldırıya geçelim, Kentin kalelerini yerle bir edelim.”
Kwa hiyo inukeni, tufanye mashambulizi usiku, na kuharibu ngome zake!”
6 Her Şeye Egemen RAB diyor ki, “Ağaçları kesin, Yeruşalim'e karşı kuşatma rampaları yapın. Bu kent cezalandırılmalı, İçinde zorbalıktan başka bir şey yok.
Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Kateni miti mjenge boma kuzunguka Yerusalemu. Mji huu ni lazima uadhibiwe, umejazwa na uonevu.
7 Kuyu suyunu nasıl taze tutuyorsa, Yeruşalim de kötülüğünü öyle taze tutuyor. Şiddet ve yıkım yankılanıyor orada, Karşımda hep hastalık ve yaralar var.
Kama vile kisima kinavyomwaga maji yake, ndivyo anavyomwaga uovu wake. Ukatili na maangamizi yasikika ndani yake, ugonjwa wake na majeraha yake viko mbele yangu daima.
8 Uyarılara kulak ver, ey Yeruşalim! Yoksa seni bırakacağım, Seni bir viraneye, Oturulmaz bir ülkeye çevireceğim.”
Pokea onyo, ee Yerusalemu, la sivyo nitageukia mbali nawe na kuifanya nchi yako kuwa ukiwa, asiweze mtu kuishi ndani yake.”
9 Her Şeye Egemen RAB diyor ki, “Asmadan nasıl üzüm toplanırsa, İsrail halkından geride kalanları da öyle toplayacaklar. Üzüm toplayan biri gibi Elini yine asma dallarına uzat.”
Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Wao na wayakusanye mabaki ya Israeli kwa uangalifu kama kwenye mzabibu; pitisha mkono wako kwenye matawi tena, kama yeye avunaye zabibu.”
10 İşitsinler diye kiminle konuşayım, Kimi uyarayım? Kulakları tıkalı, işitemiyorlar. RAB'bin sözünü aşağılıyor, Ondan hoşlanmıyorlar.
Niseme na nani na kumpa onyo? Ni nani atakayenisikiliza mimi? Masikio yao yameziba, kwa hiyo hawawezi kusikia. Neno la Bwana ni chukizo kwao, hawalifurahii.
11 Bu yüzden RAB'bin öfkesiyle doluyum, Kendimi tutmaktan yoruldum. “Sokaktaki çocukların, Toplanan gençlerin üzerine boşalt öfkeni. Nasıl olsa karı da koca da, Yaşlı da yıllarca yaşamış olan da kurtulamayacak.
Lakini nimejaa ghadhabu ya Bwana, nami siwezi kuizuia. “Wamwagie watoto walioko barabarani, na juu ya vijana waume waliokusanyika; mume na mke watakumbwa pamoja ndani yake, hata nao wazee waliolemewa na miaka.
12 Evleri, tarlaları, karıları Başkalarına verilecek, Çünkü ülkede yaşayanlara karşı Elimi kaldıracağım” diyor RAB.
Nyumba zao zitapewa watu wengine, pamoja na mashamba yao na wake zao, nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya wale waishio katika nchi,” asema Bwana.
13 “Küçük büyük herkes kazanç peşinde, Peygamberler, kâhinler, hepsi halkı aldatıyor.
“Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa, wote wana tamaa ya kupata faida zaidi; manabii na makuhani wanafanana, wote wanafanya udanganyifu.
14 Esenlik yokken, ‘Esenlik, esenlik’ diyerek Halkımın yarasını sözde iyileştirdiler.
Wanafunga majeraha ya watu wangu bila uangalifu. Wanasema, ‘Amani, amani,’ wakati hakuna amani.
15 Yaptıkları iğrençliklerden utandılar mı? Hayır, ne utanması? Kızarıp bozarmanın ne olduğunu bile bilmiyorlar. Bu yüzden onlar da düşenlerin arasında yer alacak, Onları cezalandırdığımda sendeleyip düşecekler” diyor RAB.
Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao inayochukiza mno? Hapana, hawana aibu hata kidogo; hawajui hata kuona haya. Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka, watashushwa chini nitakapowaadhibu,” asema Bwana.
16 RAB diyor ki, “Yol kavşaklarında durup bakın, Eski yolları sorun, İyi yol nerede, öğrenin, O yolda yürüyün, Canlarınız rahata kavuşur. Ama onlar, ‘O yolda yürümeyiz’ dediler.
Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Simama kwenye njia panda utazame, ulizia mapito ya zamani, ulizia wapi ilipo njia nzuri, uifuate hiyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. Lakini ninyi mlisema, ‘Hatutaipita hiyo.’
17 Size bekçiler atayıp, ‘Boru sesini dinleyin’ dedim, Ama onlar, ‘Dinlemeyiz’ dediler.
Niliweka walinzi juu yenu na kusema, ‘Sikieni sauti ya tarumbeta!’ Lakini mkasema, ‘Hatutasikiliza.’
18 Bundan ötürü, ey uluslar, Başlarına neler geleceğini işitin! Sen de anla, ey topluluk!
Kwa hiyo sikilizeni, enyi mataifa, angalieni, enyi mashahidi, lile litakalowatokea.
19 Dinle, ey yeryüzü! Bu halkın üzerine felaket, Kendi kurduğu düzenin sonucunu getirmek üzereyim. Çünkü sözlerime kulak asmadılar, Kutsal Yasam'ı reddettiler.
Sikia, ee nchi: Ninaleta maafa juu ya watu hawa, matunda ya mipango yao, kwa sababu hawakusikiliza maneno yangu na wameikataa sheria yangu.
20 Neden bana Saba'dan günnük, Uzak bir ülkeden güzel kokulu kamış getiriliyor? Yakmalık sunularınızı kabul etmiyorum, Kurbanlarınızdan hoşnut değilim.”
Unanifaa nini uvumba kutoka Sheba, au udi wa harufu nzuri kutoka nchi ya mbali? Sadaka zako za kuteketezwa hazikubaliki, dhabihu zako hazinifurahishi mimi.”
21 Bu yüzden RAB diyor ki, “Bu halkın önüne tökezler koyacağım, Babalar da oğullar da Tökezleyip birlikte düşecek, Komşu dostuyla birlikte yok olacak.”
Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Nitaweka vikwazo mbele ya watu hawa. Baba na wana wao watajikwaa juu yake, majirani na marafiki wataangamia.”
22 RAB diyor ki, “İşte kuzeyden bir ordu geliyor. Dünyanın uçlarından Büyük bir ulus harekete geçiyor.
Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Tazama, jeshi linakuja kutoka nchi ya kaskazini, taifa kubwa linaamshwa kutoka miisho ya dunia.
23 Yay, pala kuşanmışlar, Gaddar ve acımasızlar. Atlara binmiş gelirken, Kükreyen denizi andırıyor sesleri. Savaşa hazır savaşçılar Karşına dizilecekler, ey Siyon kızı!”
Wamejifunga pinde na mkuki, ni wakatili na hawana huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao. Wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Sayuni.”
24 Haberlerini aldık, Ellerimizde derman kalmadı. Doğuran kadın gibi Üzüntü, sancı sardı bizi.
Tumesikia taarifa zao, nayo mikono yetu imelegea. Uchungu umetushika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
25 Kırlara çıkmayın, Yolda yürümeyin! Düşmanın kılıcı orada, Her yer dehşet içinde.
Usitoke kwenda mashambani au kutembea barabarani, kwa kuwa adui ana upanga, na kuna vitisho kila upande.
26 Ey halkım, çula sarın, Kül içinde yuvarlan. Biricik oğul için yas tutar gibi Acı acı dövün. Çünkü yok edici ansızın gelecek üzerimize.
Enyi watu wangu, vaeni magunia mjivingirishe kwenye majivu, ombolezeni kwa kilio cha uchungu kama amliliaye mwana pekee, kwa maana ghafula mharabu atatujia.
27 “Seni halkımı deneyesin diye atadım, Öyle ki, onları tanıyıp yollarını sınayasın.
“Nimekufanya wewe kuwa kitu cha kujaribu chuma, nao watu wangu kama mawe yenye madini, ili upate kuzijua na kuzijaribu njia zao.
28 Hepsi de çok dikbaşlı, Onu bunu çekiştirerek dolaşan insanlardır, Tunç kadar, demir kadar katıdırlar. Hepsi baştan çıkmıştır.
Wote ni waasi sugu, wakienda huku na huko kusengenya. Wao ni shaba na chuma, wote wanatenda upotovu.
29 Körük üfürdükçe üfürüyor, Kurşunu ateşte eritiyor, Ama boşunadır yapılan işlem, Çünkü kötüler arınmıyor.
Mivuo inavuma kwa nguvu, kinachoungua kwa huo moto ni risasi, lakini pamoja na kusafisha kote huku ni bure; waovu hawaondolewi.
30 Onlara gümüş artığı denecek, Çünkü RAB onları reddetti.”
Wanaitwa fedha iliyokataliwa, kwa sababu Bwana amewakataa.”

< Yeremya 6 >