< Amos 9 >

1 Rab'bi gördüm, Sunağın yanında duruyordu. “Sütun başlıklarına vur, Eşikler sarsılsın” dedi, “Başlıkları insanların başında parala. Sağ kalanları kılıçtan geçireceğim. Kaçan, kurtulan olmayacak,
Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema: “Piga vichwa vya nguzo ili vizingiti vitikisike. Viangushe juu ya vichwa vya watu wote; na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga. Hakuna awaye yote atakayekimbia, hakuna atakayetoroka.
2 Ölüler diyarını delip girseler, Elimi uzatıp onları çıkaracağım. Göklere çıksalar, Onları oradan indireceğim. (Sheol h7585)
Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha. (Sheol h7585)
3 Karmel Dağı'nın doruklarına gizlenseler, Artlarına düşüp onları yakalayacağım. Gözümün önünden uzağa, denizin dibine girseler, Orada yılana buyruk vereceğim, Onları sokacak.
Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli, huko nitawawinda na kuwakamata. Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu katika vilindi vya bahari, huko nako nitaamuru joka kuwauma.
4 Düşmanlarınca sürgün edilseler, Orada kılıca buyruk vereceğim, Onları biçecek. Gözümü üzerlerinden ayırmayacağım, Ama iyilik için değil, kötülük için.”
Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao, huko nako nitaamuru upanga uwaue. Nitawakazia macho yangu kwa mabaya wala si kwa mazuri.”
5 Rab, Her Şeye Egemen RAB Yere dokununca yer erir, Üzerinde yaşayan herkes yasa bürünür, Bütün yeryüzü Nil gibi kabarır, Mısır'ın ırmağı gibi yine alçalır.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza: nayo nchi yote huinuka kama Naili, kisha hushuka kama mto wa Misri;
6 Yukarı odalarını gökyüzünde yapan, Kubbesini yeryüzünde kuran, Denizin sularını çağırıp yeryüzüne döken O'dur; O'nun adı RAB'dir.
yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu na kuisimika misingi yake juu ya dunia, yeye aitaye maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake.
7 “Ey İsrailliler, Benim için Kûşlular'dan ne farkınız var?” Diyor RAB. “İsrailliler'i Mısır'dan, Filistliler'i Kaftor'dan, Aramlılar'ı Kîr'den çıkaran ben değil miyim?
“Je, Waisraeli, ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?” asema Bwana. “Je, sikuleta Israeli kutoka Misri, Wafilisti kutoka Kaftori, na Washamu kutoka Kiri?
8 “İşte, Egemen RAB'bin gözleri Bu günahlı krallığın üzerindedir. Onu yeryüzünden söküp atacağım, Ancak Yakup soyunu büsbütün yok etmeyeceğim” Diyor RAB.
“Hakika macho ya Bwana Mwenyezi yako juu ya ufalme wenye dhambi. Nami nitauangamiza kutoka kwenye uso wa dunia: hata hivyo sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,” asema Bwana.
9 “İşte buyruk vereceğim, Bütün uluslar arasından İsrail'i kalburla eler gibi eleyeceğim, Bir çakıl bile yere düşmeyecek.
“Kwa kuwa nitatoa amri, na nitaipepeta nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote, kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo, na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
10 Halkımın arasındaki bütün günahlılar, ‘Kötülük bizi bulmaz, bize erişmez’ diyenler Kılıçtan geçirilecek.”
Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu watauawa kwa upanga, wale wote wasemao, ‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
11 “O gün Davut'un yıkık çardağını yeniden kuracağım, Gediklerini kapayacak, Yıkık yerlerini onaracağım, Onu eskisi gibi yapacağım,
“Katika siku ile nitaisimamisha hema ya Daudi iliyoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
12 Öyle ki, Edomlular'ın sağ kalanlarını, Bana ait olan bütün ulusları sahiplensinler.” Bunu yapacak olan RAB böyle diyor.
ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.
13 “İşte, günler geliyor” diyor RAB, “Çift süren orakçıya, Üzüm basan ekin ekene erişecek, Dağlardan tatlı şarap damlayacak, Bütün tepelerden akacak.
“Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote.
14 Sürgün halkım İsrail'i geri getireceğim, Yıkık kentleri onarıp orada yaşayacaklar, Bağlar dikip şarabını içecekler, Bahçeler yapıp meyvesini yiyecekler.
Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani mwake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake.
15 Onları topraklarına dikeceğim, Bir daha sökülmeyecekler Kendilerine verdiğim topraktan.” Tanrınız RAB böyle diyor.
Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatangʼolewa tena kutoka nchi ambayo nimewapa,” asema Bwana Mungu wenu.

< Amos 9 >