< Ester 3 >

1 Bu olaylardan sonra Kral Ahaşveroş, Agaklı Hammedata'nın oğlu Haman'ı yüksek bir göreve atayıp onurlandırdı. Onu bütün önderlerden daha yetkili kıldı.
Baada ya matukio haya, Mfalme Ahasuero alimheshimu Hamani mwana wa Hamedatha, Mwagagi, akampandisha na kumpa kiti chake cha heshima cha juu sana kuliko wakuu wengine wote.
2 Kralın buyruğu üzerine saray kapısında çalışan herkes Haman'ın önünde eğilip yere kapanırdı. Ama Mordekay ne eğildi, ne de yere kapandı.
Maafisa wote wa mfalme waliokaa langoni mwa mfalme walipiga magoti na kumpa Hamani heshima, kwa kuwa mfalme alikuwa ameamuru hili kuhusu Hamani. Lakini Mordekai hakumpigia magoti wala kumheshimu.
3 Kralın kapı görevlileri Mordekay'a, “Kralın buyruğuna neden karşı geliyorsun?” diye sordular.
Kisha maafisa wa mfalme waliokuwa langoni mwa mfalme walimuuliza Mordekai, “Kwa nini hutii agizo la mfalme?”
4 Görevliler ona bu soruyu her gün sordularsa da Mordekay onlara kulak asmadı. Bunun üzerine durumu Haman'a bildirdiler. Çünkü Mordekay onlara kendisinin Yahudi olduğunu söylemişti ve böyle davranmaya devam edip etmeyeceğini görmek istiyorlardı.
Siku baada ya siku walizungumza naye lakini hakukubali. Kwa hiyo walimweleza Hamani kuona kama tabia ya Mordekai itaweza kuvumiliwa, kwa maana alikuwa amewaambia kuwa yeye ni Myahudi.
5 Haman, Mordekay'ın eğilip yere kapanmadığını görünce öfkeden kudurdu.
Wakati Hamani alipoona kuwa Mordekai hampigii magoti wala kumpa heshima alighadhibika.
6 Yalnız onu öldürmeyi düşünmekle kalmadı, onun hangi halktan geldiğini bildiği için bütün halkını, Ahaşveroş'un egemenliğinde yaşayan bütün Yahudiler'i ortadan kaldırmaya karar verdi.
Hata hivyo baada ya kujulishwa watu wa Mordekai ni akina nani, alibadili wazo la kumuua Mordekai peke yake. Badala yake Hamani alitafuta njia ya kuwaangamiza watu wote wa Mordekai, yaani, Wayahudi, walio katika ufalme wote wa Ahasuero.
7 Bu işe en uygun ayı ve günü belirlemek için Ahaşveroş'un krallığının on ikinci yılında, birinci ay olan Nisan ayında Haman'ın önünde pur, yani kura çekildi. Kura, on ikinci ay olan Adar ayına düştü.
Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Mfalme Ahasuero, katika mwezi wa kwanza uitwao Nisani, walipiga puri (yaani kura) mbele ya Hamani ili kuchagua siku na mwezi. Kura ikaangukia kwenye mwezi wa kumi na mbili, yaani Adari.
8 Haman Kral Ahaşveroş'a şöyle dedi: “Krallığının bütün illerinde, öbür halkların arasına dağılmış, onlardan ayrı yaşayan bir halk var. Yasaları bütün öbür halklarınkinden farklı; kendileri de kralın yasalarına uymazlar. Onları kendi hallerine bırakmak kralın çıkarlarına uygun düşmez.
Kisha Hamani akamwambia Mfalme Ahasuero, “Wako watu fulani wameenea na kutawanyika miongoni mwa watu katika majimbo yote ya ufalme wako, ambao desturi zao ni tofauti na zile za watu wengine wote, nao hawatii sheria za mfalme. Haifai mfalme kuwavumilia watu hawa.
9 Kral uygun görüyorsa, yok edilmeleri için yazılı bir buyruk verilsin. Ben de hazineye ödenmek üzere kralın memurlarına on bin talant gümüş vereceğim.”
Kama inampendeza mfalme, itolewe amri kuwaangamiza, nami nitaweka talanta 10,000 za fedha katika hazina ya mfalme kwa ajili ya watu watakaoshughulikia jambo hili.”
10 Bunun üzerine kral mühür yüzüğünü parmağından çıkartıp Agaklı Hammedata'nın oğlu Yahudi düşmanı Haman'a verdi.
Basi mfalme alichukua pete yake ya muhuri kutoka kwenye kidole chake na kumpa Hamani mwana wa Hamedatha, Mwagagi, adui wa Wayahudi.
11 Ona, “Para sende kalsın; o halka da ne istersen yap” dedi.
Mfalme akamwambia Hamani, “Baki na fedha yako na uwatendee hao watu utakavyo.”
12 Birinci ayın on üçüncü günü kralın yazmanları çağrıldı ve Haman'ın buyruğu her ile kendi işaretleriyle ve her halka kendi diliyle yazılarak satraplara, il valilerine ve bütün halk önderlerine gönderildi. Buyruk Kral Ahaşveroş'un adını ve yüzüğünün mührünü taşıyordu.
Kisha siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kwanza waandishi wa mfalme waliitwa. Wakaandika barua kwa kila jimbo na katika kila lugha ya watu kama agizo la Hamani lilivyotoka kwa mfalme, kwa watawala wa majimbo mbalimbali, na wakuu wa watu mbalimbali. Hizi ziliandikwa kwa jina la Mfalme Ahasuero mwenyewe na kutiwa muhuri wa pete yake mwenyewe.
13 Krallığın bütün illerine ulaklar aracılığıyla mektuplar gönderildi. Bu mektuplar, on ikinci ay olan Adar ayının on üçüncü günü, genç, yaşlı, kadın, çocuk, bütün Yahudiler'in bir günde öldürülüp yok edilmesini, kökünün kurutulup mal mülklerinin de yağmalanmasını buyuruyordu.
Barua zilipelekwa na tarishi katika majimbo yote ya mfalme zikiwa na amri ya kuharibu, kuua na kuangamiza Wayahudi wote, wadogo kwa wakubwa, wanawake na watoto wadogo, siku moja, yaani siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari, na pia kuteka nyara vitu vyao.
14 Bu fermanın metni her ilde yasa olarak duyurulacak ve bütün halklara bildirilecekti. Öyle ki, herkes belirlenen gün için hazır olsun.
Nakala ya andiko la amri ilipaswa kutolewa kama sheria katika kila jimbo, na kufahamishwa kwa watu wa kila taifa ili waweze kuwa tayari kwa siku ile.
15 Ulaklar kralın buyruğuyla hemen yola çıktılar. Ferman Sus Kalesi'nde de duyuruldu. Sus halkı şaşkınlık içindeyken kral ile Haman oturmuş içki içiyorlardı.
Kwa kuharakishwa na amri ya mfalme, matarishi walikwenda na andiko lilitolewa katika mji wa ngome ya Shushani. Mfalme na Hamani waliketi na kunywa, lakini mji wa Shushani ulifadhaika.

< Ester 3 >