< Yeşaya 34 >

1 Ey uluslar, işitmek için yaklaşın! Ey halklar, kulak verin! Dünya ve üzerindeki herkes, Yeryüzü ve ondan türeyenlerin hepsi işitsin!
Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize; sikilizeni kwa makini, enyi kabila za watu! Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake, ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!
2 RAB bütün uluslara öfkelendi, Onların ordularına karşı gazaba geldi. Onları tümüyle mahvolmaya, Boğazlanmaya teslim edecek.
Bwana ameyakasirikia mataifa yote; ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote. Atawaangamiza kabisa, atawatia mikononi mwa wachinjaji.
3 Ölüleri dışarı atılacak, Pis kokacak cesetleri; Dağlar kanlarıyla sulanacak.
Waliouawa watatupwa nje, maiti zao zitatoa uvundo, milima itatota kwa damu zao.
4 Bütün gök cisimleri küçülecek, Gökler bir tomar gibi dürülecek; Gök cisimleri, asma yaprağı, İncir yaprağı gibi dökülecek.
Nyota zote za mbinguni zitayeyuka na anga litasokotwa kama kitabu, jeshi lote la angani litaanguka kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu, kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.
5 “Kılıcım göklerde kanıncaya kadar içti. Şimdi de Edom'un, Tümüyle yıkmaya karar verdiğim halkın Üzerine inecek” diyor RAB.
Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni, tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu, wale watu ambao nimeshawahukumu, kuwaangamiza kabisa.
6 RAB'bin kılıcı kana, Kuzu ve teke kanına doydu; Yağla, koç böbreklerinin yağıyla kaplandı. Çünkü RAB'bin Bosra'da bir kurbanı, Edom'da büyük bir kıyımı var.
Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.
7 Onlarla birlikte yaban öküzleri, Körpe boğalarla güçlü boğalar da yere serilecek. Toprakları kana doyacak, yağla sulanacak.
Nyati wataanguka pamoja nao, ndama waume na mafahali wakubwa. Nchi yao italowana kwa damu, nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.
8 Çünkü RAB'bin bir öç günü, Siyon'un davasını güdeceği bir karşılık yılı olacak.
Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.
9 Edom dereleri zifte, toprağı kükürde dönecek; ülkenin her yanı yanan zift olacak.
Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami, mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho, nchi yake itakuwa lami iwakayo!
10 Zift gece gündüz sönmeyecek, dumanı hep tütecek. Ülke kuşaklar boyu ıssız kalacak, sonsuza dek oradan kimse geçmeyecek.
Haitazimishwa usiku wala mchana, moshi wake utapaa juu milele. Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa, hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.
11 Baykuşların mülkü olacak orası, büyük baykuşlarla kargalar yaşayacak orada. RAB, Edom'un üzerine kargaşa ipini, boşluk çekülünü gerecek.
Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki, bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo. Mungu atanyoosha juu ya Edomu kamba ya kupimia ya machafuko matupu, na timazi ya ukiwa.
12 Kral ilan edebilecekleri soylular kalmayacak, bütün önderlerinin sonu gelecek.
Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote kitakachoitwa ufalme huko, nao wakuu wao wote watatoweka.
13 Saraylarında dikenler, kalelerinde ısırganlarla böğürtlenler bitecek. Orası çakalların barınağı, baykuşların yurdu olacak.
Miiba itaenea katika ngome za ndani, viwawi na michongoma itaota kwenye ngome zake. Itakuwa maskani ya mbweha, makao ya bundi.
14 Yabanıl hayvanlarla sırtlanlar orada buluşacak, tekeler karşılıklı böğürecek. Lilit oraya yerleşip rahata kavuşacak.
Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi, nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana; huko viumbe vya usiku vitastarehe pia na kujitafutia mahali pa kupumzika.
15 Baykuşlar orada yuva kurup yumurtlayacak, kuluçkaya yatıp yavrularını kendi gölgelerinde toplayacak. Çaylaklar eşleşip orada toplanacaklar.
Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai, atayaangua na kutunza makinda yake chini ya uvuli wa mabawa yake; pia huko vipanga watakusanyika, kila mmoja na mwenzi wake.
16 RAB'bin kitabını okuyup araştırın: Bunlardan hiçbiri eksik kalmayacak, eşten yoksun hiçbir hayvan olmayacak. Çünkü bu buyruk RAB'bin ağzından çıktı, Ruhu da onları toplayacak.
Angalieni katika gombo la Bwana na msome: Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana, hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake. Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza, na Roho wake atawakusanya pamoja.
17 RAB onlar için kura çekti, ülkeyi ölçüp aralarında pay etti. Orayı sonsuza dek sahiplenip kuşaklar boyu orada yaşayacaklar.
Huwagawia sehemu zao, mkono wake huwagawanyia kwa kipimo. Wataimiliki hata milele na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.

< Yeşaya 34 >