< Josua 19 >
1 Och den andra lotten föll ut för Simeon, för Simeons barns stam, efter deras släkter; och de fingo sin arvedel inom Juda barns arvedel.
Upigaji wa pili wa kura uliangukia kwa Simoni na waligawiwa kwa kila ukoo wao. Urithi wao ulikuwa katikati ya urithi ulikuwa ni mali ya kabila la Yuda.
2 De fingo inom dessas arvedel Beer-Seba, Seba, Molada,
Urithi waliokuwa nao ni Beerisheba, Sheba, Molada,
3 Hasar-Sual, Bala, Esem,
Hazari Shuali, Bala, Ezemu,
Elitoladi, Bethuli na Horma.
5 Siklag, Bet-Hammarkabot, Hasar-Susa,
Simoni alikuwa pia na Ziklagi, Bethi Markabothi, Hazari Susa,
6 Bet-Lebaot och Saruhen -- tretton städer med deras byar;
Bethi Lebaothi, na Sharuheni. Kulikuwa na miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake. Vile vile
7 Ain, Rimmon, Eter och Asan -- fyra städer med deras byar;
Simoni alimiliki Aini, Rimon, Etheri, na Ashani. Hii ilikuwa ni miji minne pamoja na vijiji vyake.
8 därtill alla de byar som lågo runt omkring dessa städer, ända till Baalat-Beer, det sydliga Rama. Detta var Simeons barns arvedel, efter deras släkter.
Miji hii pamoja na vijiji vilivyoizunguka hata kufika Baalathi Beeri (ambao ndio Rama katika Negevu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simoni, waliopewa kwa koo zao.
9 Ur Juda barns skifte fingo Simeons barn sin arvedel, ty Juda barns lott var för stor för dem; därför fingo Simeons barn sin arvedel inom deras arvedel.
Urithi wa kabila la Simoni ulikuwa sehemu ya himaya ya kabila la Yuda. Hii ni kwasababu nchi waliyopewa kabila la Yuda ilikuwa ni kubwa kwao, na hivyo kabila la Simoni lilipokea urithi wao kutoka katika sehemu yao ya katikati.
10 Den tredje lotten drogs ut för Sebulons barn, efter deras släkter; och gränsen för deras arvedel gick ända till Sarid.
Upigaji wa kura ya tatu uliangukia kwa kabila la Zabuloni, na walipewa kwa koo zao. Mpaka wa urithi wao ulianzia huko Saridi.
11 Därifrån drog sig deras gräns västerut uppåt till Mareala och träffade Dabbeset och träffade vidare dalen som ligger gent emot Jokneam.
Mpaka wao ulipanda upande wa magharibi kuelekea Marala na ukaigusa Dabeshethi, na kisha ukasonga kuelekea kijito kilichokuwa mkabala na Yokineamu.
12 På andra sidan från Sarid, österut mot solens uppgång, vände den sig åt Kislot-Tabors område och gick vidare till Dobrat och upp till Jafia.
Kutoka Saridi mpaka ulizunguka upande wa mashariki kuelekea mashariki na ulienda hadi mpaka wa Kislothi Tabori. Kutoka hapo uliendelea hadi Daberathi na kisha ulipanda hata Yafia.
13 Därifrån gick den fram österut mot solens uppgång till Gat-Hefer och Et-Kasin och vidare till det Rimmon som sträcker sig till Nea.
Kutoka hapo ulipita katika upande wa mashariki mwa Gathi Heferi, na kisha ukafika Ethikazini, baadaye ulienda hadi Rimoni na kisha ukageuka kuelekea Nea.
14 Härförbi böjde sig gränsen i norr till Hannaton och gick så ut vid Jifta-Els dal.
Mpaka ulizunguka kueleka kaskazini ukafika Hanathoni na ulikomea katika bonde la Ifta Eli.
15 Och den omfattade Kattat, Nahalal, Simron, Jidala och Bet-Lehem -- tolv städer med deras byar.
Mkoa huu ulijumuisha miji ya Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala, na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
16 Detta var Sebulons barns arvedel, efter deras släkter, de nämnda städerna med sina byar.
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Zabuloni, waliopewa kwa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
17 För Isaskar föll den fjärde lotten ut, för Isaskars barn, efter deras släkter.
Upigaji kura wa nne uliangukia kwa Isakari, na waligawiwa kufuatana na koo zao.
18 Och deras gräns omfattade Jisreel, Kesullot, Sunem,
Eneo lao lilijumuisha Jezreelli, Kesuloothi, Shunemu,
19 Hafaraim, Sion, Anaharat,
Hafaraimu, Shioni, na Anaharathi.
Pia ilijumuisha miji ya Rabithi, Kishioni, Ebezi,
21 Remet, En-Gannim, En-Hadda och Bet-Passes;
Remethi, Enganimu, Enihada, na Bethipazezi.
22 och gränsen träffade Tabor, Sahasuma och Bet-Semes; och deras gräns gick ut vid Jordan -- sexton städer med deras byar.
Mpaka wao ulifika Tabor, Shahazuma, na Bethi Shemeshi, na ukakomea katika Yordani. Ilikuwa ni miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
23 Detta var Isaskars barns stams arvedel, efter deras släkter, städerna med sina byar.
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Isakari, na walipewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
24 Den femte lotten föll ut för Asers barns stam, efter deras släkter.
Upigaji wa kura ya tano uliangukia kwa kabila la Asheri, na walipewa kwa koo zao.
25 Och deras gräns omfattade Helkat, Hali, Beten, Aksaf,
Eneo lao lilijumuisha miji ya Helikathi, Hali, Beteni, Akashafu,
26 Alammelek, Amead och Miseal; och vid havet träffade den Karmel och Sihor-Libnat.
Alameleki, Amadi, na Mshali. Mpaka wa magharibi ulitanuka hadi Karmeli na Shihori Libnathi.
27 Därefter vände den sig åt öster till Bet-Dagon och träffade Sebulon och Jifta-Els dal i norr, vidare Bet-Haemek och Negiel och gick så ut till Kabul i norr.
Kisha ulizunguka upande wa mashariki kueleka Bethi Dagoni na ukaenda hadi Zabuloni, na kisha ukafika katika bonde la ifutaheli, upande wa kaskazini mwa Bethemeki na Neieli. Baadaye uliendelea mbele hata Kabuli kueleka upande wa Kaskazini.
28 Och den omfattade Ebron, Rehob, Hammon och Kana, ända upp till Stora Sidon.
Na kisha ulienda hadi Ebroni, Rehobu, Hammoni, na Kana, hata kufika mji mkubwa wa Sidoni.
29 Och gränsen vände sig till Rama och gick fram till den befästa staden Tyrus; sedan vände sig gränsen till Hosa och gick så ut vid havet där landsträckan vid Aksib begynner.
Mpaka ulirudi nyuma kuelekea Rama, na kisha ukafika kwenye mji wa Tiro uliokuwa na ngome. Baada ya hapo mpaka ulizunguka kuelekea Hosa na ulikomea katika bahari, katika mkoa wa Akizibu,
30 Och den omfattade Umma, Afek och Rehob -- tjugutvå städer med deras byar.
Umma, Afeki, na Rehobu. Kulikuwa na miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
31 Detta var Asers barns stams arvedel, efter deras släkter, de nämnda städerna med sina byar.
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Asheri, na waliopewa kwa koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
32 För Naftali barn föll den sjätte lotten ut, för Naftali barn, efter deras släkter.
Upigaji wa kura wa mara ya sita uliangukia kwa kabila la Nafutali, na walipewa kufuatana na koo zao.
33 Och deras gräns gick från Helef, från terebinten i Saanannim till Adami-Hannekeb och Jabneel, ända till Lackum, och gick så ut vid Jordan.
Mpaka wao ulianzia Helefu, kutoka katika mwaloni huko Zaananimu, ulipanda hadi Adaminekebu na Yabneeli, umbali kama Lakumu; na ulikomea katka Yordani.
34 Och gränsen vände sig västerut till Asnot-Tabor och gick vidare därifrån till Huckok; den träffade Sebulon i söder, och Aser träffade den i väster och Juda med Jordan i öster.
Mpaka ule ulizunguka upande wa magharibi kuelekea Aznothi Tabori na ulipanda hadi Hukoki; uligusa Zabuloni katika upande wa kusini, na ulifika hata Asheri katika upande wa magharibi, na Yuda katika upande wa mashariki huko katika mto Yordani.
35 Och den omfattade de befästa städerna Siddim, Ser och Hammat, Rackat och Kinneret,
Miji yenye ngome ilikuwa ni Zidimu, Zeri, Hammathi, Rakathi, Kinnerethi,
37 Kedes, Edrei, En-Hasor,
Kedeshi, Edrei, na Eni Hazori.
38 Jireon och Migdal-El, Horem, Bet-Anat och Bet-Semes -- nitton städer med deras byar.
Pia kulikuwa na miji ya Yironi, Migdaleli, Horemu, Bethi Anathi, na Bethi Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa, pamoja na vijiji vyake.
39 Detta var Naftali barns stams arvedel efter deras släkter, städerna med sina byar.
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Nafutali, na walipewa miji pamoja na vijiji vyake kufuatana na koo zao.
40 För Dans barns stam, efter deras släkter, föll den sjunde lotten ut.
Upigaji wa kura ya saba uliangukia kwa kabila la Dani, na walipewa kufuatana na koo zao.
41 Och gränsen för deras arvedel omfattade Sorga, Estaol, Ir-Semes,
Eneo lao la urithi lilijumuisha miji ya Zora, Eshitaoli, Iri Shemeshi,
42 Saalabbin, Ajalon, Jitla,
Shaalabini, Aijaloni, na Ithila.
Vile vile lilijumuisha miji ya Eloni, Timna, Ekroni,
44 Elteke, Gibbeton, Baalat,
Eliteke, Gibethoni, Baalathi,
45 Jehud, Bene-Berak, Gat-Rimmon,
Yehudi, Bene - Beraki, Gathi Rimoni,
46 Me-Hajarkon och Harackon, tillika med området framför Jafo.
Me -Yarkoni, na Rakoni sambamba na eneo la karibu na Yopa.
47 (Men när sedan Dans barns område gick förlorat för dem, drogo Dans barn upp och belägrade Lesem och intogo det och slogo dess invånare med svärdsegg; och sedan de så hade tagit det i besittning, bosatte de sig där och kallade Lesem för Dan, efter Dans, sin faders, namn.)
Ilitokea wakati mpaka wa kabila la Dani ulipowapotea, kabila la Dani waliishambulia Leshemu, wakapigana nao, na wakauteka. Waliua kila mtu kwa upanga, wakauchukua ukawa mali yao, na wakakaa ndani yake. Wakauita mji ule Dani jina la babu yao badala ya Leshemu.
48 Detta var Dans barns stams arvedel, efter deras släkter, de nämnda städerna med sina byar.
Huu ulikuwa urithi wa kabila la Dani, waliopewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
49 När Israels barn så hade utskiftat landet efter dess gränser, gåvo de åt Josua, Nuns son, en särskild arvedel ibland sig.
Walipomaliza kugawana urithi wa nchi, watu wa Israeli walimpa urithi Yoshua mwana wa Nuni kutoka miongoni mwao.
50 Efter HERRENS befallning gåvo de honom nämligen den stad som han begärde, Timnat-Sera i Efraims bergsbygd; och han bebyggde staden och bosatte sig där.
Kwa amri ya Yahweh walimpatia mji wa Timnathi Sera ambao aliuomba, ulikuwa katika nchi ya milima ya Efraimu. Aliujenga mji na akaishi huko.
51 Dessa voro de arvslotter som prästen Eleasar och Josua, Nuns son, och huvudmännen för familjerna inom Israels barns stammar utskiftade genom lottkastning i Silo inför HERRENS ansikte, vid ingången till uppenbarelsetältet. Så avslutade de nu fördelningen av landet.
Na huu ndio urithi ambao Eliazari kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli, waligawa kwa kupiga kura huko Shilo, mbele za Yahweh katika mlango wa hema la kukutania. Na hivyo wakamaliza kuigawa nchi.