< Yeremya 3 >

1 “Diyelim ki, bir adam karısını boşar, Kadın da onu bırakıp başka biriyle evlenir. Adam bir daha o kadına döner mi? Bu davranış ülkeyi büsbütün kirletmez mi? Oysa sen pek çok oynaşla fahişelik ettin, Yine bana mı dönmek istiyorsun?” diyor RAB.
“Kama mtu akimpa talaka mkewe, naye akamwacha na akaolewa na mtu mwingine, je, huyo mume aweza kumrudia tena? Je, hiyo nchi haitanajisika kabisa? Lakini umeishi kama kahaba na wapenzi wengi: je, sasa utanirudia tena?” asema Bwana.
2 “Çıplak tepelere bak da gör. Sevişmediğin yer mi kaldı? Çölde yaşayan bedevi gibi Yol kenarlarında oynaşlarını bekleyip durdun. Fahişeliğinle, kötülüklerinle ülkeyi kirlettin.
“Inua macho utazame miinuko iliyo kame na uone. Je, pana mahali ambapo hawajalala nawe? Uliketi kando ya barabara ukiwasubiri wapenzi, ukakaa kama yeye ahamahamaye jangwani. Umeinajisi nchi kwa ukahaba wako na uovu wako.
3 Bu yüzden yağmurların ardı kesildi, Son yağmur yağmadı. Yüzsüz bir fahişeye benzedin, Utanç duymak istemedin.
Kwa hiyo mvua imezuiliwa, nazo mvua za vuli hazikunyesha. Hata hivyo, una uso usio na haya kama wa kahaba; unakataa kutahayari kwa aibu.
4 ‘Baba, gençliğimden beri Benim dostumsun’ diye az önce bana seslenmedin mi?
Je, wewe hujaniita hivi punde tu: ‘Baba yangu, rafiki yangu tangu ujana wangu,
5 ‘Sonsuza dek kızgın mı kalacaksın? Öfken sonsuza dek mi sürecek?’ Evet, böyle konuşuyor, Ama elinden gelen her kötülüğü yapıyorsun.”
je, utakasirika siku zote? Je, ghadhabu yako itaendelea milele?’ Hivi ndivyo unavyozungumza, lakini unafanya maovu yote uwezayo.”
6 Kral Yoşiya döneminde RAB bana, “Dönek İsrail'in yaptığını gördün mü?” dedi, “Her yüksek tepenin üzerine, her bol yapraklı ağacın altına gidip fahişelik etti.
Wakati wa utawala wa Mfalme Yosia, Bwana aliniambia, “Umeona kile Israeli asiye mwaminifu amekifanya? Amepanda juu ya kila kilima kirefu, na chini ya kila mti uliotanda na amefanya uzinzi huko.
7 Bütün bunları yaptıktan sonra bana geri döneceğini düşündüm, ama dönmedi. Hain kızkardeşi Yahuda da gördü bunları.
Mimi nilifikiri kuwa baada ya kuyafanya yote haya angelinirudia, lakini hakurudi, naye dada yake Yuda mdanganyifu aliona hili.
8 Fahişeliği yüzünden dönek İsrail'i boşayıp ona boşanma belgesini verdiğim halde, kızkardeşi hain Yahuda'nın hiç korkmadığını, gidip fahişelik ettiğini gördüm.
Nilimpa Israeli asiye mwaminifu hati yake ya talaka, na kumfukuza kwa ajili ya uzinzi wake wote. Hata hivyo nikaona kuwa Yuda dada yake mdanganyifu hakuogopa. Yeye pia alitoka na kufanya uzinzi.
9 Hiç umursamadan fahişeliğiyle ülkeyi kirletti; taşla, ağaçla zina etti.
Kwa sababu uasherati wa Israeli haukuwa kitu kwake, Yuda aliinajisi nchi kwa kuzini na mawe na miti.
10 Bütün bunlara karşın, hain kızkardeşi Yahuda içtenlikle değil, göstermelik olarak bana döndü.” Böyle diyor RAB.
Pamoja na hayo yote, Yuda dada yake mdanganyifu hakunirudia kwa moyo wake wote, bali kwa kujifanya tu,” asema Bwana.
11 RAB bana, “Dönek İsrail hain Yahuda'dan daha doğru olduğunu gösterdi” dedi,
Bwana akaniambia, “Israeli asiye mwaminifu ana haki kuliko Yuda mdanganyifu.
12 “Git, bu sözleri kuzeye duyur. De ki, “‘Ey dönek İsrail, geri dön’ diyor RAB. ‘Size artık öfkeyle bakmayacağım, Çünkü ben sevecenim’ diyor RAB. ‘Öfkemi sonsuza dek sürdürmem.
Nenda, ukatangaze ujumbe huu kuelekea kaskazini: “‘Rudi, Israeli usiye mwaminifu,’ asema Bwana, ‘sitakutazama tena kwa uso uliokunjamana, kwa kuwa mimi ni mwenye huruma,’ asema Bwana, ‘Sitashika hasira yangu milele.
13 Ancak suçunu kabul et: Tanrın RAB'be başkaldırdın, Her bol yapraklı ağacın altında Sevgini yabancı ilahlarla paylaştın, Beni dinlemedin.’” Böyle diyor RAB.
Ungama dhambi zako tu: kwamba umemwasi Bwana Mungu wako, umetapanya wema wako kwa miungu ya kigeni chini ya kila mti unaotanda, nawe hukunitii mimi,’” asema Bwana.
14 “Geri dön, ey dönek halk” diyor RAB, “Çünkü kocan benim. Birinizi kentten, ikinizi bir boydan alıp Siyon'a geri getireceğim.
“Rudini, enyi watu msio waaminifu, kwa kuwa mimi ni mume wenu,” asema Bwana. “Nitawachagua ninyi, mmoja kutoka kwenye mji, na wawili kutoka kwenye ukoo, nami nitawaleta Sayuni.
15 Size gönlüme göre çobanlar vereceğim; sizi bilgiyle, sağduyuyla güdecekler.
Kisha nitawapeni wachungaji wanipendezao moyo wangu, ambao watawaongoza kwa maarifa na ufahamu.
16 Ülkede büyüyüp sayıca çoğaldığınız günlerde” diyor RAB, “Halk artık, ‘RAB'bin Antlaşma Sandığı’ demeyecek. Sandık bir daha kimsenin aklına gelmeyecek; anımsanmayacak, özlenmeyecek, bir yenisi de yapılmayacak.
Katika siku hizo, idadi yenu itakapokuwa imeongezeka sana katika nchi, watu hawatasema tena, ‘Sanduku la Agano la Bwana,’” asema Bwana. “Halitaingia tena kwenye mawazo yao wala kukumbukwa, hawatalihitaji wala halitatengenezwa jingine.
17 O zaman Yeruşalim'e, ‘RAB'bin Tahtı’ diyecekler. RAB'bin adını onurlandırmak için bütün uluslar Yeruşalim'de toplanacak. Bundan böyle kötü yüreklerinin inadı uyarınca davranmayacaklar.
Wakati huo, wataita Yerusalemu kuwa Kiti cha Enzi cha Bwana, nayo mataifa yote watakusanyika Yerusalemu kuliheshimu jina la Bwana. Hawatafuata tena ukaidi wa mioyo yao miovu.
18 O günlerde Yahuda halkıyla İsrail halkı kuzeyde bir ülkeden birlikte yürüyecek, atalarına mülk olarak vermiş olduğum ülkede bir araya gelecekler.
Katika siku hizo, nyumba ya Yuda itaungana na nyumba ya Israeli, wao kwa pamoja watakuja kutoka nchi ya kaskazini hadi nchi niliyowapa baba zenu kama urithi.
19 “Ben RAB, demiştim ki, ‘Ne kadar isterdim Seni çocuklarımdan saymayı; Sana güzel ülkeyi, Ulusların en güzel mülkünü vermeyi! Bana baba diyeceğini, Benden hiç ayrılmayacağını düşündüm.
“Mimi mwenyewe nilisema, “‘Tazama jinsi nitakavyowatunza kwa furaha kama wana na kuwapa nchi nzuri, urithi ulio mzuri kuliko wa taifa jingine lolote.’ Nilidhani mngeniita ‘Baba,’ na msingegeuka, mkaacha kunifuata.
20 Ama bir kadın kocasına nasıl ihanet ederse, Sen de bana öyle ihanet ettin, ey İsrail halkı!’” Böyle diyor RAB.
Lakini kama mwanamke asiye mwaminifu kwa mumewe, vivyo hivyo mmekosa uaminifu kwangu pia, ee nyumba ya Israeli,” asema Bwana.
21 Çıplak tepelerde bir ses duyuluyor, İsrail halkının ağlayışı ve yakarışı. Çünkü doğru yoldan saptılar, Tanrıları RAB'bi unuttular.
Kilio kinasikika juu ya miinuko iliyo kame, kulia na kuomboleza kwa watu wa Israeli, kwa sababu wamepotoka katika njia zao na wamemsahau Bwana Mungu wao.
22 “Geri dönün, ey dönek çocuklar, Dönekliğinizi iyileştireyim.” Halk, “İşte buradayız, sana geliyoruz!” diyor, “Çünkü Tanrımız RAB sensin.
“Rudini, enyi watu msio waaminifu, nami nitawaponya ukengeufu wenu.” “Naam, tutakuja kwako, kwa maana wewe ni Bwana Mungu wetu.
23 Kuşkusuz dağlardan, Tepelerden gelen tapınma sesleri aldatıcıdır. Kuşkusuz İsrail'in kurtuluşu Tanrımız RAB'dedir.
Hakika zile ghasia za kuabudu sanamu kwenye vilima na milimani ni udanganyifu; hakika katika Bwana, Mungu wetu, uko wokovu wa Israeli.
24 Gençliğimizden bu yana Atalarımızın emeğinin ürününü, Davarlarını, sığırlarını, Oğullarını, kızlarını Utanılası putlar yedi.
Tangu ujana wetu miungu ya aibu imeyala matunda ya kazi za baba zetu: makundi yao ya kondoo na ngʼombe, wana wao na binti zao.
25 Utanç içinde yatalım, Rezilliğimiz bizi örtsün! Çünkü biz de atalarımız da Gençliğimizden bu yana Tanrımız RAB'be karşı günah işledik, Tanrımız RAB'bin sesine kulak asmadık.”
Sisi na tulale chini katika aibu yetu, na fedheha yetu itufunike. Tumetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wetu, sisi na mababa zetu; tangu ujana wetu hadi leo hatukumtii Bwana Mungu wetu.”

< Yeremya 3 >