< Matta 24 >

1 I'sa Allahne Xaane məhleençe qığeç'umee, Mang'usqa telebabı qeebaxhe. Manbışis Allahne Xaana binaa Mang'us bıkırba haagvas vukkiykan.
Yesu akatoka Hekaluni na alipokuwa akienda zake, wanafunzi wake wakamwendea ili kumwonyesha majengo ya Hekalu.
2 I'see manbışik'le eyhen: – Şok'le in gırgın g'ecenne? Zı şok'le hək'edacad eyhe, mançina g'aye-g'ayel aaxvas deş, man gırgın ot'al-oxal ha'asın.
Ndipo Yesu akawauliza, “Je, mnayaona haya yote? Amin, nawaambia, hakuna hata jiwe moja hapa litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
3 I'sa Zeytunne suval gyu'uring'a, Mang'usqa telebabı qabı qiyghanan: – Ğu şak'le eyhelan, man Ğu eyhen karbı mısane ixhes? Sayır Ğu qalesnang'a hucoone ixhes, dyunyeyn exır hiyxharang'a? (aiōn g165)
Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake wakamjia faraghani, wakamuuliza, “Tuambie, mambo haya yatatukia lini, nayo dalili ya kuja kwako na ya mwisho wa dunia ni gani?” (aiōn g165)
4 I'see manbışis inəxdun alidghıniy qele: – Yugba ilyaake, şu neng'veecad yəqqı'le qığmaa'acen.
Yesu akawajibu, “Jihadharini, mtu yeyote asiwadanganye.
5 «Zı Masixhva» geed insanaaşe qabı eyhes. Manbışe məxüb geebbı yəqqı'le qığaa'as.
Kwa maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye Kristo,’nao watawadanganya wengi.
6 Şok'le muhariba əəva, muhariba vuxhesva g'ayxhes. Şu mançile qıməəq'ən. Man gırgın ixhes ıkkan. Man gırgın eyxhenbı – dyunyeyn exır k'ane qıxhava eyhen vodun.
Mtasikia habari za vita na matetesi ya vita. Angalieni msitishike, kwa maana haya hayana budi kutukia. Lakini ule mwisho bado.
7 Millet milletılqa, devlet devletılqa g'elil qixhes. Sassa cigabışee mısvalybı ixhes, ç'iyebı ı'ğiykaras.
Taifa litainuka dhidi ya taifa, na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na njaa na mitetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali.
8 Man gırgın «k'oybı giyğalanbıva» eyhen vodun.
Haya yote yatakuwa ndio mwanzo wa utungu.
9 Mane gahıl şos əq'übabı heles, gyapt'asınbı. Zal-alla şu gırgıne milletbışik'le g'umooce vuxhes.
“Ndipo mtasalitiwa, ili mteswe na kuuawa, nanyi mtachukiwa na mataifa yote kwa ajili yangu.
10 Manke gellesın insanar Allahne yəqqı'le savk'alasınbı, manbışik'le sana-sanbı g'umooce qeepxhes, manbışe sana-sanbı duşmanaaşine xılyaqa qevles.
Wakati huo, wengi wataacha imani yao, nao watasalitiana kila mmoja na mwenzake na kuchukiana.
11 Horalay geeb peyğambarar qavaales, manbışe geebbı yəqqı'le qığaa'as.
Watatokea manabii wengi wa uongo, nao watawadanganya watu wengi.
12 Pisvalla geeb quvxhaylette gellesınbışin sana-sanbı vukkiykıniy k'ıl qıxhes.
Kwa sababu ya kuongezeka kwa uovu upendo wa watu wengi utapoa,
13 Vuşuyiy k'anyaqqamee örxür g'attixhanasda.
lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa.
14 Mana Xəybışde Paççahiyvaline hək'eena yugna xabar dyunyevollete yuşan haa'asda. Gırgıne milletbışilqa mana xabar hipxhırmee, dyunyeyn exır ixhes.
Injili ya Ufalme itahubiriwa ulimwenguni kote kuwa ushuhuda kwa mataifa yote. Ndipo mwisho utakapokuja.
15 Şok'le Daniyal peyğambaree uvhuna xhinnena, «Muq'addasne cigeena həlyvəəq'ənasda xhinnena q'əralla» g'avcumee (hasre qədəqqəng'ulqa hixherecen),
“Hivyo mtakapoona lile ‘chukizo la uharibifu’ lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu (asomaye na afahamu),
16 yahudeebınbı manke suvabışilqa heepxecen.
basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani.
17 Hasre mane gahıl, daxalyna xaadın karbı aalyat'asva avqa gimeç'ecen,
Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke ili kuchukua chochote kutoka ndani ya nyumba.
18 çoleenar tanalinçılqava xaaqa sımiyk'alcen.
Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake.
19 Vuxhne avxuynbışeyiy uşax gyoqa'anbışe mane yiğbışil əq'üba ts'ıts'a'as.
Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo!
20 Düə hee'e, vuşun heepxiy q'ı'dmilqayiy Şabbatne yiğılqa gimexhacen.
Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi au siku ya Sabato.
21 Mane yiğbışil məxdın divan qixhas, dyunye itxhıniyle həşdilqameeyid həşdiyle şaqad mısacad ixhes deş.
Kwa maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa dunia mpaka sasa: wala haitakuwako tena kamwe.
22 Man yiğbı cit'a qıdi'iynbıxhiy, sang'ussecar g'attixhanas əxəs deşdiy. Allahee g'əvxüynbışil-alla man yiğbı cit'a qa'as.
Kama siku hizo zisingefupishwa, hakuna hata mtu mmoja ambaye angeokoka. Lakini kwa ajili ya wateule, siku hizo zitafupizwa.
23 Mane gahıl şok'le şavaamecad, «İlyaakende, Masixh inyaa vor, şaa vor» uvheene, mançil haymeebaxhe.
Wakati huo kama mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazama, Kristo huyu hapa!’ Au, ‘Kristo yuko kule,’ msisadiki.
24 Horalay peyğambarariy horalay masixhar qavaales. Manbışe ç'ak'ın əlaamatbıyiy gorsatmabı hagvas. Manbışis g'əvxüynbıb yəqqı'le qığa'as vukkiykanas.
Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo, nao watafanya ishara kubwa na maajabu mengi ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale wateule hasa.
25 İlyaake, Zı şok'le vuşde vuk'lelqa qalesınbı uvhu.
Angalieni, nimekwisha kuwaambia mapema.
26 Mançil-allad şavaamecad şok'le uvhee «Mana şaa'ar sahree vor», «Mana anne gozee vor» mançilqa haymeebaxhe, maqa hımaak'an.
“Kwa hiyo mtu yeyote akiwaambia, ‘Yule kule nyikani,’ msiende huko. Au akisema, ‘Yuko kwenye chumba,’ msisadiki.
27 Nəxüdiy ts'ayılpan şargıl ı'xı'mee garbıl g'ece, həməxüdud İnsanna Dix, Zı, siyk'almee ixhes.
Kwa maana kama vile umeme utokeavyo mashariki na kuonekana hata magharibi, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.
28 Leşnane cigeeqa mayit otxhanan şityarxhe sadaylenbı.
Kwa maana popote ulipo mzoga, huko ndiko wakusanyikapo tai.
29 Mane yiğbışil qitxhuyne divanıle qiyğa, «Verığ avqas, Vaz k'yooçes, Xənebı k'yoharas, Xəybışeedın gucbı ı'ğiykaras».
“Mara baada ya dhiki ya siku zile, “‘jua litatiwa giza, nao mwezi hautatoa nuru yake; nazo nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za anga zitatikisika.’
30 Manke İnsanne Duxayn əlaamat xəybışee g'aces. Ç'iyeyne aq'valin gırgın milletbı ts'irbı ha'a geşşes. Manbışik'le İnsanna Dix xəybışeene buludbışil xənne gucukayiy nuruka qöö g'aces.
“Ndipo itakapotokea ishara ya Mwana wa Adamu angani, na makabila yote ya dunia yataomboleza. Nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya angani, katika uwezo na utukufu mkuu.
31 Mang'vee Cun malaaikar g'axuvles, malaaikaaşed gaçeençe qığəəne it'umne syuttyuka Mang'un g'əvxüynbı dyunyeyne yoq'ne surale, q'omançe k'anyaqqamee sa'asınbı.
Naye atawatuma malaika zake kwa sauti kuu ya tarumbeta, nao watawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwisho mwingine.
32 İnciliyne yiveyne hək'eene misaalal k'ırı alixhxhe: mançin t'ur g'avhu t'ele aleylya'ang'a, g'ı'l k'ane qexheva şok'le ats'axhxhen.
“Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
33 Şok'led man gırgın kar g'acumee ats'axhxhe, İnsanna Dix k'ane vor, Mana akkayne ghalee vor.
Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yote, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni.
34 Zı şok'le hək'edacad eyhe, ine gahılyın insanar əlyhəəssecad man gırgın kar ixhes.
Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
35 Xəybıyiy ç'iye əlyhəəsınbı, Zı uvhuyn cuvab əlyhəəs deş.
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
36 Man yiğ mısayiy ixhesva, sə'ət xhulençiliy ixhesva xəybışeene malaaikaaşik'leyiy Allahne Duxayk'le ats'a deş. Man saccu Dekkık'le ats'a.
“Kwa habari ya siku ile na saa, hakuna ajuaye, hata malaika walio mbinguni wala Mwana, ila Baba peke yake.
37 Nüh peyğambarıne gahıl nəxüdiy ıxha, həməxüdud İnsanna Dix siyk'almeeyid ixhes.
Kama ilivyokuwa wakati wa Noa, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.
38 Q'ıfrımıle ögiyl, Nüh gameeqa ikkeç'esde yiğılqamee, insanaaşe otxhan-ulyoğa, adameeşe xhunaşşer haa'a, yedarıb adameeşis əlyhəə vuxha.
Kwa maana siku zile kabla ya gharika, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka siku ile Noa alipoingia katika safina.
39 Q'ıfrım qabı manbışin gırgınbı vukkeesmee, manbışik'le vuççud ats'a deşdiy. Həməxüdud İnsanna Dix sak'alasnang'a ixhes.
Nao hawakujua lolote mpaka gharika ilipokuja ikawakumba wote. Hivyo ndivyo itakavyokuwa atakapokuja Mwana wa Adamu.
40 Mane gahıl çolee iş haa'anbışda sa alyart'u, sa g'alerçesda.
Watu wawili watakuwa shambani, naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.
41 Yöxxee suk g'iviyxərne q'öne zəiyfayna sa alyart'u, sa g'alerçesda.
Wanawake wawili watakuwa wanasaga pamoja, naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.
42 Mançil-allab muğurba vuxhe, şok'le vuşda Xərna mısa ayres ıxhay ats'a deş.
“Basi kesheni, kwa sababu hamjui ni siku gani atakapokuja Bwana wenu.
43 Şok'le innıd ats'axhxhe, xaane iyesiyk'le sixnariy mısa ayresva ats'axhxhanxhiy, mana g'ilydirxhu, sixnariy xaaqa ikkeç'escar hassaras deşdiy.
Lakini fahamuni jambo hili: Kama mwenye nyumba angejua ni wakati gani wa usiku ambao mwizi atakuja, angekesha na hangekubali nyumba yake kuvunjwa.
44 Mançil-allab yugba ilyaake, sok'le İnsanna Dix mısa ayres ıxhay ats'a deş.
Kwa hiyo ninyi pia hamna budi kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja saa msiyotazamia.
45 Nukaraaşis cine gahıl otxhuniy helecenva, manbışil ooqa iyesee gixhxhına qorkuna, ək'elynana nukar vuşune?
“Ni nani basi aliye mtumishi mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake amemweka kusimamia watumishi wengine katika nyumba yake, ili awape chakula chao kwa wakati unaofaa?
46 İyesiy xaaqa sak'ımee, vucee uvhuna iş haa'a g'oocena nukar nimee baxtivariy!
Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
47 Zı şok'le hək'edacad eyhe, iyesee mang'uke cune gırgıneecar karana xərnaniy ha'as.
Amin, nawaambia, atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa mali yake yote.
48 Hucooniyxan ixhes manacar nukar pisda ıxhanaxhiy? Mang'vee «Yizda xərna həşdebışee qales deşva» uvhu,
Lakini kama huyo mtumishi ni mwovu, naye akasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu atakawia muda mrefu,’
49 giğalasdaniy vuc xhinnen nukarar gyoota, p'iyanınbşika otxhun-ulyoğa.
kisha akaanza kuwapiga watumishi wenzake, na kula na kunywa pamoja na walevi.
50 Mang'una xərna, mang'une ək'eleeqacar qidyalesde yiğıl, sə'ətıl qarı,
Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua.
51 mang'us yı'q'na caza huvu q'öbvalla haa'anbışika sacigeeniy havaces. Mançe geşşuybıyiy ık'arıke silibı sana-sançil qadaxan ses qöö ixhes.
Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wanafiki, mahali ambako kutakuwa ni kulia na kusaga meno.

< Matta 24 >