< Yeşaya 8 >

1 RAB bana şöyle dedi: “Büyük bir levha alıp okunaklı harflerle üzerine, ‘Maher-Şalal-Haş-Baz’ yaz.
Bwana akaniambia, “Chukua gombo kubwa, uandike juu yake kwa kalamu ya kawaida jina: Maher-Shalal-Hash-Bazi.
2 Kâhin Uriya ile Yeverekya oğlu Zekeriya'yı kendime güvenilir tanık seçiyorum.”
Nami nitawaita kuhani Uria, na Zekaria mwana wa Yeberekia kama mashahidi wangu waaminifu.”
3 Peygamber olan karım bundan bir süre sonra gebe kaldı ve bir erkek çocuk doğurdu. RAB bana, “Adını ‘Maher-Şalal-Haş-Baz’ koy” dedi,
Kisha nikaenda kwa nabii mke, naye akapata mimba, akazaa mwana. Kisha Bwana akaniambia, “Mwite huyo mtoto Maher-Shalal-Hash-Bazi.
4 “Çocuk daha ‘Anne, baba’ demesini öğrenmeden, Şam'ın serveti ve Samiriye'nin ganimeti Asur Kralı'na götürülecek.”
Kabla mtoto hajaweza kusema ‘Baba yangu’ au ‘Mama yangu,’ utajiri wa Dameski na nyara za Samaria zitachukuliwa na mfalme wa Ashuru.”
5 RAB bana yine seslenip dedi ki,
Bwana akasema nami tena:
6 “Bu halk usul usul akan Şiloah sularını reddettiği, Resin'le Remalya'nın oğluyla mutlu olduğu için,
“Kwa sababu watu hawa wamekataa maji ya Shilo yatiririkayo taratibu wakamfurahia Resini na mwana wa Remalia,
7 ben Rab, Fırat'ın kabaran güçlü sularını –bütün dehşetiyle Asur Kralı'nı– üzerlerine salacağım. Yatağından taşan ırmak, kıyılarını su altında bırakacak.
kwa hiyo Bwana yu karibu kuleta dhidi yao mafuriko makubwa ya Mto: yaani mfalme wa Ashuru na fahari yake yote. Yatafurika juu ya mifereji yake yote, yatamwagikia juu ya kingo zake zote,
8 Yahuda'yı kaplayan sular her şeyi silip süpürerek adam boyu yükselecek, ülkeni boydan boya dolduracak, ey İmmanuel!”
na kufika hadi Yuda, yakizunguka kwa kasi juu yake, yakipita katikati na yakifika hadi shingoni. Mabawa yake yaliyokunjuliwa yatafunika upana wa nchi yako, Ee Imanueli!”
9 Ey halklar, yıkıma, bozguna uğrayacaksınız. Yeryüzünün en uç köşeleri, kulak verin. Savaşmaya, bozguna uğramaya hazırlanın. Evet, savaşa ve bozguna hazır olun.
Inueni kilio cha vita, enyi mataifa, na mkavunjwevunjwe! Sikilizeni, enyi nyote nchi za mbali. Jiandaeni kwa vita, nanyi mkavunjwevunjwe! Jiandaeni kwa vita, nanyi mkavunjwevunjwe!
10 İstediğinizi tasarlayın, hepsi boşa gidecek. İstediğiniz kadar konuşun, hiçbiri gerçekleşmeyecek. Çünkü Tanrı bizimledir.
Wekeni mikakati yenu, lakini itashindwa; fanyeni mipango yenu, lakini haitafanikiwa, kwa maana Mungu yu pamoja nasi.
11 RAB beni halkın tuttuğu yoldan gitmeme konusunda şiddetle uyararak şöyle dedi:
Bwana alisema nami mkono wake wenye nguvu ukiwa juu yangu, akinionya nisifuate njia za taifa hili. Akasema:
12 “Onların entrika dediği her şeye Siz entrika demeyin; Onların korktuğundan korkmayın, yılmayın.
“Usiite fitina kila kitu ambacho watu hawa hukiita fitina, usiogope kile wanachokiogopa, wala usikihofu.
13 “Her Şeye Egemen RAB'bi kutsal sayın. Korkunuz, yılgınız O'ndan olsun.
Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye peke yake ikupasaye kumheshimu kuwa mtakatifu, ndiye peke yake utakayemwogopa, ndiye peke yake utakayemhofu,
14 Tapınak O olacak. İsrail'in iki krallığı içinse Sürçme taşı ve tökezleme kayası, Yeruşalim'de yaşayanlar için Kapan ve tuzak olacak.
naye atakuwa mahali patakatifu; lakini kwa nyumba zote mbili za Israeli atakuwa jiwe lile linalosababisha watu kujikwaa na mwamba wa kuwaangusha. Kwa watu wa Yerusalemu, atakuwa mtego na tanzi.
15 Birçokları sendeleyip düşecek, parçalanacak, Tuzağa düşüp ele geçecek.”
Wengi wao watajikwaa; wataanguka na kuvunjika, watategwa na kunaswa.”
16 Ya RAB, öğrencilerim arasında bildirimi koru, Öğretimi mühürle!
Funga ushuhuda na kutia muhuri sheria miongoni mwa wanafunzi wangu.
17 Kendini Yakup'un soyundan gizleyen RAB'bi özlemle bekliyorum, umudum O'nda.
Nitamngojea Bwana, ambaye ameificha nyumba ya Yakobo uso wake. Nitaliweka tumaini langu kwake.
18 Ben ve RAB'bin bana verdiği çocuklar, Siyon Dağı'nda oturan Her Şeye Egemen RAB'bin İsrail'deki belirtileri ve işaretleriyiz.
Niko hapa, pamoja na watoto ambao Bwana amenipa. Sisi ni ishara na mfano wake katika Israeli, kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayeishi juu ya Mlima Sayuni.
19 Birileri size, “Fısıldaşıp mırıldanan medyumlarla ruh çağıranlara danışın” dediğinde, “Halk kendi Tanrısı'na danışmaz mı; yaşayanlar için ölülere mi danışılır?” deyin.
Wakati watu wanapowaambia ninyi kutafuta ushauri kwa waaguzi na wenye kuongea na mizimu, ambao hunongʼona na kunungʼunika, je, watu wasingeuliza kwa Mungu wao? Kwa nini watake shauri kwa wafu kwa ajili ya walio hai?
20 Tanrı'nın öğretisine ve bildirisine dönmek gerek! Böyle düşünmezlerse, onlar için hiç şafak sökmeyecek.
Kwa sheria na kwa ushuhuda! Kama hawatasema sawasawa na neno hili, hawana mwanga wa mapambazuko.
21 Aç ve çaresiz, ülkede dolanıp duracaklar. Aç kalınca öfkelenip krallarına, Tanrıları'na lanet edecekler. Yukarıya da
Watazunguka katika nchi yote, wakiwa na dhiki na njaa. Watakapotaabika kwa njaa, watapatwa na hasira kali, nao, wakiwa wanatazama juu, watamlaani mfalme wao na Mungu wao.
22 dünyaya da baksalar sıkıntıdan, karanlıktan, korkunç karanlıktan başka bir şey görmeyecekler. Kovulacakları yer koyu karanlıktır.
Kisha wataangalia duniani na kuona tu dhiki na giza, hofu na huzuni tupu, nao watasukumiwa kwenye giza nene kabisa.

< Yeşaya 8 >