< 1 Samuel 14 >

1 Bir gün Saul oğlu Yonatan, silahını taşıyan genç hizmetkârına, “Gel, karşı taraftaki Filist ordugahına geçelim” dedi. Ama bunu babasına haber vermedi.
Siku moja, Yonathani mwana wa Sauli alimwambia mbeba silaha wake aliye mdogo, “Njoo, hebu twende hadi upande mwingine kwenye ngome ya Wafilisti.” Lakini hakumjulisha baba yake.
2 Saul, Giva Kenti yakınındaki Migron'da bir nar ağacının altında oturmaktaydı. Yanında altı yüz kadar asker vardı.
Sauli alikuwa akikaa nje ya mji wa Gibea chini ya mti wa mkomamanga ulio katika Migroni. Takribani watu mia sita walikwa pamoja naye,
3 Efod giymiş olan Ahiya da aralarındaydı. Ahiya Şilo'da RAB'bin kâhini olan Eli oğlu Pinehas oğlu İkavot'un erkek kardeşi Ahituv'un oğluydu. Halk Yonatan'ın gittiğini farketmemişti.
akiwemo Ahiya mwana wa Ahitubu (nduguye Ikabodi) mwana wa Finehasi, mwana wa Eli, kuhani wa BWANA huko Shilo, aliyevaa naivera. Watu hao hawakujua kwamba Yonathani ameondoka.
4 Yonatan'ın Filist ordugahına ulaşmak için geçmeyi tasarladığı geçidin her iki yanında iki sivri kaya vardı; birine Boses, öbürüne Sene denirdi.
Katikati ya vichochoro, ambavyo Yonathani alinuia kuvipita hadi ngome ya Wafilisti, kulikuwa na mwamba wenye mteremko mkali upande mmoja, na mteremko mkali upande mwingine. Jabali moja liliitwa Bosesi, na jingine liliitwa Sene.
5 Kayalardan biri kuzeyde Mikmas'a, öbürü güneyde Giva'ya bakardı.
Lile jabali lenye mteremko mkali zaidi liliinuka upande wa kaskazini mbele ya Mikmashi, na jingine upande wa kusini mbele ya Geba.
6 Yonatan silahını taşıyan genç hizmetkârına, “Gel, şu sünnetsizlerin ordugahına gidelim” dedi, “Belki RAB bizim için bir şeyler yapar. Çünkü gerek çoklukta, gerekse azlıkta RAB'bin zafere ulaştırmasına engel yoktur.”
Yonathani akamwambia kijana mbeba silaha, “Njoo, na tuvuke hadi ngome ya hawa wasiotahiriwa. Pengine BWANA atatenda kwa niaba yetu, kwa maana hakuna kitu kiwezacho kumzuia BWANA asiokoe kwa wengi au kwa watu wachache.”
7 Silahını taşıyan genç, “Ne düşünüyorsan öyle yap” diye yanıtladı, “Haydi yürü! Düşündüğün her şeyde seninleyim.”
Mbeba silaha wake akajibu, “Fanya kila kitu kilicho ndani ya moyo wako. Songa mbele, tazama, niko pamoja nawe, nitatii maagizo yako yote.”
8 Yonatan, “Bu adamlara gidelim, bizi görsünler” dedi,
Ndipo Yonathani akasema, “Tutavuka twende kwa watu hao, na tutajionesha wenyewe kwao.
9 “Eğer bize, ‘Yanınıza gelene dek bekleyin’ derlerse, olduğumuz yerde kalırız, gitmeyiz.
Kama watatuambia, 'Subirini hapo hadi tutakapokuja kwenu' - basi tutabaki katika sehemu yetu na hatutavuka kwenda kwao.
10 Ama, ‘Yanımıza gelin’ derlerse, gideriz. Çünkü bu, RAB'bin Filistliler'i elimize teslim ettiğine ilişkin bir belirti olacak bizim için.”
Lakini kama watajibu, 'Njoni kwetu,' ndipo tutavuka; kwa sababu BWANA amewaweka mkononi mwetu. Hii ndiyo itakuwa ishara yetu.”
11 Böylece ikisi de Filistliler'in askerlerine göründüler. Filistliler, “Bakın! İbraniler gizlendikleri çukurlardan çıkmaya başlıyor!” dediler.
Kwa hiyo wote wawili wakajifunua mbele ya ngome ya Wafilisti. Wafilisti wakasema, “Angalia, Webrania wanakuja kutokea kwenye mashimo walimojificha.”
12 Sonra Yonatan'la silahını taşıyan gence, “Buraya, yanımıza gelin, size bir şey söyleyeceğiz” diye seslendiler. Bunun üzerine Yonatan silahını taşıyana, “Ardımdan gel” dedi, “RAB onları İsrailliler'in eline teslim etti.”
Ndipo watu wa ile ngome wakamwita Yonathani na mbeba silaha wake, wakisema, “Njoni huku kwetu, tutawaonesha jambo fulani.” Na Yonathani akamwambia mbeba silaha wake; “Nifuate nyuma yangu, kwa sababu BWANA amewaweka katika mkono wa Israeli.”
13 Yonatan elleriyle ayaklarını kullanarak yukarıya tırmandı; silahını taşıyan genç de onu izledi. Yonatan Filistliler'i yenilgiye uğrattı. Silahını taşıyan genç de onu izliyor ve Filistliler'i öldürüyordu.
Yonathani alipanda juu kwa mikono na miguu yake, na mbeba silaha akimfuata nyuma yake. Wafilisti waliuwawa mbele ya Yonathani, na mbeba silaha wake akiwaua baadhi nyuma yake.
14 Yonatan'la silahını taşıyan genç bu ilk saldırıda iki dönümlük bir alanda yirmi kadar asker öldürdüler.
Hilo shambulio la kwanza walilofanya Yonathani na mbeba silaha wake, waliua watu wapatao ishirini katika urefu wa nusu handaki kwenye eka moja ya ardhi.
15 Ordugahta ve kırsal alanda bütün Filist halkı arasında dehşet hüküm sürüyordu. Askerlerle akıncılar bile titriyordu. Derken yer sarsıldı; sanki Tanrı'dan gelen bir titremeydi bu.
Kukawa na hofu kubwa katika kambi, uwandani, na katika watu. Hata ngome ya jeshi na watekaji nyara nao wakawa na hofu kubwa
16 Benyamin topraklarındaki Giva Kenti'nde Saul'un nöbetçileri büyük bir kalabalığın oraya buraya dağıldığını gördüler.
Ndipo walinzi wa Sauli huko Gibea ya Benyamini wakaona kundi la askari wa Wafilisti likitawanyika, wakienda kule na huku.
17 Bunun üzerine Saul yanındaki adamlara, “Yoklama yapın da aramızdan kimin ayrıldığını görün” dedi. Yoklama yapılınca Yonatan'la silahını taşıyan gencin orada olmadığını anladılar.
Kisha Sauli akawaambia watu aliokuwa nao, “Mjihesabu ili muone nani hayupo hapa.”Walipokuwa wamehesabu, wakagundua kuwa Yonathani na mbebaji wa silaha zake hawapo.
18 Saul Ahiya'ya, “Tanrı'nın Sandığı'nı getir” dedi. O sırada Tanrı'nın Sandığı İsrail halkındaydı.
Sauli akamwambia Ahiya, “Lete hapa naivera ya Mungu”- kwa maana siku hiyo Ahiya alivaa naivera akiwa pamoja na askari wa Israeli.
19 Saul kâhinle konuşurken, Filistliler'in ordugahındaki kargaşa da giderek artmaktaydı. Bunun üzerine Saul kâhine, “Elini çek” dedi.
Wakati Sauli akiongea na kuhani, kelele na ghasia kubwa iliendelea na kuongezeka katika kambi ya Wafilisti. dipo sauli akamwambia kuhani, “Acha kazi unayofanya.”
20 Saul'la yanındaki askerlerin tümü toplanıp savaş alanına gittiler. Orada büyük bir kargaşa vardı. Herkes birbirine kılıç çekiyordu.
Sauli na watu wote aliokuwa nao wakajipanga na kwenda kwenye mapigano. Upanga wa kila Mfilisti ulikwa juu ya Mfilisti mwenzake, na kulikuwa na ghasia kubwa.
21 Daha önce Filistliler'in yanında yer alıp onların ordugahına katılan İbraniler bile saf değiştirerek Saul'la Yonatan'ın yanındaki İsrail birliklerine katıldılar.
Basi Waebrania ambao mwanzoni walijiunga na Wafilisti, na kwenda kwenye kambi yao, wao pia waliungana na Waisraeli waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani.
22 Efrayim dağlık bölgesinde gizlenen İsrailliler de Filistliler'in kaçtığını duyunca onları savaş alanında kovalamaya başladılar.
Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika milima karibu na Efraimu waliposikia kwamba Wafilisti wamekimbia, nao pia wakawafuata Wafilisti nakuwafukuza kwenye hiyo vita.
23 Böylece RAB İsrail'i o gün zafere ulaştırdı. Savaş Beytaven'in ötesine dek yayıldı.
Hivyo siku hiyo BWANA aliwaokoa Israeli, na mapigano yalivuka kupitiliza Beth aveni.
24 O gün İsrailliler bitkindi. Çünkü Saul, “Ben düşmanlarımdan öç alıncaya kadar, akşama dek kim yemek yerse lanetli olsun!” diye halka ant içirmişti. Bu yüzden de kimse bir şey yememişti.
Siku hiyo watu wa Israeli walifadhaika kwa sababu Sauli aliwaweka watu chini ya kiapo akasema, “Na alaaniwe mtu atakaye kula chakula kabla ya jioni na kabla sijalipiza kisasi kwa maadui zangu.” Hivyo hakuna hata mmoja kati ya watu wote aliyeonja chakula.
25 Derken, her yanı bal dolu bir ormana vardılar. Askerler ormana girince, toprakta akan balları gördüler. Ne var ki, içtikleri anttan korktukları için hiçbiri bala dokunmadı.
Ndipo watu wote wakaingia msituni na kuona asali ikiwa juu ya ardhi.
Watu walipoingia humo msituni, asali ilitiririka, lakini hakuna aliyeweka mkono wake kinywani kwa maana watu waliogopa kiapo.
27 Yonatan babasının halka ant içirdiğini duymamıştı. Elindeki değneği uzatıp ucunu bal gümecine batırdı. Biraz bal tadar tatmaz gözleri parladı.
Lakini Yonathani alikuwa hajasikia kwamba baba yake amewaagiza watu kwa kiapo. Akanyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kuichovya kwenye sega la asali. Kisha akanyoosha mkono wake hadi kinywani mwake, na macho yake yakaangaziwa.
28 Bunun üzerine oradakilerden biri Yonatan'a, “Baban askerlere, ‘Bugün kim yemek yerse lanetli olsun’ diye ant içirdi” dedi, “Askerlerin bitkin düşmesi de bundan.”
Ndipo mmoja wa watu hao, akamwambia, “Baba yako aliwaagiza watu kwa mkazo na kwa kiapo, kwa kusema, 'Alaaniwe mtu atakaye kula chakula kwa siku ya leo,' ingawa watu wamedhoofika kwa ajili ya njaa.”
29 Yonatan, “Babam halka sıkıntı verdi” diye yanıtladı, “Bakın, bu baldan biraz tadınca gözlerim nasıl da parladı!
Baadaye Yonathani alisema, “Baba yangu amefanya matatizo katika nchi. Angalia jinsi macho yangu alivyotiwa nuru kwa sababu nilionja asali hii kidogo.
30 Bugün halk düşmanlarından yağmaladığı yiyeceklerden özgürce yeseydi, çok daha iyi olurdu! O zaman Filistliler'in yenilgisi de daha ağır olmaz mıydı?”
Je, siyo vivuri sana kama leo watu wangekula bila kizuizi nyara walizopata kutoka kwa maadui zao? Kwa sababu sasa mauaji hayakuwa makubwa katikati ya Wafilisti.”
31 O gün İsrailliler, Filistliler'i Mikmas'tan Ayalon'a kadar yenilgiye uğrattılar. Ama İsrail askerleri o kadar bitkindi ki,
Siku hiyo waliwashambulia Wafilisti kutoka Mikmashi hadi Aiyaloni. Na watu walikuwa wamechoka sana.
32 yağmaladıkları mallara saldırdılar; davarları, sığırları, buzağıları yakaladıkları gibi hemen oracıkta kesip kanını akıtmadan yediler.
Hivyo watu wakazivamia nyara na kuchukua kondoo, ng'ombe na ndama na kuwachinja hapo chini. Watu walikula nyama zao pamoja na damu.
33 Durumu Saul'a bildirerek, “Bak, askerlerin kanlı eti yemekle RAB'be karşı günah işliyor!” dediler. Bunun üzerine Saul, “Hainlik ettiniz!” dedi, “Hemen büyük bir taş yuvarlayın bana.”
KIsha wakamwambia Sauli, “Tazama, watu wanamtenda BWANA dhambi kwa kula pamoja na damu.” Sauli akasema, “Mmetenda isivyo haki. Sasa, viringisheni jiwe kubwa kwangu.” Sauli akasema,
34 Sonra ekledi: “Halkın arasına varıp herkesin öküzünü, koyununu bana getirmesini söyleyin. Onları burada kesip yesinler. Eti kanıyla birlikte yiyerek RAB'be karşı günah işlemeyin.” O gece herkes öküzünü getirip orada kesti.
“Nendeni kati watu, na muwaambie, 'Kila mtu alete ng'ombe na kondoo wake, wawachinje hapa, na kuwala. Msimtende BWANA dhambi kwa kula na damu.”' Kwa hiyo watu wote wakaleta kila mtu na ng'ombe wake usiku huo na kuwachinja mahali hapo.
35 O sırada Saul RAB'be bir sunak yaptı. RAB'be yaptığı ilk sunaktı bu.
Sauli akamjengea BWANA madhabahu, ambayo ilikuwa ya kwanza kwake kumjengea BWANA.
36 Saul adamlarına, “Haydi, bu gece Filistliler'e saldıralım” dedi, “Tan ağarıncaya dek mallarını yağmalayalım, onlardan bir tekini bile sağ bırakmayalım.” Adamlar, “Sence uygun olan neyse onu yap” diye karşılık verdiler. Ama kâhin, “Burada Tanrı'ya danışalım” dedi.
Ndipo Sauli akasema, “Haya tuwafukuze Wafilisti usiku na kuwateka nyara hadi asubuhi; tusimwache hata mtu mmoja akiwa hai.” Nao wakamjibu, “Fanya unaloona linakupendeza.” Lakini kuhani akasema, “Hebu na tumkaribie Mungu mahali hapa.”
37 Bunun üzerine Saul Tanrı'ya, “Filistliler'e saldırmaya gideyim mi? Onları İsrailliler'in eline teslim edecek misin?” diye sordu. Ama Tanrı o gün yanıt vermedi.
Sauli alitaka kumuuliza Mungu maswali zaidi, “Je, inanipasa kuwafukuza Wafilisti? Je, utawaweka katika mkono wa Israeli?” Lakini siku hiyo BWANA hakumjibu kitu.
38 Bunun için Saul, “Ey halkın önderleri! Buraya yaklaşın da bugün işlenen bu günahın nasıl işlendiğini ortaya çıkaralım” dedi,
Ndipo Sauli akasema, “Njoni hapa, viongozi wote wa watu; mjue na kuona jinsi dhambi hii ilivyotokea leo.
39 “İsrail'i kurtaran yaşayan RAB'bin adıyla derim ki, bu günaha yol açan oğlum Yonatan bile olsa kesinlikle öldürülecektir.” Ama kimse bir şey söylemedi.
Kwa maana, kama BWANA aishivyo, aliyewaokoa Israeli, hata kama angekuwa mwanangu Yonathani, atapaswa kufa.” Lakini hakuna hata mtu mmoja miongoni mwa watu aliye mjibu neno.
40 Bunun üzerine Saul halka, “Siz bir yanda durun, oğlum Yonatan'la ben öbür yanda duracağız” dedi. Halk, “Sence uygun olan neyse onu yap” diye karşılık verdi.
Basi akawaambia Waisraeli wote, “Simameni upande mmoja, na mimi na Yonathani tutasimama upande mwingine.” Kisha watu wakamwambia Sauli, “Fanya lile unaloona jema kwako.”
41 Saul İsrail'in Tanrısı RAB'be, “Bana doğru yanıtı ver” dedi. Kura Yonatan'la Saul'a düştü, halk aklandı.
Kwa hiyo, Sauli akamwambia BWANA, Mungu wa Israeli, “Tuoneshe Thumimu.” Yonathani na Sauli wakatwaliwa, lakini watu walinusurika kuchaguliwa.
42 Saul bu kez, “Benimle oğlum Yonatan arasında kura çekin” dedi. Kura Yonatan'a düştü.
Basi Sauli akasema, “Tupa mawe ya bahati nasibu tuone kati yangu na mwanangu Yonathani.” Ndipo Yonathani akatwaliwa.
43 Bunun üzerine Saul Yonatan'a, “Söyle bana, ne yaptın?” diye sordu. Yonatan, “Ben yalnızca elimdeki değneğin ucuyla biraz bal alıp tattım. Şimdi ölmem mi gerek?” diye karşılık verdi.
Kisha Sauli akamwambia Yonathani, “Niambie umefanya nini.” Yonathani akamwambia baba yake, “Nilionja asali kidogo kwa kutumia ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwangu. Niko hapa; Nitakufa.”
44 Saul, “Yonatan, eğer seni öldürtmezsem, Tanrı bana aynısını, hatta daha kötüsünü yapsın!” dedi.
Sauli akasema, “Mungu afanye hivyo na kuzidi hata kwangu, kama Yonathani hautakufa.”
45 Ama halk Saul'a, “İsrail'i bu büyük zafere ulaştıran Yonatan'ı mı öldürteceksin?” dedi, “Asla! Yaşayan RAB'bin adıyla deriz ki, saçının bir teline bile zarar gelmeyecektir. Çünkü bugün o ne yaptıysa Tanrı'nın yardımıyla yapmıştır.” Böylece halk Yonatan'ı öldürülmekten kurtardı.
Basi watu wakamuuliza Sauli, “Je, inampasa Sauli afe, ni nani aliyetekeleza ushindi huu mkubwa kwa ajili ya Israeli? Mbali na hayo! Kama BWANA aishivyo, hata unywele mmoja wa kichwa chake hautaanguka chini, kwa maana leo amefanya kazi pamoja na Mungu.” Hivyo hao watu walimuokoa Yonathani ili asife.
46 Bundan sonra Saul Filistliler'i kovalamaktan vazgeçti. Filistliler de yerlerine döndüler.
Basi Sauli akasita kuwafuatia Wafilisti, nao wakarudi katika makao yao.
47 Saul İsrail'e kral atandıktan sonra, her yandaki düşmanlarına –Moav, Ammon, Edom halkları, Sova kralları ve Filistliler'e– karşı savaştı. Gittiği her yerde zafer kazandı.
Sauli alipoanza kutawala juu ya Israeli, alipigana na adui zake wote kila upande. Alipigana dhidi ya Moabu, dhidi ya watu wa Amoni, Edomu, wafalme wa Zoba, na Wafilisti. Popote alipogeukia aliwapiga kwa adhabu adui zake.
48 Yiğitçe savaşarak Amalekliler'i yenilgiye uğrattı, İsrailliler'i düşmanın yağmasından kurtardı.
Alitenda kwa ushujaa mkubwa na kuwashinda Waamaleki. Aliwaokoa Israeli kutoka mikono ya watu ambao waliwateka nyara.
49 Saul'un oğulları Yonatan, Yişvi ve Malkişua idi. İki kızından büyüğünün adı Merav, küçüğünün adı Mikal'dı.
Basi wana wa Sauli walikuwa ni hawa Yonathani, Ishvi, na Malkishua. Na majina ya binti zake wawili yalikuwa ni haya, Merabu mzaliwa wa kwanza, na mdogo aliitwa Mikali.
50 Karısı, Ahimaas'ın kızı Ahinoam'dı. Ordusunun başkomutanı amcası Ner oğlu Avner'di.
Jina la mke wa Sauli aliitwa Ahinoamu; naye alikuwa binti Ahimaasi. Na jina la Jemedari wa jeshi lake aliitwa Abneri mwana wa Neri, baba mdogo wa Sauli.
51 Saul'un babası Kiş'le Avner'in babası Ner, Aviel'in oğullarıydı.
Kishi alikuwa baba yake Sauli; na Neri alikuwa baba yake na Abneri, wote walikuwa wana wa Abieli.
52 Saul yaşamı boyunca Filistliler'le kıyasıya savaştı. Nerede yiğit, güçlü birini görse kendi ordusuna kattı.
Kulikuwa na mapigano makali dhidi ya Wafilisti katika siku zote za Sauli. Naye alipomwona mtu yeyote mwenye nguvu, au mtu yeyote jasiri, alimuunganisha kwake.

< 1 Samuel 14 >