< 2 Tarihler 8 >
1 Süleyman RAB'bin Tapınağı'yla kendi sarayını yirmi yılda bitirdi.
Miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Solomoni alilijenga Hekalu la Bwana na jumba lake mwenyewe la kifalme,
2 Sonra Hiram'ın kendisine verdiği kentleri onarıp İsrailliler'in buralara yerleşmesini sağladı.
Solomoni akajenga tena vijiji vile ambavyo Hiramu alikuwa amempa, naye akawapa Waisraeli waishi humo.
3 Ardından Hamat-Sova üzerine yürüyerek orayı ele geçirdi.
Kisha Solomoni akaenda Hamath-Soba na kuuteka.
4 Çölde Tadmor Kenti'ni onardı. Hama yöresinde yaptırdığı bütün ambarlı kentlerin yapımını bitirdi.
Pia akajenga mji wa Tadmori katika jangwa na miji yote ya kuhifadhia vitu katika Hamathi.
5 Yukarı ve Aşağı Beythoron'u yeniden kurup çevrelerini surlarla, sürgülü kapılarla sağlamlaştırdı.
Akajenga tena Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, miji yenye ngome, kuta, malango na makomeo.
6 Baalat'ı ve yönetimindeki bütün ambarlı kentleri, savaş arabalarıyla atların bulunduğu kentleri de onarıp güçlendirdi. Böylece Yeruşalim'de, Lübnan'da, yönetimi altındaki bütün topraklarda her istediğini yaptırmış oldu.
Solomoni pia akajenga Baalathi na miji yake yote ya kuhifadhia vitu, na miji kwa ajili ya magari yake na kwa ajili ya farasi wake, chochote alichotaka kujenga katika Yerusalemu, katika Lebanoni na katika nchi yote aliyotawala.
7 İsrail halkından olmayan Hititler, Amorlular, Perizliler, Hivliler ve Yevuslular'dan artakalanlara gelince,
Watu wote waliosalia kutoka kwa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi (haya mataifa hayakuwa Waisraeli),
8 Süleyman İsrail halkının yok etmediği bu insanların soyundan gelip ülkede kalanları angaryaya koştu. Bu durum bugün de sürüyor.
yaani, wazao wao waliobakia katika nchi, ambao Waisraeli hawakuwa wamewaangamiza: hawa Solomoni akawalazimisha kuwa watumwa katika shokoa, kama ilivyo hadi leo.
9 Ancak İsrail halkından hiç kimseye kölelik yaptırmadı. Onlar savaşçı, birlik komutanı, savaş arabalarıyla atlıların komutanı olarak görev yaptılar.
Lakini Solomoni hakuwafanya Waisraeli watumwa kwa ajili ya kazi yake, bali walikuwa wapiganaji, majemadari, maafisa wake, majemadari wa magari yake ya vita na waendesha magari ya vita.
10 Kral Süleyman adına halkı denetleyen iki yüz elli görevli de İsrail halkındandı.
Pia walikuwa maafisa wakuu wa Mfalme Solomoni, yaani, maafisa wakaguzi 250 waliosimamia watu.
11 Süleyman, “Karım İsrail Kralı Davut'un sarayında kalmamalı. Çünkü RAB'bin Antlaşma Sandığı'nın girdiği yerler kutsaldır” diyerek firavunun kızını Davut Kenti'nden kendisi için yaptırdığı saraya getirtti.
Solomoni akampandisha mke wake binti Farao kutoka Mji wa Daudi na kumleta jumba la kifalme alilokuwa amemjengea, kwa kuwa alisema, “Mke wangu hataishi katika jumba la kifalme la Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu mahali ambapo Sanduku la Bwana limefika ni patakatifu.”
12 Tapınağın eyvanının önünde, yaptırdığı sunakta RAB'be yakmalık sunular sundu.
Mfalme Solomoni akamtolea Bwana dhabihu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana ambayo alikuwa ameijenga mbele ya ukumbi,
13 Şabat Günü, Yeni Ay, yılın üç bayramı –Mayasız Ekmek, Haftalar ve Çardak bayramları– için Musa'nın buyurduğu sunuları günü gününe sundu.
kulingana na mahitaji ya kila siku kwa ajili ya sadaka zilizoamriwa na Mose kwa ajili ya Sabato, Mwezi Mwandamo na sikukuu nyingine tatu za mwaka, yaani, Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma na Sikukuu ya Vibanda.
14 Babası Davut'un koyduğu kural uyarınca, kâhin bölüklerine ayrı ayrı görevler verdi. Levililer'i Tanrı'yı övme ve her günün gerektirdiği işlerde kâhinlere yardım etme görevine atadı. Kapı nöbetçilerini de bölüklerine göre değişik kapılarda görevlendirdi. Çünkü Tanrı adamı Davut böyle buyurmuştu.
Kwa kushika maagizo ya Daudi baba yake, aliweka migawanyo ya makuhani kwa ajili ya kazi zao, nao Walawi kuongoza kusifu na kusaidia makuhani kufuatana na mahitaji ya kila siku. Pia akaweka mabawabu katika migawanyo kwa ajili ya malango mbalimbali, kwa sababu hili ndilo Daudi mtu wa Mungu alilokuwa ameagiza.
15 Bunlar, hazine odalarına ilişkin konular dahil, hiçbir konuda kralın kâhinlerle Levililer'e verdiği buyruklardan ayrılmadılar.
Nao hawakuziacha amri za mfalme alizoamuru makuhani au Walawi katika jambo lolote, ikiwa ni pamoja na zile za hazina.
16 RAB'bin Tapınağı'nın temelinin atıldığı günden bitimine dek Süleyman'ın yapmak istediği her iş yerine getirildi. Böylece RAB'bin Tapınağı'nın yapımı tamamlanmış oldu.
Kazi yote ya Mfalme Solomoni ilifanyika kuanzia siku msingi wa Hekalu la Bwana ulipowekwa mpaka kukamilika kwake. Kwa hiyo Hekalu la Bwana likamalizika kujengwa.
17 Bundan sonra Süleyman Esyon-Gever'e, Edom kıyısındaki Eylat'a gitti.
Ndipo Solomoni akaenda Esion-Geberi na Elathi katika pwani ya Edomu.
18 Hiram ona denizi bilen gemiciler ve kendi görevlileri aracılığıyla gemiler gönderdi. Kral Süleyman'ın adamlarıyla birlikte Ofir'e giden bu gemiciler, dört yüz elli talant altın getirdiler.
Naye Hiramu alimpelekea meli zilizoongozwa na maafisa wake mwenyewe, watu waliokuwa na ujuzi wa baharini. Hawa watu pamoja na wale wa Solomoni wakasafiri kwa bahari mpaka Ofiri, wakaleta kutoka huko talanta 450 za dhahabu, ambazo walimkabidhi Mfalme Solomoni.