< Hoşea 4 >
1 Ey İsrailliler, dinleyin RAB'bin sözünü, Çünkü RAB'bin davası var bu ülkede yaşayanlarla; “Yok olmuş sevgi, sadakat, Tanrı bilgisi.
Sikieni neno la Bwana, enyi Waisraeli, kwa sababu Bwana analo shtaka dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi: “Hakuna uaminifu, hakuna upendo, hakuna kumjua Mungu katika nchi.
2 Lanet, yalan, adam öldürme, hırsızlık, Zina almış her şeyin yerini. Zorbalık ediyorlar, Kan üstüne kan döküyorlar.
Kuna kulaani tu, uongo na uuaji, wizi na uzinzi, bila kuwa na mipaka, nao umwagaji damu mmoja baada ya mwingine.
3 Bu yüzden ülke yas tutuyor, Tükeniyor orada yaşayan herkes, Kırdaki hayvanlar, gökteki kuşlar Denizdeki balıklar...
Kwa sababu hii nchi huomboleza, wote waishio ndani mwake wanadhoofika, wanyama wa kondeni, ndege wa angani na samaki wa baharini wanakufa.
4 “Ancak kimse kimseyle çekişmesin, Kimse kimseyi suçlamasın, Çünkü halkın kâhinle çekişenlere benziyor.
“Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka, mtu yeyote na asimlaumu mwenzake, kwa maana watu wako ni kama wale waletao mashtaka dhidi ya kuhani.
5 Sen gündüz tökezleyeceksin, Peygamber de gece seninle birlikte, Yok edeceğim anneni.
Unajikwaa usiku na mchana, nao manabii hujikwaa pamoja nawe. Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:
6 “Yok oldu halkım bilgisizlikten, Sen bilgiyi reddettiğin için, Ben de seni reddedeceğim, Bana kâhinlik etmeyesin diye. Sen Tanrın'ın yasasını unuttuğun için, Ben de senin çocuklarını unutacağım.
watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa, “Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako mimi nami sitawajali watoto wako.
7 Kâhinler çoğaldıkça Daha çok günah işlediler bana karşı, Onların onurunu utanca çevireceğim.
Kadiri makuhani walivyoongezeka, ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu, walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.
8 Halkımın günahlarıyla besleniyorlar, Onların suç işlemesini istiyorlar.
Hujilisha dhambi za watu wangu na kupendezwa na uovu wao.
9 Halkın başına gelenler kâhinlerin başına da gelecek, Tuttukları yol yüzünden cezalandıracağım onları, Yaptıklarının karşılığını vereceğim.
Hata itakuwa: Kama walivyo watu, ndivyo walivyo makuhani. Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao na kuwalipa kwa matendo yao.
10 Yiyecekler, ama doymayacaklar, Zina edecekler, ama çoğalmayacaklar. Çünkü RAB'bi dinlemekten vazgeçtiler.
“Watakula lakini hawatashiba; watajiingiza katika ukahaba lakini hawataongezeka, kwa sababu wamemwacha Bwana na kujiingiza wenyewe
11 “Zina, yeni ve eski şarap insanın aklını başından alır.
katika ukahaba, divai ya zamani na divai mpya, ambavyo huondoa ufahamu
12 Halkım tahta puta danışıyor, Değneğinden yanıt alıyor. Çünkü zina ruhu onları saptırdı, Kendi Tanrıları'ndan ayrılarak zina ettiler.
wa watu wangu. Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti nao hujibiwa na fimbo ya mti. Roho ya ukahaba imewapotosha, hawana uaminifu kwa Mungu wao.
13 Dağ başlarında kurban kesiyor, Tepelerde meşe, aselbent, yabanıl fıstık ağaçları altında buhur yakıyorlar, Gölgeleri güzel olduğu için. Bu yüzden kızlarınız fahişelik ediyor, Gelinleriniz zina.
Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima, chini ya mialoni, milibua na miela, ambako kuna vivuli vizuri. Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba na wake za wana wenu uzinzi.
14 Fahişelik ettiklerinde kızlarınızı, Zina ettiklerinde gelinlerinizi cezalandırmayacağım. Çünkü erkekleriniz fahişelerle oynaşıyor, Putların tapınağında fuhuş yapanlarla kurban kesiyorlar. Anlayışsız halk mahvolacak.
“Sitawaadhibu binti zenu wakati wanapogeukia ukahaba, wala wake za wana wenu wanapofanya uzinzi, kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya na kutambikia pamoja na makahaba wa mahali pa kuabudia miungu: watu wasiokuwa na ufahamu wataangamia!
15 “Ey İsrail, sen zina etsen de, Yahuda suç işlemese bari. “Gilgal'a gitmeyin, Beytaven'e çıkmayın. ‘Yaşayan RAB'bin hakkı için’ diye ant içmeyin.
“Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli, Yuda naye asije akawa na hatia. “Usiende Gilgali, usipande kwenda Beth-Aveni Wala usiape, ‘Hakika kama Bwana aishivyo!’
16 Çünkü İsrail inatçı bir inek gibi inat etti, Şimdi RAB nasıl güder onları otlakta kuzu gibi?
Waisraeli ni wakaidi, kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi. Ni jinsi gani basi Bwana anaweza kuwachunga kama wana-kondoo katika shamba la majani?
17 Efrayim putlarına sarıldı, Bırak onu!
Efraimu amejiunga na sanamu, ondokana naye!
18 İçkileri tükendi, Hâlâ zina ediyorlar; Önderleri rezilliğe gönül verdi.
Hata wakati wamemaliza vileo vyao wanaendelea na ukahaba wao, watawala wao hupenda sana njia za aibu.
19 Rüzgar onları kanatlarına sardı, Kurbanları yüzünden utanacaklar.
Kisulisuli kitawafagilia mbali na dhabihu zao zitawaletea aibu.