< 2 Mosebok 39 >

1 Och av det mörkblåa, det purpurröda och det rosenröda garnet gjorde man stickade kläder till tjänsten i helgedomen; och man gjorde de andra heliga kläderna som Aron skulle hava, såsom HERREN hade bjudit Mose.
Na kutokana na ule uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili wakafanya mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Basi wakafanya yale mavazi matakatifu yaliyokuwa kwa ajili ya Aruni, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
2 Efoden gjorde man av guld och av mörkblått, purpurrött, rosenrött och tvinnat vitt garn.
Basi akaifanya ile naivera ya dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.
3 Man hamrade ut guldet till tunna plåtar och skar dessa i trådar, så att man kunde väva in det i det mörkblåa, det purpurröda, det rosenröda och det vita garnet, med konstvävnad.
Kisha wakafua mabamba ya dhahabu yawe mabamba membamba, naye akakata nyuzi za kufuma pamoja na ule uzi wa bluu na ile sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kile kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kile kitani bora, kama kazi ya mjenzi.
4 Till den gjorde man axelstycken, som skulle fästas ihop; vid sina båda ändar fästes den ihop.
Wakaifanyia vipande vya begani vilivyounganishwa. Iliunganishwa kwenye miisho yake miwili.
5 Och skärpet, som skulle sitta på efoden och sammanhålla den, gjordes i ett stycke med den och av samma slags vävnad: av guld och av mörkblått, purpurrött, rosenrött och tvinnat vitt garn, allt såsom HERREN hade bjudit Mose.
Nao mshipi, uliokuwa juu yake ili kuifunga, ulikuwa wa kitambaa kilekile kulingana na ufundi wake, wa dhahabu, uzi wa bluu, na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
6 Och onyxstenarna omgav man med flätverk av guld; på dem voro Israels söners namn inristade, på samma sätt som man graverar signetringar.
Kisha wakafanya mawe ya shohamu yaliyopangwa kwenye mapambo ya dhahabu, yaliyochongwa kwa michoro ya muhuri kulingana na majina ya wana wa Israeli.
7 Och man satte dem på efodens axelstycken, för att stenarna skulle bringa Israels barn i åminnelse, allt såsom HERREN hade bjudit Mose.
Bezaleli akayaweka kwenye vile vipande vya begani vya naivera yawe mawe ya ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
8 Bröstskölden gjorde man i konstvävnad, i samma slags vävnad som efoden: av guld och av mörkblått, purpurrött, rosenrött och tvinnat vitt garn.
Kisha akafanya kile kifuko cha kifuani kwa ufundi wa mjenzi, kama ule ufundi wa naivera, kutokana na dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.
9 Bröstskölden gjordes liksidigt fyrkantig, i form av en väska gjorde man den: ett kvarter lång och ett kvarter bred, i form av en väska.
Kilikuwa mraba kilipokunjwa. Walikifanya kile kifuko cha kifuani, kinapokunjwa, shubiri moja urefu wake na shubiri moja upana wake.
10 Och man besatte den med fyra rader stenar: i första raden en karneol, en topas och en smaragd;
Kisha wakakijaza kwa mistari minne ya mawe. Mstari wa zabarijadi, topazi na zumaridi ulikuwa mstari wa kwanza.
11 i andra raden en karbunkel, en safir och en kalcedon;
Nao mstari wa pili ulikuwa feruzi, yakuti na yaspi.
12 i tredje raden en hyacint, en agat och en ametist;
Nao mstari wa tatu ulikuwa jiwe la leshemi, akiki na amethisti.
13 i fjärde raden en krysolit, en onyx och en jaspis. Med flätverk av guld blevo de omgivna i sina infattningar.
Nao mstari wa nne ulikuwa krisolito na shohamu na yashefi. Yaliwekwa katika mapambo ya dhahabu katika mahali pake.
14 Stenarna voro tolv, efter Israels söners namn, en för vart namn; var sten bar namnet på en av de tolv stammarna, inristat på samma sätt som man graverar signetringar.
Na mawe hayo yalikuwa kulingana na majina ya wana wa Israeli. Yalikuwa kumi na mawili kulingana na majina yao, kwa michongo ya muhuri, kila moja kulingana na jina lake kwa ajili ya yale makabila kumi na mawili.
15 Och man gjorde till bröstskölden kedjor i virat arbete, såsom man gör snodder, av rent guld.
Nao wakafanya juu ya kile kifuko cha kifuani minyororo yenye mashada, msokoto wa kamba, wa dhahabu safi.
16 Man gjorde vidare två flätverk av guld och två ringar av guld och satte dessa båda ringar i två av bröstsköldens hörn.
Kisha wakafanya mapambo mawili ya dhahabu na pete mbili za dhahabu na kuziweka hizo pete mbili kwenye ile miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani.
17 Och man fäste de båda guldsnodderna vid de båda ringarna, i bröstsköldens hörn.
Baada ya hilo wakapitisha zile kamba mbili za dhahabu kwenye zile pete mbili zilizo kwenye miisho ya kile kifuko cha kifuani.
18 Och de två snoddernas båda andra ändar fäste man vid de två flätverken och fäste dem så vid efodens axelstycken på dess framsida.
Nao wakapitisha ile miisho miwili ya zile kamba mbili kwenye yale mapambo mawili. Halafu wakaiweka juu ya vile vipande vya begani vya naivera, mbele yake.
19 Och man gjorde två andra ringar av guld och satte dem i bröstsköldens båda andra hörn, vid den kant därpå, som var vänd inåt mot efoden.
Kisha wakafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka kwenye ile miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani kwenye upindo wake ulio upande unaoelekea ile efodi upande wa ndani.
20 Och ytterligare gjorde man två ringar av guld och fäste dem vid efodens båda axelstycken, nedtill på dess framsida, där den fästes ihop, ovanför efodens skärp.
Halafu wakafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka juu ya vile vipande viwili vya begani vya efodi upande wake wa chini, sehemu yake ya mbele, karibu na mahali pake pa kuungania, juu ya ule mshipi wa naivera.
21 Och man knöt fast bröstskölden med ett mörkblått snöre, som gick från dess ringar in i efodens ringar, så att den satt ovanför efodens skärp, på det att bröstskölden icke skulle lossna från efoden, allt såsom HERREN hade bjudit Mose.
Mwishowe wakakifunga kile kifuko cha kifuani kwa pete zake kwenye zile pete za efodi kwa uzi wa bluu, ili kipate kuwa juu ya mshipi wa efodi na kile kifuko cha kifuani kisiondoke juu ya efodi, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
22 Efodkåpan gjorde man av vävt tyg, helt och hållet mörkblått.
Bezaleli akafanya lile koti la naivera, lote la uzi wa zambarau, kazi ya mshonaji.
23 Och mitt på kåpan gjordes en öppning, lik öppningen på en pansarskjorta; öppningen omgavs nämligen med en kant, för att den icke skulle slitas sönder.
Na sehemu wazi ya hilo koti ilikuwa katikati yake, kama sehemu wazi ya vazi la chuma. Sehemu hiyo iliyo wazi ilikuwa na ukingo kuizunguka pande zote ili isiraruke.
24 Och på kåpans nedre fåll satte man granatäpplen, gjorda av mörkblått, purpurrött och rosenrött tvinnat garn.
Halafu wakafanya kwenye upindo wa hilo koti makomamanga ya uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, vilivyosokotwa pamoja.
25 Och man gjorde bjällror av rent guld och satte dessa bjällror mellan granatäpplena runt omkring fållen på kåpan, mellan granatäpplena:
Wakafanya kengele za dhahabu safi na kuziweka kengele hizo katikati ya makomamanga kwenye upindo wa lile koti kuzunguka pande zote, katikati ya makomamanga;
26 en bjällra och så ett granatäpple, sedan en bjällra och så åter ett granatäpple, runt omkring fållen på kåpan, att bäras vid tjänstgöringen, såsom HERREN hade bjudit Mose.
kengele na komamanga, kengele na komamanga kwenye upindo wa hilo koti kuzunguka pande zote, kwa ajili ya kuhudumu, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
27 Och man gjorde åt Aron och hans söner livklädnaderna av vitt garn, i vävt arbete,
Kisha wakafanya zile kamba za kitani bora, kwa ajili ya Haruni na wanawe.
28 huvudbindeln av vitt garn, högtidshuvorna av vitt garn och linnebenkläderna av tvinnat vitt garn,
Na kile kilemba cha kitani bora na yale mavalio ya kichwani ya mapambo ya kitani bora na zile suruali za kitani bora kilichosokotwa,
29 äntligen bältet av tvinnat vitt garn och av mörkblått, purpurrött och rosenrött garn, i brokig vävnad, allt såsom HERREN hade bjudit Mose.
na ule ukumbuu wa kitani bora kilichosokotwa na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, kazi ya mfumaji, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
30 Och man gjorde plåten till det heliga diademet av rent guld, och på den skrev man, såsom man graverar signetringar: »Helgad åt HERREN.»
Mwishowe wakafanya lile bamba linalong’aa, ishara takatifu ya wakfu, kutokana na dhahabu safi na kuandika juu yake maandishi kwa mchongo wa muhuri: “Utakatifu kwa Yahweh.”
31 Och man fäste vid den ett mörkblått snöre och satte den ovanpå huvudbindeln, allt såsom HERREN hade bjudit Mose.
Kisha wakalitia uzi wa bluu ili waliweke juu ya kile kilemba upande wa juu. Kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
32 Så blev då allt arbetet på uppenbarelsetältets tabernakel fullbordat. Israels barn utförde det; de gjorde i alla stycken såsom HERREN hade bjudit Mose.
Basi kazi ya ile maskani ya hema la mkutano ikafikia mwisho wake. Kwa maana wana wa Israeli waliendelea kufanya kulingana na yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa.
33 Och de förde fram till Mose tabernaklet, dess täckelse och alla dess tillbehör, dess häktor, bräder, tvärstänger, stol par och fotstycken,
Nao wakaileta maskani kwa Musa, lile hema pamoja na vyombo vyake vyote, kulabu zake, viunzi vyake vya mbao, miti yake na nguzo zake na vikalio vyake,
34 överdraget av rödfärgade vädurskinn och överdraget av tahasskinn och den förlåt som skulle hänga framför arken,
na kifuniko chake cha ngozi za kondoo-dume zilizotiwa rangi nyekundu na kifuniko chake cha ngozi za sili na pazia la kisitiri,
35 vidare vittnesbördets ark med dess stänger, så ock nådastolen,
na sanduku la ushuhuda na miti yake na kifuniko.
36 bordet med alla dess tillbehör och skådebröden,
Wakaleta meza, vyombo vyake vyote, na ule mkate wa wonyesho,
37 den gyllene ljusstaken, lamporna som skulle sättas på den och alla dess andra tillbehör, oljan till ljusstaken,
kile kinara cha taa cha dhahabu safi, taa zake, ule mstari wa taa, na vyombo vyake vyote na yale mafuta ya kuangazia taa,
38 det gyllene altaret, smörjelseoljan och den välluktande rökelsen, förhänget för ingången till tältet,
na madhabahu ya dhahabu na yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na ule uvumba uliotiwa manukato na kile kisitiri kwa ajili ya mwingilio wa hema,
39 kopparaltaret med tillhörande koppargaller, dess stänger och alla dess tillbehör, bäckenet med dess fotställning.
ile madhabahu ya shaba na kile kiunzi chake cha shaba, miti yake na vyombo vyake vyote, ile beseni na kinara chake,
40 omhängena till förgården, dess stolpar och fotstycken, förhänget för porten till förgården, dess streck och pluggar, alla redskap till arbetet vid uppenbarelsetältets tabernakel
Wakaleta mapazia ya ua, nguzo zake na vikalio vyake na kile kisitiri kwa ajili ya lango la ua, kamba zake za hema na misumari yake ya hema na vyombo vyote kwa ajili ya utumishi wa maskani, kwa ajili ya hema ya kukutania.
41 äntligen de stickade kläderna till tjänsten i helgedomen och prästen Arons andra heliga kläder, så ock hans söners prästkläder.
Wakaleta yale mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika patakatifu, yale mavazi matakatifu kwa ajili ya Aruni kuhani na mavazi ya wanawe ya kutumikia wakiwa makuhani.
42 Såsom HERREN hade bjudit Mose så hade Israels barn i alla stycken gjort allt arbete.
Kulingana na yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa, hivyo ndivyo wana wa Israeli walivyoufanya utumishi wote.
43 Och Mose besåg allt arbetet och fann att de hade utfört det, att de hade gjort såsom HERREN hade bjudit. Och Mose välsignade dem
Naye Musa akaiona ile kazi yote, na, tazama, walikuwa wameifanya kama vile Yahweh alivyokuwa ameamuru. Hivyo ndivyo walivyokuwa wamefanya. Basi Musa akawabariki.

< 2 Mosebok 39 >