< Yaratiliş 14 >
1 Bu arada Şinar Kralı Amrafel, Ellasar Kralı Aryok, Elam Kralı Kedorlaomer ve Goyim Kralı Tidal
Ikiwa katika siku za Amrafeli, mfalme wa shinari, Arioko, mfalme wa Elasari, Kedorlaoma, mfalme wa Elam na Tidali, mfalme wa Goimu,
2 Sodom Kralı Bera'ya, Gomora Kralı Birşa'ya, Adma Kralı Şinav'a, Sevoyim Kralı Şemever'e ve Bala –Soar– Kralı'na karşı savaş açtı.
walifanya vita dhidi ya Bera mfalme wa Sodoma, Birsha, mfalme wa Gomora, Shinabu, mfalme wa Adma, Shemeberi, mfalme wa Seboim, na mfalme wa Bela(pia ikiitwa Soari).
3 Bu son beş kral bugün Lut Gölü olan Siddim Vadisi'nde güçlerini birleştirmişti.
Hawa wafalme watano wa mwisho waliungana pamoja katika bonde la Sidim (pia likiitwa bahari ya chumvi).
4 Bu krallar on iki yıl Kedorlaomer'in egemenliği altında yaşamış, on üçüncü yıl ona başkaldırmışlardı.
Kwa miaka kumi na mbili walimtumikia Kedorlaoma, lakini katika mwaka wa kumi na tatu waliasi.
5 On dördüncü yıl Kedorlaomer'le onu destekleyen öbür krallar gelip Aşterot-Karnayim'de Refalılar'ı, Ham'da Zuzlular'ı, Şave-Kiryatayim'de Emliler'i, çöl kenarındaki El-Paran'a kadar uzanan dağlık Seir bölgesinde Horlular'ı bozguna uğrattılar.
Kisha katika mwaka wa kumi na nne, Kedorlaoma na wafalme waliokuwa pamoja nae walikuja na kuwashambulia Warefai katika Ashteroth Karnaimu, na Wazuzi katika Hamu, Waemi katika Shawe Kiriathaimu,
na Wahori katika mlima wao wa Seiri, mpaka El Parani iliyo karibu na jangwa.
7 Oradan geri dönüp Eyn-Mişpat'a –Kadeş'e– gittiler. Amalekliler'in bütün topraklarını alarak Haseson-Tamar'da yaşayan Amorlular'ı bozguna uğrattılar.
Kisha wakarudi wakaja En Misifati (Pia ikiitwa Kadeshi), na kuishinda nchi yote ya Waamaleki, na pia Waamori ambao waliishi Hasasoni Tamari.
8 Bunun üzerine Sodom, Gomora, Adma, Sevoyim, Bala –Soar– kralları yola çıktı. Bu beş kral dört krala –Elam Kralı Kedorlaomer, Goyim Kralı Tidal, Şinar Kralı Amrafel, Ellasar Kralı Aryok'a– karşı Siddim Vadisi'nde savaş düzenine girdiler.
Kisha mfalme wa Sodoma, mfalme wa Gomora, mfalme wa Adma, mfalme wa Seboim, na mfalme wa Bela (pia ikiitwa Soari) walikwenda na kuandaa vita
dhidi ya Kadorlaoma, mfalme wa Elam, Tidali mfalme wa Goim, Amrafeli, mfalme wa Shinari, Arioki, mfalme wa Elasari; wafme wanne dhidi ya wale watano.
10 Siddim Vadisi zift çukurlarıyla doluydu. Sodom ve Gomora kralları kaçarken adamlarından bazıları bu çukurlara düştü. Sağ kalanlarsa dağlara kaçtı.
Na sasa bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, na wafalme wa Sodoma na Gomora walipokimbia, wakaanguka pale. Wale waliosalia wakakimbilia milimani.
11 Dört kral Sodom ve Gomora'nın bütün malını ve yiyeceğini alıp gitti.
Kwa hiyo adui akachukua mali zote za Sodoma na Gomora na vyakula vyao vyote, na wakaenda zao,
12 Avram'ın yeğeni Lut'la mallarını da götürdüler. Çünkü o da Sodom'da yaşıyordu.
walipoondoka, wakamchukua pia Lutu, mtoto wa ndugu yake na Abram ambaye aliishi Sodoma, pamoja na mali zake zote.
13 Oradan kaçıp kurtulan biri gelip İbrani Avram'a durumu bildirdi. Avram Eşkol'la Aner'in kardeşi Amorlu Mamre'nin meşeliğinde yaşıyordu. Bunların hepsi Avram'dan yanaydılar.
Mmoja ambaye alitoroka alikuja na kumwambia Abram mwebrania. Alikuwa anaishi katika mialoni ya Mamre, mwamori ambaye alikuwa ni ndugu wa Eshkoli na Aneri ambao walikuwa washirika wa Abram.
14 Avram yeğeni Lut'un tutsak alındığını duyunca, evinde doğup yetişmiş üç yüz on sekiz adamını yanına alarak dört kralı Dan'a kadar kovaladı.
Abram aliposikia kuwa maadui wamemteka ndugu yake, akawaongoza wanaume waliofunzwa na kuzaliwa nyumbani mwake 318 na akawaongoza hadi Dani.
15 Adamlarını gruplara ayırdı, gece saldırıp onları bozguna uğratarak Şam'ın kuzeyindeki Hova'ya kadar kovaladı.
Akawagawanya watu wake dhidi yao usiku na kuwavamia, na kuwafukuza mpaka Hoba, ambayo iko kaskazini mwa Dameski.
16 Yağmalanan bütün malı, yeğeni Lut'la mallarını, kadınları ve halkı geri getirdi.
Kisha akarudisha mali zote, pia akamrudisha ndugu yake Lutu na mali zake, pamoja na wanawake na watu wengine.
17 Avram Kedorlaomer'le onu destekleyen kralları bozguna uğratıp dönünce, Sodom Kralı onu karşılamak için Kral Vadisi olan Şave Vadisi'ne gitti.
Baada ya Abram kurudi kutoka kumpiga Kadorlaoma na wafalme waliokuwa pamoja nae, mfalme wa Sodoma akatoka kuonana nae katika bonde la Shawe (pia iliitwa bonde la mfalme).
18 Yüce Tanrı'nın kâhini olan Şalem Kralı Melkisedek ekmek ve şarap getirdi.
Melkizedeki, mfalme wa Salem, akaleta mkate na divai. Alikuwa ni kuhani wa Mungu aliye juu sana.
19 Avram'ı kutsayarak şöyle dedi: “Yeri göğü yaratan yüce Tanrı Avram'ı kutsasın,
Alimbariki akisema, “Abarikiwea Abram na Mungu aliye juu sana, muumba wa mbingu na nchi.
20 Düşmanlarını onun eline teslim eden yüce Tanrı'ya övgüler olsun.” Bunun üzerine Avram her şeyin ondalığını Melkisedek'e verdi.
Abarikiwe Mungu aliye juu sana, ambaye amekupatia adui zako katika mikono yako.” Kisha Abram akampatia sehemu ya kumi ya kila kitu.
21 Sodom Kralı Avram'a, “Adamlarımı bana ver, mallar sana kalsın” dedi.
Mfalme wa Sodama akamwambia Abram, “Nipatie watu, na ujichukulie wewe mwenyewe mali.”
22 Avram Sodom Kralı'na, “Yeri göğü yaratan yüce Tanrı RAB'bin önünde sana ait hiçbir şey, bir iplik, bir çarık bağı bile almayacağıma ant içerim” diye karşılık verdi, “Öyle ki, ‘Avram'ı zengin ettim’ demeyesin.
Abram akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua juu mkono wangu kwa Yahwe, Mungu aliye juu sana, muumbaji wa mbingu na nchi,
kwamba sitachukua uzi wala gidamu ya kiatu, au kitu chochote ambacho ni chako, 'ili kwamba usiseme, nimemfanya Abram kuwa tajiri.'
24 Yalnız, adamlarımın yedikleri bunun dışında. Bir de beni destekleyen Aner, Eşkol ve Mamre paylarına düşeni alsınlar.”
Sitachukua chochote isipokuwa kile ambacho vijana wamekula na sehemu za watu waliokwenda nami. Aneri, Eskoli, na Mamre na wachukue sehemu zao.”