< 2 Krallar 7 >
1 Elişa, “RAB'bin sözüne kulak verin!” dedi, “RAB diyor ki, ‘Yarın bu saatlerde Samiriye Kapısı'nda bir sea ince un da, iki sea arpa da birer şekele satılacak.’”
Elisha akasema, “Sikiliza neno la Bwana. Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha, na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”
2 Kralın özel yardımcısı olan komutan, Tanrı adamına, “RAB göklerin kapaklarını açsa bile olacak şey değil bu!” dedi. Elişa, “Sen her şeyi gözlerinle göreceksin, ama onlardan hiçbir şey yiyemeyeceksin!” diye karşılık verdi.
Yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake akamwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?” Elisha akajibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!”
3 Kent kapısının girişinde deri hastalığına yakalanmış dört adam vardı. Birbirlerine, “Ne diye ölene dek burada kalalım?” diyorlardı,
Basi kulikuwepo na watu wanne wenye ukoma katika ingilio la lango la mji. Wakaambiana, “Kwa nini tukae hapa mpaka tufe?
4 “Kente girelim desek, orada kıtlık var, ölürüz; burada kalsak da öleceğiz. Bari gidip Aram ordugahına teslim olalım. Canımızı bağışlarlarsa yaşarız, öldürürlerse de öldürsünler.”
Kama tukisema, ‘Tutaingia mjini,’ mjini kuna njaa, nasi tutakufa humo. Kama tukikaa hapa, tutakufa. Kwa hiyo twende kwenye kambi ya Waaramu na tujisalimishe. Kama wakituacha hai, tutaishi; kama wakituua, basi na tufe.”
5 Akşam karanlığında kalkıp Aram ordugahına doğru gittiler. Ordugaha yaklaştıklarında, orada kimseyi göremediler.
Wakati wa giza la jioni, wakaondoka na kwenda kwenye kambi ya Waaramu. Walipofika mwanzo wa kambi, hapakuwa na mtu,
6 Çünkü Rab Aram ordugahında savaş arabalarıyla, atlarıyla yaklaşan büyük bir ordunun çıkardığı seslerin duyulmasını sağlamıştı. Aramlılar da birbirlerine, “Bakın, İsrail Kralı bize saldırmak için Hitit ve Mısır krallarını kiralamış!” demişlerdi.
kwa kuwa Bwana alilifanya jeshi la Waaramu lisikie sauti kama ya magari ya vita, farasi na jeshi kubwa, kiasi kwamba waliambiana, “Tazama, mfalme wa Israeli ameajiri mfalme wa Wahiti na mfalme wa Wamisri kuja kutushambulia sisi!”
7 Böylece, gün batarken çadırlarını, atlarını, eşeklerini bırakıp kaçmışlar, canlarını kurtarmak için ordugahı olduğu gibi bırakmışlardı.
Kwa hiyo wakaondoka na kukimbia wakati wa giza la jioni na kuacha mahema yao, farasi wao na punda wao. Wakakimbia kuokoa maisha yao na kuacha kila kitu ndani ya kambi kama kilivyokuwa.
8 Deri hastalığına yakalanmış adamlar ordugaha varıp çadırların birine girdiler. Yiyip içtikten sonra oradaki altın, gümüş ve giysileri götürüp gizlediler. Sonra dönüp başka bir çadıra girdiler, orada bulduklarını da götürüp gizlediler.
Wale watu wenye ukoma walipofika mwanzoni mwa kambi, wakaingia kwenye mojawapo ya mahema. Wakala na kunywa, na kuchukua fedha, dhahabu na nguo, wakaenda kuvificha. Wakarudi na kuingia katika hema jingine, na kuchukua baadhi ya vitu kutoka ndani yake na kuvificha pia.
9 Ardından birbirlerine, “Yaptığımız doğru değil” dediler, “Bugün müjde günü. Oysa biz susuyoruz. Gün doğuncaya kadar beklersek, cezaya çarptırılacağımız kesin. Haydi saraya gidip durumu bildirelim.”
Kisha wakaambiana, “Hili tunalolifanya sio jema. Hii ni siku ya habari njema, nasi tunakaa kimya. Kama tukisubiri mpaka mapambazuko, maafa yatatupata. Twendeni mara moja tukatoe habari hizi katika jumba la mfalme.”
10 Böylece gidip kent kapısındaki nöbetçilere seslendiler. “Aram ordugahına gittik” dediler, “Hiç kimseyi göremedik; ne de bir insan sesi duyduk. Yalnızca bağlı atlar, eşekler vardı. Çadırları da olduğu gibi bırakıp gitmişler.”
Hivyo wakaenda mjini na kuwaita walinzi wa langoni, wakawaambia, “Tulikwenda katika kambi ya Waaramu lakini hapakuwepo na mtu huko, hata sauti ya mtu yeyote, ila farasi na punda waliofungwa na mahema yaliyoachwa kama yalivyokuwa.”
11 Kapı nöbetçileri haberi duyurdu. Haber kralın sarayına ulaştırıldı.
Walinzi wa langoni wakatangaza habari ile kwa sauti kuu, na taarifa hii ikatolewa ndani ya jumba la mfalme.
12 Kral gece kalkıp görevlilerine, “Aramlılar'ın ne tasarladığını size söyleyeyim” dedi, “Aç kaldığımızı biliyorlar. Onun için ordugahlarını bırakıp kırda gizlenmişler. Kentin dışına çıktığımızda, bizi canlı yakalayıp kenti ele geçirmeyi düşünüyorlar.”
Mfalme akaamka usiku na kuwaambia maafisa wake, “Nitawaambia kile Waaramu walichotufanyia. Wanajua kwamba tuna njaa, hivyo wameacha kambi yao ili kujificha mashambani, wakifikiri, ‘Kwa hakika watatoka nje ya mji, nasi tutawakamata wakiwa hai na kuingia ndani ya mji.’”
13 Görevlilerden biri, “Kentte kalan beş atla birkaç adam gönderelim, o zaman durumu anlarız” dedi, “Nasıl olsa gidecek olanlar da burada, kentte kalan nice İsrailli gibi ölüme mahkûm!”
Mmoja wa maafisa wake akajibu, “Waamuru watu wachache wakawachukue farasi watano kati ya wale waliobaki katika mji. Hatima yao itakuwa kama ya Waisraeli wote walio hapa. Watakuwa tu kama Waisraeli hawa ambao wanangoja kifo. Hivyo tuwatumeni wajue kumetendeka nini.”
14 Adamlar yanlarına iki atlı araba aldılar. Kral, “Gidin, ne olduğunu öğrenin” diyerek onları Aram ordusunun ardından gönderdi.
Ndipo wakachagua magari mawili ya vita pamoja na farasi wake, naye mfalme akawatuma wafuatilie jeshi la Waaramu. Akawaamuru waendeshaji akisema, “Nendeni mkaone ni nini kilichotokea.”
15 Adamlar Şeria Irmağı'na kadar Aram ordusunu izlediler. Yol baştan sona kadar Aramlılar'ın kaçarken attıkları giysi ve eşyalarla doluydu. Haberciler dönüp krala durumu bildirdiler.
Wakawafuatia hadi Yordani, nao wakakuta barabara yote ikiwa imetapakaa nguo na vyombo vya Waaramu walivyokuwa wamevitupa walipokuwa wanatoroka. Basi wale wajumbe wakarudi na kutoa taarifa kwa mfalme.
16 Bunun üzerine halk kentten çıkıp Aram ordugahını yağmaladı. RAB'bin dediği gibi, bir sea ince unun da, iki sea arpanın da fiyatı bir şekele düştü.
Kisha watu wakatoka na kuteka nyara kambi ya Waaramu. Kwa hiyo kipimo cha unga mzuri kikauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
17 Kral özel yardımcısı olan komutanı kentin kapısında bırakmıştı. Halk onu kapının ağzında çiğneyerek öldürdü. Kral Elişa'nın evine gittiğinde, Tanrı adamı ona olacakları önceden bildirmişti.
Basi mfalme alikuwa amemweka yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake awe msimamizi wa lango. Nao watu wakamkanyaga walipoingia langoni, naye akafa, kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa ametangulia kusema wakati mfalme alipofika nyumbani kwake.
18 Her şey Tanrı adamının krala dediği gibi oldu. “Yarın bu saatlerde Samiriye Kapısı'nda bir sea ince un da, iki sea arpa da birer şekele satılacak” demişti.
Ikatokea kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa amemwambia mfalme: “Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha, na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”
19 Komutan da Tanrı adamına şöyle karşılık vermişti: “RAB göklerin kapaklarını açsa bile, olacak şey değil bu!” Elişa, “Sen her şeyi gözlerinle görecek, ama onlardan hiçbir şey yiyemeyeceksin!” demişti.
Yule afisa alikuwa amemwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?” Naye yule mtu wa Mungu alikuwa amemjibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!”
20 Tam dediği gibi oldu. Komutan kentin kapısında halk tarafından çiğnenerek öldü.
Ndivyo hasa ilivyotokea kwake, kwa kuwa watu walimkanyaga langoni, naye akafa.