< Nehemja 3 >

1 Och översteprästen Eljasib och hans bröder, prästerna, stodo upp och byggde Fårporten, vilken de helgade, och i vilken de sedan satte in dörrarna. Vidare byggde de ända fram till Hammeatornet, som de helgade, och vidare fram till Hananeltornet.
Eliashibu kuhani mkuu na makuhani wenzake walikwenda kufanya kazi na kulijenga upya Lango la Kondoo. Waliliweka wakfu na kuweka milango mahali pake, wakajenga hadi kufikia Mnara wa Mia, ambao waliuweka wakfu hadi Mnara wa Hananeli.
2 Därbredvid byggde Jerikos män; och därbredvid byggde Sackur, Imris son.
Watu wa Yeriko wakajenga sehemu zilizopakana nao, naye Zakuri mwana wa Imri akajenga karibu nao.
3 Fiskporten byggdes av Hassenaas barn; de timrade upp den och satte in dess dörrar, dess riglar och bommar.
Lango la Samaki lilijengwa upya na wana wa Hasenaa. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango yake na makomeo na nondo.
4 Därbredvid arbetade Meremot, son till Uria, son till Hackos, på att sätta muren i stånd; därbredvid arbetade Mesullam, son till Berekja, son till Mesesabel; och därbredvid arbetade Sadok, Baanas son.
Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu iliyofuatia. Baada yake Meshulamu mwana wa Berekia, mwana wa Meshezabeli, alifanya ukarabati na aliyemfuatia ni Sadoki mwana wa Baana.
5 Därbredvid arbetade tekoaiterna, men de förnämsta bland dem ville icke böja sin hals till att tjäna sin Herre.
Sehemu iliyofuatia ilikarabatiwa na watu kutoka Tekoa, lakini wakuu wao walikataa kufanya kazi chini ya wasimamizi wao.
6 Gamla porten sattes i stånd av Jojada, Paseas son, och Mesullam, Besodjas son; de timrade upp den och satte in dess dörrar, dess riglar och bommar.
Lango la Yeshana lilikarabatiwa na Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango, makomeo na nondo.
7 Därbredvid arbetade gibeoniten Melatja och meronotiten Jadon jämte männen från Gibeon och Mispa, som lydde under ståthållaren i landet på andra sidan floden.
Karibu nao ukarabati ulifanywa na watu kutoka Gibeoni na Mispa, yaani Melati Mgibeoni, na Yadoni Mmeronothi, sehemu hizi zikiwa chini ya mamlaka ya mtawala wa Ngʼambo ya Frati.
8 Därbredvid arbetade Ussiel, Harhajas son, jämte guldsmederna; och därbredvid arbetade Hananja, en av salvoberedarna. Det nästföljande stycket av Jerusalem lät man vara, ända till Breda muren.
Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa masonara, alikarabati sehemu iliyofuatia, naye Hanania mmoja wa watengenezaji marashi akakarabati sehemu iliyofuatia. Walitengeneza Yerusalemu mpaka kufikia Ukuta Mpana.
9 Därbredvid arbetade Refaja, Hurs son, hövdingen över ena hälften av Jerusalems område.
Refaya mwana wa Huri, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia.
10 Därbredvid arbetade Jedaja, Harumafs son, mitt emot sitt eget hus; och därbredvid arbetade Hattus, Hasabnejas son.
Kupakana na sehemu hii, Yedaya mwana wa Harumafu alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba yake, naye Hatushi mwana wa Hashabnea akakarabati sehemu iliyofuatia.
11 En annan sträcka sattes i stånd av Malkia, Harims son, och av Hassub, Pahat-Moabs son, och därjämte Ugnstornet.
Malkiya mwana wa Harimu, na Hashubu mwana wa Pahath-Moabu walikarabati sehemu nyingine pamoja na Mnara wa Matanuru.
12 Därbredvid arbetade Sallum, Hallohes' son, hövdingen över andra hälften av Jerusalems område, han själv med sina döttrar.
Shalumu mwana wa Haloheshi, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia akisaidiwa na binti zake.
13 Dalporten sattes i stånd av Hanun och Sanoas invånare; de byggde upp den och satte in dess dörrar, dess riglar och bommar. De byggde ock ett tusen alnar på muren, ända fram till Dyngporten.
Lango la Bondeni lilikarabatiwa na Hanuni na wakazi wa Zanoa. Walilijenga upya, na kuweka milango yake na makomeo na nondo mahali pake. Pia walikarabati ukuta wenye urefu wa mita 450 hadi Lango la Samadi.
14 Och Dyngporten sattes i stånd av Malkia, Rekabs son, hövdingen över Bet-Hackerems område; han byggde upp den och satte in dess dörrar, dess riglar och bommar.
Lango la Samadi lilikarabatiwa na Malkiya mwana wa Rekabu, mtawala wa wilaya ya Beth-Hakeremu. Alilijenga upya, na kuweka milango yake, na makomeo na nondo.
15 Och Källporten sattes i stånd av Sallun, Kol-Hoses son, hövdingen över Mispas område; han byggde upp den och lade tak därpå och satte in dess dörrar, dess riglar och bommar. Han byggde ock muren vid Vattenledningsdammen, invid den kungliga trädgården, ända fram till trapporna som föra ned från Davids stad.
Lango la Chemchemi lilikarabatiwa na Shalumu mwana wa Kolhoze, mtawala wa wilaya ya Mispa. Alilijenga upya, akaliezeka na kuweka milango yake, na makomeo na nondo mahali pake. Pia alikarabati ukuta wa Bwawa la Siloamu karibu na Bustani ya Mfalme, hadi kwenye ngazi zinazoshuka kutoka Mji wa Daudi.
16 Därnäst sattes ett stycke i stånd av Nehemja, Asbuks son, hövdingen över ena hälften av Bet-Surs område, nämligen stycket ända fram till platsen mitt emot Davidsgravarna och vidare fram till den grävda dammen och till Hjältehuset.
Baada yake, Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-Suri, alikarabati kufikia mkabala na makaburi ya Daudi, mpaka kwenye bwawa lililotengenezwa, na kufikia Nyumba ya Mashujaa.
17 Därnäst arbetade leviterna under Rehum, Banis son; därbredvid arbetade Hasabja, hövdingen över ena hälften av Kegilas område, för sitt område.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na Walawi chini ya uongozi wa Rehumu mwana wa Bani. Aliyefuatia ni Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, aliyekarabati sehemu ya wilaya yake.
18 Därnäst arbetade deras bröder under Bavai, Henadads son, hövdingen över andra hälften av Kegilas område.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na ndugu zao chini ya usimamizi wa Binui mwana wa Henadadi, mtawala wa nusu hiyo ingine ya wilaya ya Keila.
19 Därbredvid sattes en annan sträcka i stånd av Eser, Jesuas son, hövdingen över Mispa, nämligen från platsen mitt emot uppgången till tyghuset i Vinkeln.
Baada yao, Ezeri mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia ile sehemu inayotazamana na mwinuko wa kuelekea kwenye ghala la kuhifadhia silaha, mpaka kwenye pembe ya ukuta.
20 Därnäst sattes, under ivrigt arbete, en annan sträcka i stånd av Baruk, Sabbais son, från Vinkeln ända fram till ingången till översteprästen Eljasibs hus.
Baada yake, Baruku mwana wa Zakai alikarabati kwa bidii sehemu nyingine kuanzia ile pembe, mpaka kwenye lango la nyumba ya Eliashibu kuhani mkuu.
21 Därnäst sattes en annan sträcka i stånd av Meremot, son till Uria, son till Hackos, från ingången till Eljasibs hus ända dit där Eljasibs hus slutar.
Kupakana naye, Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia penye lango la nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wake.
22 Därnäst arbetade prästerna, männen från Jordanslätten.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na makuhani waliotoka eneo lililouzunguka mji.
23 Därnäst arbetade Benjamin och Hassub, mitt emot sitt eget hus; därnäst arbetade Asarja, son till Maaseja, son till Ananja, utmed sitt eget hus.
Baada yao Benyamini na Hashubu walikarabati mbele ya nyumba zao, na baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania alifanya ukarabati kando ya nyumba yake.
24 Därnäst sattes en annan sträcka i stånd av Binnui, Henadads son, från Asarjas hus ända fram till Vinkeln och vidare fram till Hörnet.
Baada yake, Binui mwana wa Henadadi alikarabati sehemu nyingine, kuanzia kwenye nyumba ya Azaria mpaka kwenye pembe ya ukuta.
25 Palal, Usais son, satte i stånd stycket från platsen mitt emot Vinkeln och det torn som skjuter ut från det övre konungshuset, vid fängelsegården; därnäst kom Pedaja, Pareos' son.
Naye Palali, mwana wa Uzai alijenga sehemu iliyokuwa mkabala na pembe ya ukuta, mpaka kwenye mnara wa juu ambao unajitokeza kuanzia kwenye jumba la kifalme, kando ya ua wa walinzi. Baada yake, Pedaya mwana wa Paroshi,
26 (Men tempelträlarna bodde på Ofel ända fram till platsen mitt emot Vattenporten mot öster och det utskjutande tornet.)
na watumishi wa Hekalu walioishi juu ya kilima cha Ofeli walikarabati hadi kufikia mkabala na Lango la Maji, kuelekea mashariki na ule mnara uliojitokeza.
27 Därnäst sattes en annan sträcka i stånd av tekoaiterna, från platsen mitt emot det stora utskjutande tornet ända fram till Ofelmuren.
Baada yao, watu wa Tekoa walikarabati sehemu nyingine, kuanzia mnara mkubwa utokezao hadi ukuta wa Ofeli.
28 Ovanför Hästporten arbetade prästerna, var och en mitt emot sitt eget hus.
Makuhani walifanya ukarabati juu ya Lango la Farasi, kila mmoja mbele ya nyumba yake.
29 Därnäst arbetade Sadok, Immers son, mitt emot sitt eget hus; och därnäst arbetade Semaja, Sekanjas son, som hade vakten vid Östra porten.
Baada yao, Sadoki mwana wa Imeri alifanya ukarabati mkabala na nyumba yake. Baada yake, Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa Lango la Mashariki, alifanya ukarabati.
30 Därnäst sattes en annan sträcka i stånd av Hananja, Selemjas son, och Hanun, Salafs sjätte son; därnäst arbetade Mesullam, Berekjas son, mitt emot sin tempelkammare.
Baada yake, Hanania mwana wa Shelemia, na Hanuni mwana wa sita wa Salafu walikarabati sehemu nyingine. Baada yao, Meshulamu mwana wa Berekia alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba zake za kuishi.
31 Därnäst sattes ett stycke i stånd av Malkia, en av guldsmederna, ända fram till tempelträlarnas och köpmännens hus, mitt emot Mönstringsporten och vidare fram till Hörnsalen.
Baada yake Malkiya, mmoja wa masonara, alifanya ukarabati mpaka kwenye nyumba za watumishi wa Hekalu na wafanyabiashara, mkabala na Lango la Ukaguzi, hadi kufikia chumba kilicho juu ya pembe.
32 Och mellan Hörnsalen och Fårporten arbetade guldsmederna och köpmännen på att sätta muren i stånd.
Masonara na wafanyabiashara walifanya ukarabati kutoka chumba kilichoko juu ya pembe hadi Lango la Kondoo.

< Nehemja 3 >