< 2 Samuel 9 >

1 Davut, “Saul'un ailesinden daha sağ kalan, Yonatan'ın hatırı için iyilik edebileceğim kimse var mı?” diye sordu.
Daudi akauliza, “Je, hakuna mtu hata mmoja wa nyumba ya Sauli aliyebaki ambaye naweza kumtendea wema kwa ajili ya Yonathani?”
2 Saul'un ailesinin Siva adında bir hizmetkârı vardı. Onu Davut'un yanına çağırdılar. Kral, “Siva sen misin?” diye sordu. Siva, “Evet, ben kulunum” diye yanıtladı.
Basi palikuwepo mtumishi wa nyumba ya Sauli aliyeitwa Siba. Wakamwita aje mbele ya Daudi, naye mfalme akamwambia, “Wewe ndiwe Siba?” Akamjibu, “Naam, mimi ndiye mtumishi wako.”
3 Kral, “Saul'un ailesinden sağ kalan kimse yok mu?” diye sordu, “Tanrı'nın iyiliğini ona göstereyim.” Siva, “Yonatan'ın iki ayağı sakat bir oğlu var” diye yanıtladı.
Mfalme akauliza, “Je, hakuna yeyote ambaye amebaki wa nyumba ya Sauli ninayeweza kumwonyesha wema wa Mungu?” Siba akamjibu mfalme, “Bado yupo mwana wa Yonathani, yeye ni kiwete miguu yote.”
4 Kral, “Nerede o?” diye sordu. Siva, “Ammiel oğlu Makir'in Lo-Devar'daki evinde” diye karşılık verdi.
Mfalme akauliza, “Yuko wapi?” Siba akajibu, “Yuko nyumbani kwa Makiri mwana wa Amieli huko Lo-Debari.”
5 Böylece Kral Davut, Lo-Devar'dan Ammiel oğlu Makir'in evinden onu yanına getirtti.
Basi Mfalme Daudi akamtaka aletwe kutoka Lo-Debari, kutoka nyumbani kwa Makiri mwana wa Amieli.
6 Saul oğlu Yonatan oğlu Mefiboşet, Davut'un yanına gelince, onun önünde yere kapandı. Davut, “Mefiboşet!” diye seslendi. Mefiboşet, “Evet, ben kulunum” diye yanıtladı.
Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, alipofika kwa Daudi, akainama kumpa mfalme heshima. Daudi akamwita, “Mefiboshethi!” Mefiboshethi akajibu, “Ndimi mtumishi wako.”
7 Davut ona, “Korkma!” dedi, “Çünkü baban Yonatan'ın hatırı için, sana kesinlikle iyilik edeceğim. Atan Saul'un bütün toprağını sana geri vereceğim. Ve sen her zaman soframda yemek yiyeceksin.”
Daudi akamwambia, “Usiogope, kwa maana hakika nitakutendea wema kwa ajili ya baba yako Yonathani. Nitakurudishia ardhi yote iliyokuwa mali ya Sauli baba yako, nawe daima utakula chakula mezani pangu.”
8 Mefiboşet yere kapanıp şöyle dedi: “Kulun ne ki, benim gibi ölmüş bir köpekle ilgileniyorsun?”
Mefiboshethi akasujudu akasema, “Mimi mtumishi wako ni nini hata uangalie mbwa mfu kama mimi?”
9 Kral Davut, Saul'un hizmetkârı Siva'yı çağırtıp, “Önceden efendin Saul ile ailesine ait her şeyi torunu Mefiboşet'e verdim” dedi,
Ndipo mfalme akamwita Siba mtumishi wa Sauli na kumwambia, “Nimempa mwana wa bwana wako kila kitu kilichokuwa mali ya Sauli na jamaa yake.
10 “Sen, oğulların ve kölelerin onun için toprağı işleyip ürünü getireceksiniz. Öyle ki, efendinizin torununun yiyecek gereksinimi sağlansın. Efendinin torunu Mefiboşet her zaman benim soframda yemek yiyecektir.” Siva'nın on beş oğlu ve yirmi kölesi vardı.
Wewe, wanao na watumishi wako mtamlimia mashamba Mefiboshethi na kumletea mavuno, ili kwamba mwana wa bwana wako apate mahitaji yake. Naye Mefiboshethi mwana wa bwana wako atakula chakula mezani pangu daima.” (Siba alikuwa na wana kumi na watano, na watumishi ishirini.)
11 Siva, “Efendim kralın buyurduğu her şeyi yapacağım” dedi. Mefiboşet kralın çocuklarından biri gibi onun sofrasında yemek yedi.
Ndipo Siba akamwambia mfalme, “Mtumishi wako atafanya chochote bwana wangu mfalme atakachoagiza mtumishi wake kufanya.” Basi Mefiboshethi akala chakula mezani pa Daudi kama mmoja wa wana wa mfalme.
12 Mefiboşet'in Mika adında küçük bir oğlu vardı. Siva'ya bağlı herkes Mefiboşet'e hizmet ediyordu.
Mefiboshethi alikuwa na mwanawe mdogo aliyeitwa Mika, nao watu wote wa nyumba ya Siba walikuwa watumishi wa Mefiboshethi.
13 İki ayağı sakat Mefiboşet hep kralın sofrasında yemek yediğinden Yeruşalim'de oturuyordu.
Naye Mefiboshethi akaishi huko Yerusalemu, kwa sababu daima alikula mezani pa mfalme, naye alikuwa kiwete miguu yote.

< 2 Samuel 9 >