< Hezekiel 26 >

1 Sürgünlüğümüzün on birinci yılı, ayın birinci günü RAB bana şöyle seslendi:
Mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
2 “İnsanoğlu, madem Sur Kenti, Yeruşalim için, ‘Oh, oh! Ulusların kapısı olan kent yıkıldı, kapıları bana açıldı. O viraneye döndü, ben zenginleşeceğim’ dedi,
“Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu, ‘Aha! Lango la kwenda kwa mataifa limevunjika, nayo milango yake iko wazi mbele yangu, sasa kwa kuwa amekuwa magofu nitastawi.’
3 Egemen RAB şöyle diyor: Ey Sur, sana karşıyım! Deniz dalgalarını nasıl kabartırsa, ben de ulusları senin üzerine öyle saldırtacağım.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na wewe, ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi dhidi yako, kama bahari inayovurumisha mawimbi yake.
4 Sur'un duvarlarını yıkacak, kulelerini yerle bir edecekler. Toprağını kazıp süpürecek, seni çıplak bir kayalık haline getireceğim.
Watavunja kuta za Tiro na kuibomoa minara yake, nitakwangua udongo wake na kuufanya mwamba mtupu.
5 Sur denizin ortasında, balıkçıların ağ gerdikleri bir yer olacak. Egemen RAB böyle diyor. Uluslar Sur'u yağmalayacak,
Itakuwa huko katikati ya bahari patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki, kwa maana nimenena, asema Bwana Mwenyezi. Atakuwa nyara kwa mataifa,
6 Sur'a bağlı kıyı kentlerinde yaşayanları kılıçtan geçirecek. O zaman Surlular benim RAB olduğumu anlayacaklar.
nayo makao yake huko bara yataangamizwa kwa upanga. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.
7 “Egemen RAB şöyle diyor: Krallar kralı Babil Kralı Nebukadnessar'ı atlarla, savaş arabalarıyla, atlılarla, büyük bir orduyla kuzeyden Sur'a getiriyorum.
“Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kutoka kaskazini nitamleta dhidi ya Tiro Mfalme Nebukadneza wa Babeli, mfalme wa wafalme, akiwa na farasi na magari ya vita, wapanda farasi na jeshi kubwa.
8 Sur'a bağlı kıyı kentlerinde yaşayanları kılıçtan geçirecek, size karşı kuşatma duvarları, toprak rampalar yapacak, kalkanını size karşı kaldıracak.
Atayaharibu makao yako huko bara kwa upanga, ataweka jeshi kukuzingira, atakuzingira mpaka kwenye kuta za ngome zako na kuinua ngao zake dhidi yako.
9 Duvarlarınızda gedik açmak için kütükler yerleştirecek, silahlarıyla kulelerinizi yıkacak.
Ataelekeza mapigo ya vyombo vyake vya kubomolea dhidi ya kuta zako na kubomoa minara yako kwa silaha zake.
10 Sayısız atının çıkardığı toz sizi örtecek. Duvarlarında gedik açılmış bir kente girer gibi kent kapılarınızdan girdiğinde, atlıların, tekerleklerin, savaş arabalarının gürültüsünden duvarlarınız sarsılacak.
Farasi zake zitakuwa nyingi sana kiasi kwamba utafunikwa na mavumbi watakayotimua. Kuta zako zitatikisika kwa mshindo wa farasi wa vita, magari makubwa na magari ya vita wakati aingiapo malango yako kama watu waingiao mji ambao kuta zake zimebomolewa kote.
11 Atlarının tırnakları bütün sokaklarınızı çiğneyecek. Halkınız kılıçtan geçirilecek, güçlü sütunlarınız devrilecek.
“Kwato za farasi zake zitakanyaga barabara zako zote, atawaua watu wako kwa upanga na nguzo zako zilizo imara zitaanguka chini.
12 Servetinizi alacak, mallarınızı yağmalayacaklar. Duvarlarınızı yıkacak, güzel evlerinizi yerle bir edecekler. Taşlarınızı, kerestenizi, toprağınızı denize atacaklar.
Watateka utajiri wako na kuchukua nyara bidhaa zako, watazivunja kuta zako na kuzibomoa nyumba zako nzuri, watatupa baharini mawe yako, mbao zako na kifusi chako.
13 Okuduğunuz gürültülü şarkılara son vereceğim. Lirlerinizin sesi bir daha duyulmayacak.
Nitakomesha kelele za nyimbo zako, na uimbaji wako wa kinubi kamwe hautasikika tena.
14 Sizi çıplak bir kayalık haline getireceğim, balıkçıların ağ gerdikleri bir yer olacaksınız. Bir daha kurulmayacaksınız. Çünkü ben RAB söylüyorum. Egemen RAB böyle diyor.
Nitakufanya mwamba mtupu, nawe utakuwa mahali pa kutandazia nyavu za kuvulia samaki. Kamwe hutajengwa tena, kwa maana Mimi Bwana nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
15 “Egemen RAB Sur'a şöyle diyor: Yıkımının sesinden, yaralıların iniltisinden, senin içinde yapılan kıyım yüzünden kıyı halkları titreyecek.
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa Tiro: ‘Je, nchi za pwani hazitatetemeka kwa kishindo cha anguko lako, wakati majeruhi wanapolia kwa maumivu makali na wakati mauaji yanaendelea ndani yako?
16 Kıyıda yaşayan bütün önderler tahtlarından inecek; kaftanlarını, işlemeli giysilerini çıkaracaklar. Dehşet içinde yere oturup her an titreyerek başlarına gelenlere şaşacaklar.
Ndipo wakuu wote wa mataifa ya pwani watashuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuweka kando majoho yao na kuvua nguo zao zilizotariziwa. Wakiwa wamevikwa hofu kuu, wataketi chini ardhini, wakiwa wanatetemeka kila dakika na wakikustajabia.
17 Sonra senin için şöyle bir ağıt yakacaklar: “‘Nasıl oldu da yıkıldın, Ey denizcilerin oturduğu ünlü kent! Sen ve sende oturanlar, Denizde güçlüydünüz. Dehşet salmıştınız Orada yaşayan herkese.
Ndipo wao watakuombolezea na kukuambia: “‘Tazama jinsi ulivyoharibiwa, ee mji uliokuwa na sifa, wewe uliyekaliwa na mabaharia! Ulikuwa na nguvu kwenye bahari, wewe na watu wako; wote walioishi huko, uliwatia hofu kuu.
18 Yıkımın olduğu gün Kıyı halkları titreyecek, Orada yaşayanlar Çöküşüne şaşacaklar.’
Sasa nchi za pwani zinatetemeka katika siku ya anguko lako; visiwa vilivyomo baharini vinaogopa kwa kuporomoka kwako.’
19 “Egemen RAB şöyle diyor: Issız kalmış kentler gibi seni viran bir kent yaptığım, engin denizleri üzerine boşalttığım, derin sular seni örttüğü zaman,
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapokufanya uwe mji wa ukiwa, kama miji isiyokaliwa tena na watu, nitakapoleta vilindi vya bahari juu yako na maji yake makuu yatakapokufunika,
20 ölüm çukuruna inenlerle birlikte seni eski zaman insanlarının yanına indireceğim. Ölüm çukuruna inenlerle birlikte eski kalıntılar arasına, yeryüzünün derinliklerine yerleştireceğim. Öyle ki, bir daha dönüp yaşayanlar diyarında yerini almayasın.
ndipo nitakapokushusha chini pamoja na wale washukao shimoni, kwa watu wa kale, nami nitakufanya uishi katika pande za chini za nchi kama katika magofu ya kale, pamoja na wale washukao shimoni, nawe hutarudi au kurejea kwenye makao yako katika nchi ya walio hai.
21 Seni yılgınlığa düşüreceğim, bu senin sonun olacak. Seni arayacaklar ama bulamayacaklar. Egemen RAB böyle diyor.”
Nitakufikisha mwisho wa kutisha wala hutakuwepo tena. Watu watakutafuta, lakini kamwe hutaonekana tena, asema Bwana Mwenyezi.”

< Hezekiel 26 >