< 2 Krallar 7 >
1 Elişa, “RAB'bin sözüne kulak verin!” dedi, “RAB diyor ki, ‘Yarın bu saatlerde Samiriye Kapısı'nda bir sea ince un da, iki sea arpa da birer şekele satılacak.’”
Elisha akasema, “Sikiliza neno la Yahwe. Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kesho mda kama huu kipimo cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, kwenye lango la Samaria.””
2 Kralın özel yardımcısı olan komutan, Tanrı adamına, “RAB göklerin kapaklarını açsa bile olacak şey değil bu!” dedi. Elişa, “Sen her şeyi gözlerinle göreceksin, ama onlardan hiçbir şey yiyemeyeceksin!” diye karşılık verdi.
Basi yule nahodha ambaye alikuwa akitegemea mkono wake amemjibu mtu wa Mungu, na kusema, “Ona, hata kama Yahwe ataweka madirisha mbinguni, je jambo hili linawezekana?” Elisha akajibu, “Ona, utaona ikitokea kwa macho yako mwenyewe, lakini hutakula chochote katika hilo.”
3 Kent kapısının girişinde deri hastalığına yakalanmış dört adam vardı. Birbirlerine, “Ne diye ölene dek burada kalalım?” diyorlardı,
Basi, kulikuwa na watu wanne wenye ukoma upande wa nje wa lango la mji. Wakaambizana kila mmoja, “Kwa nini tukae hapa hadi hapo tutakapokufa?
4 “Kente girelim desek, orada kıtlık var, ölürüz; burada kalsak da öleceğiz. Bari gidip Aram ordugahına teslim olalım. Canımızı bağışlarlarsa yaşarız, öldürürlerse de öldürsünler.”
Kama tukisema kwamba tutaenda kwenye ule mji, maana mjini kuna njaa, na tutakufa hapo. Lakini kama tukiendelea kukaa hapa, bado tutakufa. Sawa, njoni, twendeni kwenye lile jeshi la Washami. Kama wakitupa uhai, tutakuwa hai, na kama wakituua, tutakufa tu.”
5 Akşam karanlığında kalkıp Aram ordugahına doğru gittiler. Ordugaha yaklaştıklarında, orada kimseyi göremediler.
Hivyo wakaamka asubuhi kabla giza halijaisha kwenda kwenye kambi ya Washami; Wakati walipofika sehemu ya mwanzo wa kambi, hapakuwa na mtu hapo.
6 Çünkü Rab Aram ordugahında savaş arabalarıyla, atlarıyla yaklaşan büyük bir ordunun çıkardığı seslerin duyulmasını sağlamıştı. Aramlılar da birbirlerine, “Bakın, İsrail Kralı bize saldırmak için Hitit ve Mısır krallarını kiralamış!” demişlerdi.
Kwa kuwa Bwana alikuwa ameunda jeshi la Washami kusikia sauti ya magari ya farasi, na sauti za farasi-sauti za jeshi jingine kubwa, ndipo wakaambizana kila mmoja wao, “Yule mfalme wa Israeli amekodisha wafalme wa Wahiti na Wamisri waje wapigane dhidi yetu.”
7 Böylece, gün batarken çadırlarını, atlarını, eşeklerini bırakıp kaçmışlar, canlarını kurtarmak için ordugahı olduğu gibi bırakmışlardı.
Hivyo wale maaskari wakaondoka kungali giza; waliacha mahema yao, punda zao, na kambi kama ilivyokuwa, na kukimbia kwa ajili ya maisha yao.
8 Deri hastalığına yakalanmış adamlar ordugaha varıp çadırların birine girdiler. Yiyip içtikten sonra oradaki altın, gümüş ve giysileri götürüp gizlediler. Sonra dönüp başka bir çadıra girdiler, orada bulduklarını da götürüp gizlediler.
Wakati wale watu wenye ukoma walipokuja sehemu ya mwisho wa kambi, wakaenda kwenye hema moja na kula na kunywa, na kubeba fedha na dhahabu na nguo, na kwenda na kuzificha. Wakarudi na kuingia kwenye hema nyingine na kubeba kutoka pale pia, na kwenda kuvificha.
9 Ardından birbirlerine, “Yaptığımız doğru değil” dediler, “Bugün müjde günü. Oysa biz susuyoruz. Gün doğuncaya kadar beklersek, cezaya çarptırılacağımız kesin. Haydi saraya gidip durumu bildirelim.”
Basi, wakaambizana kila mmoja, “Hatufanyi sahihi. Siku hii ni siku ya habari njema, lakini tunanyamaza kimya kuhusu hili. Kama tukisubiri mpaka kutakapopambazuka, adhabu itakuwa juu yetu. Basi, njoni, twendeni na kuwaambia nyumba ya mfalme.”
10 Böylece gidip kent kapısındaki nöbetçilere seslendiler. “Aram ordugahına gittik” dediler, “Hiç kimseyi göremedik; ne de bir insan sesi duyduk. Yalnızca bağlı atlar, eşekler vardı. Çadırları da olduğu gibi bırakıp gitmişler.”
Kwa hiyo wakaenda na kuwaita mabawabu wa mji. Wakawaambia, wakisema, “Tumeenda kambi ya Washami, lakini hapakuwa na mtu pale, hakuna sauti ya mtu yeyote, lakini kulikuwa na farasi wamefungwa, na punda wamefungwa, na zile hema kama zilivyokuwa.”
11 Kapı nöbetçileri haberi duyurdu. Haber kralın sarayına ulaştırıldı.
Ndipo mabawabu wakatoa habari, ndipo wakaambiwa ndani ya nyumba ya mfalme.
12 Kral gece kalkıp görevlilerine, “Aramlılar'ın ne tasarladığını size söyleyeyim” dedi, “Aç kaldığımızı biliyorlar. Onun için ordugahlarını bırakıp kırda gizlenmişler. Kentin dışına çıktığımızda, bizi canlı yakalayıp kenti ele geçirmeyi düşünüyorlar.”
Basi yule mfalme akainuka usiku nakusema kwa watumishi wake, “Nitawaambia sasa kile ambacho Washami walichotufanyia. Wanajua kwamba tunanjaa, hivyo wameondoka kwenye kambi kwenda kujificha kwenye mashamba. Wanasema, 'Wakati watakapotoka mjini, tutawakamata wakiwa hai, na kuingia mjini.”
13 Görevlilerden biri, “Kentte kalan beş atla birkaç adam gönderelim, o zaman durumu anlarız” dedi, “Nasıl olsa gidecek olanlar da burada, kentte kalan nice İsrailli gibi ölüme mahkûm!”
Mmoja wa wale watumishi wa mfalme akajibu na kusema, “Nakuomba, ngoja baadhi ya watu wachukue farasi watano wale waliosalia, ambao wamebaki kwenye mji. Wako kama mkutano wote wa Israeli waliobaki-wengi wamekufa; ngoja tuwatume na tuone.”
14 Adamlar yanlarına iki atlı araba aldılar. Kral, “Gidin, ne olduğunu öğrenin” diyerek onları Aram ordusunun ardından gönderdi.
Hivyo wakachukua magari mawili ya farasi pamoja na farasi, na mfalme akawatuma baada ya jeshi la Washami, akisema, “Enendeni mkaone.”
15 Adamlar Şeria Irmağı'na kadar Aram ordusunu izlediler. Yol baştan sona kadar Aramlılar'ın kaçarken attıkları giysi ve eşyalarla doluydu. Haberciler dönüp krala durumu bildirdiler.
Wakawafuata kwenda Yordani, na barabara zote zilikuwa zimejaa na vifaa ambavyo Washami walivitupa wapate kukimbia haraka. Kwa hiyo wale wajumbe wakarudi na kumwambia mfalme.
16 Bunun üzerine halk kentten çıkıp Aram ordugahını yağmaladı. RAB'bin dediği gibi, bir sea ince unun da, iki sea arpanın da fiyatı bir şekele düştü.
Wale watu wakatoka nje na wakaziteka nyara zile kambi za Washami. Hivyo kipimo cha unga mzuri uliuzwa kwa shekeli moja, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli moja, kama vile ambavyo neno la Yahwe lilivyosema.
17 Kral özel yardımcısı olan komutanı kentin kapısında bırakmıştı. Halk onu kapının ağzında çiğneyerek öldürdü. Kral Elişa'nın evine gittiğinde, Tanrı adamı ona olacakları önceden bildirmişti.
Naye mfalme alimwagiza yule nahodha ambaye alitegemea mkono wake kuwa mkuu wa lango, na watu wakamkanyaga chini langoni. Alikufa kama mtu wa Mungu alivyosema, ambaye ameongea wakati yule mfalme alipomshukia.
18 Her şey Tanrı adamının krala dediği gibi oldu. “Yarın bu saatlerde Samiriye Kapısı'nda bir sea ince un da, iki sea arpa da birer şekele satılacak” demişti.
Basi ikatokea kama yule mtu wa Mungu alivyosema kwa mfalme akisema, “Mda kama huu kwenye lango la Samaria, vipimo viwili vya shayiri vitapatikana kwa shekeli, na kipimo cha unga mzuri kwa shekeli.”
19 Komutan da Tanrı adamına şöyle karşılık vermişti: “RAB göklerin kapaklarını açsa bile, olacak şey değil bu!” Elişa, “Sen her şeyi gözlerinle görecek, ama onlardan hiçbir şey yiyemeyeceksin!” demişti.
Yule nahodha alimjibu yule mtu wa Mungu na kusema, “Tazama, hata kama Yahwe angefanya madirisha mbinguni, je hiki kitu kingeweza kutokea” Elisha akasema, “Tazama, utaona kikitokea kwa macho yako mwenyewe, lakini hutakula chochote katika hicho.”
20 Tam dediği gibi oldu. Komutan kentin kapısında halk tarafından çiğnenerek öldü.
Hivyo ndivyo haswa kilichompata, kwa kuwa watu wakamkanyaga kwenye lango, na kufa.