< 2 Tarihler 17 >
1 Asa'nın yerine oğlu Yehoşafat kral oldu. Yehoşafat İsrail'e karşı krallığını pekiştirdi.
Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake na akajiimarisha dhidi ya Israeli.
2 Yahuda'nın bütün surlu kentlerine askeri birlikler yerleştirdi; Yahuda'ya ve babası Asa'nın ele geçirmiş olduğu Efrayim kentlerine de asker yerleştirdi.
Akaweka jeshi katika miji yote ya Yuda yenye ngome na kuweka askari walinzi katika Yuda na katika miji ya Efraimu ile ambayo baba yake Asa alikuwa ameiteka.
3 RAB Yehoşafat'laydı. Çünkü Yehoşafat atası Davut'un başlangıçtaki yollarını izledi; Baallar'a yöneleceğine,
Bwana Mungu alikuwa na Yehoshafati kwa sababu katika miaka yake ya mwanzoni alienenda katika njia za Daudi baba yake. Hakutafuta Mabaali
4 babasının Tanrısı'na yöneldi; İsrail halkının yaptıklarına değil, Tanrı'nın buyruklarına uydu.
bali alimtafuta Mungu wa baba yake na kuzifuata amri zake badala ya kufuata desturi za watu wa Israeli.
5 RAB onun yönetimi altındaki krallığı pekiştirdi. Bütün Yahudalılar ona armağanlar getirdi. Böylece Yehoşafat büyük zenginliğe ve onura kavuştu.
Kwa hiyo Bwana akauimarisha ufalme chini ya uongozi wake, nao Yuda wote wakamletea Yehoshafati zawadi, hivyo akawa na utajiri mwingi na heshima.
6 Yüreği RAB'de cesaret buldu, puta tapılan yerleri ve Aşera putlarını Yahuda'dan kaldırdı.
Moyo wake ukawa hodari katika njia za Bwana na zaidi ya yote, akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na nguzo za Maashera katika Yuda.
7 Yehoşafat krallığının üçüncü yılında halka öğretmek amacıyla görevlilerinden Ben-Hayil'i, Ovadya'yı, Zekeriya'yı, Netanel'i, Mikaya'yı Yahuda kentlerine gönderdi.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa akatuma maafisa wake ambao ni: Ben-Haili, Obadia, Zekaria, Nethaneli na Mikaya ili kufundisha katika miji ya Yuda.
8 Onlarla birlikte şu Levililer'i de gönderdi: Şemaya, Netanya, Zevadya, Asahel, Şemiramot, Yehonatan, Adoniya, Toviya, Tov-Adoniya. Kâhinlerden Elişama ile Yehoram'ı gönderdi.
Pamoja nao walikuwepo Walawi fulani nao ni: Shemaya, Nethania, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobia, Tob-Adonia, pamoja nao walikuwepo makuhani Elishama na Yehoramu.
9 RAB'bin Yasa Kitabı'nı yanlarına alıp Yahuda'da halka öğrettiler. Bütün Yahuda kentlerini dolaşarak halka ders verdiler.
Wakafundisha Yuda yote, wakiwa wamechukua Kitabu cha Sheria ya Bwana wakazunguka miji yote ya Yuda na kufundisha watu.
10 Yahuda'yı çevreleyen ülkelerin krallıklarını RAB korkusu sardı. Bu yüzden Yehoşafat'a karşı savaşamadılar.
Hofu ya Bwana ikawa juu ya falme zote za nchi zilizozunguka Yuda, hivyo hawakufanya vita na Yehoshafati.
11 Bazı Filistliler Yehoşafat'a haraç olarak armağanlar ve gümüş verdiler. Araplar da ona davar getirdiler: Yedi bin yedi yüz koçla yedi bin yedi yüz teke.
Baadhi ya Wafilisti wakamletea Yehoshafati zawadi na fedha kama ushuru, nao Waarabu wakamletea mifugo: kondoo dume 7,700 na mbuzi 7,700.
12 Yehoşafat giderek güçlendi. Yahuda'da kaleler, ambarlı kentler yaptırdı.
Yehoshafati akaendelea kupata nguvu zaidi na zaidi, akajenga ngome na miji ya hazina katika Yuda
13 Yahuda kentlerinde birçok işler yaptı. Yeruşalim'e deneyimli yiğit savaşçılar yerleştirdi.
na akawa na wingi mkubwa wa vitu katika miji ya Yuda. Pia aliweka askari wa vita wenye uzoefu huko Yerusalemu.
14 Bunlar boylarına göre şöyle kaydedilmişlerdi: Yahuda'dan binbaşılar: Komutan Adna ve komutasında 300 000 yiğit asker;
Wakaandikishwa katika jamaa zao kama ifuatavyo: Kutoka Yuda, majemadari wa vikosi vya elfu: Jemadari Adna akiwa na askari wa vita 300,000;
15 Yanında Komutan Yehohanan ve komutasında 280 000 asker;
aliyefuata ni jemadari Yehohanani, akiwa na askari 280,000 walio tayari kwa vita;
16 Onun yanında kendini RAB'bin hizmetine adayan Zikri oğlu Amatsya ve komutasında 200 000 yiğit asker.
aliyefuata ni Amasia mwana wa Zikri, ambaye alijitolea kwa ajili ya kazi ya Bwana, akiwa na askari 200,000.
17 Benyamin oymağından: Yiğit bir savaşçı olan Elyada ile komutasında yay ve kalkanla silahlanmış 200 000 asker;
Kutoka Benyamini: Eliada, askari shujaa akiwa na watu 200,000 wenye silaha za nyuta na ngao;
18 Yanında Yehozavat ve komutasında savaşmak üzere donatılmış 180 000 asker.
aliyefuata ni Yehozabadi, akiwa na askari 180,000 wenye silaha za vita.
19 Bunlar kralın surlu Yahuda kentlerine yerleştirdiği askerlerin yanısıra, ona hizmet ediyorlardı.
Hawa ndio waliomtumikia mfalme, mbali na wale mfalme aliweka katika miji yenye ngome huko Yuda yote.