< Nyingnam 20 >
1 Yalungyachung rinya nam kochingso, Paul mvngjwngnv vdwa gokkum nyatola okv bunua lvkobv gamgo mintvmiru nyapi kula alvbv vla bunua mintoku. Vbvrikunamv hv vnglin lakula okv Mesedonia bv vngtoku.
Baada ya zile ghasia kumalizika, Paulo aliwaita wanafunzi pamoja akawatia moyo, akawaaga, akaanza safari kwenda Makedonia.
2 Hv mooku mvnwnglo vngpikla okv mintvmiru karla nyitwng nga lvkobv doin awgo minggo kartoku. Vbvripikula hv Akaia lo aatoku,
Alipita katika sehemu zile, akinena na watu maneno mengi ya kuwatia moyo. Ndipo hatimaye akawasili Uyunani,
3 hoka hv poolu pwkgumgo dootoku. Hv gwngrap toku Sairia lo vngdu kubv vdwlo hv chinsu pvkudw Jius vdwgv ninyia nyiru rusvnga; vkvlvgabv hv mvngtoku Mesedonia bv vngkur dvkubv.
ambako alikaa kwa muda wa miezi mitatu. Alipokuwa anakaribia kuanza safari kwa njia ya bahari kwenda Shamu, kwa sababu Wayahudi walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yake, aliamua kurudi kupitia njia ya Makedonia.
4 Beria lokv, Pirhus gv kuunyilo Sopatarnyi lvkobv vngming gvvto; Tesalonika lokv Aristarkas okv Sekundas; Derbe lokv, Gaius; Asia mooku lokv, Taikikas okv Tropimus; okv Timoti.
Paulo alikuwa amefuatana na Sopatro mwana wa Piro, Mberoya, Aristarko na Sekundo kutoka Thesalonike na Gayo, mtu wa Derbe, Timotheo pamoja na Tikiko na Trofimo kutoka sehemu ya Asia.
5 Bunu vngcho nyala okv Troas lo ngonua kaariala doonya toku.
Hawa watu walitutangulia wakaenda kutungojea Troa.
6 Ngonu Pilippi lokv vngraptoku vtwnglo vpap lvkmanam dvbam alulo okv alu longu kochingbv ngonu bunua Troas lo ribam tvku, hoka ngonu alu kanwgo ribam tvku.
Lakini sisi tukasafiri kwa njia ya bahari kwa siku tano kutoka Filipi baada ya siku za Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, nasi tukaungana na wengine huko Troa, ambako tulikaa kwa siku saba.
7 Karbualu gv arium ngonu mvnwng ngv lvkobv aakumchaakum nyatoku dvnam dvbam dubv. Paul nyitwng nga mintoku okv yupra lo gobv mimbwng la, hv logonvlo vngyu tvvkunam lvkwngbv.
Siku ya kwanza ya juma tulikutana pamoja kwa ajili ya kumega mkate. Paulo akaongea na watu, naye kwa kuwa alikuwa amekusudia kuondoka kesho yake, aliendelea kuongea mpaka usiku wa manane.
8 Mvdurupum awgo hungdungto ngonu mvnwng gv doopam dooku gv hogv karchung lo.
Kwenye chumba cha ghorofani walimokuwa wamekutania kulikuwa na taa nyingi.
9 Yaapa ako aminv Iutikas vla minam angv kirki lo dooto, okv Paul japbwngto, Yutikas yumi la okv yuptab toku, anyunganya nga ninyi yupngak tvku okv holutvku naam hogv karchung aom lokv kvdwlo hopvtoku. Vdwlo bunu ninyia svvrap tokudw okv hv siro tvku.
Kijana mmoja jina lake Eutiko, alikuwa amekaa dirishani, wakati Paulo alipokuwa akihubiri kwa muda mrefu, alipatwa na usingizi mzito, akaanguka kutoka ghorofa ya tatu, wakamwinua akiwa amekufa.
10 Vbvritola Paul itoku okv atubongv ninyi gvlo joklwkla okv ninyia jarbwng toku. “Mvngdwk mabvka,” hv mintoku, “Hv vjak turdvdu!”
Paulo akashuka chini, akajitupa juu yake na kumkumbatia, akasema, “Msishtuke, uzima wake bado umo ndani yake.”
11 Vbvrikunamv hv chaakur tvku hogv karchung bv, vtwng nga pimwkto, okv dvtoku. Bunu hum lvkobv awgo raami siro koching bv, Doonyi vka poklin dvkubv, Paul vngtoku.
Kisha Paulo akapanda tena ghorofani, akamega mkate na kula. Baada ya kuongea mpaka mapambazuko, akaondoka.
12 Bunu naatoku vmi yaapa anga turdubv naam lo chaagv toku okv mvnwng ngv hinging nyatoku.
Watu wakamrudisha yule kijana nyumbani akiwa hai nao wakafarijika sana.
13 Ngonu svpwbv vngcho yala vngtoku okv Assos lo aalwk tvvto hoka ngonu Paulnyi svpwlo vnggv tvvto. Hv ngonua sibv ritokv vla mintoku, ogulvgavbolo hv hoka kvdwbv vngtvtvto.
Tukatangulia melini tukasafiri mpaka Aso ambako tungempakia Paulo. Alikuwa amepanga hivyo kwa maana alitaka kufika kwa miguu.
14 Vdwlo hv ngonua Assos lo paami sipvkudw, hv svpwbv vnggla okv Mitiline lo aagv toku.
Alipotukuta huko Aso, tulimpakia melini, tukasafiri wote mpaka Mitilene.
15 Ngonu hokv gvngv durapla okv Kios lo logo nvnga aachi toku. Alu gonvgv kochingbv ngonu Samos lo aatoku, okv ho alu ngonu Miletus lo aachitoku.
Kutoka huko tuliendelea kwa njia ya bahari, na kesho yake tukafika mahali panapokabili Kio. Siku iliyofuata tukavuka kwenda Samo, na kesho yake tukawasili Mileto.
16 Paul svpw lokv Epesus nga vngbo dubv mvngtoku, Asia mookulo dwa nyemu manam lvkwngbv. Vdwgo rinyupvdw, hv Pentikos alulo Jerusalem lo baapu alvbv aalwk dvkubv vla.
Paulo alikuwa ameamua tusipitie Efeso ili asitumie muda mwingi huko sehemu za Asia, kwa sababu alikuwa anatamani kama ikiwezekana kufika Yerusalemu kabla ya siku ya Pentekoste.
17 Miletus lokv Paul Epesus lo gaam go milwkto, Gvrja gv nyigagatv vdwa ninyi kaarwk sudubv mintoku.
Paulo akiwa Mileto, alituma mjumbe kwenda Efeso kuwaita wazee wa kanisa waje wakutane naye.
18 Bunu vdwlo aachi tokudw, ninyi bunua mintoku, “Nonuno chindu oguaingbv ngoogv dwa nonu gvlo lvkobv rilariya kunama, Asia mooku lo ngoogv atuake bv aalwkri alu lokv.
Walipofika akawaambia, “Ninyi wenyewe mnajua jinsi nilivyoishi katikati yenu muda wote tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia.
19 Jius nyi meegonv nga rinyingriruto okv nga achialvbv mvngdwkmvngku okv hirukaaya moto. Vbvritola ngo mvngdwkla nyikla sarla okv nyanyak alvbv Ahtu gv lvgabv ritoku.
Nilimtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote na kwa machozi nikivumilia taabu na mapingamizi yaliyonipata kutokana na hila za Wayahudi.
20 Nonuno ho chindo ngo oguguka mvngtung mabv minjito nonu gvbv alv jinvgo okv mvngtoku mvnwng gvbv okv nonugv naam gvbv.
Mnajua kwamba sikusita kuhubiri jambo lolote ambalo lingekuwa la kuwafaa ninyi, lakini nilifundisha hadharani na nyumba kwa nyumba.
21 Jius okv Jentail vdwa ngo dinchi rungbv gamrw jitoku bunu atugv rimur am mvngdin lakula Pwknvyarnv gvloku okv ngonugv Ahtu Jisunyi mvngjwng dvkubv.
Nimewashuhudia Wayahudi na Wayunani kwamba inawapasa kumgeukia Mungu kwa kutubu dhambi na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.
22 Okv vjak, Darwknv Dowa tvvla kuju ngo Jerusalem bv vngjikunv, ngo chinsuma ogugo alo ririkudw.
“Nami sasa nimesukumwa na Roho, ninakwenda Yerusalemu wala sijui ni nini kitakachonipata huko.
23 Ngo mvngchik chindu ho pamtv mvnwng lo Darwknv Dowv gamrw toku nga ho patwk lo dosv nga okv ngoogv hirukaya svngaka.
Ila ninachojua tu ni kwamba Roho Mtakatifu amenionya kuwa vifungo na mateso vinaningoja.
24 Vbvritola ngo atugv singdung nga oguka mvngsuma; ngoogv mvngnam mvngchik vv ho Ahtu Jisu nga ritokv vla jinama, Pwknvyarnv gv anyuaya lokv Alvnv Yunying nga rinyadoonya dukubv mvngmwng dunv.
Lakini siyahesabu maisha yangu kuwa ya thamani kwangu, kama kuyamaliza mashindano na kukamilisha ile kazi Bwana Yesu aliyonipa, yaani, kazi ya kuishuhudia Injili ya neema ya Mungu.
25 “Ngo Pwknvyarnv gv Karv nga nonu mvnwng gv, pingkolo vngkarla japji kartoku. Okv vjv ngo chinduku ho nonuno nga lvkoka kaapa kumare.
“Nami sasa najua ya kuwa hakuna hata mmoja miongoni mwenu ambaye nimemhubiria Ufalme wa Mungu katika kwenda kwangu huku na huko, atakayeniona uso tena.
26 Vkvlvgabv ngo silu gv alu lokv nonuna jvjvklvbv mirw doonv la: Vdwlo nonu akonvka nyenam goka dubolo, ngo ogugoka nonu lvlo ajv laya kumare.
Kwa hiyo nawatangazia leo, sina hatia ya damu ya mtu awaye yote.
27 Ngo Pwknvyarnv gv nonua chinsv gui vla mvngnam ogumvnwng nga nonua minji pvkunv.
Kwa kuwa sikusita kuwatangazia mapenzi yote ya Mungu.
28 Vkvlvgabv nonu atubongv chvrv bv kaala dosutvka okv Darwknv Dow gv nonua svlar kaaria dubv jinam vdwaka. Pwknvyarnv gv goklin kunam nyi vdwa rigv nvgobv ritokuka, hv ninyigv atubogv kuunyilo gv oyi lokv ninyigvbv mvpv kunv.
Jilindeni nafsi zenu na mlilinde lile kundi lote ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi wake. Lichungeni kanisa lake Mungu alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.
29 Ngo chindo ho ngoogv vngrokochingbv, nonugv pingkolo nyi vv busunam svcha jvbv rinv ngv aari nvpv okv gwngkw rinvpv nonua domumare.
Najua kwamba baada yangu kuondoka, mbwa mwitu wakali watakuja katikati yenu ambao hawatalihurumia kundi.
30 Dwv aari kunvpv noogv atubogv nyi lokv, vnggv rikunvpv mvngjwngnv vdwa bunugv koching bv.
Hata kutoka miongoni mwenu watainuka watu na kuupotosha ukweli ili wawavute wanafunzi wawafuate.
31 Vkvlvgabv bununo atuv hindum silaka! mvngpa laka ngoogv nam doomadakma bv nyiksinyikla dwkla nyingum go ho aluayu bv nonu mvnwng nga okv akinakin bv minpv nama.
Hivyo jilindeni! Kumbukeni kwamba kwa miaka mitatu sikuacha kamwe kuwaonya kila mmoja kwa machozi usiku na mchana.
32 “Okv vjak ngo nonuam Pwknvyarnv gv ringnam lo okv ninyigv ayanv doin lo tulwk jidunv, si nonua gwlwk am jiriku okv Pwknvyarnv gv anyuaya kunam ninyigv nyi mvnwng nga jiriku.
“Sasa nawakabidhi kwa Mungu na kwa neno la neema yake, linaloweza kuwajenga na kuwapa ninyi urithi miongoni mwa wote ambao wametakaswa.
33 Ngo vdwloka mvngma dvnv Yvvgvloka morkoain go okv vji vbego.
Sikutamani fedha wala dhahabu wala vazi la mtu yeyote.
34 Nonuno chindo oguaingbv ngo kudungkua ridudw ngoogv atugv laak lokv atubongv svngsu dubv okv ajin vdwaka.
Ninyi wenyewe mnajua kwamba mikono yangu hii imetumika kwa mahitaji yangu na ya wale waliokuwa pamoja nami.
35 Ogumvnwng nga ngo ritoku, ngo kaatamto oguaingbv ridur svngvdw ngonu heema nvnga ridur svvgorung. Mvngpa laka ngonugv Ahtu Jisu gv gaama ninyi atubongv minto, ‘Jinam si laanam amamsvnga mvngpu yadunv.’”
Katika kila jambo nimewaonyesha kwamba kwa njia hii ya kufanya kazi kwa bidii imetupasa kuwasaidia wadhaifu, mkikumbuka maneno ya Bwana Yesu mwenyewe jinsi alivyosema, ‘Ni heri kutoa kuliko kupokea.’”
36 Paul ninyigv minyaro koching bv, hv lvbwng lokv kompv tvla nyi mvnwng nga okv kumtoku.
Paulo alipomaliza kusema haya akapiga magoti pamoja nao wote akaomba.
37 Bunu mvnwng ngv kapnya toku okv chvgap toku okv mopup tvku ninyia.
Wote wakalia, wakamkumbatia Paulo na kumbusu,
38 Bunu mvnwng ngv mvngru nyatoku ogulvgavbolo Paul bunua mintoku, “nonuno nga vdwloka lvkodv kaapa kumare.” Vkvlvgabv bunu ninyia svpwlo vnglwk minggv toku.
Kilichowahuzunisha zaidi ni kwa sababu ya yale maneno aliyosema kwamba kamwe hawatauona uso wake tena. Wakaenda naye mpaka kwenye meli.