< 1 Samuel 14 >
1 Bir gün Saul oğlu Yonatan, silahını taşıyan genç hizmetkârına, “Gel, karşı taraftaki Filist ordugahına geçelim” dedi. Ama bunu babasına haber vermedi.
Siku moja Yonathani mwana wa Sauli akamwambia kijana mbeba silaha wake, akasema, “Njoo, tuwavukie Wafilisti kwenye doria upande ule mwingine.” Lakini hakumwambia baba yake.
2 Saul, Giva Kenti yakınındaki Migron'da bir nar ağacının altında oturmaktaydı. Yanında altı yüz kadar asker vardı.
Sauli alikuwa akikaa kwenye viunga vya Gibea chini ya mkomamanga huko Migroni. Alikuwa pamoja na watu kama 600,
3 Efod giymiş olan Ahiya da aralarındaydı. Ahiya Şilo'da RAB'bin kâhini olan Eli oğlu Pinehas oğlu İkavot'un erkek kardeşi Ahituv'un oğluydu. Halk Yonatan'ın gittiğini farketmemişti.
miongoni mwao alikuwepo Ahiya, ambaye alikuwa amevaa kisibau. Alikuwa mwana wa Ikabodi, nduguye Ahitubu mwana wa Finehasi, mwana wa Eli, kuhani wa Bwana huko Shilo. Hakuna yeyote aliyekuwa na habari kwamba Yonathani alikuwa ameondoka.
4 Yonatan'ın Filist ordugahına ulaşmak için geçmeyi tasarladığı geçidin her iki yanında iki sivri kaya vardı; birine Boses, öbürüne Sene denirdi.
Kila upande wa njia ambayo Yonathani alikusudia kupita ili kuvuka kufikia doria ya Wafilisti kulikuwepo na jabali; moja lilikuwa linaitwa Bosesi, na jingine Sene.
5 Kayalardan biri kuzeyde Mikmas'a, öbürü güneyde Giva'ya bakardı.
Jabali moja lilisimama kaskazini kuelekea Mikmashi na jingine upande wa kusini kuelekea Geba.
6 Yonatan silahını taşıyan genç hizmetkârına, “Gel, şu sünnetsizlerin ordugahına gidelim” dedi, “Belki RAB bizim için bir şeyler yapar. Çünkü gerek çoklukta, gerekse azlıkta RAB'bin zafere ulaştırmasına engel yoktur.”
Yonathani akamwambia kijana wake mbeba silaha, “Njoo, tuvukie doria ya wale jamaa wasiotahiriwa. Huenda Bwana atatenda kwa ajili yetu. Hakuna chochote kitakachoweza kumzuia Bwana kuokoa, kwamba ni kwa wingi au kwa uchache.”
7 Silahını taşıyan genç, “Ne düşünüyorsan öyle yap” diye yanıtladı, “Haydi yürü! Düşündüğün her şeyde seninleyim.”
Mbeba silaha wake akamwambia, “Fanya yale yote uliyo nayo katika moyo wako. Songa mbele; moyo wangu na roho yangu viko pamoja nawe.”
8 Yonatan, “Bu adamlara gidelim, bizi görsünler” dedi,
Yonathani akasema, “Basi njoo; tutavuka kuwaelekea hao watu na kuacha watuone.
9 “Eğer bize, ‘Yanınıza gelene dek bekleyin’ derlerse, olduğumuz yerde kalırız, gitmeyiz.
Kama wakituambia, ‘Subirini hapo mpaka tuje kwenu,’ tutakaa pale tulipo na hatutakwea kwao.
10 Ama, ‘Yanımıza gelin’ derlerse, gideriz. Çünkü bu, RAB'bin Filistliler'i elimize teslim ettiğine ilişkin bir belirti olacak bizim için.”
Lakini kama watasema, ‘Pandeni mje kwetu,’ tutakwea, kwa sababu hiyo itakuwa ishara yetu kwamba Bwana amewatia mikononi mwetu.”
11 Böylece ikisi de Filistliler'in askerlerine göründüler. Filistliler, “Bakın! İbraniler gizlendikleri çukurlardan çıkmaya başlıyor!” dediler.
Basi wote wawili wakajionyesha kwa doria ya Wafilisti. Wafilisti wakasema, “Tazama! Waebrania wanatambaa toka mashimoni walimokuwa wamejificha.”
12 Sonra Yonatan'la silahını taşıyan gence, “Buraya, yanımıza gelin, size bir şey söyleyeceğiz” diye seslendiler. Bunun üzerine Yonatan silahını taşıyana, “Ardımdan gel” dedi, “RAB onları İsrailliler'in eline teslim etti.”
Watu wa kwenye doria wakawapigia kelele Yonathani na mbeba silaha wake, wakisema, “Njooni, pandeni kwetu nasi tutawakomesha.” Basi Yonathani akamwambia mbeba silaha wake, “Panda nyuma yangu; Bwana amewatia mikononi mwa Israeli.”
13 Yonatan elleriyle ayaklarını kullanarak yukarıya tırmandı; silahını taşıyan genç de onu izledi. Yonatan Filistliler'i yenilgiye uğrattı. Silahını taşıyan genç de onu izliyor ve Filistliler'i öldürüyordu.
Yonathani akapanda juu, akitumia mikono yake na miguu, pamoja na mbeba silaha wake papo hapo nyuma yake. Wafilisti wakaanguka mbele ya Yonathani, naye mbeba silaha wake akamfuata akiwaua nyuma yake.
14 Yonatan'la silahını taşıyan genç bu ilk saldırıda iki dönümlük bir alanda yirmi kadar asker öldürdüler.
Katika hilo shambulio la kwanza, Yonathani na mbeba silaha wake waliua kama watu ishirini kwenye eneo kama la nusu eka.
15 Ordugahta ve kırsal alanda bütün Filist halkı arasında dehşet hüküm sürüyordu. Askerlerle akıncılar bile titriyordu. Derken yer sarsıldı; sanki Tanrı'dan gelen bir titremeydi bu.
Kisha fadhaa ikawapata jeshi lote, wale waliokuwa kambini na shambani, wale waliokuwa katika doria na makundi ya washambuliaji, nayo nchi ilitetemeka. Ilikuwa ni hofu ya ghafula iliyotumwa na Mungu.
16 Benyamin topraklarındaki Giva Kenti'nde Saul'un nöbetçileri büyük bir kalabalığın oraya buraya dağıldığını gördüler.
Wapelelezi wa Sauli huko Gibea ya Benyamini wakaona jeshi likitokomea pande zote.
17 Bunun üzerine Saul yanındaki adamlara, “Yoklama yapın da aramızdan kimin ayrıldığını görün” dedi. Yoklama yapılınca Yonatan'la silahını taşıyan gencin orada olmadığını anladılar.
Ndipo Sauli akawaambia watu wale waliokuwa pamoja naye, “Kagueni jeshi mkaone ni nani ameondoka katikati yetu.” Walipokagua, akawa ni Yonathani na mbeba silaha wake ambao hawakuwepo.
18 Saul Ahiya'ya, “Tanrı'nın Sandığı'nı getir” dedi. O sırada Tanrı'nın Sandığı İsrail halkındaydı.
Sauli akamwambia Ahiya, “Leta Sanduku la Mungu.” (Wakati huo lilikuwa kwa Waisraeli.)
19 Saul kâhinle konuşurken, Filistliler'in ordugahındaki kargaşa da giderek artmaktaydı. Bunun üzerine Saul kâhine, “Elini çek” dedi.
Wakati Sauli alipokuwa akisema na kuhani, makelele katika kambi ya Wafilisti yakaongezeka zaidi na zaidi. Hivyo Sauli akamwambia kuhani, “Rudisha mkono wako.”
20 Saul'la yanındaki askerlerin tümü toplanıp savaş alanına gittiler. Orada büyük bir kargaşa vardı. Herkes birbirine kılıç çekiyordu.
Kisha Sauli na watu wake wote wakakusanyika na kwenda vitani. Wakawakuta Wafilisti wakiwa wamechanganyikiwa kabisa, wakitiana panga kila mmoja na wenzake.
21 Daha önce Filistliler'in yanında yer alıp onların ordugahına katılan İbraniler bile saf değiştirerek Saul'la Yonatan'ın yanındaki İsrail birliklerine katıldılar.
Wale Waebrania ambao walishakuwa pamoja na Wafilisti, na waliokuwa wamepanda pamoja nao katika kambi zao, wakaenda upande wa Waisraeli waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani.
22 Efrayim dağlık bölgesinde gizlenen İsrailliler de Filistliler'in kaçtığını duyunca onları savaş alanında kovalamaya başladılar.
Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika nchi ya milima ya Efraimu waliposikia kuwa Wafilisti wamekimbia, wakajiunga vitani na kuwafuata kwa bidii.
23 Böylece RAB İsrail'i o gün zafere ulaştırdı. Savaş Beytaven'in ötesine dek yayıldı.
Hivyo Bwana akawaokoa Waisraeli siku ile, navyo vita vilienea hadi kupita Beth-Aveni.
24 O gün İsrailliler bitkindi. Çünkü Saul, “Ben düşmanlarımdan öç alıncaya kadar, akşama dek kim yemek yerse lanetli olsun!” diye halka ant içirmişti. Bu yüzden de kimse bir şey yememişti.
Basi watu wa Israeli walikuwa katika dhiki siku ile, kwa sababu Sauli alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, akisema, “Alaaniwe mtu yeyote ambaye atakula chakula kabla ya jioni, kabla sijalipiza kisasi juu ya adui zangu!” Kwa hiyo hakuna mtu yeyote katika jeshi aliyeonja chakula.
25 Derken, her yanı bal dolu bir ormana vardılar. Askerler ormana girince, toprakta akan balları gördüler. Ne var ki, içtikleri anttan korktukları için hiçbiri bala dokunmadı.
Jeshi lote liliingia mwituni, na huko kulikuwepo na asali ardhini.
Walipoingia mwituni, wakaona asali ikitiririka, hata hivyo hakuna mtu yeyote aliyetia mkono wake kinywani, kwa sababu waliogopa kiapo.
27 Yonatan babasının halka ant içirdiğini duymamıştı. Elindeki değneği uzatıp ucunu bal gümecine batırdı. Biraz bal tadar tatmaz gözleri parladı.
Lakini Yonathani alikuwa hajasikia kuwa baba yake alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, hivyo akainyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kuichovya katika sega la asali. Akainua mkono wake na kuutia kinywani mwake, nayo macho yake yakawa maangavu.
28 Bunun üzerine oradakilerden biri Yonatan'a, “Baban askerlere, ‘Bugün kim yemek yerse lanetli olsun’ diye ant içirdi” dedi, “Askerlerin bitkin düşmesi de bundan.”
Kisha mmoja wa askari wake akamwambia, “Baba yako alilifunga jeshi kwa kiapo kikali, akisema, ‘Alaaniwe mtu yeyote alaye chakula leo!’ Ndiyo sababu watu wanalegea.”
29 Yonatan, “Babam halka sıkıntı verdi” diye yanıtladı, “Bakın, bu baldan biraz tadınca gözlerim nasıl da parladı!
Yonathani akasema, “Baba yangu ameitaabisha nchi. Ona jinsi nilivyopata nguvu mpya nilipoonja asali hii kidogo.
30 Bugün halk düşmanlarından yağmaladığı yiyeceklerden özgürce yeseydi, çok daha iyi olurdu! O zaman Filistliler'in yenilgisi de daha ağır olmaz mıydı?”
Ingekuwa bora zaidi mara ngapi kama watu wangalikula leo baadhi ya nyara walizoteka kutoka kwa adui zao. Je, mauaji ya Wafilisti yasingekuwa makubwa zaidi?”
31 O gün İsrailliler, Filistliler'i Mikmas'tan Ayalon'a kadar yenilgiye uğrattılar. Ama İsrail askerleri o kadar bitkindi ki,
Siku ile baada ya Waisraeli kuwaua Wafilisti kutoka Mikmashi mpaka Aiyaloni, walikuwa wamechoka.
32 yağmaladıkları mallara saldırdılar; davarları, sığırları, buzağıları yakaladıkları gibi hemen oracıkta kesip kanını akıtmadan yediler.
Watu wakarukia zile nyara, wakichukua kondoo, ngʼombe na ndama, wakawachinja hapo juu ya nchi na kuwala, pamoja na damu.
33 Durumu Saul'a bildirerek, “Bak, askerlerin kanlı eti yemekle RAB'be karşı günah işliyor!” dediler. Bunun üzerine Saul, “Hainlik ettiniz!” dedi, “Hemen büyük bir taş yuvarlayın bana.”
Kisha mtu mmoja akamwambia Sauli, “Tazama, watu wanatenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama yenye damu.” Akasema, “Mmevunja uaminifu. Livingirisheni jiwe kubwa hapa mara moja.”
34 Sonra ekledi: “Halkın arasına varıp herkesin öküzünü, koyununu bana getirmesini söyleyin. Onları burada kesip yesinler. Eti kanıyla birlikte yiyerek RAB'be karşı günah işlemeyin.” O gece herkes öküzünü getirip orada kesti.
Kisha Sauli akasema, “Nendeni miongoni mwa watu, mwaambie, ‘Kila mmoja wenu aniletee ngʼombe wake na kondoo, mwachinjie hapa na mle. Msitende dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama ikiwa na damu ndani yake.’” Hivyo kila mmoja akaleta ngʼombe wake jioni ile na kumchinja hapo.
35 O sırada Saul RAB'be bir sunak yaptı. RAB'be yaptığı ilk sunaktı bu.
Ndipo Sauli akamjengea Bwana madhabahu, na ndiyo ilivyokuwa mara yake ya kwanza kujenga madhabahu.
36 Saul adamlarına, “Haydi, bu gece Filistliler'e saldıralım” dedi, “Tan ağarıncaya dek mallarını yağmalayalım, onlardan bir tekini bile sağ bırakmayalım.” Adamlar, “Sence uygun olan neyse onu yap” diye karşılık verdiler. Ama kâhin, “Burada Tanrı'ya danışalım” dedi.
Sauli akasema, “Tuteremke tufuatie Wafilisti usiku na kuwateka nyara mpaka mapambazuko, nasi tusiache hata mmoja wao hai.” Wakajibu, “Fanya lolote lile uonalo jema zaidi kwako.” Lakini kuhani akasema, “Tuulize kwa Mungu mahali hapa.”
37 Bunun üzerine Saul Tanrı'ya, “Filistliler'e saldırmaya gideyim mi? Onları İsrailliler'in eline teslim edecek misin?” diye sordu. Ama Tanrı o gün yanıt vermedi.
Basi Sauli akamuuliza Mungu, akisema, “Je, niteremke kuwafuatia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwa Israeli?” Lakini Mungu hakumjibu siku ile.
38 Bunun için Saul, “Ey halkın önderleri! Buraya yaklaşın da bugün işlenen bu günahın nasıl işlendiğini ortaya çıkaralım” dedi,
Kwa hiyo Sauli akasema, “Njooni hapa, ninyi nyote ambao ni viongozi wa jeshi, na tutafute ni dhambi gani imefanywa leo.
39 “İsrail'i kurtaran yaşayan RAB'bin adıyla derim ki, bu günaha yol açan oğlum Yonatan bile olsa kesinlikle öldürülecektir.” Ama kimse bir şey söylemedi.
Kwa hakika kama Bwana aiokoaye Israeli aishivyo, hata kama itakuwa juu ya mwana wangu Yonathani, ni lazima afe.” Lakini hakuna mtu yeyote aliyesema neno.
40 Bunun üzerine Saul halka, “Siz bir yanda durun, oğlum Yonatan'la ben öbür yanda duracağız” dedi. Halk, “Sence uygun olan neyse onu yap” diye karşılık verdi.
Kisha Sauli akawaambia Waisraeli wote, “Ninyi simameni huko; mimi na mwanangu Yonathani tutasimama hapa.” Watu wakajibu, “Fanya lile unaloona jema zaidi kwako.”
41 Saul İsrail'in Tanrısı RAB'be, “Bana doğru yanıtı ver” dedi. Kura Yonatan'la Saul'a düştü, halk aklandı.
Kisha Sauli akamwomba Bwana, Mungu wa Israeli, akisema, “Nipe jibu lililo sawa.” Yonathani na Sauli wakatolewa kwa kura, nao watu wakawa salama.
42 Saul bu kez, “Benimle oğlum Yonatan arasında kura çekin” dedi. Kura Yonatan'a düştü.
Sauli akasema, “Pigeni kura kati yangu na mwanangu Yonathani.” Kura ikamwangukia Yonathani.
43 Bunun üzerine Saul Yonatan'a, “Söyle bana, ne yaptın?” diye sordu. Yonatan, “Ben yalnızca elimdeki değneğin ucuyla biraz bal alıp tattım. Şimdi ölmem mi gerek?” diye karşılık verdi.
Basi Sauli akamwambia Yonathani, “Niambie ni nini ulichokifanya.” Hivyo Yonathani akamwambia, “Nilionja tu asali kidogo kwa ncha ya fimbo yangu. Je, sasa ni lazima nife?”
44 Saul, “Yonatan, eğer seni öldürtmezsem, Tanrı bana aynısını, hatta daha kötüsünü yapsın!” dedi.
Sauli akasema, “Mungu na anishughulikie kwa ukali zaidi kama wewe Yonathani hutakufa.”
45 Ama halk Saul'a, “İsrail'i bu büyük zafere ulaştıran Yonatan'ı mı öldürteceksin?” dedi, “Asla! Yaşayan RAB'bin adıyla deriz ki, saçının bir teline bile zarar gelmeyecektir. Çünkü bugün o ne yaptıysa Tanrı'nın yardımıyla yapmıştır.” Böylece halk Yonatan'ı öldürülmekten kurtardı.
Lakini watu wakamwambia Sauli, “Je, Yonathani atakufa, yeye ambaye ameleta wokovu huu mkubwa Israeli? Hasha! Hakika kama Bwana aishivyo, hakuna hata unywele wa kichwa chake utakaoanguka juu ya ardhi, kwa kuwa alifanya jambo hili leo kwa msaada wa Mungu.” Basi watu wakamwokoa Yonathani, wala hakuuawa.
46 Bundan sonra Saul Filistliler'i kovalamaktan vazgeçti. Filistliler de yerlerine döndüler.
Kisha Sauli akaacha kuwafuata Wafilisti, nao wakajiondoa na kurudi katika nchi yao.
47 Saul İsrail'e kral atandıktan sonra, her yandaki düşmanlarına –Moav, Ammon, Edom halkları, Sova kralları ve Filistliler'e– karşı savaştı. Gittiği her yerde zafer kazandı.
Baada ya Sauli kujitwalia utawala katika Israeli, alipigana dhidi ya adui zake kila upande: Moabu, Waamoni, Edomu, wafalme wa Soba, na Wafilisti. Popote alipogeukia, aliwashinda.
48 Yiğitçe savaşarak Amalekliler'i yenilgiye uğrattı, İsrailliler'i düşmanın yağmasından kurtardı.
Akapigana kishujaa na kuwashinda Waamaleki, akiikomboa Israeli kutoka mikono ya wale waliokuwa wamewateka nyara.
49 Saul'un oğulları Yonatan, Yişvi ve Malkişua idi. İki kızından büyüğünün adı Merav, küçüğünün adı Mikal'dı.
Wana wa Sauli walikuwa Yonathani, Ishvi na Malki-Shua. Jina la binti yake mkubwa lilikuwa Merabu, naye mdogo aliitwa Mikali.
50 Karısı, Ahimaas'ın kızı Ahinoam'dı. Ordusunun başkomutanı amcası Ner oğlu Avner'di.
Jina la mkewe Sauli aliitwa Ahinoamu binti wa Ahimaasi. Jina la jemadari wa jeshi la Sauli aliitwa Abneri mwana wa Neri, naye Neri alikuwa babaye mdogo Sauli.
51 Saul'un babası Kiş'le Avner'in babası Ner, Aviel'in oğullarıydı.
Babaye Sauli yaani, Kishi na Neri baba yake Abneri walikuwa wana wa Abieli.
52 Saul yaşamı boyunca Filistliler'le kıyasıya savaştı. Nerede yiğit, güçlü birini görse kendi ordusuna kattı.
Siku zote za utawala wa Sauli zilikuwa za vita vikali dhidi ya Wafilisti, na wakati wowote Sauli alimwona mtu mwenye nguvu au shujaa, alimchukua kwa utumishi wake.