< Hezekiel 15 >

1 RAB bana şöyle seslendi:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 “İnsanoğlu, asma odununun herhangi bir orman ağacının dalından daha fazla değeri var mı?
“Mwanadamu, je, ni vipi mti wa mzabibu unaweza kuwa bora zaidi kuliko tawi la mti mwingine wowote ndani ya msitu?
3 Asma odunundan yararlı bir şey yapılabilir mi? Ya da üzerine eşya asmak için ondan askı yaparlar mı?
Je, mti wake kamwe huchukuliwa na kutengeneza chochote cha manufaa? Je, watu hutengeneza vigingi vya kuningʼinizia vitu kutokana na huo mti wake?
4 Yakıt olarak ateşe atılır da ateş odunun iki ucunu yakıp ortasını kömürleştirince, işe yarar mı?
Nao baada ya kutiwa motoni kama nishati na moto ukateketeza ncha zote mbili na kuunguza sehemu ya kati, je, unafaa kwa lolote?
5 Yanmadan önce işe yaramadıysa, yanıp kömür haline geldikten sonra bir işe yarar mı?
Kama haukufaa kitu chochote ulipokuwa mzima, je, si zaidi sana sasa ambapo hauwezekani kufanyishwa chochote cha kufaa baada ya moto kuuchoma na kuuunguza?
6 “Bu nedenle Egemen RAB şöyle diyor: Orman ağaçları arasında asma odununu nasıl yakıt olarak ateşe verdimse, Yeruşalim'de yaşayan halka da aynısını yapacağım.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kama nilivyoutoa mti wa mzabibu miongoni mwa miti ya msituni kuwa nishati kwa ajili ya moto, hivyo ndivyo nitakavyowatendea watu waishio Yerusalemu.
7 Onlara yüz çevireceğim. Şimdi ateşten kurtulsalar bile, ateş onları yine de yakıp yok edecek. Onlara yüz çevirince, benim RAB olduğumu anlayacaksınız.
Nitaukaza uso wangu dhidi yao. Ingawa watakuwa wameokoka kwenye moto, bado moto utawateketeza. Nami nitakapoukaza uso wangu dhidi yao, ninyi mtajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
8 Ülkeyi viraneye çevireceğim. Çünkü bana sadakatsizlik ettiler. Egemen RAB böyle diyor.”
Nitaifanya nchi kuwa ukiwa kwa sababu wamekuwa si waaminifu, asema Bwana Mwenyezi.”

< Hezekiel 15 >