< Hezekiel 32 >
1 Sürgünlüğümüzün on ikinci yılı, on ikinci ayın birinci günü RAB bana şöyle seslendi:
Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema:
2 “İnsanoğlu, firavun için bir ağıt yak. Ona de ki, “‘Uluslar arasında genç bir aslan gibi kendini öne sürdün, Ama sen denizlerdeki bir canavar gibisin. Irmaklarını karıştırır, Ayaklarınla suları çalkalar, Irmakları bulandırırsın.’”
“Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Farao mfalme wa Misri na umwambie: “‘Wewe ni kama simba miongoni mwa mataifa, wewe ni kama joka kubwa baharini, unayevuruga maji kwa miguu yako na kuchafua vijito.
3 Egemen RAB şöyle diyor: “Büyük bir kalabalıkla Ağımı senin üzerine atacağım; Onlar seni ağımla çekecekler.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Nikiwa pamoja na wingi mkubwa wa watu nitautupa wavu wangu juu yako, nao watakukokota katika wavu wangu.
4 Seni karaya atacak, Kırlara fırlatacağım. Gökte uçan kuşların senin üzerine konmalarını sağlayacağım, Yeryüzündeki yabanıl hayvanlara Seni yem olarak vereceğim.
Nitakutupa nchi kavu na kukuvurumisha uwanjani. Nitawafanya ndege wote wa angani watue juu yako na wanyama wote wa nchi watajishibisha nyama yako.
5 Bedenini dağların üzerine serecek, Vadileri çürüyen bedeninle dolduracağım.
Nitatawanya nyama yako juu ya milima na kujaza mabonde kwa mabaki yako.
6 Ülkeyi dağlara dek akan kanınla ıslatacağım, Vadiler seninle dolacak.
Nitailowanisha nchi kwa damu yako inayotiririka njia yote hadi milimani, nayo mabonde yatajazwa na nyama yako.
7 Seni ortadan kaldırdığım zaman Gökleri örtecek, Yıldızları karartacak, Güneşi bulutla kapatacağım. Ay ışığını vermeyecek.
Nitakapokuzimisha, nitafunika mbingu na kuzitia nyota zake giza; nitalifunika jua kwa wingu, nao mwezi hautatoa nuru yake.
8 Senin yüzünden gökte ışık veren bütün cisimleri karartacak, Ülkeni karanlığa gömeceğim.” Böyle diyor Egemen RAB.
Mianga yote itoayo nuru angani nitaitia giza juu yako; nitaleta giza juu ya nchi yako, asema Bwana Mwenyezi.
9 “Seni tanımadığın ülkelere, Ulusların arasına sürgüne gönderdiğimde, Pek çok halkın yüreği üzüntüyle sarsılacak.
Nitaifadhaisha mioyo ya mataifa mengi nitakapokuangamiza miongoni mwa mataifa, nikikuleta uhamishoni miongoni mwa nchi ambazo haujapata kuzijua.
10 Başına gelenlerden ötürü Pek çok halkı şaşkına çevireceğim. Kılıcımı önlerinde salladığım zaman, Senin yüzünden krallar dehşetle ürperecek. Yıkıma uğradığın gün Hepsi kendi canı için Her an korkuyla titreyecek.
Nitayafanya mataifa mengi wakustaajabie, wafalme wao watatetemeka kwa hofu kwa ajili yako nitakapotikisa upanga wangu mbele yao. Siku ya anguko lako kila mmoja wao atatetemeka kila dakika kwa ajili ya maisha yake.
11 Egemen RAB şöyle diyor: Babil Kralı'nın kılıcı üzerine gelecek.
“‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja dhidi yako.
12 Yiğitlerin, ulusların en acımasızının, Senin halkını kılıçtan geçirmesine izin vereceğim. Mısır'ın gururunu kıracak, Bütün ordusunu yok edecekler.
Nitafanya makundi yako ya wajeuri kuanguka kwa panga za watu mashujaa, taifa katili kuliko mataifa yote. Watakivunjavunja kiburi cha Misri, nayo makundi yake yote ya wajeuri yatashindwa.
13 Bol suların yanında bütün sığırlarını yok edeceğim. Bundan böyle insan ayağı da hayvan ayağı da Suları karıştırıp bulandırmayacak.
Nitaangamiza mifugo yake yote wanaojilisha kando ya maji mengi, hayatavurugwa tena kwa mguu wa mwanadamu wala kwato za mnyama hazitayachafua tena.
14 O zaman sularını dupduru kılacak, Irmaklarını yağ gibi akıtacağım. Egemen RAB böyle diyor.
Kisha nitafanya maji yake yatulie na kufanya vijito vyake vitiririke kama mafuta, asema Bwana Mwenyezi.
15 Mısır'ı viraneye çevirdiğimde, Ülkeyi her şeyden yoksun bıraktığımda, Orada yaşayan herkesi yok ettiğimde, Benim RAB olduğumu anlayacaklar.
Nitakapoifanya Misri kuwa ukiwa na kuiondolea nchi kila kitu kilichomo ndani yake, nitakapowapiga wote waishio humo, ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
16 “Ona yakacakları ağıt budur. Ulusların kızları bu ağıtı yakacaklar. Mısır için, halkı için bu ağıtı yakacaklar.” Egemen RAB böyle diyor.
“Hili ndilo ombolezo watakalomwimbia. Binti za mataifa wataliimba, kwa kuwa Misri na makundi yake yote ya wajeuri wataliimba, asema Bwana Mwenyezi.”
17 Sürgünlüğümüzün on ikinci yılı, ayın on beşinci günü RAB bana şöyle seslendi:
Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kwanza, siku ya kumi na tano ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
18 “Ey insanoğlu, Mısır halkı için yas tut. Onları ve güçlü ulusların kızlarını ölüm çukuruna inenlerle birlikte yerin derinliklerine indir.
“Mwanadamu, omboleza kwa ajili ya makundi ya wajeuri wa Misri na uwatupe kuzimu yeye na binti za mataifa yenye nguvu, waende huko pamoja nao washukao shimoni. ()
19 Onlara de ki, ‘Sen başkalarından daha mı güzelsin? Aşağı in ve oradaki sünnetsizlere katıl.’
Je, ninyi mnamzidi nani kwa uzuri? Shukeni chini! Nanyi mkalazwe pamoja na hao wasiotahiriwa!
20 Mısır halkı kılıçla öldürülenlerin arasına düşecek. Kılıç hazır, bırakın Mısır bütün halkıyla birlikte sürüklensin.
Wataanguka miongoni mwa wale waliouawa kwa upanga. Upanga umefutwa, mwache aburutwe mbali pamoja na hao wajeuri wake wote.
21 Güçlü önderler, ölüler diyarından, Mısır ve onu destekleyenler için, ‘Aşağı indiler, kılıçla öldürülen sünnetsizlerle birlikte burada yatıyorlar’ diyecekler. (Sheol )
Kutoka kuzimu viongozi hodari watanena kuhusu Misri pamoja na wale walioungana nao, ‘Wameshuka chini, nao wamelala kimya pamoja na hao wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.’ (Sheol )
22 “Asur bütün ordusuyla orada. Kılıçtan geçirilmiş, ölmüş askerlerinin mezarları çevresini sarmış.
“Ashuru yuko huko pamoja na jeshi lake lote, amezungukwa na makaburi ya watu wake wote waliouawa, wale wote walioanguka kwa upanga.
23 Mezarları ölüm çukurunun en dibinde, ordusu mezarının çevresinde duruyor. Yaşayanlar diyarında korku salanların hepsi kılıçtan geçirilmiş, ölmüş.
Makaburi yao yako kwenye kina cha chini cha shimo na jeshi lake limelala kulizunguka kaburi lake. Wote waliokuwa wameeneza hofu kuu katika nchi ya walio hai wameuawa, wameanguka kwa upanga.
24 “Elam bütün halkıyla kendi mezarının çevresinde duruyor. Hepsi kılıçtan geçirilmiş, ölmüş, sünnetsiz olarak yerin derinliklerine inmiş. Yaşayanlar diyarında korku salmışlardı, şimdiyse utanç içinde ölüm çukuruna inenlere katıldılar.
“Elamu yuko huko, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote wameuawa, wameanguka kwa upanga. Wote waliokuwa wameeneza hofu katika nchi ya walio hai walishuka kuzimu bila kutahiriwa. Wanaichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni. ()
25 Elam için öldürülenler arasında bir yatak yapıldı. Bütün halkı mezarının çevresinde. Hepsi sünnetsiz, kılıçtan geçirilerek ölmüş. Yaşayanlar diyarında korku salmışlardı, şimdiyse utanç içinde ölüm çukuruna inenlere katıldılar, öldürülenlerin arasına yerleştirildiler.
Kitanda kimetandikwa kwa ajili yake miongoni mwa waliouawa, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote ni watu wasiotahiriwa, wameuawa kwa upanga. Kwa sababu vitisho vyao vilienea katika nchi ya walio hai, wameichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni, nao wamewekwa miongoni mwa waliouawa.
26 “Meşek ve Tuval bütün halkıyla kendi mezarları çevresinde duruyor. Hepsi sünnetsiz, kılıçtan geçirilerek öldürülmüş. Yaşayanlar diyarında korku salmışlardı.
“Mesheki na Tubali wako humo, pamoja na makundi yao ya wajeuri wakiwa wameyazunguka makaburi yao. Wote hawakutahiriwa, wameuawa kwa upanga kwa sababu walieneza vitisho vyao katika nchi ya walio hai.
27 Ölüler diyarına savaş silahlarıyla inen, kılıçları başlarının altına konan, kalkanları kemikleri üzerine yerleştirilen öbür öldürülmüş sünnetsiz yiğitlerle birlikte mezara konmayacak mı onlar? Oysa bu yiğitler yaşayanlar diyarında korku salmışlardı. (Sheol )
Je, hawakulala na mashujaa wengine wasiotahiriwa waliouawa, ambao wameshuka kaburini wakiwa na silaha zao za vita, ambao panga zao ziliwekwa chini ya vichwa vyao na uovu wao juu ya mifupa yao? Adhabu kwa ajili ya dhambi zao ilikuwa juu ya mifupa yao, ingawa vitisho vya mashujaa hawa vilikuwa vimeenea hadi kwenye nchi ya walio hai. (Sheol )
28 “Sen de, ey firavun, düşecek ve kılıçla öldürülenlerle birlikte sünnetsizlerin arasına konacaksın.
“Wewe pia, ee Farao, utavunjwa nawe utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.
29 “Edom, kralları ve önderleriyle orada. Güçlü olmalarına karşın kılıçla öldürülenlerin yanına kondular. Ölüm çukuruna inenlerin, sünnetsizlerin yanında yatıyorlar.
“Edomu yuko humo, wafalme wake wote na wakuu wake wote, ambao ijapokuwa wana nguvu, wamelazwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga. Wamelala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale washukao shimoni.
30 “Bütün kuzey önderleri, bütün Saydalılar orada. Güçleriyle korku saldıkları halde öldürülenlerle birlikte utanç içinde indiler. Sünnetsiz olarak kılıçla öldürülenlerle birlikte utanç içinde ölüm çukuruna inenlerin yanına kondular.
“Wakuu wote wa kaskazini na Wasidoni wote wako huko, wameshuka chini pamoja na waliouawa kwa aibu ijapokuwa kuna vitisho vilivyosababishwa na nguvu zao. Wamelala bila kutahiriwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga na kuchukua aibu yao pamoja na wale washukao chini shimoni.
31 “Firavunla ordusu kılıçla öldürülmüş bu büyük kalabalığı görünce avunç bulacak.” Böyle diyor Egemen RAB.
“Farao, yeye pamoja na jeshi lake lote, atakapowaona atafarijiwa kwa ajili ya makundi yake yote ya wajeuri, wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.
32 “Yaşayanlar diyarında korku salmasını sağladığım halde, firavunla halkı, kılıçla öldürülenlerle birlikte sünnetsizlerin yanına konacak.” Böyle diyor Egemen RAB.
Ingawa nilimfanya Farao aeneze vitisho vyake katika nchi ya walio hai, Farao pamoja na makundi yake yote ya wajeuri watalazwa miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.”