< 2 Krallar 3 >

1 Yahuda Kralı Yehoşafat'ın krallığının on sekizinci yılında Ahav oğlu Yoram Samiriye'de İsrail Kralı oldu ve on iki yıl krallık yaptı.
Yehoramu mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili.
2 Yoram RAB'bin gözünde kötü olanı yaptıysa da annesiyle babası kadar kötü değildi. Çünkü babasının yaptırdığı Baal'ı simgeleyen dikili taşı kaldırıp attı.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini sio kama baba yake na mama yake walivyokuwa wamefanya. Akaondoa nguzo ya ibada ya Baali ambayo baba yake alikuwa ameitengeneza.
3 Bununla birlikte Nevat oğlu Yarovam'ın İsrail'i sürüklediği günahlara o da katıldı ve bu günahlardan ayrılmadı.
Hata hivyo akashikamana na dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, wala hakuziacha.
4 Moav Kralı Meşa koyun yetiştirirdi. İsrail Kralı'na her yıl yüz bin kuzu, yüz bin de koç yünü sağlamak zorundaydı.
Basi Mesha mfalme wa Moabu akafuga kondoo, naye akawa ampatie mfalme wa Israeli wana-kondoo 100,000 pamoja na sufu ya kondoo dume 100,000.
5 Ama Ahav'ın ölümünden sonra, Moav Kralı İsrail Kralı'na karşı ayaklandı.
Lakini baada ya Ahabu kufa, mfalme wa Moabu aliasi dhidi ya mfalme wa Israeli.
6 O zaman Kral Yoram Samiriye'den ayrıldı ve bütün İsrailliler'i bir araya topladı.
Kwa hiyo wakati ule Mfalme Yehoramu akaondoka kutoka Samaria na kukusanya Israeli yote tayari kwenda vitani.
7 Yahuda Kralı Yehoşafat'a da şu haberi gönderdi: “Moav Kralı bana başkaldırdı, benimle birlikte Moavlılar'a karşı savaşır mısın?” Yehoşafat, “Evet, savaşırım. Beni kendin, halkımı halkın, atlarımı atların say” dedi.
Akapeleka pia ujumbe ufuatao kwa Yehoshafati mfalme wa Yuda: “Mfalme wa Moabu ameasi dhidi yangu. Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Moabu?” Akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe. Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
8 Sonra, “Hangi yönden saldıralım?” diye sordu. Yoram, “Edom kırlarından” diye karşılık verdi.
Akauliza, “Je, tutashambulia kupitia njia gani?” Akajibu, “Kupitia Jangwa la Edomu.”
9 İsrail, Yahuda ve Edom kralları birlikte yola çıktılar. Dolambaçlı yollarda yedi gün ilerledikten sonra suları tükendi. Askerler ve hayvanlar susuz kaldı.
Hivyo mfalme wa Israeli akaondoka akiwa pamoja na mfalme wa Yuda na mfalme wa Edomu. Baada ya kuzunguka kwa siku saba, jeshi likawa limeishiwa maji kwa matumizi yao na kwa ajili ya wanyama waliokuwa nao.
10 İsrail Kralı, “Eyvah!” diye bağırdı, “RAB, Moavlılar'ın eline teslim etmek için mi üçümüzü bir araya topladı?”
Mfalme wa Israeli akamaka, “Nini! Je, Bwana ametuita sisi wafalme watatu ili tu kututia mikononi mwa Moabu?”
11 Yehoşafat, “Burada RAB'bin peygamberi yok mu? Onun aracılığıyla RAB'be danışalım” dedi. İsrail Kralı'nın adamlarından biri, “Şafat oğlu Elişa burada. İlyas'ın ellerine o su dökerdi” diye yanıtladı.
Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa, ili tuweze kumuuliza Bwana kupitia kwake?” Afisa mmoja wa mfalme wa Israeli akajibu, “Elisha mwana wa Shafati yuko hapa. Ndiye alikuwa akimimina maji juu ya mikono ya Eliya.”
12 Kral Yehoşafat, “O, RAB'bin ne düşündüğünü bilir” dedi. Bunun üzerine Yehoşafat, İsrail ve Edom kralları birlikte Elişa'nın yanına gittiler.
Yehoshafati akasema, “Neno la Bwana liko pamoja naye.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli na Yehoshafati pamoja na mfalme wa Edomu wakamwendea.
13 Elişa İsrail Kralı'na, “Ne diye bana geldin?” dedi, “Git, annenle babanın peygamberlerine danış.” İsrail Kralı, “Olmaz! Demek RAB üçümüzü Moavlılar'ın eline teslim etmek için bir araya toplamış” diye karşılık verdi.
Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Nina nini mimi nawe? Nenda kwa manabii wa baba yako na manabii wa mama yako.” Mfalme wa Israeli akajibu, “La hasha, kwa sababu ni Bwana ambaye ametuita pamoja sisi wafalme watatu ili atutie mikononi mwa Moabu.”
14 Elişa şöyle dedi: “Hizmetinde olduğum, Her Şeye Egemen, yaşayan RAB'bin adıyla derim ki, Yahuda Kralı Yehoşafat'a saygım olmasaydı, sana ne bakardım, ne de ilgilenirdim.
Elisha akasema, “Hakika, kama Bwana Mwenye Nguvu Zote aishivyo ambaye ninamtumikia, kama si kuheshimu Yehoshafati mfalme wa Yuda, nisingekutazama wala hata kukutupia jicho.
15 Şimdi bana lir çalan bir adam getirin.” Getirilen adam lir çalarken, RAB'bin gücü Elişa'nın üzerine indi.
Lakini sasa, nileteeni mpiga kinubi.” Mpiga kinubi alipokuwa akipiga, mkono wa Bwana ukaja juu ya Elisha,
16 Elişa şöyle dedi: “RAB diyor ki, ‘Bu vadinin başından sonuna kadar hendekler kazın.
naye akasema, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Chimbeni bonde hili lijae mahandaki.’
17 Ne rüzgar göreceksiniz, ne yağmur. Öyleyken vadi suyla dolup taşacak. Sizler, sürüleriniz ve öteki hayvanlarınız doyasıya içeceksiniz.
Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana: Hamtaona upepo wala mvua, lakini bonde hili litajaa maji, nanyi pamoja na ngʼombe wenu na wanyama wenu wengine mtakunywa.
18 RAB için bunu yapmak kolaydır. O, Moavlılar'ı da sizin elinize teslim edecek.
Hili ni jambo rahisi machoni pa Bwana. Pia ataitia Moabu mikononi mwenu.
19 Onların önemli surlu kentlerinin tümünü ele geçireceksiniz. Meyve ağaçlarının hepsini kesecek, su kaynaklarını kurutacak, verimli tarlalarına taş dolduracaksınız.’”
Mtaushinda kila mji wenye ngome na kila mji mkubwa. Mtakata kila mti ulio mzuri, mtaziba chemchemi zote, na kuharibu kila shamba zuri kwa mawe.”
20 Ertesi sabah, sununun sunulduğu saatte, Edom yönünden akan sular her yeri doldurdu.
Kesho yake asubuhi, karibu na wakati wa kutoa dhabihu ya asubuhi, tazama, maji yakawa yanatiririka kutoka upande wa Edomu! Nayo nchi ikajaa maji.
21 Moavlılar kralların kendilerine saldırmak üzere yola çıktıklarını duydular. Genç, yaşlı eli silah tutan herkes bir araya toplanıp sınırda beklemeye başladı.
Basi Wamoabu wote walikuwa wamesikia kuwa wale wafalme wamekuja kupigana dhidi yao. Hivyo kila mtu, kijana na mzee, ambaye angeweza kushika silaha akaitwa na kuwekwa mpakani.
22 Ertesi sabah erkenden kalktılar. Güneş ışınlarının kızıllaştırdığı suyu kan sanarak,
Walipoamka asubuhi na mapema, jua likawa linamulika juu ya maji. Wamoabu waliokuwa upande wa pili wakaona maji ni mekundu, kama damu.
23 “Kan bu!” diye haykırdılar, “Krallar kendi aralarında savaşıp birbirlerini öldürmüş olsalar gerek. Haydi, Moavlılar, yağmaya!”
Wamoabu wakasema, “Ile ni damu! Lazima hao wafalme wamepigana na kuchinjana wao kwa wao. Sasa Moabu, twendeni tukateke nyara!”
24 Ama Moavlılar İsrail ordugahına vardıklarında, İsrailliler saldırıp onları püskürttü. Moavlılar kaçmaya başladı. İsrailliler peşlerine düşüp onları öldürdüler.
Lakini Wamoabu walipofika kwenye kambi ya Israeli, Waisraeli wakainuka na kuwapiga mpaka wakakimbia. Nao Waisraeli wakaivamia nchi na kuwachinja Wamoabu.
25 Kentlerini yıktılar. Her İsrailli verimli tarlalara taş attı. Bütün tarlalar taşla doldu. Su kaynaklarını kuruttular, meyve ağaçlarını kestiler. Yalnız Kîr-Hereset'in taşları yerinde kaldı. Sapancılar kenti kuşatıp saldırıya geçti.
Wakaiharibu miji, kila mtu akatupa jiwe juu ya kila shamba zuri mpaka likafunikwa. Wakaziba chemchemi zote na kukata kila mti mzuri. Kir-Haresethi peke yake ndio uliobaki na mawe yake yakiwa mahali pake. Lakini hata hivyo watu waliokuwa na makombeo wakauzunguka na kuushambulia vilevile.
26 Moav Kralı, savaşı kaybettiğini anlayınca, yanına yedi yüz kılıçlı adam aldı; Edom kuvvetlerini yarıp kaçmak istediyse de başaramadı.
Mfalme wa Moabu alipoona kuwa vita vimekuwa vikali dhidi yake, akachukua watu 700 wenye panga ili kuingia kwa mfalme wa Edomu, lakini wakashindwa.
27 Bunun üzerine tahtına geçecek en büyük oğlunu surların üzerine götürüp yakmalık sunu olarak sundu. İsrailliler bu olaydan doğan büyük öfke karşısında oradan ayrılıp ülkelerine döndüler.
Ndipo akamchukua mwanawe mzaliwa wake wa kwanza, ambaye angekuwa mfalme baada yake, akamtoa kama dhabihu ya kuteketezwa juu ya ukuta wa mji. Ghadhabu ikawa kubwa dhidi ya Israeli; wakajiondoa kwake na kurudi katika nchi yao wenyewe.

< 2 Krallar 3 >