< Misir'Dan Çikiş 7 >

1 RAB, “Bak, seni firavuna karşı Tanrı gibi yaptım” dedi, “Ağabeyin Harun senin peygamberin olacak.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Tazama, nimekufanya kuwa kama Mungu kwa Farao, naye Aroni, huyo ndugu yako, atakuwa nabii wako.
2 Sana buyurduğum her şeyi ağabeyine anlat. O da firavuna İsrailliler'i ülkesinden salıvermesini söylesin.
Utasema kila kitu nitakachokuagiza, naye Aroni ndugu yako atamwambia Farao awaachie Waisraeli watoke katika nchi yake.
3 Ben firavunu inatçı yapacağım ki, belirtilerimi ve şaşılası işlerimi Mısır'da artırabileyim.
Lakini nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu. Ingawa nitazidisha ishara na maajabu katika Misri,
4 Ama firavun sizi dinlemeyecek. O zaman elimi Mısır'ın üzerine koyacağım ve onları ağır biçimde cezalandırarak halkım İsrail'i ordular halinde Mısır'dan çıkaracağım.
hatawasikiliza. Kisha nitaupeleka mkono wangu juu ya Misri, na kwa matendo makuu ya hukumu nitavitoa vikundi vyangu, watu wangu Waisraeli.
5 Mısır'a karşı elimi kaldırdığım ve İsrailliler'i aralarından çıkardığım zaman Mısırlılar benim RAB olduğumu anlayacak.”
Nao Wamisri watajua kuwa Mimi ndimi Bwana nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli watoke humo.”
6 Musa'yla Harun RAB'bin buyurduğu gibi yaptılar.
Mose na Aroni wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyowaagiza.
7 Firavunla konuştuklarında Musa seksen, Harun seksen üç yaşındaydı.
Mose alikuwa na umri wa miaka themanini na Aroni alikuwa na umri wa miaka themanini na mitatu walipozungumza na Farao.
8 RAB Musa'yla Harun'a şöyle dedi:
Bwana akamwambia Mose na Aroni,
9 “Firavun size, ‘Bir mucize yapın’ dediğinde, söyle Harun'a, değneğini alıp firavunun önüne atsın. Değnek yılan olacak.”
“Farao atakapowaambia, ‘Fanyeni muujiza,’ basi mwambie Aroni, ‘Chukua fimbo yako na uitupe chini mbele ya Farao,’ nayo fimbo itakuwa nyoka.”
10 Böylece Musa'yla Harun firavunun yanına gittiler ve RAB'bin buyurduğu gibi yaptılar. Harun değneğini firavunla görevlilerinin önüne attı. Değnek yılan oluverdi.
Ndipo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyoagiza. Aroni akaitupa ile fimbo yake chini mbele ya Farao na maafisa wake, nayo ikawa nyoka.
11 Bunun üzerine firavun kendi bilgelerini, büyücülerini çağırdı. Mısırlı büyücüler de büyüleriyle aynı şeyi yaptılar.
Farao naye akawaita watu wenye maarifa na wachawi na waganga wa Kimisri, nao wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao.
12 Her biri değneğini attı, değnekler yılan oldu. Ancak Harun'un değneği onların değneklerini yuttu.
Kila mmoja alitupa fimbo yake chini, nayo ikawa nyoka. Lakini fimbo ya Aroni ikazimeza zile fimbo zao.
13 Yine de, RAB'bin söylediği gibi firavun inat etti ve Musa'yla Harun'u dinlemedi.
Hata hivyo moyo wa Farao ukawa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
14 RAB Musa'ya, “Firavun inat ediyor, halkı salıvermeyi reddediyor” dedi,
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Moyo wa Farao ni mgumu, anakataa kuwaachia watu kuondoka.
15 “Sabah git, firavun Nil'e inerken onu karşılamak için ırmak kıyısında bekle. Yılana dönüşen değneği eline al
Nenda kwa Farao asubuhi wakati anapokwenda mtoni. Ngoja ukingoni mwa Naili ili uonane naye, na uchukue mkononi mwako fimbo ile iliyobadilishwa kuwa nyoka.
16 ve ona de ki, ‘Halkımı salıver, çölde bana tapsınlar, demem için İbraniler'in Tanrısı RAB beni sana gönderdi. Ama sen şu ana kadar kulak asmadın.
Kisha umwambie, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania, amenituma nikuambie: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu jangwani. Lakini hadi sasa hujasikiliza.
17 Benim RAB olduğumu şundan anla, diyor RAB. İşte, elimdeki değneği ırmağın sularına vuracağım, sular kana dönecek.
Hili ndilo Bwana asemalo: Kwa hili utajua kuwa Mimi ndimi Bwana: Fimbo iliyo mkononi mwangu nitapiga nayo maji ya Naili nayo yatabadilika kuwa damu.
18 Irmaktaki balıklar ölecek, ırmak leş gibi kokacak, Mısırlılar artık ırmağın suyunu içemeyecekler.’”
Samaki waliomo katika Mto Naili watakufa, nao mto utanuka vibaya, Wamisri hawataweza kunywa hayo maji yake.’”
19 Sonra RAB Musa'ya şöyle buyurdu: “Harun'a de ki, ‘Değneğini al ve elini Mısır'ın suları üzerine –ırmakları, kanalları, havuzları, bütün su birikintileri üzerine– uzat, hepsi kana dönsün. Bütün Mısır'da tahta ve taş kaplardaki sular bile kana dönecek.’”
Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Chukua ile fimbo yako unyooshe mkono wako juu ya maji ya Misri, juu ya chemchemi na mifereji, juu ya madimbwi na mabwawa yote,’ navyo vitabadilika kuwa damu. Damu itakuwa kila mahali katika Misri, hata kwenye vyombo vya miti na vya mawe.”
20 Musa'yla Harun RAB'bin buyurduğu gibi yaptılar. Harun firavunla görevlilerinin gözü önünde değneğini kaldırıp ırmağın sularına vurdu. Bütün sular kana dönüştü.
Mose na Aroni wakafanya kama vile Bwana alivyokuwa amewaagiza. Akainua fimbo yake machoni pa Farao na maafisa wake na kuyapiga maji ya Mto Naili, na maji yote yakabadilika kuwa damu.
21 Irmaktaki balıklar öldü, ırmak kokmaya başladı. Mısırlılar ırmağın suyunu içemez oldular. Mısır'ın her yerinde kan vardı.
Samaki katika Mto Naili wakafa, nao mto ukanuka vibaya sana kiasi kwamba Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Damu ilikuwa kila mahali katika nchi ya Misri.
22 Mısırlı büyücüler de kendi büyüleriyle aynı şeyi yaptılar. RAB'bin söylediği gibi firavun inat etti ve Musa'yla Harun'u dinlemedi.
Lakini waganga wa Misri kwa kutumia siri ya uganga wao wakafanya vivyo hivyo, nao moyo wa Farao ukawa mgumu, hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
23 Olanlara aldırmadan sarayına döndü.
Badala yake, Farao akageuka, akaenda kwenye jumba lake la kifalme, wala hakulitia hili moyoni.
24 Mısırlılar içecek su bulmak için ırmak kıyısını kazmaya koyuldular. Çünkü ırmağın suyunu içemiyorlardı.
Nao Wamisri wote wakachimba kandokando ya Mto Naili kupata maji ya kunywa, kwa sababu hawakuweza kunywa maji ya mto.
25 RAB'bin ırmağı vurmasının üzerinden yedi gün geçti.
Zilipita siku saba baada ya Bwana kuyapiga maji ya Mto Naili.

< Misir'Dan Çikiş 7 >