< 1 Samuel 17 >
1 Savaşmak üzere ordularını bir araya getiren Filistliler, Yahuda'nın Soko Kenti'nde toplandılar. Soko ile Azeka Kenti arasındaki Efes-Dammim'de ordugah kurdular.
Wakati huu Wafilisti wakakusanya majeshi yao kwa ajili ya vita, nao wakakusanyika huko Soko katika Yuda. Wakapiga kambi huko Efes-Damimu, kati ya Soko na Azeka.
2 Saul ile İsrailliler de toplandılar. Ela Vadisi'nde ordugah kurup Filistliler'e karşı savaş düzeni aldılar.
Sauli na Waisraeli wakakusanyika na kupiga kambi katika Bonde la Ela na kupanga jeshi ili kupigana vita na Wafilisti.
3 Filistliler tepenin bir yanında, İsrailliler de karşı tepede yerlerini aldı. Aralarında vadi vardı.
Wafilisti wakawa katika kilima kimoja na Waisraeli katika kilima kingine, hilo bonde likiwa kati yao.
4 Filist ordugahından Gatlı Golyat adında usta bir dövüşçü ortaya çıktı. Boyu altı arşın bir karıştı.
Shujaa aliyeitwa Goliathi, aliyetoka Gathi, akajitokeza kutoka kambi ya Wafilisti. Alikuwa na urefu dhiraa sita na shibiri moja.
5 Başına tunç miğfer takmış, pullu bir zırh kuşanmıştı. Tunç zırhın ağırlığı beş bin şekeldi.
Alikuwa na chapeo ya shaba kichwani mwake, na alivaa dirii ya shaba kifuani mwake yenye uzito wa shekeli elfu tano.
6 Baldırları zırhlarla korunmuştu. Omuzları arasında tunç bir pala asılıydı.
Miguuni mwake alivaa mabamba ya shaba, na alikuwa na mkuki wa shaba mgongoni mwake.
7 Mızrağının sapı dokumacı tezgahının sırığı gibiydi. Mızrağın demir başının ağırlığı altı yüz şekeldi. Golyat'ın önüsıra kalkanını taşıyan bir adam yürüyordu.
Mpini wa huo mkuki ulikuwa kama mti wa mfumaji, na ncha ya chuma yake ilikuwa na uzito wa shekeli mia sita. Mbeba ngao wake alitangulia mbele yake.
8 Golyat durup İsrail ordusuna, “Neden savaş düzeni aldınız?” diye haykırdı, “Ben Filistli'yim, sizse Saul'un kölelerisiniz. Aranızdan karşıma çıkacak birini seçin.
Goliathi alisimama na kuwapigia kelele majeshi ya Israeli, akisema, “Kwa nini mmetoka kupanga vita? Je, mimi si Mfilisti, na ninyi ni watumishi wa Sauli? Chagueni mtu na anishukie mimi.
9 Dövüşte beni yenip öldürebilirse, biz sizin köleniz oluruz. Ama ben üstün gelip onu yok edebilirsem, siz bizim kölemiz olur, bize kulluk edersiniz.”
Kama anaweza kupigana nami na kuniua, tutakuwa chini yenu; lakini kama nikimshinda na kumuua, ninyi mtakuwa chini yetu na mtatutumikia.”
10 Filistli Golyat konuşmasını şöyle sürdürdü: “Bugün İsrail ordusuna meydan okuyorum! Benimle dövüşecek birini çıkarın karşıma!”
Kisha yule Mfilisti akasema, “Siku hii ya leo nayatukana majeshi ya Israeli! Nipeni mtu tupigane.”
11 Filistli'nin bu sözlerini duyunca, Saul da İsrailliler de çok korkup dehşet içinde kaldılar.
Kwa kusikia maneno ya Wafilisti, Sauli na Waisraeli wote wakafadhaika na kuogopa.
12 Davut Yahuda'nın Beytlehem Kenti'nden Efratlı İşay adında bir adamın oğluydu. İşay'ın sekiz oğlu vardı. Saul'un krallığı döneminde İşay'ın yaşı oldukça ilerlemişti.
Basi Daudi alikuwa mwana wa Mwefrathi jina lake Yese aliyekuwa ametoka Bethlehemu ya Yuda. Yese alikuwa na wana wanane, naye wakati wa Sauli alikuwa mzee tena wa umri mkubwa.
13 İşay'ın üç büyük oğlu Saul'la birlikte savaşa katılmıştı. Savaşa giden en büyük oğlunun adı Eliav, ikincisinin adı Avinadav, üçüncüsünün adıysa Şamma'ydı.
Wana wakubwa watatu wa Yese walikuwa wamefuatana na Sauli vitani: Mzaliwa wa kwanza alikuwa Eliabu, wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama.
14 Davut en küçükleriydi. Üç büyük oğul Saul'un yanındaydı.
Daudi ndiye alikuwa mdogo wa wote. Hao wakubwa watatu wakamfuata Sauli,
15 Davut ise babasının sürüsüne bakmak için Saul'un yanından ayrılıp Beytlehem'e gider gelirdi.
lakini Daudi alikuwa akienda kwa Sauli na kurudi ili kuchunga kondoo wa baba yake huko Bethlehemu.
16 Filistli Golyat kırk gün boyunca sabah akşam ortaya çıkıp meydan okudu.
Kwa siku arobaini huyo Mfilisti alikuwa akija mbele kila siku asubuhi na jioni na kujionyesha.
17 Bir gün İşay, oğlu Davut'a şöyle dedi: “Kardeşlerin için şu kavrulmuş bir efa buğdayla on somun ekmeği al, çabucak ordugaha, kardeşlerinin yanına git.
Wakati huo Yese akamwambia mwanawe Daudi, “Chukua hii efa ya bisi na hii mikate kumi kwa ajili ya ndugu zako uwapelekee upesi kambini mwao.
18 Şu on parça peyniri de birlik komutanına götür. Kardeşlerinin ne durumda olduğunu öğren ve iyi olduklarına ilişkin bir belirti getir.
Chukua pamoja na hizi jibini kumi kwa jemadari wa kikosi chao. Ujue hali ya ndugu zako na uniletee taarifa za uhakika kutoka kwao.
19 Kardeşlerin Saul ve öbür İsrailliler'le birlikte Ela Vadisi'nde Filistliler'e karşı savaşıyorlar.”
Wao wako pamoja na Sauli na watu wote wa Israeli huko kwenye Bonde la Ela, wakipigana na Wafilisti.”
20 Ertesi sabah Davut erkenden kalktı. Sürüyü bir çobana bıraktı. İşay'ın buyurduğu gibi erzağı alıp yola koyuldu. Ordugaha vardığı sırada askerler savaş naraları atarak savaş düzenine giriyorlardı.
Asubuhi na mapema Daudi akaondoka, akaliacha kundi la kondoo pamoja na mchungaji, akapakia vitu vile na kuondoka, kama vile Yese alivyokuwa amemwagiza. Akafika kambini wakati jeshi lilikuwa likitoka kwenda kwenye sehemu yake ya kupigania, huku wakipiga kelele za vita.
21 İsrailliler'le Filistliler karşı karşıya savaş düzeni almışlardı.
Israeli na Wafilisti walikuwa wakipanga safu zao wakitazamana.
22 Davut getirdiklerini levazım görevlisine bırakıp cepheye koştu; kardeşlerinin yanına varıp onları selamladı.
Daudi akaacha vile vitu vyake kwa mtunza vifaa, akakimbilia katika safu za vita na kuwasalimu ndugu zake.
23 Davut onlarla konuşurken, Gatlı Filistli, Golyat adındaki dövüşçü Filist cephesinden ileri çıkarak daha önce yaptığı gibi meydan okudu. Davut bunu duydu.
Alipokuwa akisema nao, Goliathi, yule Mfilisti shujaa kutoka Gathi, akajitokeza mbele ya safu zake na kupiga ile kelele yake ya kawaida ya matukano, naye Daudi akayasikia.
24 İsrailliler Golyat'ı görünce büyük korkuyla önünden kaçıştılar.
Waisraeli walipomwona yule mtu, wote wakamkimbia kwa woga mkuu.
25 Birbirlerine, “İsrail'e meydan okumak için ortaya çıkan şu adamı görüyorsunuz ya!” diyorlardı, “Kral onu öldürene büyük bir armağanın yanısıra kızını da verecek. Babasının ailesini de İsrail'e vergi ödemekten muaf tutacak.”
Basi Waisraeli walikuwa wakisema, “Je, mnaona jinsi mtu huyu anavyoendelea kujitokeza. Hujitokeza ili kutukana Israeli. Mfalme atatoa utajiri mwingi kwa yule mtu atakayemuua. Pia atamwoza binti yake na atasamehe jamaa ya baba yake kulipa kodi katika Israeli.”
26 Davut yanındakilere, “Bu Filistli'yi öldürüp İsrail'den bu utancı kaldıracak kişiye ne verilecek?” diye sordu, “Bu sünnetsiz Filistli kim oluyor da yaşayan Tanrı'nın ordusuna meydan okuyor?”
Daudi akauliza watu waliokuwa wamesimama karibu naye, “Je, atafanyiwa nini mtu atakayemuua huyu Mfilisti na kuondoa aibu hii katika Israeli? Ni nani huyu Mfilisti asiyetahiriwa hata atukane majeshi ya Mungu aliye hai?”
27 Adamlar daha önce verilmiş olan söze göre Golyat'ı öldürecek kişiye neler verileceğini anlattılar.
Wakarudia yale yaliyokuwa yamesemwa na kumwambia kuwa, “Hili ndilo atakalotendewa mtu yule atakayemuua.”
28 Ağabeyi Eliav Davut'un adamlarla konuştuğunu duyunca öfkelendi. “Ne işin var burada?” dedi, “Çöldeki üç beş koyunu kime bıraktın? Ne kadar kendini beğenmiş ve ne kadar kötü yürekli olduğunu biliyorum. Sadece savaşı görmeye geldin.”
Eliabu nduguye mkubwa Daudi alipomsikia akizungumza na watu hasira ikawaka juu yake akamuuliza, “Kwa nini umeteremka kuja hapa? Nao wale kondoo wachache kule nyikani umewaacha na nani? Ninajua jinsi ulivyo na kiburi na jinsi moyo wako ulivyo mwovu; umekuja hapa kutazama vita tu.”
29 Davut, “Ne yaptım ki?” dedi, “Bir soru sordum, o kadar.”
Daudi akasema, “Sasa nimefanya nini? Je, siwezi hata kuongea.”
30 Sonra başka birine dönüp aynı soruyu sordu. Adamlar öncekine benzer bir yanıt verdiler.
Daudi akamgeukia mtu mwingine na kumuuliza jambo lilo hilo, nao watu wakamjibu vilevile kama mwanzo.
31 Davut'un söylediklerini duyanlar Saul'a ilettiler. Saul onu çağırttı.
Lile Daudi alilosema likasikiwa na kuelezwa kwa Sauli, naye Sauli akatuma aitwe.
32 Davut Saul'a, “Bu Filistli yüzünden kimse yılmasın! Ben kulun gidip onunla dövüşeceğim!” dedi.
Daudi akamwambia Sauli, “Mtu yeyote asife moyo kwa habari ya huyu Mfilisti; mtumishi wako atakwenda kupigana naye.”
33 Saul, “Sen bu Filistli'yle dövüşemezsin” dedi, “Çünkü daha gençsin, o ise gençliğinden beri savaşçıdır.”
Sauli akamjibu Daudi, “Wewe hutaweza kwenda kupigana dhidi ya huyu Mfilisti; wewe ni kijana tu, naye amekuwa mtu wa vita tangu ujana wake.”
34 Ama Davut, “Kulun babasının sürüsünü güder” diye karşılık verdi, “Bir aslan ya da ayı gelip sürüden bir kuzu kaçırınca,
Lakini Daudi akamwambia Sauli, “Mtumishi wako amekuwa akichunga kondoo wa baba yake. Wakati simba au dubu alikuja na kuchukua kondoo kutoka kundi,
35 peşinden gidip ona saldırır, kuzuyu ağzından kurtarırım. Eğer aslan ya da ayı üzerime gelirse, boğazından tuttuğum gibi vurur öldürürüm.
nilifuatia, nikampiga na nikampokonya kondoo kwenye kinywa chake. Aliponigeukia, nilimkamata nywele zake, nikampiga na kumuua.
36 Kulun, aslan da ayı da öldürmüştür. Bu sünnetsiz Filistli de onlar gibi olacak. Çünkü yaşayan Tanrı'nın ordusuna meydan okudu.
Mtumishi wako ameshaua simba na dubu pia; huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wa hao, kwa sababu ameyatukana majeshi ya Mungu aliye hai.
37 Beni aslanın, ayının pençesinden kurtaran RAB, bu Filistli'nin elinden de kurtaracaktır.” Saul, “Öyleyse git, RAB seninle birlikte olsun” dedi.
Bwana ambaye aliniokoa toka katika makucha ya simba na makucha ya dubu ataniokoa kutoka mikono ya huyu Mfilisti.” Sauli akamwambia Daudi, “Nenda, naye Bwana na awe pamoja nawe.”
38 Sonra kendi giysilerini Davut'a verdi; başına tunç miğfer taktı, ona bir zırh giydirdi.
Ndipo Sauli akamvika Daudi silaha zake mwenyewe za vita. Akamvika dirii na chapeo ya shaba kichwani mwake.
39 Davut giysilerinin üzerine kılıcını kuşanıp yürümeye çalıştı. Çünkü bu giysilere alışık değildi. Saul'a, “Bunlarla yürüyemiyorum” dedi, “Çünkü alışık değilim.” Sonra giysileri üzerinden çıkardı.
Daudi akajifunga upanga juu ya hayo mavazi na kujaribu kutembea kwa sababu alikuwa hana uzoefu navyo. Daudi akamwambia Sauli, “Siwezi kwenda nikiwa nimevaa hivi, kwa sababu sina uzoefu navyo.” Hivyo akavivua.
40 Değneğini alıp dereden beş çakıl taşı seçti. Bunları çoban dağarcığının cebine koyduktan sonra sapanını alıp Filistli Golyat'a doğru ilerledi.
Kisha akachukua fimbo yake mkononi, akachagua mawe laini matano kutoka kwenye kijito, akayaweka kwenye kifuko ndani ya mfuko wake wa kichungaji, akiwa na kombeo yake mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti.
41 Filistli de, önünde kalkan taşıyıcısı, Davut'a doğru ilerliyordu.
Wakati ule ule, yule Mfilisti, akiwa na mbeba ngao wake mbele yake, akaendelea kujongea karibu na Daudi.
42 Davut'u tepeden tırnağa süzdü. Kızıl saçlı, yakışıklı bir genç olduğu için onu küçümsedi.
Mfilisti akamwangalia Daudi kote na kumwona kuwa ni kijana tu, mwekundu na mzuri wa kupendeza, naye akamdharau.
43 “Ben köpek miyim ki, üzerime değnekle geliyorsun?” diyerek kendi ilahlarının adıyla Davut'u lanetledi.
Akamwambia Daudi, “Je, mimi ni mbwa, hata unanijia na fimbo?” Yule Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.
44 “Bana gelsene! Bedenini gökteki kuşlara ve kırdaki hayvanlara yem edeceğim!” dedi.
Tena Mfilisti akamwambia, “Njoo hapa, nami nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni nyama yako.”
45 Davut, “Sen kılıçla, mızrakla, palayla üzerime geliyorsun” diye karşılık verdi, “Bense meydan okuduğun İsrail ordusunun Tanrısı, Her Şeye Egemen RAB'bin adıyla senin üzerine geliyorum.
Daudi akamwambia yule Mfilisti. “Wewe unanijia na upanga, mkuki na fumo, lakini mimi ninakujia kwa jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa majeshi ya Israeli, ambaye wewe umemtukana.
46 Bugün RAB seni elime teslim edecek. Seni vurup başını gövdenden ayıracağım. Bugün Filistli askerlerin leşlerini gökteki kuşlarla yerdeki hayvanlara yem edeceğim. Böylece bütün dünya İsrail'de Tanrı'nın var olduğunu anlayacak.
Siku hii leo Bwana atakutia mkononi mwangu, nami nitakupiga na kukukata kichwa chako. Leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya jeshi la Wafilisti, nayo dunia yote itajua kuwa yuko Mungu katika Israeli.
47 Bütün bu topluluk RAB'bin kılıçla, mızrakla kurtarmadığını anlayacak. Çünkü savaş zaten RAB'bindir! O sizi elimize teslim edecek.”
Wale wote waliokusanyika hapa watajua kuwa Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; kwa kuwa vita ni vya Bwana, naye atawatia wote mikononi mwetu.”
48 Golyat saldırmak amacıyla Davut'a doğru ilerledi. Davut da onunla dövüşmek üzere hemen Filist cephesine doğru koştu.
Yule Mfilisti aliposogea karibu ili kumshambulia, Daudi akaenda mbio kuelekea safu ya vita kukutana naye.
49 Elini dağarcığına sokup bir taş çıkardı, sapanla fırlattı. Taş Filistli'nin alnına çarpıp saplandı. Filistli yüzükoyun yere düştü.
Daudi akatia mkono wake mfukoni na kuchukua jiwe, akalirusha kwa kombeo, nalo likampiga yule Mfilisti kwenye paji la uso. Lile jiwe likaingia kipajini mwa uso, akaanguka chini kifudifudi.
50 Böylece Davut Filistli Golyat'ı sapan ve taşla yendi. Elinde kılıç olmaksızın onu yere serdi.
Basi Daudi akamshinda huyo Mfilisti kwa kombeo na jiwe; bila kuwa na upanga mikononi mwake akampiga huyo Mfilisti na kumuua.
51 Sonra koşup üzerine çıktı. Golyat'ın kılıcını tutup kınından çektiği gibi onu öldürdü ve başını kesti. Kahraman Golyat'ın öldüğünü gören Filistliler kaçtılar.
Daudi akakimbia na kusimama juu yake. Akaushika upanga wa huyo Mfilisti na kuuvuta toka kwenye ala yake. Baada ya kumuua, akakata kichwa chake kwa ule upanga. Wafilisti walipoona kuwa shujaa wao amekufa, wakageuka na kukimbia.
52 İsrailliler'le Yahudalılar kalkıp Gat'ın girişine ve Ekron kapılarına kadar nara atarak onları kovaladılar. Filistliler'in ölüleri Gat'a, Ekron'a kadar Şaarayim yolunda yerlere serildi.
Ndipo watu wa Israeli na Yuda wakainuka kwenda mbele wakipiga kelele na kufuatia Wafilisti mpaka kwenye ingilio la Gathi kwenye malango ya Ekroni. Maiti zao zilitawanyika kando ya barabara ya Shaaraimu hadi Gathi na Ekroni.
53 Filistliler'i kovaladıktan sonra geri dönen İsrailliler Filist ordugahını yağmaladılar.
Waisraeli waliporudi kutoka kuwafukuza Wafilisti, waliteka nyara kutoka kambi yao.
54 Davut Filistli Golyat'ın başını alıp Yeruşalim'e götürdü, silahlarını da kendi çadırına koydu.
Daudi akachukua kichwa cha yule Mfilisti na kukileta Yerusalemu, naye akaweka silaha za huyo Mfilisti katika hema lake mwenyewe.
55 Saul, Davut'un Golyat'la dövüşmeye çıktığını görünce, ordu komutanı Avner'e, “Ey Avner, kimin oğlu bu genç?” diye sormuştu. Avner de, “Yaşamın hakkı için, ey kral, bilmiyorum” diye yanıtlamıştı.
Sauli alipomwona Daudi anakwenda kukabiliana na huyo Mfilisti, alimwambia Abneri, jemadari wa jeshi, “Abneri, yule kijana ni mwana wa nani?” Abneri akajibu, “Hakika kama uishivyo, ee mfalme, mimi sifahamu.”
56 Kral Saul, “Bu gencin kimin oğlu olduğunu öğren” diye buyurmuştu.
Mfalme akasema, “Uliza huyu kijana ni mwana wa nani.”
57 Davut Golyat'ı öldürüp ordugaha döner dönmez, Avner onu alıp Saul'a götürdü. Golyat'ın kesik başı Davut'un elindeydi.
Mara Daudi aliporudi kutoka kumuua huyo Mfilisti, Abneri akamchukua na kumleta mbele ya Sauli. Daudi alikuwa bado anakishikilia kichwa cha yule Mfilisti.
58 Saul, “Kimin oğlusun, delikanlı?” diye sordu. Davut, “Kulun Beytlehemli İşay'ın oğluyum” diye karşılık verdi.
Sauli akamuuliza, “Kijana, wewe ni mwana wa nani?” Daudi akasema, “Mimi ni mwana wa mtumishi wako Yese wa Bethlehemu.”