< 1 Samuel 23 >
1 Davut'a, “Filistliler Keila Kenti'ne saldırıp harmanları yağmalıyorlar” diye haber verdiler.
Wakamwambia Daudi, “Tazama, Wafilisti wanaupiga Keila na wanapora nafaka inayopurwa.”
2 Davut RAB'be, “Gidip şu Filistliler'e saldırayım mı?” diye danıştı. RAB, “Git, Filistliler'e saldır ve Keila Kenti'ni kurtar” diye yanıtladı.
Hivyo Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya msaada, na akamuuliza,” Je, niondoke niwapige hawa Wafilisti? BWANA akamwambia Daudi, “Nenda ukawapige Wafilisti na kuokoa Keila.”
3 Ama adamları Davut'a, “Bak, biz burada Yahuda'dayken korkuyoruz” dediler, “Keila'ya Filist ordusuna karşı savaşmaya gidersek büsbütün korkarız.”
Daudi akaambiwa na watu wake, “Angalia, hapa Yuda tunaogopa. Je, si zaidi sana kama tutaenda Keila kupambana na majeshi ya Wafilisti?”
4 Bunun üzerine Davut RAB'be bir kez daha danıştı. RAB ona yine, “Kalk, Keila'ya git! Çünkü Filistliler'i senin eline ben teslim edeceğim” dedi.
Ndipo Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya msaada, bado tena, BWANA akamjibu, “Amka, uteremke hadi Keila. Maana nitakupatia ushindi dhidi ya Wafilisti.”
5 Böylece Davut'la adamları Keila'ya gidip Filistliler'e karşı savaştılar. Davut onların hayvanlarını ele geçirdi. Filistliler'i ağır bir yenilgiye uğratarak Keila halkını kurtardı.
Daudi na watu wake wakaenda Keila na kupigana na Wafilisti. Wakahamisha ng'ombe wao na kuwapiga kwa mauaji makubwa mno. Hivyo Daudi akawaokoa wenyeji wa Keila.
6 Ahimelek'in oğlu Aviyatar kaçıp Keila'da bulunan Davut'a gittiğinde, efodu da birlikte götürmüştü.
Abiathari mwana wa Ahimeleki alipokuwa amekimbilia kwa Daudi huko Keila, alibeba naivera mkononi mwake.
7 Saul, Davut'un Keila Kenti'ne gittiğini duyunca, “Tanrı Davut'u elime teslim etti” dedi, “Davut sürgülü kapıları olan bir kente girmekle kendini hapsetmiş oldu.”
Sauli aliambiwa kwamba Daudi amekwenda Keila. Sauli akasema, “Mungu amemweka mkononi mwangu. Bila shaka amefungiwa ndani kwa sababu ameingia katika mji ulio na malango na makomeo.”
8 Böylece Saul, Keila'ya yürüyüp Davut'la adamlarını kuşatmak amacıyla bütün halkı savaşa çağırdı.
Sauli akayaita majeshi yake yote kwa ajili ya vita, waende hadi Keila, wamteke Daudi na watu wake.
9 Davut, Saul'un kendisine bir düzen kurduğunu duyunca, Kâhin Aviyatar'a, “Efodu getir” dedi.
Daudi alijua kwamba Sauli alikuwa anapanga njama za kumdhuru yeye. Ndipo akamwambia kuhani Abiathari kuhani, “Ulete hapa naivera.”
10 Sonra şöyle yakardı: “Ey İsrail'in Tanrısı RAB! Ben kulun yüzünden Saul'un gelip Keila'yı yıkmayı tasarladığına dair kesin haber aldım.
Kisha Daudi akasema, “BWANA, Mungu wa Israeli, mtumishi wako hakika amesikia kwamba Sauli anatafuta namna ya kuja Keila, ili auteketeze mji kwa ajili yangu.
11 Keila halkı beni onun eline teslim eder mi? Kulunun duymuş olduğu gibi Saul gelecek mi? Ey İsrail'in Tanrısı RAB, yalvarırım, kuluna bildir!” RAB, “Saul gelecek” yanıtını verdi.
Je, watu wa Keila watanisalimisha mkononi mwake? Je, Sauli atashuka hadi huko, kama mtumishi wako alivyosikia? BWANA, Mungu wa Israeli, nakusihi, tafadhali mwambie mtumishi wako. “BWANA akasema, “Atakuja huko.”
12 Davut RAB'be, “Keila halkı beni ve adamlarımı Saul'un eline teslim edecek mi?” diye sordu. RAB, “Teslim edecek” dedi.
Kisha Daudi akauliza, “Je, watu wa Keila watanisalimisha mimi na watu wangu katika mkono wa Sauli?” BWANA akasema, “Watu hao watawasalimisha kwao.”
13 Bunun üzerine Davut ile yanındaki altı yüz kadar kişi Keila'dan ayrılıp oradan oraya yer değiştirmeye başladılar. Davut'un Keila'dan kaçtığını öğrenen Saul oraya gitmekten vazgeçti.
Kisha Daudi na watu wake, waliokuwa kama mia sita, walitoka na kwenda mbali na Keila, na wakazunguka kila sehemu. Kisha Sauli akaambiwa kwamba Daudi ametoroka kutoka Keila, hivyo akasitisha kumfuatia.
14 Davut kırsal bölgedeki sığınaklarda ve Zif Çölü'nün dağlık kesiminde kaldı. Saul her gün Davut'u aradığı halde, Tanrı onu Saul'un eline teslim etmedi.
Daudi alikaa ngomeni katika jangwa, kwenye nchi ya milima katika jangwa la Zifu. Kila siku Sauli alimtafuta, lakini Mungu hakumweka mkononi mwake.
15 Davut Zif Çölü'nde, Horeş'teyken, Saul'un kendisini öldürmek için yola çıktığını öğrendi.
Daudi aliona kwamba Sauli amejitokeza kuangamiza maisha yake; basi Daudi alikuwa katika jjangwa la Zifu huko Horeshi.
16 Bu arada Saul oğlu Yonatan kalkıp Horeş'e, Davut'un yanına gitti ve onu Tanrı'nın adıyla yüreklendirdi.
Kisha Yonathani, mwana wa Sauli, akaamuka akaenda kwa Daudi huko Horshi, naye akamtia moyo amtumainie Mungu.
17 “Korkma!” dedi, “Babam Saul sana dokunmayacak. Sen İsrail Kralı olacaksın, ben de senin yardımcın olacağım. Babam Saul da bunu biliyor.”
Akamwambia, “Usiogope. Kwa maana mkono wa baba yangu Sauli hautakupata. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, na mimi nitakuwa msaidizi wako. Baba yangu Sauli pia anajua hivyo.”
18 İkisi de RAB'bin önünde aralarındaki antlaşmayı yenilediler. Sonra Yonatan evine döndü, Davut ise Horeş'te kaldı.
Basi wote wawili wakafanya agano mbele za BWANA. Kisha Daudi alibaki Horeshi, na Yonathani akaenda nyumbani.
19 Zifliler Giva'ya gidip Saul'a, “Davut aramızda” dediler, “Yeşimon'un güneyinde, Hakila Tepesi'ndeki Horeş sığınaklarında gizleniyor.
Nndipo Wazifi wakamwendea Sauli huko Gibea wakisema, “Je, Daudi hakujificha kati yetu kwenye ngome huko Horeshi, juu ya mlima wa Hakila, ulioko kusini mwa Yeshimoni?
20 Ey kral, ne zaman gelmek istersen gel! Davut'u kralın eline teslim etmeyi ise bize bırak.”
Basi uje, mfalme! Kulingana na matakwa yako, uje! Kazi yetu itakuwa kumtia katika mkono wa mfalme.”
21 Saul, “RAB sizi kutsasın! Bana acıdınız” dedi,
Sauli akasema, “Mbarikiwe na BWANA. Kwa sababu mmenihurumia.
22 “Gidin ve bir daha araştırın; Davut'un genellikle nerelerde gizlendiğini, orada onu kimin gördüğünü iyice öğrenin. Çünkü onun çok kurnaz olduğunu söylüyorlar.
Nendeni, mhakikishe sawasawa. Tafuteni na kujua maficho yake yako wapi na ni nani amemwona huko. Nimeambiwa kwamba yeye ni mjanja sana.
23 Gizlendiği yerlerin hepsini öğrenip bana kesin bir haber getirin. O zaman ben de sizinle gelirim. Eğer Davut o bölgedeyse, bütün Yahuda boyları içinde onu arayıp bulacağım.”
Kwa hiyo chunguzeni, mjue sehemu zote anakojificha. Baadaye rudini kwangu mkiwa na taarifa kamili, na kisha nitaongozana nanyi. Ikiwa yupo katika nchi, nitamtafuta kutoka miongoni mwa elfu zote za Yuda.”
24 Böylece Zifliler kalkıp Saul'dan önce Zif'e gittiler. O sırada Davut'la adamları Yeşimon'un güneyindeki Arava'da, Maon Çölü'ndeydiler.
Ndipo wakaamka na kwenda hadi Zifu mbele ya Sauli. Wakati huo Daudi na watu wake walikuwa katika jangwa la Maoni, huko Araba upande wa kusini mwa Yeshimoni.
25 Saul ile adamlarının kendisini aramaya geldiklerini öğrenince Davut aşağıya inip Maon Çölü'ndeki kayalığa sığındı. Saul bunu duyunca Davut'un ardından Maon Çölü'ne gitti.
Sauli na watu wake wakaenda kumtafuta Daudi. Na Daudi akaambiwa habari hiyo, hivyo akateremka hadi kwenye mlima wa miamba na akakaa katika jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hivyo, akamfukuza Daudi katika Jangwa la Maoni.
26 Saul dağın bir yanından, Davut'la adamları ise öbür yanından ilerliyordu. Davut Saul'dan kaçıp kurtulmaya çalışıyordu. Saul'la askerleri Davut'la adamlarını yakalamak üzere yaklaşırken,
Sauli akaenda akawa upande mmoja wa mlima, na Daudi na watu wake walikuwa wakienda upande mwingine wa mlima. Daudi kwa haraka akatoweka akae mbali na Sauli. Kwa sababu Sauli na watu wake walikuwa wakimzunguka Daudi na watu wake wawakamate,
27 bir ulak gelip Saul'a şöyle dedi: “Çabuk gel! Filistliler ülkeye saldırıyor.”
mjumbe mmoja akaja kwa Sauli na kusema, “Njoo, harakisha maana Wafilisti wamepanga uvamizi juu ya nchi.”
28 Bunun üzerine Saul Davut'u kovalamayı bırakıp Filistliler'le savaşmaya gitti. Bu yüzden oraya Sela-Hammahlekot adı verildi.
Kwa hiyo Sauli akarudi asimfuatie Daudi na akaenda kupambana na Wafilisti. Kwa hiyo sehemu ile iliitwa Mwamba wa Maficho.
29 Davut oradan ayrılıp Eyn-Gedi bölgesindeki sığınaklara gizlendi.
Daudi akapanda kutoka huko na kukaa katika ngome ya Engedi.