< Yaratiliş 45 >

1 Yusuf adamlarının önünde kendini tutamayıp, “Herkesi çıkarın buradan!” diye bağırdı. Kendini kardeşlerine tanıttığında yanında kimse olmasın istiyordu.
Hapo Yosefu hakuweza kujizuia zaidi mbele ya wote waliokuwa wamesimama karibu naye, akapaza sauti, akasema, “Mwondoeni kila mtu mbele yangu!” Kwa hiyo hapakuwepo mtu yeyote pamoja na Yosefu alipojitambulisha kwa ndugu zake.
2 O kadar yüksek sesle ağladı ki, Mısırlılar ağlayışını işitti. Bu haber firavunun ev halkına da ulaştı.
Naye akalia kwa sauti kubwa kiasi kwamba Wamisri walimsikia, hata watu wa nyumbani mwa Farao wakapata hizo habari.
3 Yusuf kardeşlerine, “Ben Yusuf'um!” dedi, “Babam yaşıyor mu?” Kardeşleri donup kaldı, yanıt veremediler.
Yosefu akawaambia ndugu zake, “Mimi ni Yosefu! Je, baba yangu angali hai bado?” Lakini ndugu zake hawakuweza kumjibu, kwa sababu walipatwa na hofu kuu mbele yake.
4 Yusuf, “Lütfen bana yaklaşın” dedi. Onlar yaklaşınca Yusuf şöyle devam etti: “Mısır'a sattığınız kardeşiniz Yusuf benim.
Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake, “Sogeeni karibu nami.” Waliposogea, akasema, “Mimi ni ndugu yenu Yosefu, yule ambaye mlimuuza Misri!
5 Beni buraya sattığınız için üzülmeyin. Kendinizi suçlamayın. Tanrı insanlığı korumak için beni önden gönderdi.
Sasa, msihuzunike wala msijichukie wenyewe kwa kuniuza huku, kwa sababu ilikuwa ni ili kuokoa maisha ya watu ndiyo sababu Mungu alinituma niwatangulie ninyi.
6 Çünkü iki yıldır ülkede kıtlık var, beş yıl daha sürecek. Kimse çift süremeyecek, ekin biçemeyecek.
Kwa miaka miwili sasa imekuwepo njaa katika nchi, pia kwa miaka mitano ijayo hapatakuwepo kulima wala kuvuna.
7 Tanrı yeryüzünde soyunuzu korumak ve harika biçimde canınızı kurtarmak için beni önünüzden gönderdi.
Lakini Mungu alinitanguliza mbele yenu ili kuhifadhi mabaki kwa ajili yenu katika nchi, na kuokoa maisha yenu kwa wokovu mkuu.
8 Beni buraya gönderen siz değilsiniz, Tanrı'dır. Beni firavunun başdanışmanı, sarayının efendisi, bütün Mısır ülkesinin yöneticisi yaptı.
“Kwa hiyo basi, si ninyi mlionileta huku, bali ni Mungu. Alinifanya kuwa baba kwa Farao, bwana wa watu wa nyumbani mwake wote, na mtawala wa Misri yote.
9 Hemen babamın yanına gidin, ona oğlun Yusuf şöyle diyor deyin: ‘Tanrı beni Mısır ülkesine yönetici yaptı. Durma, yanıma gel.
Sasa rudini haraka kwa baba yangu na mwambieni, ‘Hili ndilo mwanao Yosefu asemalo: Mungu amenifanya mimi kuwa bwana wa Misri yote. Shuka uje kwangu, wala usikawie.
10 Goşen bölgesine yerleşirsin; çocukların, torunların, davarların, sığırların ve sahip olduğun her şeyle birlikte yakınımda olursun.
Nawe utaishi katika nchi ya Gosheni na kuwa karibu nami, wewe, watoto wako na wajukuu wako, makundi yako ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, pamoja na vyote ulivyo navyo.
11 Orada sana bakarım, çünkü kıtlık beş yıl daha sürecek. Yoksa sen de ailen ve sana bağlı olan herkes de perişan olursunuz.’
Nitawatunza huko, kwa sababu bado iko miaka mingine mitano inayokuja ya njaa. La sivyo, wewe na nyumba yako na wote ulio nao mtakuwa fukara.’
12 “Hepiniz gözlerinizle görüyorsunuz, kardeşim Benyamin, sen de görüyorsun konuşanın gerçekten ben olduğumu.
“Mnaweza kujionea wenyewe, hata ndugu yangu Benyamini, kwamba hakika ni mimi ninayezungumza nanyi.
13 Mısır'da ne denli güçlü olduğumu ve bütün gördüklerinizi babama anlatın. Babamı hemen buraya getirin.”
Mwambieni baba yangu juu ya heshima yote niliyopewa huku Misri, na kuhusu kila kitu mlichokiona. Mleteni baba yangu huku haraka.”
14 Sonra kardeşi Benyamin'in boynuna sarılıp ağladı. Benyamin de ağlayarak ona sarıldı.
Ndipo akamkumbatia Benyamini ndugu yake na kulia, naye Benyamini akamkumbatia akilia.
15 Yusuf ağlayarak bütün kardeşlerini öptü. Sonra kardeşleri onunla konuşmaya başladı.
Pia akawabusu ndugu zake wote, huku akilia. Baada ya hayo ndugu zake wakazungumza naye.
16 Yusuf'un kardeşlerinin geldiği haberi firavunun sarayına ulaşınca, firavunla görevlileri hoşnut oldu.
Habari zilipofika kwenye jumba la Farao kwamba ndugu zake Yosefu wamefika, Farao na maafisa wake wote wakafurahi.
17 Firavun Yusuf'a şöyle dedi: “Kardeşlerine de ki, ‘Hayvanlarınızı yükleyip Kenan ülkesine gidin.
Farao akamwambia Yosefu, “Waambie ndugu zako, ‘Fanyeni hivi: Pakieni wanyama wenu mrudi mpaka nchi ya Kanaani,
18 Babanızı ve ailelerinizi buraya getirin. Size Mısır'ın en iyi topraklarını vereceğim. Ülkenin kaymağını yiyeceksiniz.’
mkamlete baba yenu na jamaa zenu kwangu. Nitawapa sehemu nzuri sana ya nchi ya Misri nanyi mtafurahia unono wa nchi.’
19 Onlara ayrıca şöyle demeni de buyuruyorum: ‘Çocuklarınızla karılarınız için Mısır'dan arabalar alın, babanızla birlikte buraya gelin.
“Mnaagizwa pia kuwaambia, ‘Fanyeni hivi: Chukueni magari ya kukokotwa kutoka Misri, kwa ajili ya watoto wenu na wake zenu, mkamchukue baba yenu mje.
20 Gözünüz arkada kalmasın, çünkü Mısır'da en iyi ne varsa sizin olacak.’”
Msijali kamwe kuhusu mali zenu, kwa sababu mema yote ya Misri yatakuwa yenu.’”
21 İsrail'in oğulları söyleneni yaptı. Firavunun buyruğu üzerine Yusuf onlara araba ve yol için azık verdi.
Hivyo wana wa Israeli wakafanya hivyo. Yosefu akawapa magari ya kukokotwa, kama Farao alivyoagiza, pia akawapa mahitaji kwa ajili ya safari yao.
22 Hepsine birer kat yedek giysi, Benyamin'e ise üç yüz parça gümüşle beş kat yedek giysi verdi.
Kila mmoja mavazi mapya, lakini Benyamini akampa shekeli 300 za fedha, na jozi tano za nguo.
23 Böylece babasına Mısır'da en iyi ne varsa hepsiyle yüklü on eşek, yolculuk için buğday, ekmek ve azık yüklü on dişi eşek gönderdi.
Hivi ndivyo vitu alivyotuma kwa baba yake: punda kumi waliochukua vitu vizuri vya Misri, punda wake kumi waliobeba nafaka, mikate na mahitaji mengine ya safari.
24 Kardeşlerini yolcu ederken onlara, “Yolda kavga etmeyin” dedi.
Akaagana na ndugu zake walipokuwa wakiondoka, akawaambia, “Msigombane njiani!”
25 Yusuf'un kardeşleri Mısır'dan ayrılıp Kenan ülkesine, babaları Yakup'un yanına döndüler.
Basi wakatoka Misri na kufika kwa baba yao Yakobo katika nchi ya Kanaani.
26 Ona, “Yusuf yaşıyor!” dediler, “Üstelik Mısır'ın yöneticisi olmuş.” Babaları donup kaldı, onlara inanmadı.
Wakamwambia baba yao, “Yosefu angali hai! Ukweli ni kwamba yeye ndiye mtawala wa Misri yote.” Yakobo akapigwa na bumbuazi; hakuwasadiki.
27 Yusuf'un kendilerine bütün söylediklerini anlattılar. Kendisini Mısır'a götürmek için Yusuf'un gönderdiği arabaları görünce, Yakup'un keyfi yerine geldi.
Lakini walipokwisha kumweleza kila kitu ambacho Yosefu alikuwa amewaambia, na alipoona magari ya kukokotwa Yosefu aliyokuwa amempelekea ya kumchukua aende Misri, roho ya baba yao Yakobo ikahuishwa.
28 “Tamam!” dedi, “Oğlum Yusuf yaşıyor. Ölmeden önce gidip onu göreceğim.”
Ndipo Israeli akasema, “Nimesadiki! Mwanangu Yosefu bado yu hai. Nitakwenda nikamwone kabla sijafa.”

< Yaratiliş 45 >